Mohamed Said: TANU kilikuwa chama cha Kiislam, hili hakuna mtu anayeweza kulipinga

Mohamed Said: TANU kilikuwa chama cha Kiislam, hili hakuna mtu anayeweza kulipinga

Status
Not open for further replies.
Serikali yetu haina dini tangu huko nyuma Mwalimu hakuwa na dogma ya udini mpaka leo tunaishi kwa amani na utulivu kwa falsafa za Mwalimu.Wapo hata sasa wapo viongozi wachache wenye sentiments za udini na ukabila hata vyama vyao wanachaguana kwa kujuana kabila na kwa udini lakini hawawezi kuwagawa watanzania hilo wanalifahamu na hawatafanikiwa
 
Yani mtu anajitapa kabisa kwamba "TANU kilikuwa chama cha Waislamu" kama hiyo ni sifa nzuri ya kujivunia?

Mtu anaona udini ni sifa nzuri?

Wale wazee wa TANU wa Pwani walikuwa na akili sana kujua kwamba, ingawa wao wengi walikuwa Waislamu, walihitaji kiongozi mwenye elimu dunia pana na upeo wa kwenda nchi nzima kuhamasisha watu, na kwenda UN kudai uhuru kwa hoja za kifalsafa zitakazoeleweka kimataifa.

Hawakukosea kumchagua Nyerere, licha ya kwamba hakuwa Muislamu mwenzao.

Ukimsikiliza Nyerere na hoja zake za "Enlightenment Philosophy" za watu kama John Stuart Mill, utaona alijua kuongea lugha ya falsafa ya wakoloni na kuwazidi kwa hoja katika kudai uhuru, kitu ambacho wazee wa Kiislamu wengi wa Pwani (sio wote, wengi) hawakuweza.

Wazee walikuwa na akili ya kujua kwamba tofauti za dini hizi, dini za kuletewa na wageni, zisitufanye Wwaafrika tugawanyike.

Nyerere naye alivyopata madaraka ya kuendesha nchi, akasema hataki kujenga nchi yenye matabaka ya watu, tabaka la waasisi wa TANU na tabaka la wengine, tabaka la machifu na tabaka la wengine. Akavunjilia mbali Uchifu. Akaondoa habari za waasisi wa TANU kujiona wako juu ya wengine. Aapotezea waasiskataka kujenga jamii yenye usawa kwa wote. Hapo ndipo wengine wanatafsiri kwamba aliwapotezea waasisi wa TANU.

Msikilize Nyerere anamwaga madini kipindi cha former first lady wa US, Eleanor Roosevelt, mwaka 1959 katika safari zake za UN.

Sasa wazee wa Kiislamu wangapi wangeweza kujichanganya kimataifa hivyo wakati huo?

Wazee waasisi wa TANU si ndio wazee wa DSM ambao hadi kizazi chao kinatambulika hadi leo?
 


Kwanza napenda ifahamike kuwa dhumuni la kuipandisha clip hii hapa ni kumpinga huyo anaejiita "Sungura Media" aliyeipandisha clip hii youtube na kuandika kuwa eti ni "video ya siri". Haya mafundisho ya historia ya Alama Mohamed Said siyo siri, yapo mtandaoni, yapo kwenye tovuti yake na yameshajadiliwa sana hapa JF.

Mfahamu Alama Mohamed Said:

Sheikh Mohamed Said Abdallah alizaliwa mnamo tarehe 25 Februarikatika mwaka wa 1952 huko Gerezani jijini Dar es Salaam - ambapo ndiko kulikokuwa na asili ya upinzani dhidi ya ukoloni wa Waingereza katika Tanganyika. Babu yake, Mzee Salum Abdallah Popo alikuwa muasisi wa harakati za vyama vya wafanyakazi na alikuwa mmoja kati ya watu wa awali kabisa kuanzisha upinzani na kuunga mkono hoja ya kupinga utawala wa kikoloni. Mwaka wa 1947, Mzee Popo aliongoza mgomo wa kwanza nchini Tanganyika katika majimbo ya kati nchi uliopangwa na wafanyakazi wa Tanganyika Railways. Tanganyika ilipopata uhuru wake mwaka 1961, Mzee Popo aliachana na mkono wa Nyerere kama jinsi wengi walivyofanya na alitiwa kizuizini na serikali kwa ajili ya msimamo wake wa kuwa vyama vya wafanyakazi sharti viwe huru. Akiwa mwenyekiti wa Tanganyika Railways African Union (TRAU) alipinga vyama vya wafanyakazi kuwekwa chini ya Tanganyika African National Union (TANU) chini ya Rais Julius Nyerere. Sheikh Mohamed Said ana shahada katika masuala ya Sayansi ya Siasa kutoka katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Vilevile ana Stashahada katika masuala ya Maritime Studies kutoka katika Chuo Kikuu cha Wales huko mjini [[Cardiff, Uingereza na nyingine ya BIMA kutoka katika Chuo cha Usimamizi wa Fedha cha Dar es Salaam (IFM).


Utafiti juu ya historia ya uhuru wa TangayikaEdit

Mohamed Said amefanya utafiti mwingi sana juu ya historia ya uhuru wa Tanganyika, historia ambayo kabla ya utafiti wake ilichukuliwa kama iliyohitimishwa na ameweza kufukua mambo muhimu ambayo yalifichwa katika historia iliyokuwa ikitambulikana rasmi. Alianza kufahamika zaidi katika miaka ya themanini kupitia makala zake za kusisimua zilizokuwa zinahangaisha fikra za wasomaji kwa kufichua yale yaliyofichwam zilizoelezea mchango muhimu wa Waislamu na Uislamu katika harakati za kupinga ukoloni katika Tanganyika na khiyana waliofanyiwa Waislamu na serikali zote mbili, yaani, kabla ya uhuru na baada ya uhuru - jambo ambalo kwa wakati ule lilikuwa mwiko kufanyiwa utafiti au kuandikwa. Makala hizo zilipata kuchapishwa katika magazeti na majarida maarufu barani Afrika na katika magazeti ndani na nje ya Tanzania. Baadhi tu ya makala zake za utafiti ni pamoja na "In Praise of Ancestors" (1988), "Africa Events (London), "Abdulwahid Sykes: Founder of a Political Movement" Africa Events - London (1988), "Islam and Politics in Tanzania" (1989), Al Haq Internation (Karachi), "The Plight of Tanzania Muslim" (1993) Change (Dar es Salaam) na "The Secular Unsecular State" (1995) Change (Dar es Salaam).


Tazama piaEdit



Viungo vya Nje

Chanzo: https://sw.m.wikipedia.org/wiki/Mohamed_Said

cc: Mohamed Said

Mtu mjinga mjinga tu ndo anaweza kuamini hadithi za kujitungia, ati TANU kilikuwa chama cha kiislamu.
 
Kama Nyerere aliua Uislam kweli Tanzania
Basi aliona mbali sana

Maana nikiona demand wanazotaka Waislam huku Tz Bara halafu ukilinganisha na wanachowafanyia wasio Waislam kule Zanzibar, utaona kabisa hawa watu wakiwa na nguvu sana lazima amani ya nchi itatetereka tu au watajaribu ku Islamize nchi nzima

Waislam mtaona kama nina chuki na nyie ila huu ni ukweli unaouma mtanisamehe

Mfano, India na Pakistan zilikuwa nchi moja chini ya utawala wa Mwingereza, ila kutokana na demand za Waislam na vurugu zao ikabidi waigawe iwe nchi Mbili, Waislam wakaenda Pakistan, Wahindu wakabaki India

Pakistan leo hii wote tunajua ni nchi ya aina gani
Mimi siyo muamini wa dini lakini bora nchi iwe ya kipagani kuliko kuwa ya kiislamu. Ni kweli kabisa Mwalimu aliona mbali na inatubidi tumshukuru kwa kukibadilisha chama kutoka kua cha kiislamu mpaka cha kikaffir. Tatizo wengi wanaojiita waislamu mpaka huyu wetu Said ni sawa na wale wenzao wakristu wa wskati wa Crusade. Ni watu wanaojifanya wanaijua dini lakini wanaishi katika misingi ya kitokuijua dini.

Ningependa sana serikali i adopt katiba ya china tuondokane na hii kitu dini.
 
Mimi siyo muamini wa dini lakini bora nchi iwe ya kipagani kuliko kuwa ya kiislamu. Ni kweli kabisa Mwalimu aliona mbali na inatubidi tumshukuru kwa kukibadilisha chama kutoka kua cha kiislamu mpaka cha kikaffir. Tatizo wengi wanaojiita waislamu mpaka huyu wetu Said ni sawa na wale wenzao wakristu wa wskati wa Crusade. Ni watu wanaojifanya wanaijua dini lakini wanaishi katika misingi ya kitokuijua dini.

Ningependa sana serikali i adopt katiba ya china tuondokane na hii kitu dini.
Ngumu sana hiyo katiba, Wa Tz wengi ni waamini wa dini sana
 
Kwani mnataka nini hasa kwenye historia ya nchi hii?

Maana kila siku hamuishi kulialia
Waambie Marekani imepiganiwa na wengi lakini jina kubwa lipo mpaka leo ni George Washington ingekua zenji hawa jamaa wangelalamika sana
 
Kwa hiyo basi hawajasahaulika, wana special status bado
Tatizo walitaka kutengewa privilege maalum, eti kwa sababu wanzilishi wa TANU.

Nyerere alikataa ujinga huo na kusema anajenga jamii ya watu walio sawa, hata machifu aliwapiga chini wote tuwe sawa.

Sasa watu wengine hawapendi hilo, wanataka wao wawe juu. Kifupi walitaka tuondoe ukoloni wa weupe tulete habari za tabaka la mabwana walioanzisha TANU juu na tabaka lingine watwana wengine wote chini.

Nyerere alikataa ujinga huu.

Nyerere kuna mengi alishindwa, lakini katika kupinga matabaka alifanikiwa sana.
 
Tatizo walitaka kutengewa privilege maalum, eti kwa sababu wanzilishi wa TANU.

Nyerere alikataa ujinga huo na kusema anajenga jamii ya watu walio sawa, hata machifu aliwapiga chini wote tuwe sawa.

Sasa watu wengine hawapendi hilo, wanataka wao wawe juu. Kifupi walitaka tuondoe ukoloni wa weupe tulete habari za tabaka la mabwana walioanzisha TANU juu na tabaka lingine watwana wengine wote chini.

Nyerere alikataa ujinga huu.

Nyerere kuna mengi alishindwa, lakini katika kupinga matabaka alifanikiwa sana.
Hivi TANU si ilitokana na TAA, TAA ilikuwa chama cha wafanyakazi
Sasa inakuaje TANU iwe chama cha Waislam, Waislam ndio walikua wafanyakazi tu kipindi hicho?
 
Video ya siri then ipo Youtube-ha ha haaaa!

Katika kitu ninachoshukuru maishani ni kutokuumbwa muislam!

Hii dini imekaa kikuda kikuda sana! Mijamaa haijielewi na full kubeba agenda za wengine tuu!

Useless!
 
Mengi sana, na ndio maana hivi saa kuna mgogoro wa mipaka na Kenya, bahari ya Somali imesheheni Mafuta..

Kila kwenye Uislamu kuna neema ya Mafuta..
Kwa hiyo inakuaje nchi kama Angola ambayo ina mafuta mengi tu, haina vurugu ila za Kiislam ni vurugu kila uchwao?
 
Hivi TANU si ilitokana na TAA, TAA ilikuwa chama cha wafanyakazi
Sasa inakuaje TANU iwe chama cha Waislam, Waislam ndio walikua wafanyakazi tu kipindi hicho?
Kuna majibu mawili.

Kihistoria vyama hivi vimeanzia Pwani/ Dar, ambapo kipindi hicho Waislamu walikuwa wengi.

Kwa hivyo, kwa demographics, hata wakazi tu wa Dar, Waislamu walikuwa wengi. Mimi najua kwa sababu familia yangu ni wenyeji viunga vya Dar na naijua Dar kifamilia.

Lakini ili mtu kusema "chama cha kiislamu" inabidi chama kiwe na zaidi ya wingi wa wanachama wa Kiislamu tu.

Je, katiba ya TANU ilisema kwamba chama hiki ni cha Kiislamu?

Tanzania ina Waislamu na Wakristo, lakini si nchi yenye dini rasmi ya nchi.

Hata hao Waislamu wenyewe waliokuwepo TANU ni wazi hawakuuchukulia Uislamu wao kuwa ndiyo dira katika mambo ya kisiasa.

Wangechukulia hivyo, wasingemchagua Nyerere Mkristo mgeni kutoka bara awaongoze.

Yani watu wa leo wanakuwa wajinga kuendekeza udini wa dini za kuletewa na wageni kuliko hao wazee wetu waliomchagua Nyerere!

Hawaoni kwamba umoja wetu wa Kiafrika unatuunganisha kuliko tofauti za kuletewa na watu wa nje za Uislamu na Ukristo.
 
Hawa watu wanachukiana sana na Wahindu na Wabudha kuliko hata wanavyochukiana na Wakristo

Wewe jaribu kufuatilia siasa za huko India, Pakistan na Sri lanka ndio utajua
Kaka Paskali; umeandika vema. Ila ujue kwa imani ya huyo mzee "urongo" si dhambi na adui zao wakuu ni wawili: Wakristo na Wayahudi (tatizo ni kuwa kwake Ukristo unawakilishwa na Ukatoliki). Na hiyo chuki ilianzishwa na muanzilishi wa hiyo imani yao.
 
Hebu waambie
Ni long history lakini kwa kifupi wakati India inapata Uhuru wake 1947 . Waislam hawakutaka kutawaliwa na muhindu . Basi muingereza ili kutoa kuepusha mapigano akagaigawa India katika nchi tatu ili zipate Uhuru ya Kwanza ilikuwa India, ya pili ni Pakistan na nyingine ikaitwa Barochistan. Barochistan ilikuwa na mchanganyiko wa waislam na Hindu sasa waislam wengi walipenda kuwa chini ya Pakistan na wahindu walitaka kuwa chini ya India. Ila mtawala wao alikuwa muhindu. Kwahiyo Pakistan aliivamia Barochistan ambayo Leo ndio inaitwa Kashmir. Baada ya kiongozi wa Barochistan kuona anavamiwa akaomba msaada kutoka India. Huo ndio ugomvi mkubwa Kati ya India na Pakistan dhidi ya Kashmir ulipoanzia. Inshort
 
Kwa mfano vimondo angani ni mizinga anayotumia allah kumzuia shetani asiingie mbinguni..
Jua kuzama kwenye dimbwi la maji machafu,mohamed kupasua mwezi vipande viwili,mohamed kupaa na farasi hadi mbinguni
Kwa kuwa umeshindwa kufahamu kuhusu hayo uliyoyaandika kwa kuwa umejisomea mwenyewe naomba bora mtafute mwalimu mwenye kujua tafsiri ya Quran ili upate kueleweshwa.
16. Na hakika tumeweka katika mbingu vituo vya sayari, na tumezipamba kwa wenye kuangalia
17. Na tumezilinda na kila shetani afukuzwaye
18. Isipo kuwa mwenye kusikiliza kwa kuibia, naye hufuatwa na kijinga cha moto kinacho onekana.
Hicho kijinga cha moto chenye kuonekana ndiyo umeona upuuzi?
83. Na wanakuuliza khabari za Dhul- Qarnaini. Waambie: Nitakusimulieni baadhi ya hadithi yake.
84. Sisi tulimtilia nguvu katika ardhi na tukampa njia za kila kitu.
85. Basi akaifuata njia.
86. Hata alipo fika machwea-jua aliliona linatua katika checmchem yenye matope meusi. Na hapo akawakuta watu. Tukasema: Ewe Dhul-Qarnaini! Ama uwaadhibu au watwae kwa wema.
Dhul-Qarnain ndiye aliyeona jua linatua katika hiyo chemchem yenye matope meusi, kutokana na sehemu alipokuwepo, si kusema kwamba Mungu anasema jua linazama kwenye chemchem yenye matope meusi.
Kuhusu mwezi kupasuka sehemu mbili huo ni muujiza, unatakiwa kuwa na imani ili uamini.
Buraq=lightning si farasi ni mnyama mdogo kuliko mule na mkubwa kuliko punda, na huo ni muujiza mwengine.
 
MTU yoyote mwenye ujasili wa kusema maneno magumu, makavu dhidi ya jamii zingine iwe imani, kabila, ranging au itikadi yoyote in hatari sana. CCM inatakiwa kulitafakari hili. Leo Msiba anatamka maneno magumu dhidi ya watu, wote wako kimya huwezi on a MTU anahoji ispokuwa Member aliejitokeza na kumshugulikia kisheria, inafahamika sana CCM na jamaa zao wahanga was Msiba wanaogopa wanamuogopa anaye mkingia kifua au kumlinda Msiba huu ni unafiki was kiwango cha shetani na ndio maana wanapiga na kusifia lolote lenye kuumiza wapinzani hawajari kuwa hao no ndugu zao, jamaa zao watanzania wenzao, na waumini wenzao. Wamefika hatua ya kudhuru HAKI za wengine huku wakifunga mikono kumwabudu Mungu Mwenyezi. Kufuruuuuuuu!
[emoji1] [emoji1] [emoji1] Mbona umeingia chaka? Yani ulichoandika hakiendani kabisa na mada ni mbingu na ardhi.

Alafu huyo Musiba mnamuogopa wa nini kama anawakera si mumpeleke mahakamani?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom