Mohamed Said ''Mzungu wa Unga,'' 2007 Uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere

Mohamed Said ''Mzungu wa Unga,'' 2007 Uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere

Sooth,
Swali la, ''religious distribution,'' ni swali nyeti sana Tanzania.

Huwa sipendi kulijadili ila panapo budi na nia khasa ni kuonyesha hali halisi ya
siassa nchini petu.

Katika kitabu cha Sykes (1998) niliandika maneno hayo hapo chini:
About two-thirds of East African Muslims reside in Tanzania[1] which is the most populous of the East African countries, i.e. Kenya, Uganda and Tanzania. This includes Zanzibar-a predominantly Muslim country with a 99% Muslim population and once the centre of Islamic learning in East and Central Africa. According to the 1957 population census, Muslims outnumbered Christians at a ratio of three to two. This, at that time, meant that Tanzania was a leading Muslim nation South of the Sahara. But in the first post-independence census of 1967 the total figures for Tanzania Mainland were 32% Christian, 30% Muslim and 37% local belief. These figures show Pagans as a leading majority in Tanzania. The 1967 census has not been able to show the reasons for the sudden decrease of Muslim population nor the growth of animists amidst believers in the span of the last ten years.

This was the last population census showing religious distribution. It is widely believed that the figures for the 1967 census were doctored for political reasons to show that Muslims were trailing behind Christians in numerical strength. There is evidence that the government in 1970, having realised that Muslims were a majority in Tanzania, directed the Statistical Department to destroy all the 1967 census results. [2]

Unfortunately power sharing in the political system in Tanzania is very much skewed against Muslims, although it is known that the stability of any nation depends on proper balancing of these facts. Different sources provide different Muslim-Christian religious distribution figures. These conflicting figures are as a result of sensitivity of the issue. Among African countries with sizable population of Muslims and Christians, like Tanzania and Nigeria,[3] the inquiry as to which faith commands a leading majority, is a source of potential conflict and controversy. Tanzania is of no exception. D.B. Barret[4]gives figures which show Muslims as a minority in Tanzania. The Muslim population is purported to be 26%, Christian 45%, local belief 28%. Tanzania National Demographic Survey figures for 1973 put Muslims in Tanzania slightly above Christians at 40%, Christians 38.9% and local belief 21.1%. But according to Africa South of The Sahara, [5] Muslims in Tanzania are a leading majority at 60%. This figure has remained constant in all its publications since 1982. Since research by Tanzanian Muslims on Islam is scant or almost non-existent, the issue of Muslim population has yet to be tackled from an Islamic point of view. [6]

[1] August H. Nimtz Jr, Islam and Politics in East Africa, University of Miannapolis, 1980, p.11.
[2] See Family Mirror, Second Issue, November, 1994, p. 6.
[3] Ali A. Mazrui, ‘African Islam and Competititive Religion: Between Revivalism and Expansion’, in Third World Quarterly Vol. 10. No. 2 April, 1988, pp. 499-518.
[4] D.B.Barret, Frontier Situations for Evangelisation in Africa ,Nairobi, 1976.
[5] Africa South of The Sahara, Europa Publication, London, No. 20, 1991, p. 1027.
[6]The only conclusive Muslim research is by Dar es Salaam University Muslim Trustee (DUMT), see 'The Position of Muslims and Islam in Tanzania', in Al Haq International (Karachi) September/October1992.

Sooth,
Sasa tuje kwenye takwimu za CIA.
Niko Chuo Kikuu Cha Iowa, Iowa City US nimemaliza kufanya mhadhara wangu na sasa ni zamu
ya mimi kuulizwa maswali.

Hawa jamaa ni hodari na maswali yao yote nimyajibu kadri nilivyoweza lakini kuna kitu kimoja
nahisi hawakipendi sana katika, ''presentation,'' yangu ambayo kwao juu ya ujanja wao Wamarekani
hawakuwa wanakijua.

Nacho ni, ''the Islamic movement in the struggle for peoples emancipation in Tanganyika,'' hii inawapa
shida lakini vipi watamtoa Abdul Sykes na baba yake katika African Association (1929) na Al Jamiatul
Islamiyya (1933) na TANU (1950).

Historia wanayoijua wao ni ile rasmi ya Nyerere kuasisi TANU 1954.

Zimebaki kama dakika tano tunamaliza ndipo wakaja na hizi tawimu za CIA kuwa Wakrsto ni wengi
Tanzania.

Hili swali liliwekwa mwisho ili linishinde kwa hiyo nishuke pale ulingoni kichwa chini.
Nilisimama kwa sekunde chache swali limenishtua.

Nilijua takwimu zangu hazitafua dafu mbele ya takwimu za CIA.
Niliomba dua Allah anisitiri nisiadhirike mbele ya hawa Wazungu.

Naam jibu lilikuja hapo hapo.
Jibu ambalo hata siku moja halikupata kunipitikia katika fikra zangu.

Nilianza kwa mimi kuwauliza wao swali kuwa katika historia ya dunia kuna nchi yoyote ambayo
raia ''minority,'' walishika silaha kupambana na ukoloni?

Nikaendelea kuwaeleza kuwa kuhusu Vita Vya Maji Maji na mashujaa wake akina Sultani Abdul
Rauf Songea Mbano
na vipi historia hii inavyo hujumiwa ili kuufuta Uislam katika ukombozi wa
Tanganyika.

Nikaendelea nikawaambia waisome historia ya African Association na TANU na waangalie nani
walikuwa mstari wa mbele katika siasa za utaifa na siasa za kuigania uhuru.

Nikawaambia Waislam ndiyo waasisi wa mambo yote hayo kwa kuwa wao ndiyo walikuwa, ''majority,''
katika Tanganyika.

Nikamaliza kwa kuwauliza inawezekana vipi, ''minority,'' wawaongoze, ''majority,'' katika haya yote?
Je ingewezekana kwa India harakati za uhuru zitawaliwe na Waislam ambao ni, ''minority?''

Nikahitimisha kwa kusema kuwa siku zote Waislam hatajapata kuwa pungugu si katika wala Tanganyika.

Ukumbi ulikuwa kimyaaa.
Ungeangusha sindano ungesikia mlio wake.

Nilishuka ulingoni kichwa nimekiweka chini si kwa aibu ya kushindwa ila kwa shukrani kwa muumba
wangu.

Katika ukumbi ule kulikuwa na vijana sasa maprofesa ambao walipata kuja Tanga kunihoji kuhusu
historia ya Tanzania wakati wanafanya Ph D lakini sasa nikiwaangalia wamekuwa watu wazima.

Wakati ule walikuwa bado watoto vijana wadogo.
Hapo hapo nikaombwa kwenda kufanya mhadhara kama ule Northwestern University, Evanston Chicago.

Hawa ndiyo mabingwa wa African History ulimwengu mzima.
Nilkwenda na nikafanya mhadhara katika ukumbi wa Eduardo Mondlane.

Hivi ndivyo nilivyoumaliza ubishi wa takwimu za CIA na wingi wa Waislam Tanzania.
Tatizo ninaloliona hapa ni kutaka tuamini takwimu za wakati wa majimaji na sensa ya mwaka 1957. Kuna mabadiliko makubwa ya kidemografia yametokea baada ya wakati huo. Leo hii watu wengi wanaamini katika dini mbalimbali kuliko ilivyokuwa awali. Inawezekana kabisa kutokana na utamadumi wa mikoa ya pwani waislamu walikuwa wengi kuliko wakristo mwaka 1957, lakini haimaanishi waislamu walikuwa wengi kuliko wapagani(wenye imani za kijadi) na baada ya hapo mabadiliko makubwa yametokea ikiwemo kupungua sana kwa wanaoamini imani za jadi.

Walakini mwingine ni imani yako kwamba vita vya majimaji vilipiganwa na waislamu. Yawezekana viongozi wengi walikuwa waislam, lakini haina maana wapiganaji wote walikuwa waislamu. Tena siamini kama kulikuwa na msukumo wa kidini katika kupigana, la sivyo wasingetumia uganga kuwaaminisha watu kuwa kuna dawa ya kubadilisha risasi kuwa maji.

Mwisho, mzee wetu una maisha mazuri na unasafiri sana sababu ya misimamo yako. Unakula na kuishi kwa kutumia misimamo yako. Binafsi sishangai wamarekani kukufadhili katika mihadhara yako pamoja na misimamo yako kutowapendeza. Wazungu wana akili sana kiasi cha kuwaweka 'maadui' wao karibu. Haina maana wanakubaliana na unachokisimamia. Pia, unajinasibu kama 'wa kariakoo', wasiwasi wangu upo ndani ya yai la Dar es Salaam na haujui uhalisia wa mambo nje ya Dar es Salaam. Kwa fikra zako, Kariakoo ndiyo Tanzania. Naamini una safari nyingi za nje kuliko za Nkasi kule Rukwa.
 
Frey,
Unataka Zanzibar wawepo viongozi Wakristo.
Labda nikuulize swali.

Katika historia ya Zanzibar ya kudai uhuru ulipata kusikia kama kulikuwa
na kiongozi Mkristo akipigania uhuru wa Zanzibar?

Sasa wapi atapatikana huyo kiongozi Mkristo hii leo?

Ndiyo maana Maalim Faiza hukuulizeni watu mfano wa wewe hivi nyie mmesoma
kweli?
Hivi Tito okelo ni muislam? Acha udini acha kabisa huko Libya walikouwawa Si walikuwa Waisalam kwa Waisalam?
 
Sooth,
Swali la, ''religious distribution,'' ni swali nyeti sana Tanzania.

Huwa sipendi kulijadili ila panapo budi na nia khasa ni kuonyesha hali halisi ya
siassa nchini petu.

Katika kitabu cha Sykes (1998) niliandika maneno hayo hapo chini:
About two-thirds of East African Muslims reside in Tanzania[1] which is the most populous of the East African countries, i.e. Kenya, Uganda and Tanzania. This includes Zanzibar-a predominantly Muslim country with a 99% Muslim population and once the centre of Islamic learning in East and Central Africa. According to the 1957 population census, Muslims outnumbered Christians at a ratio of three to two. This, at that time, meant that Tanzania was a leading Muslim nation South of the Sahara. But in the first post-independence census of 1967 the total figures for Tanzania Mainland were 32% Christian, 30% Muslim and 37% local belief. These figures show Pagans as a leading majority in Tanzania. The 1967 census has not been able to show the reasons for the sudden decrease of Muslim population nor the growth of animists amidst believers in the span of the last ten years.

This was the last population census showing religious distribution. It is widely believed that the figures for the 1967 census were doctored for political reasons to show that Muslims were trailing behind Christians in numerical strength. There is evidence that the government in 1970, having realised that Muslims were a majority in Tanzania, directed the Statistical Department to destroy all the 1967 census results. [2]

Unfortunately power sharing in the political system in Tanzania is very much skewed against Muslims, although it is known that the stability of any nation depends on proper balancing of these facts. Different sources provide different Muslim-Christian religious distribution figures. These conflicting figures are as a result of sensitivity of the issue. Among African countries with sizable population of Muslims and Christians, like Tanzania and Nigeria,[3] the inquiry as to which faith commands a leading majority, is a source of potential conflict and controversy. Tanzania is of no exception. D.B. Barret[4]gives figures which show Muslims as a minority in Tanzania. The Muslim population is purported to be 26%, Christian 45%, local belief 28%. Tanzania National Demographic Survey figures for 1973 put Muslims in Tanzania slightly above Christians at 40%, Christians 38.9% and local belief 21.1%. But according to Africa South of The Sahara, [5] Muslims in Tanzania are a leading majority at 60%. This figure has remained constant in all its publications since 1982. Since research by Tanzanian Muslims on Islam is scant or almost non-existent, the issue of Muslim population has yet to be tackled from an Islamic point of view. [6]

[1] August H. Nimtz Jr, Islam and Politics in East Africa, University of Miannapolis, 1980, p.11.
[2] See Family Mirror, Second Issue, November, 1994, p. 6.
[3] Ali A. Mazrui, ‘African Islam and Competititive Religion: Between Revivalism and Expansion’, in Third World Quarterly Vol. 10. No. 2 April, 1988, pp. 499-518.
[4] D.B.Barret, Frontier Situations for Evangelisation in Africa ,Nairobi, 1976.
[5] Africa South of The Sahara, Europa Publication, London, No. 20, 1991, p. 1027.
[6]The only conclusive Muslim research is by Dar es Salaam University Muslim Trustee (DUMT), see 'The Position of Muslims and Islam in Tanzania', in Al Haq International (Karachi) September/October1992.

Sooth,
Sasa tuje kwenye takwimu za CIA.
Niko Chuo Kikuu Cha Iowa, Iowa City US nimemaliza kufanya mhadhara wangu na sasa ni zamu
ya mimi kuulizwa maswali.

Hawa jamaa ni hodari na maswali yao yote nimyajibu kadri nilivyoweza lakini kuna kitu kimoja
nahisi hawakipendi sana katika, ''presentation,'' yangu ambayo kwao juu ya ujanja wao Wamarekani
hawakuwa wanakijua.

Nacho ni, ''the Islamic movement in the struggle for peoples emancipation in Tanganyika,'' hii inawapa
shida lakini vipi watamtoa Abdul Sykes na baba yake katika African Association (1929) na Al Jamiatul
Islamiyya (1933) na TANU (1950).

Historia wanayoijua wao ni ile rasmi ya Nyerere kuasisi TANU 1954.

Zimebaki kama dakika tano tunamaliza ndipo wakaja na hizi tawimu za CIA kuwa Wakrsto ni wengi
Tanzania.

Hili swali liliwekwa mwisho ili linishinde kwa hiyo nishuke pale ulingoni kichwa chini.
Nilisimama kwa sekunde chache swali limenishtua.

Nilijua takwimu zangu hazitafua dafu mbele ya takwimu za CIA.
Niliomba dua Allah anisitiri nisiadhirike mbele ya hawa Wazungu.

Naam jibu lilikuja hapo hapo.
Jibu ambalo hata siku moja halikupata kunipitikia katika fikra zangu.

Nilianza kwa mimi kuwauliza wao swali kuwa katika historia ya dunia kuna nchi yoyote ambayo
raia ''minority,'' walishika silaha kupambana na ukoloni?

Nikaendelea kuwaeleza kuwa kuhusu Vita Vya Maji Maji na mashujaa wake akina Sultani Abdul
Rauf Songea Mbano
na vipi historia hii inavyo hujumiwa ili kuufuta Uislam katika ukombozi wa
Tanganyika.

Nikaendelea nikawaambia waisome historia ya African Association na TANU na waangalie nani
walikuwa mstari wa mbele katika siasa za utaifa na siasa za kuigania uhuru.

Nikawaambia Waislam ndiyo waasisi wa mambo yote hayo kwa kuwa wao ndiyo walikuwa, ''majority,''
katika Tanganyika.

Nikamaliza kwa kuwauliza inawezekana vipi, ''minority,'' wawaongoze, ''majority,'' katika haya yote?
Je ingewezekana kwa India harakati za uhuru zitawaliwe na Waislam ambao ni, ''minority?''

Nikahitimisha kwa kusema kuwa siku zote Waislam hatajapata kuwa pungugu si katika wala Tanganyika.

Ukumbi ulikuwa kimyaaa.
Ungeangusha sindano ungesikia mlio wake.

Nilishuka ulingoni kichwa nimekiweka chini si kwa aibu ya kushindwa ila kwa shukrani kwa muumba
wangu.

Katika ukumbi ule kulikuwa na vijana sasa maprofesa ambao walipata kuja Tanga kunihoji kuhusu
historia ya Tanzania wakati wanafanya Ph D lakini sasa nikiwaangalia wamekuwa watu wazima.

Wakati ule walikuwa bado watoto vijana wadogo.
Hapo hapo nikaombwa kwenda kufanya mhadhara kama ule Northwestern University, Evanston Chicago.

Hawa ndiyo mabingwa wa African History ulimwengu mzima.
Nilkwenda na nikafanya mhadhara katika ukumbi wa Eduardo Mondlane.

Hivi ndivyo nilivyoumaliza ubishi wa takwimu za CIA na wingi wa Waislam Tanzania.
Laiti dini na madhehebu yetu yangekuwa na mikakati kama ya kanisa la Roman Catholic, tungepiga hatua sana kama taifa. Leo hii ardhi sehemu nyingi za Tanzania ni bei chee karibu na bure. Kuna sehemu unaweza ukaenda ukafyeka pori na likawa eneo lake lenye mamia ya hekari. Miaka 30 ijayo hayo maeneo ndio yatakuwa city center maana hata Sinza ilikuwa mashamba ya mpunga miaka ya 60-70.

Sasa jiulize taasisi za kiislamu zinamiliki eneo kiasi gani na RC ina miliki eneo kiasi gani. Hiyo ndiyo tofauti na mzizi wa fitna na chuki-long term planning. Umejichimbia kariakoo na sitashangaa huna hata ekari 100 za ardhi pamoja na nafasi adhimu ya kipato uliyonayo. Wewe ni mzee wa mjini, hupendi kwenda shamba.

Mzee mwenzio Njozi alipiga sana kelele na kitabu chake cha 'Mwembechai Killings', mwishowe akapata shavu la MUM na sasa ametulia maana huwezi ukaongea huku unakula. Tatizo la Njozi nae ni kwamba pamoja na elimu na uzoefu mkubwa alionao ameshindwa kukijenga chuo cha MUM kwa kukitawanya kikaenea kwa 'ndugu zake' aliokuwa anawatetea. MUM ilipaswa kuwepo Mtwara au Lindi, Tanga, Tabora au Kigoma. Kama vyuo vya juzi kama TEKU wameweza yeye anashindwa nini? SJUT ina tawi Mtwara, Njozi kafanya nini? Kuna watu wameumbwa ili kukosoa, sio kutenda.
 
Shekh. Mohamed
Binafsi nimeufuatilia uzi wako toka mwanzo mpaka hapa ulipofikia na nimeona vitu vikuu vitatu;

1.wewe ni mtu mwenye busara nyingi unaoweza kukabiliana na hali yoyote hatarishi katika namna sahihi.

2.mkufunzi mzuri mwenye kufahamu mengi kuhusiana na historia ya taifa letu hususani yale ambayo yamekuwa akifichwa na kufahamika kwa wachache.

3.ni mwana propaganda ulio makini sana unaeweza kufikisha ujumbe fulani kwa waledi wa hali ya juu sana pasipokuvuruga hali hewa kwa wale wote wasiofurahishwa na ujumbe huo.

Mimi ni msomaji mzuri sana wa makala zako siku zote na huwa nikipitia sikosi kuokota lililo jipya, nakumbuka jinsi ukivyokuja kujibu humu kuhusu ile sanamu ya bwana Bismin iliyopo pale posta ulitoa maelezo ya kutosha tu.. Vile vile pia hata kwenye huu uzi sikuwahi kudhani kama mashujaa wetu wa kiislamu legacy yao imepuuzwa namna hii ndio kwanza nimekuja kuelewa kiundani kwenye bandiko hili.

Bwana Salum Abdallah sikuwahi kumfahamu hapo kabla wewe ndio umekuja kunijuza wasifu wake alikuwa ni nani.

Baada ya kusema hayo nirudi kwenye hii comment yako!!

Mkuu naona kama umenirushia tuhuma zisizonihusu kabisa, hasa kwenye hiyo paragraph yako ya mwisho.. sijui hata ni wapi mimi nimeandika hilo neno "chokochoko" hii ni comment yangu ya pili kwenye huu uzi wako au pengine labda comment yangu uliyoquote hujaelewa ndio maana umenihisi hivyo.

Mimi nimemquote Bak kwa kumtania tu na sio vinginevyo.

Kuhusu "chokochoko" ukiisoma vizuri ile post amekuwekea alichomjibu Nanren, katika uzi mwengine.

Hiyo chokochoko ilielekezwa kwa Nanren. Kasome tena utaelewa kuwa ile post katuwekea alichomjibu Nanren.
 
Tatizo ninaloliona hapa ni kutaka tuamini takwimu za wakati wa majimaji na sensa ya mwaka 1957. Kuna mabadiliko makubwa ya kidemografia yametokea baada ya wakati huo. Leo hii watu wengi wanaamini katika dini mbalimbali kuliko ilivyokuwa awali. Inawezekana kabisa kutokana na utamadumi wa mikoa ya pwani waislamu walikuwa wengi kuliko wakristo mwaka 1957, lakini haimaanishi waislamu walikuwa wengi kuliko wapagani(wenye imani za kijadi) na baada ya hapo mabadiliko makubwa yametokea ikiwemo kupungua sana kwa wanaoamini imani za jadi.

Walakini mwingine ni imani yako kwamba vita vya majimaji vilipiganwa na waislamu. Yawezekana viongozi wengi walikuwa waislam, lakini haina maana wapiganaji wote walikuwa waislamu. Tena siamini kama kulikuwa na msukumo wa kidini katika kupigana, la sivyo wasingetumia uganga kuwaaminisha watu kuwa kuna dawa ya kubadilisha risasi kuwa maji.

Mwisho, mzee wetu una maisha mazuri na unasafiri sana sababu ya misimamo yako. Unakula na kuishi kwa kutumia misimamo yako. Binafsi sishangai wamarekani kukufadhili katika mihadhara yako pamoja na misimamo yako kutowapendeza. Wazungu wana akili sana kiasi cha kuwaweka 'maadui' wao karibu. Haina maana wanakubaliana na unachokisimamia. Pia, unajinasibu kama 'wa kariakoo', wasiwasi wangu upo ndani ya yai la Dar es Salaam na haujui uhalisia wa mambo nje ya Dar es Salaam. Kwa fikra zako, Kariakoo ndiyo Tanzania. Naamini una safari nyingi za nje kuliko za Nkasi kule Rukwa.
Sooth,
Kwanza napenda kukufahamisha ''kuwa siendeshi maisha yangu kwa kuhadhiri
wala kwa, ''royalities.'' za vitabu nilivyoandika ingawa ni moja ya vyanzo la pato
langu.

Kuhusu mabadiliko nakubaliana na wewe kuwa yapo mabadilko mengi ya, ''demography.''
Ila lazima utambue kuwa hiyo ni barabara ya njia mbili.

Kuhusu uongozi katika uhuru wa Tanganyika kuanzia 1929 hadi uhuru ulipopatika 1961
nimetafiti na nimeandika kitabu cha Sykes ambacho ndicho kinachosomeshwa katika vyuo vingi
Afrika, Ulaya na Marekani.

Kitabu hiki ndiyo kisa cha mimi kualikwa kwingi.

Hakuna popote niliposema kuwa Wamarekani wanakubaliana na mimi lakini kitu kimoja
ni wazi kuwa wamenufaika na utafiti wangu kwa kauli zao wenyewe hili wamelisema.

Hili la Kariakoo katika harakati za uhuru wa Tanganyika halina shaka.

Vita vyote vilianza hapo na hadi leo hizo nyumba mipango ya kupambana na ukoloni
ilipokuwa ikipangwa zipo na nikizijua vyema.

Sasa ikiwa na wewe unayo historia kama hii ya Kariakoo kutoka kwenu Nkasi, Rukwa
wengi naamini wangependa kusoma.

Napenda kukufahamisha kuwa katika utafiti na kuandika niko karibu zaidi na Waingereza
kuliko Wamarekani.

Dictionary of Africa Biography (DAB) ambayo naamini umesoma katika post zangu za nyuma ingawa
ulikuwa mradi wa Harvard lakini kitabu kimechapwa na Oxford University Press, New York.
 
Laiti dini na madhehebu yetu yangekuwa na mikakati kama ya kanisa la Roman Catholic, tungepiga hatua sana kama taifa. Leo hii ardhi sehemu nyingi za Tanzania ni bei chee karibu na bure. Kuna sehemu unaweza ukaenda ukafyeka pori na likawa eneo lake lenye mamia ya hekari. Miaka 30 ijayo hayo maeneo ndio yatakuwa city center maana hata Sinza ilikuwa mashamba ya mpunga miaka ya 60-70.

Sasa jiulize taasisi za kiislamu zinamiliki eneo kiasi gani na RC ina miliki eneo kiasi gani. Hiyo ndiyo tofauti na mzizi wa fitna na chuki-long term planning. Umejichimbia kariakoo na sitashangaa huna hata ekari 100 za ardhi pamoja na nafasi adhimu ya kipato uliyonayo. Wewe ni mzee wa mjini, hupendi kwenda shamba.

Mzee mwenzio Njozi alipiga sana kelele na kitabu chake cha 'Mwembechai Killings', mwishowe akapata shavu la MUM na sasa ametulia maana huwezi ukaongea huku unakula. Tatizo la Njozi nae ni kwamba pamoja na elimu na uzoefu mkubwa alionao ameshindwa kukijenga chuo cha MUM kwa kukitawanya kikaenea kwa 'ndugu zake' aliokuwa anawatetea. MUM ilipaswa kuwepo Mtwara au Lindi, Tanga, Tabora au Kigoma. Kama vyuo vya juzi kama TEKU wameweza yeye anashindwa nini? SJUT ina tawi Mtwara, Njozi kafanya nini? Kuna watu wameumbwa ili kukosoa, sio kutenda.
Sooth,
Ukitaka kuzungumza chochote kuhusu historia ya Waislam na kama ulivyojinasibu na hiyo ''yetu,''
na kusema, ''dini na madhehebu,'' ushajiweka peupe kila mtu keshakujua.

Hebu kwanza soma historia ya Sheikh Hassan bin Amir, Tewa Said Tewa, EAMWS na historia ya
Muslim Congress 1962 na 1963 ndiyo ulete hiyo hoja ya kutaka kufananisha mipango ya Kanisa
Katoliki.

Kwani ungeliyajua yaliyotokea wala usingekuwa na sauti ya siyo tu kumkejeli Njozi bali hata hii
mada usingetia neno lako.

Haipendezi kuzungumza jambo usilolijua.
 
Sooth,
Ukitaka kuzungumza chochote kuhusu historia ya Waislam na kama ulivyojinasibu na hiyo ''yetu,''
na kusema, ''dini na madhehebu,'' ushajiweka peupe kila mtu keshakujua.

Hebu kwanza soma historia ya Sheikh Hassan bin Amir, Tewa Said Tewa, EAMWS na historia ya
Muslim Congress 1962 na 1963 ndiyo ulete hiyo hoja ya kutaka kufananisha mipango ya Kanisa
Katoliki.

Kwani ungeliyajua yaliyotokea wala usingekuwa na sauti ya siyo tu kumkejeli Njozi bali hata hii
mada usingetia neno lako.

Haipendezi kuzungumza jambo usilolijua.
Mzee wangu kwa umri na elimu yako wayajua mengi kuliko mimi, lakini haina maana unajua kila kitu. Pokea ushauri ninaokupa wewe na Prof. Njozi.
 
Sooth,
.....
Hili la Kariakoo katika harakati za uhuru wa Tanganyika halina shaka.

Vita vyote vilianza hapo na hadi leo hizo nyumba mipango ya kupambana na ukoloni
ilipokuwa ikipangwa zipo na nikizijua vyema.

Sasa ikiwa na wewe unayo historia kama hii ya Kariakoo kutoka kwenu Nkasi, Rukwa
wengi naamini wangependa kusoma.
.....
.
Mzee wangu nimekupata na nitakujibu kama ifuatavyo: Mapambano hayana mwisho maana udhalimu ni sehemu ya maisha ya binadamu. Mfano mzuri wa mapambano yasiyoisha ni South Africa na USA. Katika nchi hizo watu weusi wamepitia harakati na mapambano ambayo yamewafanya wawe tofauti sana na raia wa nchi nyingine kwa sababu harakati zinaishi kizazi kimoja mpaka kingine.

Sasa mbona nyie wanaharakati wa 'Kariakoo' harakati zenu zimefikia ukingoni? Kuna mambo serikali yetu inayafanya ndivyo sivyo, mbona mko kimya? Wewe ni mfano mzuri wa watu wanaolalamika bila kuchukua hatua katika sanduku la kura. Amini nakuambia, nguvu hizo ungezielekeza katika kubadilisha mfumo wa kisiasa au ungezielekeza kwa wanasiasa, ungefanikiwa sana. Tatizo harakati zako wazielekeza kwa maskini na walalahoi walio wengi. Zikitokea fujo za kidini, wanaoumia ni maskini. Wewe mwenye kipato kizuri utapanda ndege kwenda Nigeria kwa rafiki zako maana una pasipoti kitu ambacho kwa 90% hawana. Nakuomba uelekeze nguvu zako sehemu sahihi. Vyovyote mnavyotendewa, vinatendeka chini ya serikali ya CCM ambayo wewe hauthubutu kuikosoa.
 
Freya,
Hujafikia makamo ya kufanya mjadala wa aina hii.
 
Mambo yalianza wakati sasa narudi Dar es Salaam na ndege ya Emirates iliyokuwa inatua usiku. Inaelekea maofisa wa pasi pale uwanjani walikuwa na taarifa zangu mapema na walikuwa wakinisubiri kwa hamu kubwa kwani nilipotoa pasi yangu kwa afisa wa pasi hapo ndipo shughuli za kunishughulikia zilipoaanza.

Mimi sikuwa na hili wala lile. Nikawa namuona yule dada aliyekuwa kwenye kile kizimba akikukurika na pasi yangu akiitia katika mashine na kuitoa mara kadhaa. Fikra iliyonijia kwa haraka ilikuwa mashine ni mbovu na harakati zile zilikuwa ni kurekebisha mitambo.

Kumbe sivyo wahusika nadhani walikuwa wanahakikisha kuwa mimi ndiyo huyo waliokuwa wakimwinda na kumsubiri na sasa kapatikana, kaingia mwenyewe kwenye mtego na kanasa. Yule afisa wa pasi akanambia nikae pembeni natakiwa kwa mahojiano na watu wa usalama.

Hofu haikuwa imeniingia kwa kuwa nilikuwa natambua kuwa harakati dhidi ya ugaidi zilikuwa zimepamba moto na labda nilitakiwa kwa mahojiano mafupi kutaka kujua nyendo zangu. Sikujua wala kutarajia kuwa mshtuko mkubwa ulikuwa unanisubiri.

Nilichukuliwa hadi kwenye chumba kimoja na hapo niliwakuta maofisa wa usalama watatu wakanikaribisha kwa taadhima kisha wakanambia kuwa niko chini ya ulinzi kwa kuwa zimewafikia taarifa zangu kuwa mimi nasafirisha mihadarati. Mpaka hapa sikuwa na hofu bado ilinijia picha kuwa yawezekana wamefananisha majina.

Niliwaambia huenda Mohamed Said muuza madawa ya kulevya siyo mimi niliye mbele yao. Wakaniambia kwa kujiamini kabisa kuwa taarifa zao ni madhubuti muuza unga ni mimi na wamekuwa wakinifuatilia siku nyingi. Hapo ndipo walipotoa pasi yangu na kuniomba niitambue kama hiyo pasi ni yangu au la. Niliwajibu kuwa hakika hiyo ndiyo pasi yangu khasa.

Wakaniamuru sasa tutoke twende nikachukue mizigo yangu ili wafanye upekuzi wa mihadarati katika mizigo niliyotokanayo Tehran. Hapo ndipo nilipojuwa kuwa niko katika lindi kubwa la matatizo na ubongo wangu ukaanza kufanya kazi kwa haraka huku nikisoma dua kumuomba Allah ulinzi wake kwani kwa hakika nilijua kama ni njama zimekamilika na leo imefika siku yangu.

Nikajiuliza itakuwaje watakapotoa madawa kwenye mizigo yangu. Nikaanza kufikiri vichwa vya habari vya magazeti yatakavyopambwa na habari zangu. Ikanijia yakini kuwa watu wa usalama wameniwekea madawa ya kulevya katika mizigo yangu ili waniangamize na maadui zangu wapumzike na shari yangu.

Nilimgeukia yule ofisa mkuu aliyekuwa ananihoji nikamwambia kuwa sitokubali kugusa mizigo yangu bila kuwapo mashahidi isijekuwa mizigo yangu ishawekewa hayo madawa ya kulevya kwani nilikotoka Tehran mizigo ilikuwa imekaguliwa na ilikuwa salama.

Hoja yangu kubwa kwao ilikuwa kupata uhakika kutoka kwao kuwa wananijua vizuri kiasi cha kuthibitisha kuwa kweli mie ni msafirishaji wa madawa ya kulevya. Jibu nililopewa ni kuwa wao wanafanya kazi kutokana na taarifa zilizowafikia. Wakasema, “Sisi tunazo taarifa zako kamili kuwa wewe ni msafirisha madawa ya kulevya.”

Nikawauliza,“Baada ya kupata taarifa hizo zangu nyie mmechunguza kutafuta ukweli?” Wakasema, “Ndiyo maana leo tumekukamata.” Nikawaambia, “Si kweli kama kwa sababu mie nafahamika Dar es Salaam takriban kwingi maana ndio nilikozaliwa na kukulia. Hapo Kariakoo ukiwaambia watu kuwa Mohamed ni “Mzungu wa Unga” kila mtu atacheka maana huo kwao ndugu zangu ni mzaha mbaya.”

Walitaka kujua nilkwenda kufanya nini Iran. Niliwaambia nilialikwa na serikali ya huko kuhudhuria mkutano. Wakataka kujua vipi nilipata mwaliko. Nikawajibu kuwa hilo swali sina jibu labda waiulize serikali ya Iran. Nikawaeleza kuwa mbona siku zote napita hapo uwanjani nikenda sehemu tofauti duniani kwa mialiko na kutoa mada sijakamatwa kimezidi nini katika hii safari ya Iran?

Niliwaeleza kuwa miezi michache iliyopita nilikuwa Chuo Kikuu Cha Ibadan kwa mwaliko tena mkutano umefadhiliwa na serikali ya Marekani na wamenipa na tiketi toka Dar es Salaam hadi Lagos na kuniweka hoteli na kunilipa fedha.

“Mbona hamkunikamata wakati ule?” Nikafungua mlango mwingine nikawaambia, “Nakuapieni nyie msingethubutu kumkamata Mkristo anaetoka Vatican mkutanoni. Lakini kwa kuwa mie ni Muislam sina wa kunitetea. Nchi hii nani atakuuliza kwa kumnyanyasa Muislam?” Walishtuka na wakawa wanyonge sana wakasema si kweli kuwa naponzwa na dini yangu.

Baada ya kukurukakara nyingi na mabishano makubwa kuhusu mie kukubali kufanyiwa upekuzi wa mizigo yangu alikuja binti mmoja katika wao na yeye akanihakikishia kuwa wao ni serikali na sio wahuni. Hawathubutu kuniwekea dawa katika mizigo yangu hivyo akanisihi sana kwa upole nikubali ili wajitoe wasiwasi na wataniachia endapo hakuna kitu.

Niliomba apatikane shahidi wa kushuhudia mizigo yangu kabla ya kufanyiwa upekuzi lakini hakuna mtu aliyekubali kuchukua dhima ile katika maofisa waliokuwa kazini pale uwanja wa ndege usiku ule. Upekuzi ukafanyika hadi mwilini. Hakuna kitu. Wakanipela katika choo maalum cha kutolea madawa kwa njia ya haja kubwa.

Nikakataa kujisaidia pale. Ilikuwa ndio mara yangu ya kwanza kuona choo kama kile. Choo chenyewe ni cha aluminium. Tofauti na vyoo vya pale ambavyo siku zote ni vichafu, hiki kilikuwa kisafi sana kiasi mtu unaweza hata kutengewa chakula na akala bila ya kuhisi kinyaa.

Nilitegemea wataweka ahadi yao kuwa ikiwa hawatakuta madawa ya kulevya katika mizigo yangu watanirejeshea uhuru wangu wataniachia niende nyumbani. Haikuwa hivyo. Wakanirudisha ofisini kwao. Sasa wakaacha madawa ya kulevya wakahamia katika vitabu na “audio cassette” nilizokuwa nimepewa kama zawadi kule Tehran wakaniluliza kwa nini naingiza vitu vile khasa kanda za Khomeni na vitabu vyake nchini. Nikawauliza, “Kwani kanda na vitabu vya Khomeni haviruhusiwi kuingizwa Tanzania?
Mmm
 
Mzee wangu nimekupata na nitakujibu kama ifuatavyo: Mapambano hayana mwisho maana udhalimu ni sehemu ya maisha ya binadamu. Mfano mzuri wa mapambano yasiyoisha ni South Africa na USA. Katika nchi hizo watu weusi wamepitia harakati na mapambano ambayo yamewafanya wawe tofauti sana na raia wa nchi nyingine kwa sababu harakati zinaishi kizazi kimoja mpaka kingine.

Sasa mbona nyie wanaharakati wa 'Kariakoo' harakati zenu zimefikia ukingoni? Kuna mambo serikali yetu inayafanya ndivyo sivyo, mbona mko kimya? Wewe ni mfano mzuri wa watu wanaolalamika bila kuchukua hatua katika sanduku la kura. Amini nakuambia, nguvu hizo ungezielekeza katika kubadilisha mfumo wa kisiasa au ungezielekeza kwa wanasiasa, ungefanikiwa sana. Tatizo harakati zako wazielekeza kwa maskini na walalahoi walio wengi. Zikitokea fujo za kidini, wanaoumia ni maskini. Wewe mwenye kipato kizuri utapanda ndege kwenda Nigeria kwa rafiki zako maana una pasipoti kitu ambacho kwa 90% hawana. Nakuomba uelekeze nguvu zako sehemu sahihi. Vyovyote mnavyotendewa, vinatendeka chini ya serikali ya CCM ambayo wewe hauthubutu kuikosoa.
Sooth,
Mimi silalamiki wala sipambani na yoyote kwa hiyo ndugu yangu hujanijui
toka mwanzo na hivyo yote uliyosema hayawezi kuwa yananihusu mimi au
ndugu yangu yoyote wa Kariakoo.

Mimi nimeandika historia ya uhuru wa Tanganyika historia ambayo ilikuwa
karibu ipotee kabisa.
 
Mzee wangu kwa umri na elimu yako wayajua mengi kuliko mimi, lakini haina maana unajua kila kitu. Pokea ushauri ninaokupa wewe na Prof. Njozi.
Sooth,
Kwani umenipa ushauri gani?
Wala sijasema mie najua kila kitu.

Usikose kusoma rejea nilizokuwekea unaweza ku-search:
www.mohammedsaid.com
 
Kitulo,
Unaandika huku umekasirika.
Ghadhabu humfanya mtu akasema maneno akitulia anajuta.

Tufanye mjadala wa kisomi ili jamii inufaike na haya tunayoandika
kiasi miaka 100 baadae wakija watu kutosoma watasema hakika
wazee wale waliotangulia walikuwa watu makini.

Kweli kabisa mzee Mohamed
 
= halikadhalika

Wapi Yesu amesema kuweni Wakristo?

Fungua uzi tuwekane sawa kuhusu Uislam na Ukristo, hapa si mahala pake.
Muislamu anayeamini anafanya vema, maaa anaamini bila kuona, mkristo nae anayeamini, anafanya vyema maana anaamini bila kuona.

Nyote mnaamini, hakuna ushahidi wala kigezo, mmepokea imani kutoka kwa waliotutangulia kuishi, na waliokuwa na upeo kuliko sisi, kwa hiyo, msidozoane, wala asiwepo wa kuona yeye ni bora wakati anamini kwa imani kama mwingine, kwa sababu hana kigezo anachotumia kumponda mwenzie, bali ni imani iliingia moyoni mwako kwa sababu ya kusikia tu, wala siyo kuona, kama na yeye anavyoamini kwa kusikia.
 
Muislamu anayeamini anafanya vema, maaa anaamini bila kuona, mkristo nae anayeamini, anafanya vyema maana anaamini bila kuona.

Nyote mnaamini, hakuna ushahidi wala kigezo, mmepokea imani kutoka kwa waliotutangulia kuishi, na waliokuwa na upeo kuliko sisi, kwa hiyo, msidozoane, wala asiwepo wa kuona yeye ni bora wakati anamini kwa imani kama mwingine, kwa sababu hana kigezo anachotumia kumponda mwenzie, bali ni imani iliingia moyoni mwako kwa sababu ya kusikia tu, wala siyo kuona, kama na yeye anavyoamini kwa kusikia.

Fungua uzi.
 
Sooth,
Mimi silalamiki wa;a sipambani na yoyote kwa hiyo ndugu yangu hujanijui

toka mwanzo na hivyo yote uliyosema hayawezi kuwa yananihusu mimi au
ndugu yangu yoyote wa Kariakoo.

Mimi nimeandika historia ya uhuru wa Tanganyika historia ambayo ilikuwa
karibu ipotee kabisa.
Mimi nawatambua watu kwa matendo, sio maneno wala sura.
 
Sooth,
Kwani umenipa ushauri gani?

Wala sijasema mie najua kila kitu.

Usikose kusoma rejea nilizokuwekea unaweza ku-search:
www.mohammedsaid.com
Ushauri wangu ni kwamba ni kazi ngumu na ashakum- ya kinafiki sana kuangalia na kushadidia kilichotokea miaka 70 iliyopita wakati una nafasi ya kuangalia, kupangilia na kutekeleza kitakachotokea miaka 70 ijayo. Wewe una influence, hamasisha taasisi zilizojikita Dar ziende mikoani zikanunue ardhi kwa ajili ya shughuli za ibada na huduma za jamii. Hii siri nakuibia kutoka kwa wakatoliki-wananunua ardhi kwa wanakijiji kwa bei chee, wanaisahau kwa miaka kadhaa halafu wanaipima na kuonekana prime land. Ardhi ipo ya bwerere leo, lakini kesho itatugombanisha kwa sababu tu wengine walilala wakati wengine wanakesha.
 
Back
Top Bottom