Katibu Mkuu wa CHADEMA anazungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mchakato wa wabunge wa Viti Maalum ambao wameapisha siku ya jana tarehe Novemba 24, 2020.
Tumewaita kuwaeleza kwamba CHADEMA hakijateua wabunge wa viti maalum wala hakijawasilisha orodha yoyote Tume ya Uchaguzi ya uteuzi wa wabunge wa viti maalum
Mimi kama Katibu Mkuu wa Chama sikuwahi kujaza fomu yoyote, kumthibitisha mtu yeyote mahali popote, kilichofanyika ni biashara haramu ya kugushi iliyohusisha mfumo wa kiserikali.
Mawasiliano yangu ya mwisho na Tume ya Uchaguzi zilikuwa ni barua 2, Nov 9 , niliiandika baada ya Mkurugenzi wa NEC kunukuliwa na vyombo vya habari kwamba
CHADEMA imewasilisha orodha ya wabunge wa viti maalum na yeye amekwishaipeleka bungen
Kwa katiba ya
CHADEMA mamlaka ya uteuzi wa wabunge yako kwa kamati kuu ya chama, na kamati kuu ya chama haijawahi kufanya kikao cha uteuzi wa majina ya wabunge wa viti maalum na mimi Katibu Mkuu sijawahi kuwasilisha orodha yoyote
Katibu Mkuu, John Mnyika amewataka wabunge wote walioapishwa kuwa wabunge wa Viti Maalum kufika kwenye ofisi za Makao Makuu ya Chama siku ya Novemba 27, saa mbili asubuhi bila kukosa kwa ajili ya utaratibu mwingine.
Mwanachama wetu aliyekuwa na kesi ya jinai ya kubambikiwa kwa muda mrefu Nusrat Hanje alitolewa gerezani tarehe 23 Novemba na mfumo ili watimize adhma yao.
Katibu Mkuu amesema kwamba wabunge wote walioapishwa Novemba 24 wamewekwa na mfumo na hawana baraka za chama cha Demokrasia na Maendeleo.
Kauli iliyotolewa jana na kumhusisha Mwenyekiti, Freeman Mbowe haina ukweli. Mbowe ataongoza kamati kuu na itawasikiliza wahusika. Kati ya walioapishwa kuna wajumbe wa kamati kuu wanafahamu uteuzi haukufanyika na wanajua wameshiriki biashara haramu