Mnaomtetea Magufuli mitandaoni wengi wenu hamumjui vizuri, mnamfahamu juu juu tu

Kama wewe unamuona Magufuli alikua mbaya kwa sababu zako ni haki yako, basi vile vile anaemuona Magufuli mzuri kwa sababu zake ana haki pia.

Kwa nini ulazimisha watu wawe na mtazamo kama wako?

Magufuli ndio rais bora za Tanzania baada ya Nyerere, zaidi ya hapo hakuna mwingine.
 
kwa maana nyingine, wote wanaomshabikia Magu ni mbumbumbu wa mtu wasiomjua undani wake- Period. Nimekuelewa.
 
Mimi magufuli nimemjua Toka akiwa mdogo.Alikuwa na upendo wa hali ya juu sana Kwa watu wema lakini alikuwa mkali Kwa watu wabaya kama wezi, wazembe na wasiujishughulisha.Ndiyo maana alipokuwa rais aliwanyoosha sana mafisadi.
Mwingine atajitokeza na kusema kwamba alimjua Magufuli kabla hajazaliwa.
 
We takataka kabisa.. ebu ondoa uchafu huu.. huyo samia kafanya kitu gani ambacho hakina mkono wa magufuli
 
We takataka kabisa.. ebu ondoa uchafu huu.. huyo samia kafanya kitu gani ambacho hakina mkoko wa magufuli
 
Sasa kwann uji sahaulishe chenji ya mtu?
 
Unajua ukisema wanaomtetea ina maana hukubaliani na kutofautiana mitazamo kwamba mlitaka watu wote tuwe na mitazamo sawa kuhusu Magufuli? Na ndio sababu hadi leo bado mnaendelea kueleza mabaya ya Magufuli kwa sababu kuna watu wanamtetea?
 
Aiseee wa Tz noma

Sasa kudai chenji ni Roho mbaya,
Wameamka wale wenye kutaka kulipiga viboko kaburi, kuamsha mada za Rais aliyelala kaburini miaka minne iliyopita ni roho mbaya iliyo hai inayoishi.

Ni muendelezo wa roho ya kisasi kumsema mtu eti alikuwa na kisasi alipokuwa hai.
 
Kama umenisoma vizuri, sijatoa maoni yangu ya kwamba mama yupo vizuri or not; nimesema, "wajane wapo wengi, ungeweka picha zao wote tujiridhishe"
Hivo tu
 
Hawa machawa wengi wao ni mataahira!
JPM kajenga barabara ya Mbezi -Kinyerezi!
Barabara za Buza na maeneo kibao kinondoni huko!
Huyu Mama kwangu mimi naona anafanya vitu vya kawaida tu ambavo hawa wewe ungekuwa Rais ungefanya hakuna maajabu yeyote!
Sio kweli huyu mama anakutana na upinzani wa jinsia yake atafanya mema elfu moja lakini baya moja litayachafua mema yote.

Anawasuta wote wenye kudhani kuwa mwanamke hawezi kuwa rais, tena kwa vitendo.
 
Magufuli alikuwa katili Kwa wapenda vitonga, mashoga, mafisadi, Wezi na wezembe Sasa chenji huwa ni Mali yako au ya aliyekutuma nyie ndo vidume ambao manauza ubingwa Kwa tamaa na ujinga
 
Unajua ukisema wanaomtetea ina maana hukubaliani na kutofautiana mitazamo kwamba mlitaka watu wote tuwe na mitazamo sawa kuhusu Magufuli? Na ndio sababu hadi leo bado mnaendelea kueleza mabaya ya Magufuli kwa sababu kuna watu wanamtetea?
Gazeti la Mwananchi liliwekaga link ya kupigia KURA kati ya Marais wote wa Tanzania; waliombaga msamaha haraka; marehemu walikimbiza mno yaani; Magufuli akiwa yupo mbali mno. Mleta uzi, we fanya kitu kimoja hata humu, pitisha kura ya maoni humu ndio utajua "wasio na akili" humu jukwaani wapo wangapi?
 
Kumbuka kuwa marais wote wa CCM wanatekeleza ilani ile ile, tatizo letu ni kule kuwaabudu baadhi na kuwachukia baadhi. Sisi kushabikia urais wa fulani kunatunyima uwezo wa kufahamu kuwa wote ni watimizaji wa kinachoandikwa kwenye ilani ya uchaguzi.
 
Wanaendeshwa na mahaba niue tu.

Ukiangalia mkewe alivyonawiri baada ya yule mzee kufariki tu utagundua yule mzee alikuwa tatizo lililoshindikana


Hata wewe ukifa mkeo atanawiri.
Mkeo sio mama yako ni mpenzi wa mtu yeyote na upendo unachuja isipokua upendo wa mama basi.

Hakuna nchi duniani iliyoendelea kwa kuwa na rais asiye mkali kwa mafisadi.


Kwa sasa wa WaTanzania sio wajinga tena wameshagunduq kuwa Wanasiasa wanatumia mgongo wa utawala kufuja mali za umma .

Kama unataka kuiba au kutajirika kwenye ofisi za umma basi kuwa Tayari kuzomewa mana unaiba mali za umma.

Wakati wa mkoloni zlitoza Kodi mara moja tu bila tozo lakini walitoa huduma za afya na Elimu bure na za viwango vya ulaya .
Kwa sababu gani wakoloni ambao ni wabaya na wabaguzi ,wageni ,wavamizi lakini waliweza kujenga uchumi wa nchi kwa haraka na kwa uhakika .!! ? Jibu ni kwamba hawakua wabinafsi wanapokabidhiwa ofisi za umma. Hakuna Governo aliyekua anaimba ili akajijengee nyumba binafsi ya kuishi na familia yake. Watumishi walipewa nyumba za umma na walikua hawana Tamaa ya kujilimbikizia mali kupitia ofisi za umma . Leo hii watu wa anashindana kula rushwa maofisini wengine walikua wanajiapza kabisa kuwe hawawezi kutoka ofisini wiki endi bila kuwa na mil. tatu mpaka tano. Pesa za umma zinaibiwa bila huruma halafu anatokea kiongozi asiye na huruma na mafisadi halafu WATU anatoa mapovu kwa marehemu . Hakuna mtu mbaya kwa watendaji waovu.
 
Unajua ukisema wanaomtetea ina maana hukubaliani na kutofautiana mitazamo kwamba mlitaka watu wote tuwe na mitazamo sawa kuhusu Magufuli? Na ndio sababu hadi leo bado mnaendelea kueleza mabaya ya Magufuli kwa sababu kuna watu wanamtetea?
Mna mtetea huyo mtu wenu Kwa propaganda kuliko facts na msingi wa utetezi wenu hauna mashiko.
 
Kuna tatizo kubwa kchwani mwa mleta mada na hata Kabendera.
1. Rais wa nchi kufukuza wenye vyeti feki na kuondoa watumishi hewa ni kosa?.
Ilitakiwa wakamatwe wote na kupigwa kifungo cha maisha,na waliojipatia pesa kupitia watumishi hewa ilitakiwa kinyongwa had kufa, ila hakufanya hivo.

2. Ya kwamba alitaka kumbaka ....,unao uthibitisho toka kwa mhusika kuwa alitaka kunibaka?.
Au ulikuwepo kushuhudia hilo tukio?.
Na kama ulikuwepo,nani alikualika?.

3.Mara alikuwa katili kwa familia yake.
Ni mke wake au watoto wake ndo wamekupa hizo nyepesi au ni hisia zako?.
Au nawewe ulikuwa mmoja wa wanafamilia ya Hayati?

4.Mara katoke alifukuzwa kwa kuvuta bangi,bangi na kufukuzwa kwake shule wewe kama wewe vimekuathiri au vimekusaidia kivipi?.
Je ni mwl yupi wa katoke aliye mfundisha Hayati ambaye hadi Leo yupo aliyekupa huo ushahidi?..

5. Ombi kwa vijana wote wanaopitia mada humu jamii forum,kuweni na adabu kwa viongozi wa nchi,Rais si sawa na mjomba wako ama shangazi yako,Rais wa nchi ndo nembo ama kichwa cha nchi.
Uwe mwanasiasa kijana au nani ,heshimuni sana viongozi wa nchi hasa Rais.

Binafsi mjipange kama mnataka kumchafua Magufuli,vinginevyo huyo mtu atabaki kama lulu ya taifa hili ya kila kiongozi ajaye kuiga nyendo zake za kuwaletea wanyonge maendeleo.

Kabendera nakushauri,usitumike kama pampas au condoms na huyo jamaa,yeye hana cha kupoteza achana naye.
Angalia mambo yako utayamalizaje kwa mda tulionao sasa hivi.
Lakini kama wametoa mafungu makubwa ili umchafue mzee wa watu,tambua utarudi bongo na utakaa mitaani na wanyone aliokuwa akiwatetea Magufuli.
Kaa chini utafakari,je ulichokifanya ni sahihi?.
Bila kupokea hizo hundi je ungeweza kukifanya?.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…