Mo Boxing: Ibrahim Class ashinda kwa KO dhidi ya Bondia wa Mexico

Mo Boxing: Ibrahim Class ashinda kwa KO dhidi ya Bondia wa Mexico

Hivi huyu Nyembela mnamuelewa kweli utangazaji wake
Mbona yupo biased sana
Huyu si mtangazaji wa ngumi bali ni mshabiki wa ngumi, hawezi na hata wachambuzi wao hakuna kitu ujuaji mwingi lakini kwa ndani hapa, mchambuzi wa ngumi namkubali ni mmoja tu na sikuhizi simsikii kabisa, yule kijana ' Jimmy Kabwe ' yule huwa hana upande yaani akichambua ngumi unasema huyu anaijua kazi yake na si hawa wachambuzi mandazi.

Rudi lile pambano la Mtwara kauli zao dhidi ya Refer, yaani wao wanajiona ndio wajuzi kuliko na maneno yao ndio sahihi
 
Pamoja na kwamba ameshida lakinì watanzania tumeonyesha inhuman behaviour. Hata kama ni mchezo ,mwenzako anapopata bahati mbaya ya kuumia mchezoni huwezi kushangilia ni jambo la kuanngalia usalama wake. Sasa naona bondia na wapambe wake wamevamia jukwaa wanashangilia bila kujua hali ya mpinzani anayepatiwa matibabu
Kwakweli, nimewaambia wanangu wasije kamwe wakacheza huu mchezo
 
Ibrahim Classic alivyompiga ngumi nzito mwenzake aliyekuwa amepiga magoti huku sura ipo wazi, mikono ipo chini, alikuwa anadhamiria kufanya nini?
Nadhani alikuwa anadhamilia amuue labda,huu mchezo haufai kabisa kabisa
 
Ibrahim Classic alivyompiga ngumi nzito mwenzake aliyekuwa amepiga magoti huku sura ipo wazi, mikono ipo chini, alikuwa anadhamiria kufanya nini?
No upumbafu Sana kafanya pendo njau amekozea Sana ktk pambano Hilo mtu kaweka mikono Chini na kapiga magoti ww unamrukia na kumpiga upper cut mpuuz Sana kijana yule kaniudhi mno mbna Ni was alikuwa kashinda ,Sasa nasikia kijana watu kakata kauli sijui itakuwaje tutafungiwa na shirikisho la ngumi na hili wageni hawatakuja Tena kupambana huku

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Hivi huyu Nyembela mnamuelewa kweli utangazaji wake
Mbona yupo biased sana
Yaani kama hajui anapoteza kabisa radha ya mapambano. Afu Azam wanamwona bonge la mtangazaji wa ngumi
 
Yaani kama hajui anapoteza kabisa radha ya mapambano. Afu Azam wanamwona bonge la mtangazaji wa ngumi
Azam kwa watangazaji hawajajipanga kbs. Ngoda mara ngumi mara mpira wa miguu. Huyo Nyembela kwanza sio mtu wa habari sema Regina Mengi aliimuokoa baada ya mpira wa kikapu kumtupa mkono ndio akamchomeka EastAfrika Tv. Utafurahi na roho yako waanze kuhoji kwa kidhungu ndio utajua kwanini kazi ya Uandishi wa habari wamejaa viazi. Wanawaharibia akina Paskali Mayala.
 
hiyo ni bonus, mkwanja wake upo kwenye mkataba. Acheni upuuzi
hao wengine walioshinda
wamepewa bonus gani ?
Ingekiwa busara hiyo zawadi ya bajaj wewe umeiita bonus isingetangazwa hadharani angepewa kimya kimya
 
Nadhani industry yetu ya burudani bado haijawa na uwezo wa kuleta mabondia wa viwango vya juu.....nimewatazama hawa mabondia wa Mexico ni wa viwango vya kawaida sana.......sio kama wale ninaowaona kwenye mapambano makubwa.......
 
Ibrahim Classic alivyompiga ngumi nzito mwenzake aliyekuwa amepiga magoti huku sura ipo wazi, mikono ipo chini, alikuwa anadhamiria kufanya nini?
Hakutenda haki kwakweli,jamaa tayari alikuwa amepoteza fahamu na refa akamwambia Stop,ila yeye akaendelea kushusha makonde!
 
Mtu unapigwa kama mwizi. Michezo mingine hapana kwa kweli!
rampslam_xhriirbh.gif
 
Waamuzi wa ndondi Tanzania, wanakuwa nao ni sehemu ya ushabiķi, hivi mtu amepigwa mgumi anaonekana kabisa anaweweseka unaacha kuingilia kati hadi anapigwa ngumi nyingine wakati hajiwezi? Halafu unakuta ndio anasifiwa eti refa wa kimataifa. Kiwepo kipindi cha kuchambua maamuzi ya marefa wa ndondi kama kipyenga cha mwisho kwenye soka. Starehe yetu sio mtu kupigwa kimagumashi bali tunataka sheria zifuatwe anayeshinda ashinde anayeshindwa ashindwe
 
Back
Top Bottom