Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni: Katika Mgomo wa wafanyabiashara, kosa la Mwigulu Nchemba ni lipi?

Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni: Katika Mgomo wa wafanyabiashara, kosa la Mwigulu Nchemba ni lipi?

Wakuu Salam,

Naomba nitangaze maslah, mimi ni mfanyabiashara, nipo Kariakoo, nje ya kariakoo na mkoa wa Pwani.

Malalamiko yetu wafanyabiashara mengi ni justifiable.. lakini hili la kumlaumu Mwigulu Nchemba bila supporting evidence is ungrounded.

Kuna watu wanatumia udhaifu wa migogoro ya sheria zilizopo kumgandamiza bila sababu.

Mfano.

1. Hoja ya fine ya kutokutoa EFD recept sio ya leo, na hii ilipingwa sana na aliekuwa mbunge wa Muleba Anna Tibaijuka, nilishangaa saana yale mapendekezo, kama kawaida ya bunge letu.. papatu papatu hoja ikapita ikawa sheria, Kipindi hicho Mwigulu ni Wazir wa mambo ya ndani.

2. Hoja ya ushuru wa malori, Ndugu Chuki anaweza kuwa ana issues personal na Mwigulu na siwez kuwaingilia , ila kodi ya 2.7M sio kubwa kama anavyodai, kumbuka kubeba tonneau 10 had mwanza ni zaid ya 1.5M na hiyo ni non negotiable.... kutaka hiyo gharama iingizwe kwenye diesel ni ku shift tax burden to non beneficiaries, ambayo ni unfair taxing.

3. Hoja za registration of warehouse sio kitu kipya na wengi tumesajili nikiwemo, hoja za umiliki ni jambo jingine, labda tuseme issue ya With holding Tax ndio haijakaa Sawa, lakini kulalamika kwamba tusisajili sio Sawa kabisa.
Kwenye ethical business ni lazima usajili store na ulipie usimamiz wake, ikiwa na vigezo vyote.... hii ni excuse ambayo kumlaumu nayo Mwigulu ni ku choose easy victim.

4. Hoja za task force zilikuwepo toka kipind cha mwendazake... kwamba tunasumbuliwa hili ni kweli na ni sualq la kuweka utaratibu tu wa namna ya ku control, ambayo sikuona sabab ya kumzodoa mwamba vile.

5.Utitiri wa kodi kwenye biashara na mamlaka nyingi zinazosimamia jambo moja ni suala la kurith na Mwigulu sidhan kama ni wa kulaumiwa 100% , issue hapo ni CCM kuweka na kuunda hizi taasisi kutafutia washkaj wao ulaji.
Kuna kila sabab ya kuunganisha taasisi nyingi sana ili kuondoa usumbufu.

Ni hayo tu... tumuhukumu Mwigulu kwa mengine lakini sio moja kwa moja kwa baadhi ya sheria ambazo amezikuta.
Kama hujajua basi wewe ni moja wa tatizo
 
Huwezi kuwa mfanyabiashara ukaja kumtetea Mwigulu..
Mfumo WA Kodi WA kukadiria unaotoa mwanya Kwa watu wa TRA sio fair..
Mtu anakdiriwa Kodi milioni 350 wakati Kenya Kodi milioni 45 Kwa kontena Hilo Hilo...yote hayo ni policy..na usimamizi na Mwigulu ndo mhusika wa kubadilisha vyote...na kashauriwa kagoma ....

Wewe labda kakutuma uje umsafishe
 
Huwezi kuwa mfanyabiashara ukaja kumtetea Mwigulu..
Mfumo WA Kodi WA kukadiria unaotoa mwanya Kwa watu wa TRA sio fair..
Mtu anakdiriwa Kodi milioni 350 wakati Kenya Kodi milioni 45 Kwa kontena Hilo Hilo...yote hayo ni policy..na usimamizi na Mwigulu ndo mhusika wa kubadilisha vyote...na kashauriwa kagoma ....

Wewe labda kakutuma uje umsafishe
Sasa ni Mwigulu kaleta Hilo? Hizo Sheria zinafungwa na Wataalamu wa uchumi na Kodi na zinapelekwa Baraza la Mawaziri kisha Bungeni,huko Bungeni Kuna wafanyabiashara Sasa kama ni mbaya Kwa nini wasizikatae?
 
Hayo madudu yanamtaka Waziri ashughulikiwe? Hayo si ni mambo ya Polisi,Kamishna wa TRA na Viongozi wa Mkoa?
Mwigulu/Waziri ni mtu wa sera sio mtu wa oparesheni..

Yeye kama waziri angeweza kufix mapema kabisa bila kufikia kwenye mgomo

Na Leo pm ameamua Tu kuficha aibu Yao ndio maana hakuwapa nafasi ya kuongea
 
Ila nimependa wamemnanga sana kwa maneno ya kejeli maana yeye huwa anajidai bingwa wa maneno ya kukararisha.

Kuna mwamba anasema,unajitia Dokta,Dokta wa wapi wewe[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kwamba mapolisi wanavyokula Rushwa IGP ajiuzulu na akijiuzulu ndio polisi wataacha kula Rushwa?

Hakuna kosa la Waziri hapo Kuna chuki binafsi Zenye mlengo wa kisaiasa na hapo unaweza Kuta wameshindana huko kwenye biashara.
 
Chawa kazini hivi haujaoana malalamiko ya wafanyabiashara kwamba walikuwa wanakutana naye kwenye vikao na akitoka anaenda kufanya tofauti na walivyoongea
Au hajasikia wafanyabiashara wanavyomnanga
Wanasema wakilalamika anamwambia sijadiliani na waganga wa kienyeji[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]


Sema wafanyabiashara wamejua kumchamba jamaa bila kupepesa macho.
 
Yeye kama waziri angeweza kufix mapema kabisa bila kufikia kwenye mgomo

Na Leo pm ameamua Tu kuficha aibu Yao ndio maana hakuwapa nafasi ya kuongea
Lini walienda Kwa Waziri ikashindikana? Au Kuna sehemu wamesema waliomba appointments Kwa Waziri akakataa?
Kabla ya kwenda Kwa Waziri anatakiwa.kushughulikia malalamiko ya kijinai ni Mkuu wa Mkoa na vyombo vyake, Waziri anashighulika na maswala ya kisera sio operation za watekelezaji wa sera.
 
Ila nimependa wamemnanga sana kwa maneno ya kejeli maana yeye huwa anajidai bingwa wa maneno ya kukararisha.

Kuna mwamba anasema,unajitia Dokta,Dokta wa wapi wewe[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Na hii ndio inamfanyq watu wamchukie personally.. hadi kumbandika vitu😂
 
Back
Top Bottom