Mo Dewji azidisha utata wa kutekwa kwake baada ya mahojiano BBC

Mo Dewji azidisha utata wa kutekwa kwake baada ya mahojiano BBC

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Siku chache zillizopita, mfanyibiashara maarufu nchini Mo, alihojiwa kwa mara ya kwanza tokea kuachiliwa huru mwaka jana na chombo cha habari cha nje, shirika la utangazaji la BBC

Nilisikiliza kwa makini sana clip hiyo na ningependa maswali yafuatayo yajibiwe na viongozi wetu wa serikali

1. Siku ya kwanza baada ya kutekwa kwake, tulimuona Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda, akiongea na waandishi wa habari na kutueleza watanzania kuwa mfanyibiashara huyo ametekwa na watu wasiojulikana, lakini wakati huo huo akatueleza kuwa watekaji hao ni watu wa kutoka nje, ambao wanaongea lafudhi kama vile ya kizulu toka Afrika Kusini, je yeye alijuaje kuwa watu hao ni wageni, wakati uchunguzi wa Polisi ulikuwa haujakamilika??

2. Tulimsikia pia mfanyibiashara huyo Mo "akijaribu" kuunga mkono kauli hiyo ya mkuu wa mkoa wa Dar katika mahojiano yake na BBC. Hata hivyo alieleza kwenye clip hiyo kuwa watu hao walikuwa wanataka "lumpsum" na akaendelea kueleza kuwa watu hao waliweza kumuanganisha na mtu mwingine, ambaye hakuwepo kwenye hilo eneo alilokuwa ametekwa na waliongea kuhusu madai yao ya pesa, lakini akazidi kuongea kuwa mtu huyo wa nje, alimpa "option" ya kuweza kuongea kiswahili au kiingereza, hivi inawezekanaje kwa watekaji hao, ambao tuliambiwa kuwa ni wageni wasioweza kuongea hata kidogo kiswahili na kiingereza, waweze kumuunganisha na huyo mtu wa nje ambaye anaongea kiswahili na kiingereza??

3. Tuliambiwa kuwa watekaji hao waliweza kumtelekeza eneo la Ghymkana, bila kumdhuru na wala hawakupata madai yao ya fedha, ilikuwaje walimwacha akiwa hai, iwapo hawajitimiziwa kile walichokitaka??

4. Ilikuwaje watekaji hao wa kigeni waweze kumwachia mateka wao eneo la Gymkhana, ambalo ni la wazi sana, wakati security ya nchi ilikuwa katika kiwango cha juu sana cha tahadhari ya kiusalama??

5. Je kama watekaji hao walikuwa ni wa kutoka nchi za nje, waliwezaje kutoka hapa nchini, wakati nchi ilikuwa katika kiwango cha juu sana cha tahadhari ya usalama??

6 Kama kweli waliondoka hao watekaji "wageni" ilikuwaje kwa Rais wetu hakuwatumbua wateule wake wa vyombo vya usalama, kwa kuonyesha uzembe wa hali ya juu wa kuhakikisha usalama wa raia na Mali zao??

7. Hivi watanzania kutokana na "scenario" nzima hiyo tuki-conclude kuwa watekaji hao wali-collude na watu wa serikali, tutakuwa tumekosea kweli??

Tungependa kuwaeleza watawala wetu kuwa watanzania siyo wajinga kiasi hicho cha kudanganywa kadri mnavyotaka!
 
Hilo eneo la Gymkana lina camera za kiusalama. Hata Rais alionyesha mashaka jinsi tukio lilivyokuwa
Kasema aliachwa jirani na ofisi za EU siyo kule viwanjani......ndio akajikokota taratibu hadi hotelini ambako baba yake alienda kumchukua!
 
Kama mo mwenyewe kasema hayo wewe ni nani hata utake ya ziada?

Kama una la kuongezea nenda idara husika ya upelelezi kapeleke raarifa yako kwa njia ya maandishi
 
Kasema aliachwa jirani na ofisi za EU siyo kule viwanjani......ndio akajikokota taratibu hadi hotelini ambako baba yake alienda kumchukua!
Haya maeneo yooote yana ulinzi mkali wa kamera. Hilo tukio linaweza kutafutwa na kuangaliwa lilivyotokea. Ukiangalia kwa undani utaona ni kama "anagandamizia" au kuigilizia
 
Jaribu ku-imagine tuliambiwa kuwa watekaji hao ni wageni kutoka nchi za nje, hata hivyo "anayesota" na kesi ni mtanzania taxi driver wa Whitesands Hotel!
 
hata wakina Roma walipotekwa tuliambiwa watapatikana kabla ya jumapili hapa napo naona kuna mtu aliwajua watekaji kabla ripoti ya polisi haijatoka 🙄 🙄 🙄 🙄 🏃‍♂️ 🏃‍♂️ 🏃‍♂️ 🏃‍♂️ 🏃‍♂️
😀😀
Hahaaaaa.........
 
Bora angeendelea kuukaa tu kukaa kimya ! Hii inaweza kudhihirisha kuwa hawa watu hufanyiwa " mambo" ambayo huwafanya wasithubutu kusema ukweli maishani mwao tena!
Kama amekiri walimvua nguo zote je unadhani hawakumrekodi akiwa uchi? Je, hawakumfanyia " vitendo" vya kifedhuli vya kumnyamazisha milele?
Mo alikuwa ajiumauma mno kwenye yale mahojiano ya BBC!
 
Kuna sehemu alisema alikwenda kuiona hiyo nyumba alipokuwa kipindi kimetekwa ? Najiuliza hiyo nyumba ni ya nani ? Ipo wapi ? Kwa nini wasianze na mmiliki wa nyumba pia. Alikuwa kafungwa macho. Baadae alipokwenda kuona hiyo nyumba baada ya kuachiwa alijuaje ni hiyo nyumba alimokuwepo ?
 
Kuna sehemu alisema alikwenda kuiona hiyo nyumba alipokuwa kipindi kimetekwa ? Najiuliza hiyo nyumba ni ya nani ? Ipo wapi ? Kwa nini wasianze na mmiliki wa nyumba pia. Alikuwa kafungwa macho. Baadae alipokwenda kuona hiyo nyumba baada ya kuachiwa alijuaje ni hiyo nyumba alimokuwepo ?
Ndiyo uone namna wanavyochagua "location" ya kufanyia maigizo yao
 
Nilisha acha kumfuatilia Mo 7bu alishapewa masharti na watekaji tunawajua kwa kuongea kwao kwani walikua wanampa chakula anachotaka,wanampa hadi simu yenye kifurushi,gari pamoja na bunduki
Hawa watekaji wanahuruma sana hawakutaka mo apate tabu wala shida dhumuni ni kama walimteka ili wakae wamuone one tu huyo tajiri kijana
Ila kuna MTU alishasema anataka matajiri wataishi kama mashetani
 
Back
Top Bottom