Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni: Katika Mgomo wa wafanyabiashara, kosa la Mwigulu Nchemba ni lipi?

Hili suala lina kero za kweli na mambo ya ujanja janja na hisia pia.
Ngoja nijipe ujasiri wa kujazia kwenye mabano:

"Kero za kweli" - sheria mbovu zinazoruhusu mianya ya rushwa

"Mambo ya ujanja ujanja" - wafanya biashara kutumia mianya ya ubovu wa sheria hizo hizo mbovu kutolipa kodi stahiki

"hisia" - serikali (akina Mwigulu, hadi akina Samia), na hao wafanya biashara wenyewe, hakuna malaika hapa.
 
Umesema kubeba tani 4 mpaka 10 to mwanza ni sh ngapi tena?
 
Ukikuta madudu wizarani hurekebishi?
 
Wewe ni mwenye chuki sana sema upendi mabosi wako wafanyiwe chuki.
 
Au hajasikia wafanyabiashara wanavyomnanga
Wanasema wakilalamika anamwambia sijadiliani na waganga wa kienyeji[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]


Sema wafanyabiashara wamejua kumchamba jamaa bila kupepesa macho.
Ebu shangaa vyote hajaviona mwigulu hasafishiki
 
Mwigulu ndio waziri mwenye dhamana, hivyo hakuna namna atakwepa lawama hizi.
Kwanza angekua muadilifu na kulinda heshma ndogo aliyo baki nayo, alipaswa awe amejiuzulu.
Madudu mangap yanafanyika nchi hii? Umeshawahi kuona wahusika wamejiuzulu? Au mnataka mwigulu awe wa kwanza kujiuzulu?
 
Ebu shangaa vyote hajaviona mwigulu hasafishiki
Mkuu, tatizo siyo Mwigulu. Ila ni mifumo na sheria. Sheria nyingi za kodi zinapaswa zikarekebishwe bungeni.
Tuache chuki binafsi kwa mwigulu.tuwalaumu wabunge wetu walio pitisha hizi kodi kandamizi.
 
huna duka kkoo labda kigoli
 
Sasa ni Mwigulu kaleta Hilo? Hizo Sheria zinafungwa na Wataalamu wa uchumi na Kodi na zinapelekwa Baraza la Mawaziri kisha Bungeni,huko Bungeni Kuna wafanyabiashara Sasa kama ni mbaya Kwa nini wasizikatae?
Kwani wakati wa utawala wa Nyerere , Mzee Mwinyi akiwa waziri wa Mambo ya ndani kwanini alijiudhuru Kwa kosa la police kuuwa raia ? . Kwani ni Mzee Mwinyi ndo alishika mjegeje na kuwapiga raia ?
Madudu yametokea kwenye mipaka ya utawala wako , uungwana ni kuwajibika .
 
Sawa ,nikuulize wewe ni Waziri wa Fedha na umebobea kwenye mazingira au Utawala, Ushauri gani wa kitaalamu wa Kodi na Uchumi unaweza kutoa? Sidhani kama hiyo ndio Kasi ya Waziri hata kama kasomea Uchumi ila sio msomi sheria za Kodi nk..

Swala.la.kodi.kubwa au ndogo nimewahi msikia Waziri Mwigulu akisema Bungeni kwamba angeoenda hizo kudi ziwe hata 8% lakini Kwa uchumi Wetu wa Sasa hauruhusu Hilo na sababu ni nyingi
-Tuna mahitaji makubwa vs vyanzao
-Tuna mianya Mingi ya ukwepaji Kodi na Serikali inapambana nayo,
-TRA Ina upungufu mkubwa wa staff kuweza kuwafikia watu wote.
-Wafanyabiashara wengi hawatunzi taarifa za biashara zao kitaalamu kama kampuni hivyo kuwa na Changamoto kubwa za ukadikiaji ,
-Wananchi hawana utamaduni wa kulipa Kodi achilia mbali wafanyabiashara Kwa hiyo Ili kufidia lazima kuwe na Kodi kubwa na za aina mbalimbali..

Mwisho,nikuulize wewe bwana hivi Rais akikupa uwe Waziri wa Fedha utaweza ku meet matakwa ya kibajeti Kwa mbinu zipi? Ziweke hapa Ili tuone kama kweli Mwigulu amefeli na wewe unaweza kufaulu..

Katika kundi siwezi kulitetea ni wafanyabiashara Kwa sababu nafahamu kwamba Huwa wanakwepa Kodi na hata Mimi nakwepa Kodi kwenye biashara yangu ,huu ndio ukweli lakini sababu ni hizo hizo kwamba Kuna utitiri wa Kodi na tozo ambazo sio tuu ni za TRA Bali ni za mataasisi mengine isipokuwa VAT ya TRA ni kubwa zaidi so hata iwe bei ndogo Huwa nakwepa.
 
Alikurupuka tuu na ndio maana Bado Rushwa Polisi wanakula na wanaua.raia nk so dawa sio kujiudhuru ila kutatua shina.la mzizi.
 
Kama wewe ni mfanyabiashara Kariakoo, je ulishiriki vikao na wenzako? Je kwanini hukuyasema huko vikaoni?
 
Mkuu haya mambo nakuelewa sana, hoja yangu hapa ni kwamba Mwigulu amekosea nini?
Tumelia na haya masheria mabovu kwa miaka hata kabla ya Mwigulu, leo nashangqq kishabiki kabisa anabebeshwa zigo lote.
Lazima abebeshwe kwasababu yeye ndiye waziri mwenye dhamana.Amekuta madudu kwenye wizara yake anatakiwa kuyafanyia kazi sio kuyakwepa kwakigezo cha sikuwepo.Kama huo ndio utetezi wake apishe ofisi.
 
Utakuwa mchepuko wake Mwigulu. Huwezi ona kosa lake. Naona mnajaribu sana kupapatika....
 
Nchemba ndio maana alifukuzwa na Mzee kumleta harafu kumpa sehemu muhimu ni kosa sana hakuna mtu pale yeye ndio chanzo cha matatizo yote haya sijui Mama anataka watu wafanyeje ndio atatuelewa..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…