Mnatizama lakini CNN Mahojiano ya moja kwa moja ya Mgombea Urais wa Marekani Trump na Waandishi wa Habari Weusi huko Chicago?

Mnatizama lakini CNN Mahojiano ya moja kwa moja ya Mgombea Urais wa Marekani Trump na Waandishi wa Habari Weusi huko Chicago?

..Trump ni mhuni tu ambaye amefanikiwa kuwapumbaza Wamarekani weupe wabaguzi.

..Marekani baada ya kumchagua Obama ilikuwa inaondoka ktk chuki za ubaguzi lakini Trump ameingia na kuirudisha nyuma Marekani.

..pia Trump ni muongo kwa kuendelea kudai kwamba aliibiwa uchaguzi iliyopita.

..Madai ya Trump kuwa aliibiwa uchaguzi yamekanushwa hata na aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wake.

..Marekani inahitaji kiongozi atakaye waunganisha wananchi wake wote, bila kujali rangi zao. Badala ya Trump anayechochea ubaguzi baina ya Wamarekani.
So upo upande wa upinde
 
Marekani haitaongozwa na Mwanamke kamwe.

Na huu ndo ukweli. Trump anashinda asubuhi misa ya kwanza. Kiukweli Trump alivoingia madarakani watu weusi wengi walipata ajira na kuna wasanii weusi walitolea jela kwa nguvu yake hilo hawalisemi.

Huyu bibi anataka kurudisha habari ya kutoa mimba iwe normal ilhali trump hakubali,

Huyu bibi anataka kufanya ushoga uwe normal zaidi ilhali trump anakataa kiaina.

Mwanamke hapaswi kuongoza nchi.
 
..Donald Trump na watu wake walichallenge matokeo ktk vyombo husika na madai yao yalitupiliwa mbali.

..hata aliyekuwa Mwanasheria Mkuu ktk serikali ya Donald Trump amesisitiza mara kadhaa kwamba madai kuwa Trump aliibiwa uchaguzi sio ya kweli.

..pamoja na ukweli huo bado Trump aliwashawishi wafuasi wake wakafanye fujo ili bunge la Marekani lisithibitishe matokeo ya ushindi wa Joe Biden.

..mpaka hapo utaona kwamba Donald Trump ni mwanasiasa muongo na mchochezi.

..Kuhusu UTAPELI wa Donald Trump naomba nikukumbushe kuhusu mradi wake wa " Trump University . "

..Je, unakumbuka nini kilitokea kwa wananchi wa kawaida waliojiunga na Trump University?

..Unakumbuka Senator Marco Rubio alisema nini kuhusu Donald Trump na hiyo " university "?

..Wamarekani walikuwa disappointed na political class na walitaka mabadiliko. Tatizo waliyatafuta mabadiliko kwa Donald Trump mtu ambaye hakuwa sahihi. Wamarekani walikuwa too disappointed na viongozi wao / wanasiasa kiasi kwamba walikuwa tayari kufumbia macho mapungufu ya kimaadili ya Donald Trump.

..Sikiliza hapa chini. Donald Trump ni tapeli. Ni bahati mbaya na aibu kwamba alichaguliwa kuwa Raisi. Wakati mwingine wapigakura hufanya MAKOSA.

View: https://m.youtube.com/watch?v=K00ZFy7XM2Q&pp=ygUeTWFyY28gUnViaW8gKyBUcnVtcCBVbml2ZXJzaXR5

Mimi sio shabiki wa Trump lakini mainstream media ndo ina mportray vibaya kwa makusudi. Uchaguzi wa Marekani 2020 ulikuwa na kila dalili za kuibiwa na sidhani kama ni mara yao ya kwanza USA kufanya hivyo.

Statistically, Trump amekuwa rais bora kwa blacks kuliko huo ubaguzi alionao kama kweli anao.
 
Hata huku kwetu viongozi wa upinzani huws na madai ya kuibiwa kura,madai hayo yanabaki ni maoni yao binafsi hasa yanapokuwa hayana uthibitisho na wala madai hayo hayatupi sisi concludion ya kwamba watu hao ni wabaguzi.

Madai yake hayo hayana mahusiano na ubaguzi unaoudai.

Waliompa kura akawa raisi hawakuona utapeli huo mpaka wampe kura na wewe ndio huo utapeli umeuona kuliko waliompa kura?

KWA NINI walimpa kura akawa raisi wakati wanajua ni tapeli ?

Je utapeli huo aliwatapeli watu weusi pekee hawakuwepo wazungu ?

Kuna mahusiano gani kati ya utapeli na ubaguzi ?

Kwa nini skawa raisi wa marekani licha ya utapeli huo,au wamarekani hawamjui badala yake wewe ndo unamjua zaidi trump ?
Umemjibu vyema!
Atuambie yeye mbona wanawachagua mafisadi na wanajua ?
 
..Trump ni mhuni tu ambaye amefanikiwa kuwapumbaza Wamarekani weupe wabaguzi.

..Marekani baada ya kumchagua Obama ilikuwa inaondoka ktk chuki za ubaguzi lakini Trump ameingia na kuirudisha nyuma Marekani.

..pia Trump ni muongo kwa kuendelea kudai kwamba aliibiwa uchaguzi iliyopita.

..Madai ya Trump kuwa aliibiwa uchaguzi yamekanushwa hata na aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wake.

..Marekani inahitaji kiongozi atakaye waunganisha wananchi wake wote, bila kujali rangi zao. Badala ya Trump anayechochea ubaguzi baina ya Wamarekani.
Wewe unamzungumzia Trump kwa kutumia slides za Democrats.

Mtafute Trump mwingine.

Hawa Democrats miaka na miaka wanatumia tu watu weusi, hawajawahi kuwa msaada kwa Waafrika. Hata Africa, Republican ndio walianza miradi mikubwa kama PEPFAR. Mpaka leo tunadunda na VVU.
 
Bado ni hoja za kitoto sana.

Mimi nimemsikiliza trump kwenye clip zake kibao ni mtu ana madini sana.

Kuwaponda watu weusi haujaweka ushahidi wa kutosha bali unadokoa tu.

Lakini pia kuita Afrika shit hole kama alikuwa na hoja za msingi yuko sahihi kabisa na mimi nitamuunga mkono hoja muhimu tu usimlishe maneno.

Bado sijaona hoja za msingi za kumuita trump mbaguzi maana hausemi.
Humu wanawadanganya na kuwapata wale wavivu wa kusikiliza, kufuatilia,na wanaosikiliza habari za vijiweni
 
Mimi sio shabiki wa Trump lakini mainstream media ndo ina mportray vibaya kwa makusudi. Uchaguzi wa Marekani 2020 ulikuwa na kila dalili za kuibiwa na sidhani kama ni mara yao ya kwanza USA kufanya hivyo.

Statistically, Trump amekuwa rais bora kwa blacks kuliko huo ubaguzi alionao kama kweli anao.
..Trump na genge lake wameshindwa kuthibitisha mahakamani kwamba aliibiwa.

..Trump alishindwa kwa idadi ya kura.

..pia alishindwa ktk electoral college votes [ kura zinazotokana na uzito wa majimbo.]

..kuna vyombo vyenye mlengo wa Republican na vingine ni vya mlengo wa Democrats.
 
..Trump angekuwa sio mbaguzi angefanya mojawapo kati ya haya.

1. Angechagua VP mwanamke.

2. Angechagua VP mwenye asili ya Kilatino.

3. Angechagua VP mmarekani mweusi.

..Ticket ya Uraisi wa Marekani inatakiwa itume ujumbe wa kuwaunganisha Wamarekani, na sio ujumbe kwamba Marekani ni nchi ya wanaume weupe wenye chuki na wabaguzi.
Unataka Marekani Iongozwe Kike Kike
 
Umenifanya niangalie mwanzo wa hii interview, mbona sijaona mahali Trump amezingua? In fact huyu mdada wa kwanza ndo anazingua hajibu salamu na anauliza in a very harsh way but Trump being Trump he gave her what she deserved.
Fuatilia Analysis zote za Wachambuzi wakubwa waliokuwa Wakihojiwa na CNN na BBC wote wamemlaumu Trump kwa Majibu yake hasa aliposema yule Mwandishi Dada anauliza Nasty Questions na wameendelea kusema kuwa Trump hakujiandaa kwa yale Mahojiano na kwamba bado ameendelea tu kuwa na Lugha za Kuudhi dhidi ya Jamii ya Weusi huko Marekani.
 
Wewe unamzungumzia Trump kwa kutumia slides za Democrats.

Mtafute Trump mwingine.

Hawa Democrats miaka na miaka wanatumia tu watu weusi, hawajawahi kuwa msaada kwa Waafrika. Hata Africa, Republican ndio walianza miradi mikubwa kama PEPFAR. Mpaka leo tunadunda na VVU.

..sijatumia " slides " za Democrats.

..kwa mfano niliposema Trump alikuwa mfanyabiashara tapeli nimenukuu Republicans wenzake.

..Trump ni lijizi, na tapeli, isipokuwa lina bahati kuwakuta Republicans wamechoshwa na viongozi wao.


View: https://m.youtube.com/watch?v=CR0k5xdUxBs
 
Wewe hiyo version yako ya Trump umeitoa wapi?

Acha hayo mahaba.

Eti “Trump yupi”
Kwa hiyo unashauri vipi? Tuanze kumponda na kukubali kumezeshwa mauingo bila kuyakataa ? Nikutakie Kila la kheri kwenye kumezeshwa
 
Back
Top Bottom