Mnaonaje Rais Samia akiongezwa muda wa kukaa kwenye dhamana na mamlaka yake hadi 2035?

Mnaonaje Rais Samia akiongezwa muda wa kukaa kwenye dhamana na mamlaka yake hadi 2035?

Nachokoza mada.

Wadau mnaonaje kama Samia akiongezwa muda wa kukaa kwenye dhamana na mamlaka yake hadi 2035? Kwa kuwa Samia alichukuwa nafasi yake kufuatia mauti ya mtangulizi wake mwanzo wa safari na kwamba hakukuwa na utaratibu wa mila na desturi ya uchaguzi bali ilikuwa ni kutimiza matakwa ya katiba;


Kiuhalali na kwa haki kwake, anastahili kuwa wa pili nyuma ya Mwl Nyerere kwa kukaa ofisini kwa miaka 15 kwa maana ya miaka aliyopokea kijiti kwa sharti la katiba na ndipo sasa astahili utaratibu wa mila na desturi yetu ya uchaguzi ambapo anaruhusiwa awamu mbili 2025 – 2035?

Nini maarifa yako, tupe maoni kwa vigezo na ushahidi.
Kwanini asipige kazi ya ukweli kwa miaka hii minne, matokeo yake yatawashawishi wananchi kuhusu hiyo issue.

Huu unatakiwa uwe wakati wa kuchapa kazi, kampeni baadaye.

Matokeo chanya ya kazi zake yatampigia kampeni nzuri tu kama ajira kuongezeka, biashara, uwezekaji kushamiri, masoko kwa wakulima, bei rafiki za pembejeo, mbolea, vifaa vya umwagiliaji,mazingira rafiki ya biashara, kupunguza rushwa, urasimu, kuunganisha nchi iwe yenye umoja zaidi, kupunguza matumizi yasiyo na tija kwa serikali, kuondoa au kupunguza kodi/ tozo zinazoumiza wengi. Maji, umeme kwa kila familia, kukuza utalii.

Nguvu zake zote, focus yake yote zingeelekezwa kutatua hizi changamoto.

Muda ni mchache, inabidi utumike vizuri kwa kazi aliyopewa na Watanzania,kutatua changamoto zao, sio kupiga kampeni kutoka siku za mwanzo za utawala wake.
 
Sijasoma huu upupu zaidi ya Heading, ndio maana tunataka katiba mpya ili nchi iwe na mfumo imara sio kuona mtu fulani ni bora kuliko fulani.
 
Sijasoma huu upupu zaidi ya Heading, ndio maana tunataka katiba mpya ili nchi iwe na mfumo imara sio kuona mtu fulani ni bora kuliko fulani.
Hata upupu pia una faida, una sababu kwanini uliumbwa. Soma hii uone Wascandinavia walivyowahi kuishi kwa upupu:-

Scandinavian model has made it become world low poverty rate [possibly ahead of the US] in an unbelievable anecdote that narrates that in the beginning of the past century its lineage was feeding on barks powder as main staples following dismal poverty, but accepting that challenge set the beginning of Scandinavia developing into a highly competitive service based economy with high employment levels and a generous social security system Majwala, D.O. (2019).
 
Nachokoza mada.

Wadau mnaonaje kama Rais Samia akiongezwa muda wa kukaa kwenye dhamana na mamlaka yake hadi 2035? Kwa kuwa Rais Samia alichukuwa nafasi yake kufuatia mauti ya mtangulizi wake mwanzo wa safari na kwamba hakukuwa na utaratibu wa mila na desturi ya uchaguzi bali ilikuwa ni kutimiza matakwa ya katiba.


Kiuhalali na kwa haki kwake, anastahili kuwa wa pili nyuma ya Mwl Nyerere kwa kukaa ofisini kwa miaka 15 kwa maana ya miaka aliyopokea kijiti kwa sharti la katiba na ndipo sasa astahili utaratibu wa mila na desturi yetu ya uchaguzi ambapo anaruhusiwa awamu mbili 2025 – 2035?

Nini maarifa yako, tupe maoni kwa vigezo na ushahidi.
Umeongea upuuzi sisi wapiga kura tunahitaji chama mbadala wa CCM
 
kuwa chawa ni shaida sana kuna hata wale walisemaga mwendazake alazimishwe wenyewe nao wamebadilika wanadai mama anaupiga mwingi yaani kijani wana matatizo mengi sana , they cant think poor them
Kila aliyepata dhamana ya kuongoza kwa wakati wake aliibuliwa hoja hii, hivyo siyo dhambi kama ikiibuliwa wakati wa SSH pia. Yawezekana mahitaji ya wakati yanahitaji kuwa na uamuzi kama wa China, Russia na Rwanda lakini labda hatujui au hatusikii ndiyo maana tunajikuta tunabaki kuganda kwenye hoja tu bila utekelezaji wake.
 
Hii mbona iko wazi kabisa,sijui kwa nini akina Nkamia hawakuondoa ukomo wa urais kabla kile kijamaa hakijajifia
 
Hii nchi haichezewi jamani mnavyoanza kupanga ya mbele na Mungu naye anapanga yake, bado hatujajifunza tun?
Mbona tulikuwa na dira ya 2025 iliyopangwa tangu 1999? Nchi iko, itakuwepo, Ikulu, ipo, itakuwepo, hivyo sidhani kama kupanga mapema ni dhambi. Hata kwa MUNGU hatuendagi kwa dharura bali kwa maandalizi ya kutosha (prior-preparation).
 
Nachokoza mada.

Wadau mnaonaje kama Rais Samia akiongezwa muda wa kukaa kwenye dhamana na mamlaka yake hadi 2035? Kwa kuwa Rais Samia alichukuwa nafasi yake kufuatia mauti ya mtangulizi wake mwanzo wa safari na kwamba hakukuwa na utaratibu wa mila na desturi ya uchaguzi bali ilikuwa ni kutimiza matakwa ya katiba.


Kiuhalali na kwa haki kwake, anastahili kuwa wa pili nyuma ya Mwl Nyerere kwa kukaa ofisini kwa miaka 15 kwa maana ya miaka aliyopokea kijiti kwa sharti la katiba na ndipo sasa astahili utaratibu wa mila na desturi yetu ya uchaguzi ambapo anaruhusiwa awamu mbili 2025 – 2035?

Nini maarifa yako, tupe maoni kwa vigezo na ushahidi.
Mnaanzaga hivi hivi. Mbona enzi za JK na Mkapa hamkuwa na haya mawazo?

Chawa ni janga kwa ili taifa.
 
Mnaanzaga hivi hivi. Mbona enzi za JK na Mkapa hamkuwa na haya mawazo?

Chawa ni janga kwa ili taifa.
Yalikuwepo, yaliibuka, ni kwa kuwa hukuwa na mtandao jamii, au inawezekana ulikuwa busy ku-clear supplementary za chuo kwamba hukutaka kusoma gazeti wala kufuatilia taarifa za habari.
 
Back
Top Bottom