Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Yvonne Cherrie, msanii maarufu wa filamu, Monalisa, ameweka historia baada ya kuhitimu Chuo Kikuu katika fani ya Usimamizi wa Biashara na Miradi, licha ya changamoto za dhihaka na kejeli alizokumbana nazo kutokana na umri wake.
Monalisa, ambaye alikuwa miongoni mwa mwanafunzi waliokula chumvi nyingi katika darasa lake, amesema watu walimcheka na kushangaa kwanini aliamua kurudi shule akiwa na umri mkubwa. Hata hivyo, hakukata tamaa na leo amejivunia kuhitimu akiwa mwanafunzi bora wa darasa lake.
Katika ujumbe wake, Monalisa amesisitiza kuwa mafanikio hayo ni ushuhuda wa uvumilivu, ujasiri, na uthubutu. Amesema safari yake ni kielelezo kuwa kamwe si kuchelewa kufanikisha ndoto zako, na huu ni mwanzo tu wa mambo makubwa yanayokuja.
“Nilichekwa, lakini leo nimebutua,” alisema Monalisa kwa furaha, akiongeza kuwa hakuna kurudi nyuma, na mashabiki wake waendelee kufuatilia safari yake.
Mastaa na mtoto wake wamiminika kumpongeza mitandaoni.
Monalisa, ambaye alikuwa miongoni mwa mwanafunzi waliokula chumvi nyingi katika darasa lake, amesema watu walimcheka na kushangaa kwanini aliamua kurudi shule akiwa na umri mkubwa. Hata hivyo, hakukata tamaa na leo amejivunia kuhitimu akiwa mwanafunzi bora wa darasa lake.
Katika ujumbe wake, Monalisa amesisitiza kuwa mafanikio hayo ni ushuhuda wa uvumilivu, ujasiri, na uthubutu. Amesema safari yake ni kielelezo kuwa kamwe si kuchelewa kufanikisha ndoto zako, na huu ni mwanzo tu wa mambo makubwa yanayokuja.
“Nilichekwa, lakini leo nimebutua,” alisema Monalisa kwa furaha, akiongeza kuwa hakuna kurudi nyuma, na mashabiki wake waendelee kufuatilia safari yake.
Mastaa na mtoto wake wamiminika kumpongeza mitandaoni.