Mohamed Said ''Mzungu wa Unga,'' 2007 Uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere

Mohamed Said ''Mzungu wa Unga,'' 2007 Uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere

Nanren,
Unakumbuka siku nilipokuhadithia historia ya babu yangu Salum Abdallah?

Nilikuambia uwe unafanya utafiti kabla ya kuandika.

Katika mkasa huu nakushauri urejee kukisoma kisa.

Walinikamata walinifahamisha, baada ya uchunguzi na kuridhika kuwa nauza unga.

Rudi kisome kisa upya.

Acha kupiga chenga.
Nirudi kusoma kisa kizima ili iweje?
Nimeijibu post yako kwa kui-quote. Tuendelee kuanzia hapo.
Isitoshe, si mara ya kwanza wewe kusimulia kisa hicho nimekisoma mara kadhaa.

Kama mwandishi aliyechoka, nafikiri kwa sasa umeishiwa cha kuandika. Unaandika yale yale kwenye threads tofauti. Utaongelea Habari za ibadan, na kukamatwa uwanja wa ndege, au utaanzisha thread ya Mwapachu au Kunambi au jina lolote lile, lakini hatimaye lengo ni ku-promote kitabu chako cha Sykes et al., na ku-promote chuki za kidini.

Nahisi hata wafuasi wako watakuwa wamekustukia, hawaji kwa kasi na matusi kama zamani au unaonaje kaka Moh'd?
 
Kama waislam wa Nigeria walisema ingekuwa sawa na kutangaza vita kwanini waislamu wa Tanzania msitangaze vita?
Tangazeni vita muuwe maadui zenu kwa Sababu hata uislamu unaruhusu kuua adui na ukiua adui unapata pepo.
Kuua adui wa waislamu ndio njia rahisi ya kupata pepo kwa mujibu wa uislamu.
 
kupewa kesi za kupandikizwa n kawaida sana hapa tz ila usihisishe kabisa na maswala ya kidini

tz hamana hayo mambo ya uislam au ukristo ndio kwanza nnasikia kwako
labda nchi kama marekani hayo mambo ndio yapo

usijaribu kupandikiza chuki za kidini kwa watu vita yake mbaya kuliko baa la njaa

narudia tena usipandikize chuki za kidini kwa watu ni mbaya kulikonunavyofikiri
MrOnline225,
Huijui historia ya Tanganyika.
Lakini nitakusaidia.

Msome Bergen (1981), Sivalon (1992) na
Njozi (2002).

Ukipenda msome Said (1998).

Ila kitabu cha Njozi kimepigwa marufuku
lakini kinapatikana mtandaoni.
 
Acha kupiga chenga.
Nirudi kusoma kisa kizima ili iweje?
Nimeijibu post yako kwa kui-quote. Tuendelee kuanzia hapo.
Isitoshe, si mara ya kwanza wewe kusimulia kisa hicho nimekisoma mara kadhaa.

Kama mwandishi aliyechoka, nafikiri kwa sasa umeishiwa cha kuandika. Unaandika yale yale kwenye threads tofauti. Utaongelea Habari za ibadan, na kukamatwa uwanja wa ndege, au utaanzisha thread ya Mwapachu au Kunambi au jina lolote lile, lakini hatimaye lengo ni ku-promote kitabu chako cha Sykes et al., na ku-promote chuki za kidini.

Nahisi hata wafuasi wako watakuwa wamekustukia, hawaji kwa kasi na matusi kama zamani au unaonaje kaka Moh'd?

Nanren,
Ikiwa hutaki kurudia kusoma sikulazimishi.

Kisa hiki kipo kwenye blog yangu toka 2008 na inapobidi huwa nakieleza kufatana na matokeo ya nyakati.

Labda huenda hujui.

Historia haina ukomo wa kusomwa kwani kila
siku wanakuja wasomaji wapya.

Kitabu changu kila aliyekisoma atamweleza mwenzake yale mapya aliyojifunza.

Kitabu cha Sykes hakina upungufu wa wasomaji wapya kwa hiyo hakinitaabishi.

Angalia uzi huu wamekuja watu gani?
Ninapoandika hata wewe unashindwa kujizuia.

Kama ni suala la mtu kusoma na kuchangia ni "ufuasi," hata wewe hujasalimika.
 
MrOnline225,
Huijui historia ya Tanganyika.
Lakini nitakusaidia.

Msome Bergen (1981), Sivalon (1992) na
Njozi (2002).

Ukipenda msome Said (1998).

Ila kitabu cha Njozi kimepigwa marufuku
lakini kinapatikana mtandaoni.
Mkuu samahani naweza kupata link ya hicho kitabu cha "Njozi"?
 
Kama waislam wa Nigeria walisema ingekuwa sawa na kutangaza vita kwanini waislamu wa Tanzania msitangaze vita?
Tangazeni vita muuwe maadui zenu kwa Sababu hata uislamu unaruhusu kuua adui na ukiua adui unapata pepo.
Kuua adui wa waislamu ndio njia rahisi ya kupata pepo kwa mujibu wa uislamu.
Kitulo,
Unaandika huku umekasirika.
Ghadhabu humfanya mtu akasema maneno akitulia anajuta.

Tufanye mjadala wa kisomi ili jamii inufaike na haya tunayoandika
kiasi miaka 100 baadae wakija watu kutosoma watasema hakika
wazee wale waliotangulia walikuwa watu makini.
 
Nanren,
Ikiwa hutaki kurudia kusoma sikulazimishi.

Kisa hiki kipo kwenye blog yangu toka 2008 na inapobidi huwa nakieleza kufatana na matokeo ya nyakati.

Labda huenda hujui.

Historia haina ukomo wa kusomwa kwani kila
siku wanakuja wasomaji wapya.

Kitabu changu kila aliyekisoma atamweleza mwenzake yale mapya aliyojifunza.

Kitabu cha Sykes hakina upungufu wa wasomaji wapya kwa hiyo hakinitaabishi.

Angalia uzi huu wamekuja watu gani?
Ninapoandika hata wewe unashindwa kujizuia.

Kama ni suala la mtu kusoma na kuchangia ni "ufuasi," hata wewe hujasalimika.

Kwa neno ufuasi, najua unaelewa nilichomaanisha, ila unajitoa ufahamu kijanja. Wafuasi unao, wale wanaokuona wewe ni "infalliable" na wanakutetea unapopotosha umma.
 
Labda kwann unahangaika na historia ni kama mambo yalopita pia kizazi cha sasa hawana mda wa kushugulika na historia wao wanaangalia maisha yanakwenda vipi kwa nyakati hizi,wanaoshughulika na history labda waliozaliwa kabla ya Uhuru ambao hawazidi hata 20% ya watanzania wote.
 
MrOnline225,
Huijui historia ya Tanganyika.
Lakini nitakusaidia.

Msome Bergen (1981), Sivalon (1992) na
Njozi (2002).

Ukipenda msome Said (1998).

Ila kitabu cha Njozi kimepigwa marufuku
lakini kinapatikana mtandaoni.


bro nimesoma historia tangu darasa la 3 ila sijawahi ambiwa popote uhuru ulipiganiwa na wakristu au waislam

ila wewe ndio unataka kuleta udini kutaka iwe confrmd kua waislam walipigania uhuru

fikiria kwanza madhara yake kabla hujaleta izo propaganda zako za udini
 
Labda kwann unahangaika na historia ni kama mambo yalopita pia kizazi cha sasa hawana mda wa kushugulika na historia wao wanaangalia maisha yanakwenda vipi kwa nyakati hizi,wanaoshughulika na history labda waliozaliwa kabla ya Uhuru ambao hawazidi hata 20% ya watanzania wote.
Kenstar,
Hapana sihangaiki mimi nastarehe sana ninapokuwa hapa ''ofsini,''
kwangu natoa hizi darsa.

Mimi ni mpenzi wa jazz basi ninapofungua hiki kijiofisi changu
hufungua na muziki nikiwasikiliza wapigaji wangu ninaowapenda.
dala
Yawezekana kuna watu hawapendi historia lakini wako wanaopenda
na ndiyo kama hivi wewe unachangia hapa.

Pia nina blog www.mohammed.com inasomwa dunia nzima.
Ukiingia hapo umenaswa kwani kuna mengi ambayo yatakustaajabisha.

Nimeanzisha sehemu makhsusi nimeipa jina, ''Kutoka JF,'' hapa utakutana
na zile mada ambazo mjadala ulikuwa mkali sana.

Wanangu wananishauri nihamie Macintosh wanasema ndiyo itanifaa zaidi
kwa kazi zangu.

Nawajibu kuwa siwezi kujifunza upya wao wanasema watanifundisha.
Mambo ni kama hivi.

Huwa naalikwa katika TV na radio na vipindi vyangu Alhamdulilah vinapendwa.
Hivi vipindi viko katika ''gallery,'' kwenye blog.

Niko vilevile kwenye Yuo Tube.

Tembea hii blog naamini utafaidika na elimu iliyopo mle.
Chembelecho Maalim Faiza: ''Elimu Bila Khiyana.''
 
bro nimesoma historia tangu darasa la 3 ila sijawahi ambiwa popote uhuru ulipiganiwa na wakristu au waislam

ila wewe ndio unataka kuleta udini kutaka iwe confrmd kua waislam walipigania uhuru

fikiria kwanza madhara yake kabla hujaleta izo propaganda zako za udini
MrOnline255,
Nitakupa darsa In Shaa Allah kuhusu historia ya Tanganyika na kwa nini
historia ilichakachuliwa.

Natoka kidogo.
Waalike na jamaa waje darsani wasome.

Nimerejea.

Hebu tuanze darsa na historia ya TANU tukianza na historia ya mtangulizi
wake African Association iliyoasisiwa mwaka wa 1929:
Saturday, 24 January 2015
KLEIST SYKES (1894 - 1949) KATIKA DICTIONARY OF AFRICAN BIOGRAPHY (DAB) OXFORD UNIVERSITY PRESS, NEW YORK

DSCN1129.JPG


DSCN1159.JPG


Jengo Hili la African Asociation Lilijengwa kwa Kujitolea Kiongozi Akiwa Kleist Sykes
Hapa Ndipo Palipokuja Kuzaliwa TANU Mwaka 1954

DSCN1154.JPG


Msomaji nakuwekea hapa vipande kutoka Dictionary of African Biography (DAB) ambao ni mkusanyo kwa njia ya maandishi historia ya Waafrika walioacha alama katika maendeleo ya bara hili.

Huu ulikuwa mradi wa Oxford University Press (OUP) na Chuo Cha Harvard na ulichukua miaka kadhaa kukamilika.

Nilikuwa mmoja wa waandishi waliotakiwa kuwaandika baadhi ya Watanzania na Watanganyika waliofanya makubwa katika historia ya nchi yao. Mradi huu ulikuwa chini ya Prof. Emmanuel K. Akyeampong wa Harvard na ulikusanya wanahistoria 500 kutoka Afrika na kwengineko.

Nilimshauri Prof. Akyeampong akate baadhi ya majina aliyoniletea ya Watanzania kwa kuwa kwa hakika hawakuwa na mchango wowote wa maana isipokuwa labda baadhi walipata kuwa na vyeo katika serikali uhuru ulipopatikana mwaka wa 1961. Nilifanya hivi kwa makusudi kabisa kwa kujua kuwa waliokuwa madarakani hawakutaka hata kidogo historia ya kweli ya waliopogania uhuru wa Tanganyika ifahamike na kuthaminiwa. Hii sasa ikawa nafasi yangu ambayo lau kwa uchache ningeliweza kuiweka sawa historia ya kweli ya Tanganyika.

Mimi nilisahau kabisa kuhusu kazi hii na hata ilipochapwa mwaka 2011 ilinichukua miaka minne kuja kukumbuka na kuanza kufuatilia nini ilikuwa hatima ya ule mradi na hapo ndipo nilipoona hii Dictionary of African Biography katika mtandao.
OUP wametoa volume sita za kazi hii mwaka 2011.

Volume hizi sita zinauzwa USD 1300 na vilevile zinapatikana kwenye mtandao kwa ''subscribers.'' Nimeletewa kutoka School of African Studies, London ukurasa ulio na makala niliyoandika kuhusu maisha ya Kleist Sykes (1894 - 1949) nami nimeona itakuwa vyema kama nitaweka hapa vipande vipande ili wasomaji wasome kwa faida ya kuhifadhi kumbukumbu za wazee wetu.

Labda msomaji utataka kujua kwa nini nilichagua kuandika maisha ya Kleist Sykes katika Dictionary of African Biography.

Nimemchagua Kleist Sykes kwa sababu hizi kubwa:
  1. Kwanza alikuwa ndiye katibu muasisi wa African Asociation mwaka 1929 na muasisi wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika 1933 akiwa katibu vilevile na kwa jinsi siasa za kiloloni zilivyokuwa wakati ule za ''wagawe uwatawale,'' yeye aliunganisha vyama hivi katika uongozi mmoja lau kama Al Jamiatul Islamiyya kilikuwa chama cha Waislam na wakati huo huo akaweza kuweka misingi ya kuwashirikisha Wakristo katika kupigania haki za Mwafrika wa Tanganyika katika African Association.
  2. Pili Kleist alifungua mlango wa Waislam wawe na shule zao wenyewe ili kukabiliana na shule za Wamishionari ambazo zilikuwa zikiwabatiza watoto wa Kiislam katika shule zao na hili liliwafanya wazazi wa Kiiislam kusita kuwapeleka watoto wao shule.
  3. Tatu katika kutimiza hili alianzisha shule ya Kiislam - Al Jamiatul Islamiyya Muslim School ambayo ilisomesha masomo ya kisekula na Qur'an. Inasemekana ilikuwa ndoto ya Kleist kuona Qur'an inasomeshwa kwanye madarasa juu ya madawati na wanafunzi wamekaa katika viti kama shule badala ya zile madras za asili ambazo watoto wanakaa chini katika majamvi. Nia yake ikiwa kuwa katika shule mtoto atapata yote mawili - elimu ya dini yake na masomo ya kisekula. Ndoto hii ya Kleist sasa si ndoto tena kwani shule za Kiislam nyingi zimeanzishwa nchini pote miaka mingi baada ya yeye kutangulia mbele ya haki zikisomesha Qur'an na masomo ya kisekula kwenye darasa moja na mwalimu akiwa kasimama mbele ya ubao.
  4. Jambo la nne ni lile la kuuweka wazi mlango wa TANU kwa Wakristo ambao wakati wa vuguvugu la kuanzisha African Association mwaka 1929 serikali iliwatisha wasijiunge na chama hicho. Hii inatokana na yeye kuwa na akina Cecil Matola, Raikes Kusi na Rawson Watts katika uongozi wa African Association na kwa njia hii kujenga msingi wa umoja na ushirikiano kwa Waafrika wote bila kujali dini zao. TANU ilipokuja asisiwa na wanae Abdulwahid na Ally wazalendo wengine mwaka 1954 hali ilikuwa haijabadilika lakini uongozi wa Waislam ndani ya TANU uliweka mkakati maalum wa kuhakikisha kuwa TANU haivurugwi na hisia za Uislam kiasi cha kuwaweka pembeni ndugu zao Wakristo.
Hii ndiyo sababu ikawezekana Nyerere kuchaguliwa kuongoza TAA mwaka 1953 na TANU ilipokuja asisiwa mwaka 1954 watoto wake wawili Abdulwahid na Ally wakiwa kati ya waasisi 17 kutoka sehemu mbalimbali za Tanganyika haikuwa tabu kwake yeye kukabidhiwa jukumu la kuwaunganisha Waafrika chini ya bendera moja ya kudai uhuru. Itoshe tu safari ya kwanza ya TANU kujitangaza nje ya Dar es Salaam Nyerere aliifanya 1954 Morogoro akifuatana na Zuberi Mtemvu na nyingine ilikuwa 1955 Lindi akifuatana na Rajab Diwani na Ali Mwinyi Tambwe Katibu wa Al Jamiatul Islamiyya.

Hizi ndizo sababu nne zilizonipelekea kuandika maisha ya Klesit Sykes katika Dictionary of African Biography.

ePw9MkeCrMqy1cQPcHSfimH6jI8APdg2XmaiIcdfA_25=w234-h570-no

Zuberi Mtemvu kama alivyokuwa 1962;
Picha hii ilipigwa nyumbani kwa Abbas Sykes
Shaaban Robert Street


tNMkE_w-TCB44eat2f73UwMqIHckxc0_qFFRFVLsL5ib=w404-h570-no

Kushoto Abbas Kleist Sykes na Abbas Zuberi Mtemvu
Abbas Mtemvu alipewa iina hili kwa heshima ya Abbas Sykes


2015%2B-%2B5

Abbas Sykes Wakati Akiwa Balozi Kulia ni Balozi Salim Ahmed Salim na
kushoto ni
Bhoke Munanka

DSCN1135.JPG

DSCN1131.JPG
 
Bafa,
Sasa nimekupata.
Hebu soma hapo chini:
Kilichobaki sasa ni kueleza sababu ya mimi kukamatwa. Mwaka wa 2006 Chuo Kikuu cha Ibadan, Nigeria kilifanya kongamano la kimataifa hapo chuoni kwao kuzungumza kuhusu Ugaidi katika Afrika ya Mashariki na Maendeleo (Conference on Islam, Terrorism and African Development). Mimi ninlitoa mada iliyokuwa na anuani hii: Terrorism in East Africa the Tanzanian Experience. Katika mada hii nilijikita mahsusi katika kuisema Marekani kwa udhalimu wao duniani. Nikaeleza kuwa huo udhalimu wao ndiyo unaopelekea wao kuchukiwa dunia nzima. Hapa ningependa kufahamisha kuwa mkutano huu wafadhili wakubwa walikuwa Iran na Marekani. Saudi Arabia ilikataa kuchangia mkutano ule. Wakati nasema maneno haya ya kuwakanyanga wenyewe Waamerika wapo hapo mkutanoni.

Baada ya kuwalani Waamerika sasa nikaigeukia serikali ya Tanzania na kuishutumu vikali kwa kupitisha Sheria ya Ugaidi. Hapa nikaeleza kuwa Waamerika wasione kuwa Tanzania imepitisha sheria hiyo ya ugaidi kwa haraka kwa sababu Tanzania ina tatizo na ugaidi. Nikaeleza kuwa sheria hiyo imepitishwa kwa sababu Bunge la Tanzania limehodhiwa na Kanisa na kupitishwa kwa sheria hiyo hakuna uhusiano wowote na ugaidi ila Wakristo wamepata fursa ya bure ya kupambana na Uislam wakitumia serikali ya Marekani kama upawa wao wa kuopolea chinyango ya moto kwenye chungu kinachotokota. Nikauchekesha mkutano kwa kuwaambia kuwa Wamarekani wamefanywa wajinga na Kanisa kwa kuchonganishwa na Waislam wa Tanzania ambao hawana ugomvi nao asilani. Baada ya kusema hayo nikahitimisha kwa kueleza nguvu ya Waislam Tanzania, kwanza kwa wingi wao na kisha kwa historia yao iliyotukuka iliyodumu takriban miaka mia wakipambana na ukoloni wa Wajerumani kwa silaha (1905 - 1907), kisha ukoloni wa Waingereza (1929 1961) na kuhitimisha kwa kuleta uhuru na kuanzia 1961 hadi sasa wanapambana na nguvu ya kanisa katika kupiga vita Uislam.

Kufikia hapa ukumbi ukawa umepata joto. Wanigeria wamesimama kutaka niwaeleze vipi Waislam watakuwa wamepigania uhuru kisha wako wengi nchini wanaruhusu wao kufanywa raia daraja la pili. Wakashangazwa kuwa hata historia ya mashujaa Waislam waliopigana Maji Maji na kunyongwa na wakoloni na mashujaa walipigania uhuru wa Tanganyika hawatajwi katika historia ya ukombozi. Nilitoa majibu kadri Allah alivyoniwezesha. Nakumbuka kitu kimoja walichosema wale ndugu zetu Wahausa. Walisema hali hiyo iliyoko kwenu haiwezekani kutokea Nigeria kwa kuwa hiyo itakuwa na sawa na kutangaza vita. Kisha wakanihakikishia kuwa sheria hiyo ya ugaidi haitapitishwa Nigeria hata siku moja.

Wapashaji habari wangu wakajanieleza baadae ni hili hitimisho langu ndilo lililosababisha Wamarekani kuleta taarifa Dar es Salaam kutaka taarifa zangu za “ugaidi” ikawa sasa sababu imepatikana ya mimi kushughulikiwa na vyombo vya dola. Ndipo ikatengenezwa hadithi ya kuku na ng’ombe dume (cock and bull story) kuwa Mohamed Said ni Mzungu wa Unga kwa hiyo akamatwe.
Mohamed Said,
Kwa hotuba hiyo ambayo umetubandikia na kwa wanaoelewa hali ya mambo nchini Tanzania nachelea kusema ulikuwa unamwaga sumu labda bado unaendelea kumwaga sumu kwa umma wa watanzania (waislam na wasio waislam). Tupe ushahidi kanisa kutaka kuua uislam, tupe ushahidi kwamba Waisalam nchini Tanzania ni wengi kuliko makundi mengine, tupe ushahidi pia kwamba vita vya majimaji vilipiganishwa na waislam pekee, tupe ushahidi kwamba uhuru wa Tanzania ulipiganiwa na waislam pekee na kuukabidhi kwa wakristo. Mohamed, kwa uongo huo ulistahili kubanwa na hata hivo nashangaa ni kwa nini uliachiwa huru hufai kukaa ndani ya jamii.

Nikuunge mkono kwa hili, Amerika ni mchonganishi na anachokiangalia ni maslahi yake tu. Amerika amefanikiwa kukuaminisha wewe kuwa nchini Tanzania kanisa ni adui wa uislam (you're very wrong). Kwa hali hiyo, ndio maana unapita na unataka kupita dunia nzima kutangaza uongo kwamba waislam wa Tanzania wanadhulumiwa haki zao na ni daraja la pili katika nchi ambayo wao wameiletea uhuru. Wahausa wa Nigeria walipigwa na butwaa baada ya kusikia mada yako hata mimi ningeshangaa yaani kundi Fulani limwage damu kasha matunda ya damu zao yakabidhiwe kwa kundi linguine kasha kundi kabidhiwa lianze dhuluma dhidi yao hii inasikitisha sana na kama ni sumu kweli ulimwaga. Boko Haramu kule Nigeria ilipata nguvu kupitia wamwaga sumu kama wewe. Na mashaka kama wewe haufungamani na wale magaidi wa Mkuranga na Amboni Tanga.

Nakushauri, tangaza ukweli bila kushawishiwa na makundi yaliyo nje ya mipaka ya Tanzania na uwe mwakilishi mzuri kwa nchi yako. Wanaofahamu ukweli hotuba yako haikuwa kitu kingine bali kueneza chuki kati ya makundi mawili kama ulivyosema (waislam na wakristo)
 
Kenstar,
Hapana sihangaiki mimi nastarehe sana ninapokuwa hapa ''ofsini,''
kwangu natoa hizi darsa.

Mimi ni mpenzi wa jazz basi ninapofungua hiki kijiofisi changu
hufungua na muziki nikiwasikiliza wapigaji wangu ninaowapenda.
dala
Yawezekana kuna watu hawapendi historia lakini wako wanaopenda
na ndiyo kama hivi wewe unachangia hapa.

Pia nina blog www.mohammed.com inasomwa dunia nzima.
Ukiingia hapo umenaswa kwani kuna mengi ambayo yatakustaajabisha.

Nimeanzisha sehemu makhsusi nimeipa jina, ''Kutoka JF,'' hapa utakutana
na zile mada ambazo mjadala ulikuwa mkali sana.

Wanangu wananishauri nihamie Macintosh wanasema ndiyo itanifaa zaidi
kwa kazi zangu.

Nawajibu kuwa siwezi kujifunza upya wao wanasema watanifundisha.
Mambo ni kama hivi.

Huwa naalikwa katika TV na radio na vipindi vyangu Alhamdulilah vinapendwa.
Hivi vipindi viko katika ''gallery,'' kwenye blog.

Niko vilevile kwenye Yuo Tube.

Tembea hii blog naamini utafaidika na elimu iliyopo mle.
Chembelecho Maalim Faiza: ''Elimu Bila Khiyana.''
sasa naanza amini jamaa liposema religion is opium of the people...... ni kama mzee wetu umepoteza imani na nchi yako kabisa unaanza elekea radicalism..unanikumbusha jamaa yangu tulisoma naye shule ya msingi aliishia mpiga vibao raisi mstahafu sasa hivi amekua kama amerukwa hivi...angalizo www.mohammed.com sio website na wala hakuna kitu..na swala la kusachiwa mbona hata raisi mstahafu alishawahi sema watanzania walikua wanabeba sana madawa hadi naye alisimamishwa kiwanja cha ndege ughaibuni..nadhani swala hapo ni eneo ulilotokea kipindi hicho kama tehran ndipo madawa ya kulevya yalikua yanasambazwa sana na haina haja kuituhumu serikali..nisamehe mzee wangu kama nimekukosea heshima..ni mawazi =o ya upeo wangu mdogo tu
 
Back
Top Bottom