Mnapofanya Maendeleo msisahau kushirikisha ndugu zenu hata Kama mna ugomvi

Mnapofanya Maendeleo msisahau kushirikisha ndugu zenu hata Kama mna ugomvi

Kuna Mtu mmoja naye alikuwa anajenga Nyumba yake ilifikia hatua ya kupauwa ghafla akawa haonekani wala hapatikani kwenye Simu, mmoja wa mafundi wake ambaye ni Mzee akaweka Bati baadhi ya vyumba akahamia, bahati mbaya Nyumba yenyewe ilikuwa kwenye eneo ambalo halistahili kujengwa zilipobomolewa Nyumba nyingine na yenyewe ikabomolewa.
 
Kuna Mtu mmoja naye alikuwa anajenga Nyumba yake ilifikia hatua ya kupauwa ghafla akawa haonekani wala hapatikani kwenye Simu, mmoja wa mafundi wake ambaye ni Mzee akaweka Bati baadhi ya vyumba akahamia, bahati mbaya Nyumba yenyewe ilikuwa kwenye eneo ambalo halistahili kujengwa zilipobomolewa Nyumba nyingine na yenyewe ikabomolewa.
Duuuh
 
Wakuu Habari zenu.
Kuna jirani yangu huu mwaka wa 12 haonekani na namba yake ikawa haipatikani mpaka Sasa ukipiga amepewa mtu mwingine kabisa. Sijui nini kimemkuta ila Kwa asilimia kubwa atakuwa amefariki.

Kipindi nahamia kwangu, alikuwa hajaanza ujenzi na baada ya mda akaanza ujenzi wa Bangaloo lake, alikuwa na uwezo na alijenga jumba la kifahari haswa na mafundi aliotumia aliniomba nimuunganishe wale walionijengea.

Nyumba ikiwa hatua za mwisho hii ilikuwa October 2012 jamaa akapotea, simu ikawa hazipokelewi baada ya mda hapatikani kabisa, Hakuna mtu anaejua alikuwa anakaa wapi, site tulizoea kumuona akiwa mwenyewe.

Na viwanja vilikuwa Bado havijapimwa kipindi hicho, hata Ardhi hamna detail zake.

Nyumba yenye thamani ya zaidi ya Tsh 300m inapotea pasipo ndugu kujua.

Kuna mwingine ni mwanajeshi mstaafu alinunua bonge la pori Goba - Dsm kipindi Cha zamani, Hakushirikisha familia japokuwa alikuwa na mke na watoto wakubwa sana.

Alimuachia mamlaka yote ya uangalizi wa eneo balozi wa ule mtaa, Mwaka Juzi alianza kuuza lile eneo lake baada ya kulipima, Kipindi hicho alikuwa anaumwa Yuko Nairobi, mimi nilipelekwa na Dalali nikiwa natafuta kiwanja. Unapitia Kwa Balozi unaongea akiwa Nairobi anakupa Account unalipa mnaandikisha na Balozi Kwa niaba yake, Yule Mzee sijui Nini kilimkuta alikuwa anauza viwanja Kwa bei ya chini sana sqm moja Kwa Goba alikuwa anauza Tsh 45,000/=

Nilinunua baadhi ya viwanja pale, na Bado ananidai 30m

Mwaka huu tumepata taarifa kafa nashindwa kuitafuta familia yake kuwaambia kwamba baba yao anaidai maana wanaweza kuanziaha mgogoro, Japo mke wake yupo na watoto wake.

Tulinunua maeneo Yale wote tulishabadilishq umiliki

Alikuwa na bonge la eneo hekari 10 zinafika, mjumbe kafaidi huku mke na watoto hawajui Chochote.

Wakuu tunapofanya maendeleo tujitahidi familia zijue hata kama Kuna ugomvi kiasi gani, basi kama sio mkeo Tafuta ndugu mnaoelewana waoneshe, Hatujui kesho yetu, Kuna Vifo vya ghafla.

Huyu Kwa asilimia kubwa atakuwa kashakufa. Nyumba nimebaki naipalilia Mimi Kwa sababu ni Jirani yangu ili isiwe sehemu ya kutumza wadudu. Raia wanajua ni yangu

Manzile:

Rafiki yangu alifiwa na baba yake, wakiwa msibani alitokea mzee mmoja aliyejitambulisha ni rafiki ya marehemu, alimwambia jamaa yangu ( ambaye ndiye alikuwa kaka mkubwa ) baada ya mambo ya msiba kumalizika waonane.

Baada ya msiba alipokwenda kumuona alimchukua mpaka Goba, na kumuonyesha eneo kubwa tu, na kumwambia jamaa yangu, kuwa Marehemu alimwomba amnunulie miaka mingi, lakini kila akimwambia afanye kitu alikuwa anasema subiri, Mzee huyo alitoa nyaraka zote na kumkabidhi jamaa yangu.

Kwa kifupi wanafamilia hawakuwa na rekodi yoyote ya shamba hilo katika mali za marehemu,, watoto waligawana, na pia kumjengea mama yao katika shamba hilo. Watoto na mke wa marehemu walikuwa hawajui chochote! Ni wema tu wa huyo Mzee kuirudisha mali kwa wahusika!

Hivyo mambo haya yapo!
 
Ukiona mtu kafanya jambo kwa siri ujue si kwa kupenda bali imemlazimu kufanya. Kwa familia nyingine ni bora waone matokeo kuliko mchakato wenyewe.
Inawezekanaje familia ikawa na chuki Kufikia kiwango hicho?
 
Wakuu Habari zenu.
Kuna jirani yangu huu mwaka wa 12 haonekani na namba yake ikawa haipatikani mpaka Sasa ukipiga amepewa mtu mwingine kabisa. Sijui nini kimemkuta ila Kwa asilimia kubwa atakuwa amefariki.

Kipindi nahamia kwangu, alikuwa hajaanza ujenzi na baada ya mda akaanza ujenzi wa Bangaloo lake, alikuwa na uwezo na alijenga jumba la kifahari haswa na mafundi aliotumia aliniomba nimuunganishe wale walionijengea.

Nyumba ikiwa hatua za mwisho hii ilikuwa October 2012 jamaa akapotea, simu ikawa hazipokelewi baada ya mda hapatikani kabisa, Hakuna mtu anaejua alikuwa anakaa wapi, site tulizoea kumuona akiwa mwenyewe.

Na viwanja vilikuwa Bado havijapimwa kipindi hicho, hata Ardhi hamna detail zake.

Nyumba yenye thamani ya zaidi ya Tsh 300m inapotea pasipo ndugu kujua.

Kuna mwingine ni mwanajeshi mstaafu alinunua bonge la pori Goba - Dsm kipindi Cha zamani, Hakushirikisha familia japokuwa alikuwa na mke na watoto wakubwa sana.

Alimuachia mamlaka yote ya uangalizi wa eneo balozi wa ule mtaa, Mwaka Juzi alianza kuuza lile eneo lake baada ya kulipima, Kipindi hicho alikuwa anaumwa Yuko Nairobi, mimi nilipelekwa na Dalali nikiwa natafuta kiwanja. Unapitia Kwa Balozi unaongea akiwa Nairobi anakupa Account unalipa mnaandikisha na Balozi Kwa niaba yake, Yule Mzee sijui Nini kilimkuta alikuwa anauza viwanja Kwa bei ya chini sana sqm moja Kwa Goba alikuwa anauza Tsh 45,000/=

Nilinunua baadhi ya viwanja pale, na Bado ananidai 30m

Mwaka huu tumepata taarifa kafa nashindwa kuitafuta familia yake kuwaambia kwamba baba yao anaidai maana wanaweza kuanziaha mgogoro, Japo mke wake yupo na watoto wake.

Tulinunua maeneo Yale wote tulishabadilishq umiliki

Alikuwa na bonge la eneo hekari 10 zinafika, mjumbe kafaidi huku mke na watoto hawajui Chochote.

Wakuu tunapofanya maendeleo tujitahidi familia zijue hata kama Kuna ugomvi kiasi gani, basi kama sio mkeo Tafuta ndugu mnaoelewana waoneshe, Hatujui kesho yetu, Kuna Vifo vya ghafla.

Huyu Kwa asilimia kubwa atakuwa kashakufa. Nyumba nimebaki naipalilia Mimi Kwa sababu ni Jirani yangu ili isiwe sehemu ya kutumza wadudu. Raia wanajua ni yangu
Mkuu Mungu akubariki, ebu pambana pitia maelekezo ya mdau ya kufatilia no yake ,wenda alishakufa ,na ameacha familia ipo inaangaika ,unaweza saidia sana
 
Sijui Kwa Nini watu wanakuwa na ujinga wa namna hii
Sio ujinga,unao mke unampenda vizuri unakuletea watoto sio wako.unakuta huko ndugu nao walikukataa ulikuwa mtoto haramu.
Mambo ni mengi hii dunia,kama hayajakukuta shukuru.
 
Back
Top Bottom