Moja wapo ya Fungu kwenye Biblia linalotafsiriwa vibaya: Matendo ya Mitume 10:15

Moja wapo ya Fungu kwenye Biblia linalotafsiriwa vibaya: Matendo ya Mitume 10:15

Watu wanalitumia fungu hili kuhalalisha kula wanyama ambao wamekatazwa katika kitabu cha Mambo ya walawi. Na kwa kuweka mambo sawa fungu hili halizungumzii vyakula, na kudhihirisha hili ukisoma hiyo matendo ya mitume 10 yote utaelewa.

Fungu lenyewe linasema "Sauti ikamjia mara ya pili, ikimwambia, vituvilivyotakaswa na Mungu usiviite wewe najisi." Mwisho wa kunukuu.

Kwa kifupi labda nisimulie hiki kisa kilivyokuwa,

Ukisoma Matendo ya Mitume 10 kuanzia fungu la 9 Petro alikuwa na njaa sana wakati msosi unaandaliwa alizimia na alioneshwa maono na katika maono hayo Kilishushwa Chombo chenye pembe nne kutoka mbinguni ambamo ndani yake kulikuwa na wanyama mbalimbali, kisha sauti ikasema Ondoka Petro uchinje ule, Petro akajibu akisema Hasha Bwana, kwa maana sijakula kamwe kitu kilicho kichafu wala najisi.

Na tendo hilo la kumuambia kwamba achinje ale lilifanyika mara tatu na zote Petro alikataa, ndio ile sauti ikamwambia vitu alivyovitakasa Bwana usiviite najisi. Na mwisho alipozidi kugoma kile chombo kikarudishwa juu.

Kabla sijaendelea hapa kuna mambo mawili ya kujiuliza,

1. Bila shaka wanyama walikuwepo mle ndani wote walikuwa ni Najisi ndio maana Petro aliwakataa, Na hakuwa anamkatalia Binadamu mwenzake, Bali alikuwa anaikataa sauti ya Mungu.

2. Kama sheria ile ya mambo ya walawi ilifutwa, kama watu wanavyodai kwenye Marko 7 na Mathayo 15(Hili nitaletea uzi nalo maana nalo watu wanadanganywa sana). Ni kwanini Petro alikuwa anakataa na aliwaita wale wanyama najisi na wachafu? Zingatia huyu alikuwa mmoja kati ya wanafunzi wa Yesu.

Na mwisho kabisa yale yalikuwa ni maono tu na wakati anaendelea kuyafikiria kwamba yana maana gani, Roho mtakatifu akamuambia kuna watu watatu kawatuma kuja kwake hivyo aongozane nao.

Tafsiri ya Maono yale inakuja kupatikana katika Matendo ya Mitume 10:28 ambayo inasema "Akawaambia, Ninyi mnajua kuwa si halali mtu aliye Myahudi ashikamane na mtu aliye wa taifa lingine wala kumwendea, Lakini Mungu amenionya, nisimuite mtu awaye yote mchafu wala Najisi."

Watu wanachukua vifungu kidogo ambavyo vinafavor vitu vyao ambavyo kwa macho yao vinawavutia ila hawasemu ukweli.

Jina la Bwana Libarikiwe.

Muwe na Usiku mwema.
Nik
Watu wanalitumia fungu hili kuhalalisha kula wanyama ambao wamekatazwa katika kitabu cha Mambo ya walawi. Na kwa kuweka mambo sawa fungu hili halizungumzii vyakula, na kudhihirisha hili ukisoma hiyo matendo ya mitume 10 yote utaelewa.

Fungu lenyewe linasema "Sauti ikamjia mara ya pili, ikimwambia, vituvilivyotakaswa na Mungu usiviite wewe najisi." Mwisho wa kunukuu.

Kwa kifupi labda nisimulie hiki kisa kilivyokuwa,

Ukisoma Matendo ya Mitume 10 kuanzia fungu la 9 Petro alikuwa na njaa sana wakati msosi unaandaliwa alizimia na alioneshwa maono na katika maono hayo Kilishushwa Chombo chenye pembe nne kutoka mbinguni ambamo ndani yake kulikuwa na wanyama mbalimbali, kisha sauti ikasema Ondoka Petro uchinje ule, Petro akajibu akisema Hasha Bwana, kwa maana sijakula kamwe kitu kilicho kichafu wala najisi.

Na tendo hilo la kumuambia kwamba achinje ale lilifanyika mara tatu na zote Petro alikataa, ndio ile sauti ikamwambia vitu alivyovitakasa Bwana usiviite najisi. Na mwisho alipozidi kugoma kile chombo kikarudishwa juu.

Kabla sijaendelea hapa kuna mambo mawili ya kujiuliza,

1. Bila shaka wanyama walikuwepo mle ndani wote walikuwa ni Najisi ndio maana Petro aliwakataa, Na hakuwa anamkatalia Binadamu mwenzake, Bali alikuwa anaikataa sauti ya Mungu.

2. Kama sheria ile ya mambo ya walawi ilifutwa, kama watu wanavyodai kwenye Marko 7 na Mathayo 15(Hili nitaletea uzi nalo maana nalo watu wanadanganywa sana). Ni kwanini Petro alikuwa anakataa na aliwaita wale wanyama najisi na wachafu? Zingatia huyu alikuwa mmoja kati ya wanafunzi wa Yesu.

Na mwisho kabisa yale yalikuwa ni maono tu na wakati anaendelea kuyafikiria kwamba yana maana gani, Roho mtakatifu akamuambia kuna watu watatu kawatuma kuja kwake hivyo aongozane nao.

Tafsiri ya Maono yale inakuja kupatikana katika Matendo ya Mitume 10:28 ambayo inasema "Akawaambia, Ninyi mnajua kuwa si halali mtu aliye Myahudi ashikamane na mtu aliye wa taifa lingine wala kumwendea, Lakini Mungu amenionya, nisimuite mtu awaye yote mchafu wala Najisi."

Watu wanachukua vifungu kidogo ambavyo vinafavor vitu vyao ambavyo kwa macho yao vinawavutia ila hawasemu ukweli.

Jina la Bwana Libarikiwe.

Muwe na Usiku mwema.
Tafadhali mwache mkuu wa meza
 
Hayo mengine ni maagizo na ni Mungu mwenye alizungumza na Musa, Amri ni msisitizo ndio maana Mungu aliziandika kwa kidole chake.
2 Wakorintho 3:7
Basi, ikiwa huduma ya mauti, iliyoandikwa na kuchorwa katika mawe, ilikuja katika utukufu, hata Waisraeli hawakuweza kuukazia macho uso wa Musa, kwa sababu ya utukufu wa uso wake; nao ni utukufu uliokuwa ukibatilika;

2 Wakorintho 3:8
je! Huduma ya roho haitazidi kuwa katika utukufu?

2 Wakorintho 3:15
ila hata leo, torati ya Musa isomwapo, utaji huikalia mioyo yao.

2 Wakorintho 3:16
Lakini wakati wo wote watakapomgeukia Bwana, ule utaji huondolewa.

2 Wakorintho 3:17
Basi “Bwana” ndiye Roho; walakini alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru.
 
Nioneshe Yesu aliposema Tusitunze sabato ilihali hata akina Maria Magdalene tuliowaona wakipumzika siku ya sabato masaa machache baada ya Yesu Kufa, Na hawa ni watu waliomfuata Yesu maeneo mbalimbali.
Siyo lazima aseme direct kwamba tusitunze sabato, ila baadhi ya mazungumzo yake yanathibitisha kuwa kwake yeye hakuna kutunza sabato.

Mfano:
Kwa mujibu wa torati haipaswi kufanya kazi yoyote siku ya sabato lakini Yesu alisema hivi:
Yohana 5:16
Kwa sababu hiyo Wayahudi wakamwudhi Yesu, kwa kuwa alitenda hayo siku ya sabato.

Yohana 5:17
Akawajibu, Baba yangu anatenda kazi hata sasa, nami ninatenda kazi.
[Yesu alikuwa anayafanya yote haya katika siku ya Sabato. Hivyo Wayahudi hao wakaanza kumsumbua asiendelee. Lakini yeye akawaambia, “Baba yangu hajawahi kuacha kufanya kazi, hivyo nami pia nafanya kazi.”
Yohana 5:16‭-‬17 TKU]

Mfano 2: Soma kisa marko 2 : 23-27
Marko 2:27
Akawaambia, Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, si mwanadamu kwa ajili ya sabato.

Marko 2:28
Basi Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato pia.
[Ndipo Yesu akawaambia mafarisayo, “Siku ya Sabato ilifanywa kwa faida ya watu. Watu hawakuumbwa ili watawaliwe na Sabato. Kwa hiyo Mwana wa Adamu ambaye ni Bwana juu ya kila kitu, pia ni Bwana juu ya siku ya Sabato.”
Marko 2:27‭-‬28 TKU]

Yesu kama mwanadamu mwenye roho wa Mungu alikuwa juu ya sabato (yaani anaweza kufanya chochote na asipate/asihesabiwe hatia) nasi pia wanadamu wa Leo wenye roho wa Mungu(yaani kristo anakaa ndani yetu) tupo juu yaani ni Mabwana wa Sabato tunaweza kufanya lolote na hakuna wa kukuhesabia hatia.

Nikisema hakuna wa kukuhesabia hatia inategemeana na unaemtumaini nafsini mwako, kama unamtumaini Yesu yeye mwenyewe alisema hatakushtaki.
Yohana 5:45
Msidhani kwamba mimi nitawashitaki kwa Baba; yuko anayewashitaki, ndiye Musa, mnayemtumaini ninyi.

Hii mifano michache inathibitisha kuwa hiyo sabato unayoipigania iko chini yako yaani hupaswi kuwa na wasiwasi nayo
 
NB: tunamuabudu Mungu katika roho na KWELI. Hakuna madhara wala dhambi kumla nguruwe.
Exactly, maana chakula hupita mdomoni, tumboni kisha hutupwa chooni. Ila yamtokayo mtu mdomoni hutoka moyoni hayo ndio humtia mtu unajisi.
 
Siyo lazima aseme direct kwamba tusitunze sabato, ila baadhi ya mazungumzo yake yanathibitisha kuwa kwake yeye hakuna kutunza sabato.

Mfano:
Kwa mujibu wa torati haipaswi kufanya kazi yoyote siku ya sabato lakini Yesu alisema hivi:
Yohana 5:16
Kwa sababu hiyo Wayahudi wakamwudhi Yesu, kwa kuwa alitenda hayo siku ya sabato.

Yohana 5:17
Akawajibu, Baba yangu anatenda kazi hata sasa, nami ninatenda kazi.
[Yesu alikuwa anayafanya yote haya katika siku ya Sabato. Hivyo Wayahudi hao wakaanza kumsumbua asiendelee. Lakini yeye akawaambia, “Baba yangu hajawahi kuacha kufanya kazi, hivyo nami pia nafanya kazi.”
Yohana 5:16‭-‬17 TKU]

Mfano 2: Soma kisa marko 2 : 23-27
Marko 2:27
Akawaambia, Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, si mwanadamu kwa ajili ya sabato.

Marko 2:28
Basi Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato pia.
[Ndipo Yesu akawaambia mafarisayo, “Siku ya Sabato ilifanywa kwa faida ya watu. Watu hawakuumbwa ili watawaliwe na Sabato. Kwa hiyo Mwana wa Adamu ambaye ni Bwana juu ya kila kitu, pia ni Bwana juu ya siku ya Sabato.”
Marko 2:27‭-‬28 TKU]

Yesu kama mwanadamu mwenye roho wa Mungu alikuwa juu ya sabato (yaani anaweza kufanya chochote na asipate/asihesabiwe hatia) nasi pia wanadamu wa Leo wenye roho wa Mungu(yaani kristo anakaa ndani yetu) tupo juu yaani ni Mabwana wa Sabato tunaweza kufanya lolote na hakuna wa kukuhesabia hatia.

Nikisema hakuna wa kukuhesabia hatia inategemeana na unaemtumaini nafsini mwako, kama unamtumaini Yesu yeye mwenyewe alisema hatakushtaki.
Yohana 5:45
Msidhani kwamba mimi nitawashitaki kwa Baba; yuko anayewashitaki, ndiye Musa, mnayemtumaini ninyi.

Hii mifano michache inathibitisha kuwa hiyo sabato unayoipigania iko chini yako yaani hupaswi kuwa na wasiwasi nayo
Takbirrrr.
 
2 Wakorintho 3:7
Basi, ikiwa huduma ya mauti, iliyoandikwa na kuchorwa katika mawe, ilikuja katika utukufu, hata Waisraeli hawakuweza kuukazia macho uso wa Musa, kwa sababu ya utukufu wa uso wake; nao ni utukufu uliokuwa ukibatilika;

2 Wakorintho 3:8
je! Huduma ya roho haitazidi kuwa katika utukufu?

2 Wakorintho 3:15
ila hata leo, torati ya Musa isomwapo, utaji huikalia mioyo yao.

2 Wakorintho 3:16
Lakini wakati wo wote watakapomgeukia Bwana, ule utaji huondolewa.

2 Wakorintho 3:17
Basi “Bwana” ndiye Roho; walakini alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru.
Barikiwa sana pastor
 
Back
Top Bottom