Mohamed Dewji (MO) aliyepotea, apatikana. Amerudi nyumbani akiwa salama

Mohamed Dewji (MO) aliyepotea, apatikana. Amerudi nyumbani akiwa salama

hahaa tunashukuru Ubalozi wa Marekani kwa kuwakaalia kooni bila ya hivyo wasingemuachia kirahisi..eti ile gari alionyesha IGP Ziro ndio imetelekweza Gymkhana..Yaani watekaji wamerejesha gari na MO.
Narudia IQ za wanaopanga hizi sinema zipo chini sana

HAHAHAHA
MWANA MLAAAANIWA WALAHI
USA JAMAL KHASHOGGI YUKO KOONI, hana mpango na wewe imbecile uwiii!
Vijana wamatukio mmedoda walahi
 
Kama kweli jeshi la polisi limefanikisha upatikanaji wake basi wahalifu wafikishwe mahakamani au la tuaamini vyombo vya usalama vimeanza biashara ya utekaji na ransom.
Mjadala mwingine huu
 
Vizuri kabisa ndugu yetu huyu kupatikana, namshauri ahamishie biashara kwenye nchi zenye ubepari uliokomaa kama Kenya n.k
 
Huyu jamaa ilikuwa ni lazima arudi mzima, if anybody wanted him dead angeuawa awali ya yote na sio kutekwa...
 
Hii ilikuwa ni bonge moja la political liability kama asingerudishwa mtaani akiwa hai. Wamecheza karata zao vizuri!

Yawezekana ingekuwa na nguvu kuliko hata agenda ya ufisadi, maana sidhani kama kuna mtu mzima nchi hii asiyemjua Mo Dewji. Given dramas na sintofahamu zilizoonyeshwa na watendaji flani basi mzigo wote ilikuwa inabebeshwa SIRIKALI, and they would have payed for that in political wise spheres
 
We Mungu, we we siyo sisi! Utabaki kuwa Mungu! Asante kwa kumrudisha MO salama! Tunakuomba hata wengine waliopotea na hawajulikani walipo, tenda muujiza warudi! Na nguvu yako Mungu, iwapige upofu wa macho ya akili na ya mwilini wasiendelee kufanya uhalifu huu! Ameen!
 
'Risasi tulizookota tumepeleka maabara kwa Forensic experts wetu wakapima na venier calliper wakagundua ina unene wa milimita tisa, na bado tunaendelea kuishangaa!!' Kamanda Sifuri.
 
Hii inaonyesha familia wamelipa ransom!

Moja ya masharti ya ransom ni kutozungumza kuhusu tukio lote!

Kama atazungumza kuhusu yaliyomsibu mpaka akarudi basi hiyo itaonyesha kuwa hakulipa ransom na hakuna makubaliano.

Hoja iliyopo mbele yetu kwa sasa, Je, kama amelipa ransom, nini kwa sasa nafasi ya matajiri nchini kuhusiana na usalama wao kwa sababu kulipa ransom ni kufungua mlango wa biashara ya kidnapping and ransom nchini kwa matajiri.

Kosa la kulipa ransom baada ya kutekwa ambalo nchi za kusini mwa Afrika kama Afrika Kusini na Msumbiji walilianza kwa matajiri ndilo kwa sasa linazidi kuwatafuta kwa kasi zaidi.

Je, kuna uwezekano na Tanzania tukaelekea ambako nchi za kusini mwa Afrika ziliko kwenye biashara ya kidnapping and ransom?
Mkuu kwanza heshima yako.
Pili nisema thamani ya uhai wa mtu hailingani na kitu chochote hapa duniani. Hivyo itoshe tu kumshukuru mungu kwakua MO Kapatikana Akiwa hai bila kujali kipi walichokubalina na hao watekaji.

samahani kama nimekukwaza
 
Kama kweli jeshi la polisi limefanikisha upatikanaji wake basi wahalifu wafikishwe mahakamani au la tuaamini vyombo vya usalama vimeanza biashara ya utekaji na ransom.
Katupwa jirani kabisa na jiwe,kweli awamu hii akili hawana hata kutumia akili ndogo kudanganya wameshindwa
 
WAKUU
huo mstar wa mwisho anaosema 'Na shukuru mamlaka zote ikiwemo na jeshi la polisi kuhakikisha NARUDI salama' Mmeuelewa au mnarukaruka tu? Kuna ka ujumbe hapo,
 
Back
Top Bottom