Mnaowalea watoto wa kike bila kuwafundisha kazi za nyumbani mnawaandalia mazingira gani wakiwa wakubwa?

Mnaowalea watoto wa kike bila kuwafundisha kazi za nyumbani mnawaandalia mazingira gani wakiwa wakubwa?

Ni siku ya leo nimekumbuka nikiwa kwenye mahusiano hapo miaka ya 2015 na binti moja mrembo, mapenzi yalinoga sana lakini baada yakuanza kuishi nae niliona mapungufu mengi sana, la kwanza kabisa alikuwa hajui kupika yani ugali sometimes unakuwa mbichi halafu hata hajishughulishi kuongeza mboga za pembeni wakati vitu vipo vya kutosha stoo, mambo ya kunishuguhulikia usafi wangu mwanaume wake kama kunifulia nguo nayo ni mpaka iwe vuta nikuvute tena jeans anafulia brush!!, Kwakweli taa nyekundu iliwaka kichwani suala la ndoa likafutika kabisa.

Kumuandaa mtoto wako wa kike kujua kuishi kwenye ndoa za kiafrika ni jukumu ambalo wazazi hasa mama hapaswi kulilazia damu,

Kuna wazazi tunawaona kwamba wakiwa na vijipesa basi wanamleta house girl amsaidie mtoto wa kike kazi ambazo inabidi azifanye yeye ili ziwe mazoea ya kumjengea uzoefu ya msingi ya kuwa mke anaeweza kuishi ndani ya ndoa za kiafrika.

Tutofautishe vitu viwili, kuna kufanya kitu kwa kuweza baada ya kujifunza na kufanya kitu kwa mazoea, unaweza ukajifunza leo hii kupika hata kupitia youtube ama goole lakini itachukua muda mrefu sana kujenga mazoea ya kupika, ila kama umeshazoeshwa tangu mtoto si kwamba tu unaweza lakini umepata uzoefu mwingi sana na tayari imeshakua ni mazoea, unapika bila kuhisi uchovu wala hujivuti, una enjoy kupika inakua sio shughuli bali hobby.

Sasa tukija kwa watoto hawa wanaolelewa kitamthilia inakuwa ngumu sana mwanaume wa kiafrika kumuoa maana sisi wanaume wa kiafrika suala la kwanza kwenye kuoa huwa "tunavuta jiko" hivyo vingine huwa ni vya ziada tu vikiwemo elimu, uzuri, n.k. na ukikosea ukifanya vinginevyo ujipange!! Jiko ndio kazi kuu ya mwanamke akiwa ndani ikifuatiwa na usafi wa mme wake kuanzia kumfulia nguo zake mpaka soksi, na majukumu mengine kama usafi wa nyumba, n.k.

Unakuta binti wazazi wake hawakumfundisha wala kumzoesha shughuli za kupika, matokeo yake huku kwenye ndoa anazidisha chumvi, wali boko, ugali mbichi, n.k. vinaanza kuwa kero, na hata kama anajua kupika anakuwa hana mazoea, anapika kwa kujivuta vuta sana, badala ya kujiongeza asubuhi amuandalie mme wake hata viazi vya kuchemsha yeye anaweka mkate tu, siku ya jumapili mmepumzika myumbani yeye wala hajishughulishi kupika anasonga ugali na mchicha wakati stoo kuna mchele wa kutosha, friji kuna nyama ya kutosha, yani anaona kupika pilau ni kazi nzito sana, Mwanaume anaanza kumuona mzigo tu.

Kufua nguo za mmewe wala hana muda anampa huse girl sababu huko kwao nae alikuwa anafuliwa ama hakuzoeshwa, ni mambo yanayotia aibu maana huu sio uafrika wetu, haijalishi hata kama mwanamke ana cheo kizito ni lazima amfulie mme wake nguo zake hizo ndio mila zetu waafrika tangu na tangu,
Wazazi wanawaandalia unemployment
 
Ni siku ya leo nimekumbuka nikiwa kwenye mahusiano hapo miaka ya 2015 na binti moja mrembo, mapenzi yalinoga sana lakini baada yakuanza kuishi nae niliona mapungufu mengi sana, la kwanza kabisa alikuwa hajui kupika yani ugali sometimes unakuwa mbichi halafu hata hajishughulishi kuongeza mboga za pembeni wakati vitu vipo vya kutosha stoo, mambo ya kunishuguhulikia usafi wangu mwanaume wake kama kunifulia nguo nayo ni mpaka iwe vuta nikuvute tena jeans anafulia brush!!, Kwakweli taa nyekundu iliwaka kichwani suala la ndoa likafutika kabisa.

Kumuandaa mtoto wako wa kike kujua kuishi kwenye ndoa za kiafrika ni jukumu ambalo wazazi hasa mama hapaswi kulilazia damu,

Kuna wazazi tunawaona kwamba wakiwa na vijipesa basi wanamleta house girl amsaidie mtoto wa kike kazi ambazo inabidi azifanye yeye ili ziwe mazoea ya kumjengea uzoefu ya msingi ya kuwa mke anaeweza kuishi ndani ya ndoa za kiafrika.

Tutofautishe vitu viwili, kuna kufanya kitu kwa kuweza baada ya kujifunza na kufanya kitu kwa mazoea, unaweza ukajifunza leo hii kupika hata kupitia youtube ama goole lakini itachukua muda mrefu sana kujenga mazoea ya kupika, ila kama umeshazoeshwa tangu mtoto si kwamba tu unaweza lakini umepata uzoefu mwingi sana na tayari imeshakua ni mazoea, unapika bila kuhisi uchovu wala hujivuti, una enjoy kupika inakua sio shughuli bali hobby.

Sasa tukija kwa watoto hawa wanaolelewa kitamthilia inakuwa ngumu sana mwanaume wa kiafrika kumuoa maana sisi wanaume wa kiafrika suala la kwanza kwenye kuoa huwa "tunavuta jiko" hivyo vingine huwa ni vya ziada tu vikiwemo elimu, uzuri, n.k. na ukikosea ukifanya vinginevyo ujipange!! Jiko ndio kazi kuu ya mwanamke akiwa ndani ikifuatiwa na usafi wa mme wake kuanzia kumfulia nguo zake mpaka soksi, na majukumu mengine kama usafi wa nyumba, n.k.

Unakuta binti wazazi wake hawakumfundisha wala kumzoesha shughuli za kupika, matokeo yake huku kwenye ndoa anazidisha chumvi, wali boko, ugali mbichi, n.k. vinaanza kuwa kero, na hata kama anajua kupika anakuwa hana mazoea, anapika kwa kujivuta vuta sana, badala ya kujiongeza asubuhi amuandalie mme wake hata viazi vya kuchemsha yeye anaweka mkate tu, siku ya jumapili mmepumzika myumbani yeye wala hajishughulishi kupika anasonga ugali na mchicha wakati stoo kuna mchele wa kutosha, friji kuna nyama ya kutosha, yani anaona kupika pilau ni kazi nzito sana, Mwanaume anaanza kumuona mzigo tu.

Kufua nguo za mmewe wala hana muda anampa huse girl sababu huko kwao nae alikuwa anafuliwa ama hakuzoeshwa, ni mambo yanayotia aibu maana huu sio uafrika wetu, haijalishi hata kama mwanamke ana cheo kizito ni lazima amfulie mme wake nguo zake hizo ndio mila zetu waafrika tangu na tangu,
Dunia inabadilika lakini wewe hubadiliki. Yale mambo ya kizamani siku hizi yanapotea. Umejuaje hajui kusonga Ugali wakati wewe hujui? Na kama unajua kwa nini hukusonga au hukumwonyesha namna ya kusonga?
 
Sawa mkuu naona wewe endelea huko nyumbani kwako uwe unamfulia mke wako nguo, uwe unampikia mke wako, uwe unapiga deki, uwe unampokeza kupika kwenye misiba yeye awe anaenda na wanaume kuchimba kaburi, pia wezi wakija liwe jukumu lake kukulinda wewe.
Hujaweza kujenga hoja ya kimantiki na ya kidhahania bila kumhusisha mtu moja kwa moja?

Huu ni udhaifu katika uwezo wako wa kujenga hoja. Pia ni logical fallacy ya "ad hominem".

Unashindwa kujadili hoja, unaenda kumjadili mtu.
 
Dunia inabadilika lakini wewe hubadiliki. Yale mambo ya kizamani siku hizi yanapotea. Umejuaje hajui kusonga Ugali wakati wewe hujui? Na kama unajua kwa nini hukusonga au hukumwonyesha namna ya kusonga?
Automatically jukumu la kupika ni la mwanamke kama ilivyo kwa mwanaume kukabiliana na wezi nyumba ikivamiwa, not the other way around
 
Hujaweza kujenga hoja ya kimantiki na ya kidhahania bila kumhusisha mtu moja kwa moja?

Huu ni udhaifu katika uwezo wako wa kujenga hoja. Pia ni logical fallacy ya "ad hominem".

Unashindwa kujadili hoja, unaenda kumjadili mtu.
Jioni isjafika weka simu pembeni, wahi sokoni ukanunue nyanya na nazi, ukifika home toa mbuzi uikune naze, uvae kanga uingie jikoni, upepee kigae kiwake umpikie mkeo, usisahau kumpashia maji ya kuoga.
 
Automatically jukumu la kupika ni la mwanamke kama ilivyo kwa mwanaume kukabiliana na wezi nyumba ikivamiwa, not the other way around
Haya ni mawazo ya dunia ya kijima.

Dunia ya leo, si ajabu kukuta mwanamke ni mixed martial arts champion kaolewa na mwanamme ambaye ni professional chef.

Wanasaidiana kazi vizuri tu bila prejudice za gender roles.
 
Jioni isjafika weka simu pembeni, wahi sokoni ukanunue nyanya na nazi, ukifika home toa mbuzi uikune naze, uvae kanga uingie jikoni, upepee kigae kiwake umpikie mkeo, usisahau kumpashia maji ya kuoga.
Bado unaishi kwenye ulimwengu wa kukuna nazi na kupasha moto maji ya kuoga.

We have heaters for that, unafungua bomba hata dakika haifiki maji yashashika moto.

Ndiyo maana tangu awali nilisema hatuwezi kuelewana.

Tunaishi dunia mbili tofauti kabisa na sioni hata haja ya kuendeleza mazungumzo haya na wewe.
 
Hii ni jamii ya kiafrika na Mwanamke lazima ajue kupika na mila na desturi lazima zizingatiwe. mambo ya Gender roles na bla bla za usawa hao wenye nazo wenyewe kila siku talaka na balaa zingine kama hawana akili nzuri.
 
mabinti wa siku izi ukimwambia ishu ya kupika anakwambia kwani wew huna mikono ya kupika.
Yuko sahihi wewe ndie unakuwa umekosea kuoa ungeenda kuoa kijijini kwenu.Umezaliwa porini unakomaa kuoa mtoto wa mjini ambaye maisha yake yote kazi zote zinafaywa na Houseboy na House girl ikiwemo kufua nguo zake

Ungeoa saizi Yako mliyekua naye huko maporini vijijini kwenu usingekuwa na haya malalamiko


Kaajiri house boy na house girl wafanye hizo kazi
Makosa Yako fua mwenyewe na yeye atafua zake.Tena kajitahidi kama unaona Hadi nguo zake anafua kakuvumilia sana kwao hajazoea Hilo.Kutoongeza kesi fua mwenyewe nguo zako.

Kosa lako Kwa kutooa huko porini kwenu
 
Mwaume lazima ujue kazi zote..ila mwanamke kushindwa kujua hata
Mbona unakwepa kuelezea kwamba nao wanatakiwa kufundishwa kupika wakiwa wadogo pia. Mfano mimi ni mtu mzima ila nilifundishwa shughuli zote ikiwemo kupika nikiwa mtoto na imenisaidia sana sehemu mbalimbali. Ni vijana wangapi mabachela wanaishia kula magengeni na ma chips mayai sababu hawawezi kupika!?,kama ilivyo kwa mtoto wa kike vilevile kwa mtoto wa kiume kwenye shughuli zote, huko mbele ya safari hakuna guarantee ya kuoa wala kuolewa na hujui ni nini kitampa credit kwenye mazingira tofauti maishani awe wa kike au wa kiume.

Kama mfumo dume upo dunia nzima na hautaisha, hiyo si sababu ya kuuendekeza.

Ushawahi kukataa kula kwa sababu njaa ipo dunia nzima na haitaisha?

Na mfumo dume unaomlazimisha mwanamke awe mpishi apende asipende, bila kujali anafanya kazi nje ya nyumba au hafanyi, amechoka au hajachoka, bila ya kumlazimisha mwanamme kufanya hivyo, ni mfumo onevu na wenye dhamira mbovu.

Unakosaje kuliona hilo?
Apende asipende.........askuna anayelazimisha bali anashauriwa kuwa na hizo life skills muhimu.

Akitaka aache mbona wako wengi tu na hawafanyi na life linaendelea.

Kwanini wewe unataka kuamini Mwanamke akijifunza kupika ni mfumo dume?

Sasa hapo mfumo dume uko wapi?
 
Hii ni jamii ya kiafrika na Mwanamke lazima ajue kupika na mila na desturi lazima zizingatiwe. mambo ya Gender roles na bla bla za usawa hao wenye nazo wenyewe kila siku talaka na balaa zingine kama hawana akili nzuri.
Nimegundua Africa tunaishi maisha mazuri sana pamoja na umaskini wetu.

Wanawake wetu wanatupa raha sana na sisi tu awapa raha saba.
 
Mwaume lazima ujue kazi zote..ila mwanamke kushindwa kujua hata



Apende asipende.........askuna anayelazimisha bali anashauriwa kuwa na hizo life skills muhimu.

Akitaka aache mbona wako wengi tu na hawafanyi na life linaendelea.

Kwanini wewe unataka kuamini Mwanamke akijifunza kupika ni mfumo dume?

Sasa hapo mfumo dume uko wapi?
Kwani wapi nimesema mwanamke akijifunza kupika ni mfumodume?

Nimesema kupika ni life skill, kila mtu anatakiwa kujua, mwanamke, mwanamme.

Nimesema habari za kufanya kazi ya kupika kuwa ni kazi maalum ya mwanamke ni habari iliyopitwa na wakati, ni mfumodume.

Unaelewa tofauti kati ya mawili hayo?

Unaweza kufuatilia mantiki ya hoja yangu kwa nuance?
 
Ni siku ya leo nimekumbuka nikiwa kwenye mahusiano hapo miaka ya 2015 na binti moja mrembo, mapenzi yalinoga sana lakini baada yakuanza kuishi nae niliona mapungufu mengi sana, la kwanza kabisa alikuwa hajui kupika yani ugali sometimes unakuwa mbichi halafu hata hajishughulishi kuongeza mboga za pembeni wakati vitu vipo vya kutosha stoo, mambo ya kunishuguhulikia usafi wangu mwanaume wake kama kunifulia nguo nayo ni mpaka iwe vuta nikuvute tena jeans anafulia brush!!, Kwakweli taa nyekundu iliwaka kichwani suala la ndoa likafutika kabisa.

Kumuandaa mtoto wako wa kike kujua kuishi kwenye ndoa za kiafrika ni jukumu ambalo wazazi hasa mama hapaswi kulilazia damu,

Kuna wazazi tunawaona kwamba wakiwa na vijipesa basi wanamleta house girl amsaidie mtoto wa kike kazi ambazo inabidi azifanye yeye ili ziwe mazoea ya kumjengea uzoefu ya msingi ya kuwa mke anaeweza kuishi ndani ya ndoa za kiafrika.

Tutofautishe vitu viwili, kuna kufanya kitu kwa kuweza baada ya kujifunza na kufanya kitu kwa mazoea, unaweza ukajifunza leo hii kupika hata kupitia youtube ama goole lakini itachukua muda mrefu sana kujenga mazoea ya kupika, ila kama umeshazoeshwa tangu mtoto si kwamba tu unaweza lakini umepata uzoefu mwingi sana na tayari imeshakua ni mazoea, unapika bila kuhisi uchovu wala hujivuti, una enjoy kupika inakua sio shughuli bali hobby.

Sasa tukija kwa watoto hawa wanaolelewa kitamthilia inakuwa ngumu sana mwanaume wa kiafrika kumuoa maana sisi wanaume wa kiafrika suala la kwanza kwenye kuoa huwa "tunavuta jiko" hivyo vingine huwa ni vya ziada tu vikiwemo elimu, uzuri, n.k. na ukikosea ukifanya vinginevyo ujipange!! Jiko ndio kazi kuu ya mwanamke akiwa ndani ikifuatiwa na usafi wa mme wake kuanzia kumfulia nguo zake mpaka soksi, na majukumu mengine kama usafi wa nyumba, n.k.

Unakuta binti wazazi wake hawakumfundisha wala kumzoesha shughuli za kupika, matokeo yake huku kwenye ndoa anazidisha chumvi, wali boko, ugali mbichi, n.k. vinaanza kuwa kero, na hata kama anajua kupika anakuwa hana mazoea, anapika kwa kujivuta vuta sana, badala ya kujiongeza asubuhi amuandalie mme wake hata viazi vya kuchemsha yeye anaweka mkate tu, siku ya jumapili mmepumzika myumbani yeye wala hajishughulishi kupika anasonga ugali na mchicha wakati stoo kuna mchele wa kutosha, friji kuna nyama ya kutosha, yani anaona kupika pilau ni kazi nzito sana, Mwanaume anaanza kumuona mzigo tu.

Kufua nguo za mmewe wala hana muda anampa huse girl sababu huko kwao nae alikuwa anafuliwa ama hakuzoeshwa, ni mambo yanayotia aibu maana huu sio uafrika wetu, haijalishi hata kama mwanamke ana cheo kizito ni lazima amfulie mme wake nguo zake hizo ndio mila zetu waafrika tangu na tangu,
Mtoto/Mtu yeyote yule anapaswa kujua kuandaa chakula kwa sababu kula ni jambo la lazima.
 
Huu uzi una tatizo la gender roles.

Yani, kuweka kazi ya kupika kuwa ni kazi ya watoto wa kike.

Hii ni tabia ya jamii zenye mfumodume.

Inatakiwa watoto wote wajue kazi zote.

Kujua kupika, kuosha vyombo, kufua ni life skills ambazo hata mtoto wa kiume anatakiwa kuzijua, akiwa peke yake aweze kufanya hizo kazi. Na hata akioa, aweze kusaidiana na mkewe. Kuna uzi nimeuona jana, mtu anasema anamsaidia mke eake kwa sababu anaona mke wake anachoka sana. Sasa, utamsaidiaje mkeo kupika ikiwa mwanamme hujui kupika?

Ila, jamii yetu bado iko nyuma, imefanya kupika, kufua, ni kazi ya mwanamke.

Ndiyo maana hata uzi huu una assume automatically kuwa mwanamke/ mtoto wa kike ndiye anatakiwa kujua vitu hivi, mwanamme ni mtu wa kuhudumiwa tu.

Mfumodume. Dunia fulani ya umasikini wa mawazo.

Najua kwa mfumodume wetu, inawezekana wengi hawataelewa somo.
Ndo hivyo bongo Bado sana!
Hawawezi kukuelewa
 
Kufua jmn isiwe issue
Kuna mashine sikuhizi😅
Kupika ,wote tujue,ya kesho hatuyajui!
 
Ndo maana ndoa zinageuzwa ajira na wanawake. Toa pesa ufanyiwe kazi zote. Huna pesa piga nyeto
Sisi jamii zetu tumehalalisha ndoa kuwa ni ajira.

Tena utumwa kabisa, ndiyo maana mwanamke ananunuliwa kwa mahari.

Na mwanamme anategemea mwanamke ampikie, tena anasema kabisa "nimepata jiko".
 
Binti yangu nahakikisha anajiwrka dunia ya mbele. Namfundisha namna ya kuwa na followers wengi kwenye social media na faida zake. Hayo mambo ya ujima eti mtoto sijui ajue kupika, kufua wafundisheni watoto wenu. Sisi tunasonga mbele.
 
Back
Top Bottom