Morogoro: Stand ya Daladala kuhamishiwa kilomita 2+ kutoka katikati ya mji ni kero kwa Wananchi

Morogoro: Stand ya Daladala kuhamishiwa kilomita 2+ kutoka katikati ya mji ni kero kwa Wananchi

Ndugu wanajamvi,

Nimefika mjini Morogoro kwenye hekaheka zangu nikashangazwa na kitendo cha kuhamishia stand ya daladala kutoka katikati ya mji na kuipeleka karibu na Chuo Kikuu cha Sokoine umbali wa kama Km 2+.

Ni jambo jema kuboresha huduma kwa jamii kutokana na kukua kwa mji, lakini viongozi wa jambo husika hawakaushirikisha mawazo ya wananchi katika kufikia maamuzi ya jambo walilofanya.

Daladala zinazoingia na abiria waendao kufuata mahitaji katikati ya mji wanashushwa mbali na mji na kulazimika kukodi bajaji na pikipiki ili wafike katikati ya mji kitendo ambacho kinawaongezea gharama wananchi ambao wengi wao ni wa kipato cha chini.

Bajaji ambazo ndiyo msaada wa haraka nazo zimeondolewa katikati ya mji na kulazimu wananchi kutembea umbali mrefu kwenda kutafuta usafiri wa kuunganisha ili waende waendako, mathalani mtu atokaye Msamvu kwenda Bigwa analazimika kuchukua pikipiki kwenda mpaka mjini kati ndipo apate daladala ya kwenda Bigwa.

Changamoto ni nyingi sana, nashauri mamlaka husika zishirikishe mawazo ya wananchi ili kuondoa usumbufu unaoendelea kujitokeza mapaka sasa na kuathiri kwa kiasi kikubwa majukumu ya watu na kuwaongezea gharama za maisha wananchi wa kipato cha chini.

Ikumbukwe kuwa maamuzi yalifanywa na viongozi bila kushirikisha wananchi, lakini viongozi hao hawakuvaa viatu vya wananchi husika ili nao wapate feelings ambazo wananchi wanazipata kwa sasa kwakuwa viongozi husika hawatumii daladala, laiti wangekuwa wanatumia daladala wangeona adha hizo na huenda wasingechukua uamuzi waliochukua.

Nawasilisha
Zitapatikana daladala za kupiga ruti za mjini mpaka hapo stand. Usiwe mpenda maendeleo
 
Afadhali hiyo stendi imehamishwa ilkuwa kero sana, magari yanajaa mpaka wanapakia na kushusha nje ya stendi tena kukiwa na msongamano sana, ikifika tu jioni hapapitiki. Wewe kama una duka lako hapo karibu na stendi wateja wako watakuja tu.
 
Utazoea tu usijali. Kelele za lawama kwa hiki kipind cha mwanzo ni kawaida. Muda wote stendi inajengwa unaona umekaa kimya tu sahivi unalalamika ulitegemea stend ikikamilika wataifanya soko
Tatizo watu tunapenda kulalamika bila kutimiza wajibu miradi kama hii huibuliwa na halmashauri husika kupitia vikao vya madiwani ambao ndiyo wawakirishi wa wananchi ili kutatua kero na kuongeza mapato kwenye kikao cha baraza la madiwani

Mwananchi yeyote anaruhusiwa huhudhuria ingawa haruhusiwi kuchangia lakini ana nafasi ya kuwashauri madiwani nje ya kikao akawasirisha mawazo yake nao wakayasemea kwenye vikao.

Tatizo tukiwachagua tunajiondoa kwenye nafasis yetu ya kuwashauri na kuwatuma maana kimsingi sisi ndo waajiri wao bado kuna nafasi ya kushari katika hili hasa ruti za magari kugawanywa na siyo kupuuza maendeleo
 
[emoji3][emoji3][emoji3]soon mtafika moro ... Halafu hata miaka 30 haijafika tangu waihamishie ubungo .. inavyoonekana kila kiongozi akikaa madarakani anatafuta chocho la kupiga hela
Hicho ndicho nilichokifahamu
 
Ili manispaa isipoteze mapato stand ya zamani waigeuze car parking ya kulipia patanoga kama mnazi mmoja kwa madalali na warembesha urembo wa magari kufanya kazi hapo.
 
ukweli ni kwamba ile stendi ya pale mjini Morogoro... ilikuwa ni kero kwa watumiaji wa barabara za Boma pamoja na hii ya madaraka, ile iendayo halmashauri na ile iendayo masika... na tukumbuke pia daladala zinazidi ongezeka... fujo zitapungua kwa kuihamisha hiyo stendi

Ni kweli msongamano ulikuwa cangamoto, lakini kumbuka kuwa waliokuwa wanazembea ni askari wa usalama wa barabarani, hawakuwa strategic katika kusimamia magari yanayoingia na kutoka stand
 
Ni kweli msongamano ulikuwa cangamoto, lakini kumbuka kuwa waliokuwa wanazembea ni askari wa usalama wa barabarani, hawakuwa strategic katika kusimamia magari yanayoingia na kutoka stand
na kastendi kalikuwa kadogo, wakati huohuo mji unazidi kukua, na kufanya route za daladala ziongezeke, hebu kumbuka tulikuwa na daladala za chamwino na sua, uzuri zikaja bajaji na kuua hizo route, sasa hivi tuna daladala za mkundi, azimio, manyuki, yespa na soon huenda utaona za kiyegea,
unadhani bado kale kaeneo kangetosha kwa daladala zote za mji huu wa morogoro, na ililazimu wengine kushushia abiria nje ya stendi... hakukuwa na uzembe kwa upande wa trafiki...
kuna mazingira huwezi walaumu hao...
 
na kastendi kalikuwa kadogo, wakati huohuo mji unazidi kukua, na kufanya route za daladala ziongezeke, hebu kumbuka tulikuwa na daladala za chamwino na sua, uzuri zikaja bajaji na kuua hizo route, sasa hivi tuna daladala za mkundi, azimio, manyuki, yespa na soon huenda utaona za kiyegea,
unadhani bado kale kaeneo kangetosha kwa daladala zote za mji huu wa morogoro, na ililazimu wengine kushushia abiria nje ya stendi... hakukuwa na uzembe kwa upande wa trafiki...
kuna mazingira huwezi walaumu hao...


Naafikiana nawe kuwa stand haikuwa inatosha lakini
  1. Pamoja na changamoto hizo hapakuwa na effective utilization of resources mfano ilikuwa ni kawaida kabisa askari wa usalama barabarani kutosimamia mabasi yanayoingia na kutoka stand na hata baadhi ya madereva walikuwa wanavunja sheria mbele yao na wao hawakuwa na meno kwakuwa baadhi ya daladala ni zao.
  2. Hapakuwa na proper planning ya namna sahihi ya kuondokana na hizo changamoto, kwa mfano daladala za vijijini kama Mngeta, Mzumbe nk zilikuwa zinaegesha kwa masaa mengi stand tangu asubuhi mpaka alasiri bila sababu.
  3. Route zilizoanzishwa zilitakiwa zizingatie mahitaji ya muhimu ya wananchi katikati ya mji kama vile hospitali, kituo kikuu cha polisi, ofisi za Manispaa, mabenki, mahakama nk ili kuwaondolea usumbufu wa kutembea umbali mrefu (kutoka Masika hadi katikati ya mji na kutoka katikati ya mji hadi Misitu/maliasili/Simbaoil hasa wakati wa mvua na jua kali.)
Kumbuka wanaoumia ni wananchi wa kipato cha chini, wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wanaosoma shule za serikali ambao wanatoka kwenye familia duni, mathalani, mwanafunzi anaishi Kihonda, anasoma Sumaye Bigwa, Kola Hill, Lupanga na Kingalu anashushwa Masika, anatembea kwa miguu mpaka Manispaa akavizie usafiri wa Bigwa, au mwanafunzi huyo anatoka Sumaye Bigwa, Kola Hill, Lupanga na Kingalu, anatembea kwa miguu mpaka Misitu/maliasili/Simbaoil kwenda kusubiri usafiri wa Kihonda kwa sababu Masika wapo askari wanazuia mabasi kuchukua abiria.

  1. Kusema ukweli wananchi/wanafunzi wa kipato cha chini ndiyo wanateseka, lakini endapo wanaopanga hizo route na hivyo vituo vya kupakilia na kushushia abiria wangesafiri kwa public transport kwa angalau wiki moja huenda wangeelewa kinacholalamikiwa, lakini kwakuwa wao wako kwenye magari binafsi, hawatakaa waelewe.
  2. Kama viongozi husika wangekaa na wananchi wanaotumia daladala na kujadiliana nao, wachukue concerns zao na wazifanyie kazi ingekuwa jambo la busara zaidi kuliko kuwashinikiza wananchi kukabiliana na hali mbaya ya mfumo wa usafiri iliyoamriwa kwa interests zao binafsi.
 
Naafikiana nawe kuwa stand haikuwa inatosha lakini
  1. Pamoja na changamoto hizo hapakuwa na effective utilization of resources mfano ilikuwa ni kawaida kabisa askari wa usalama barabarani kutosimamia mabasi yanayoingia na kutoka stand na hata baadhi ya madereva walikuwa wanavunja sheria mbele yao na wao hawakuwa na meno kwakuwa baadhi ya daladala ni zao.
  2. Hapakuwa na proper planning ya namna sahihi ya kuondokana na hizo changamoto, kwa mfano daladala za vijijini kama Mngeta, Mzumbe nk zilikuwa zinaegesha kwa masaa mengi stand tangu asubuhi mpaka alasiri bila sababu.
  3. Route zilizoanzishwa zilitakiwa zizingatie mahitaji ya muhimu ya wananchi katikati ya mji kama vile hospitali, kituo kikuu cha polisi, ofisi za Manispaa, mabenki, mahakama nk ili kuwaondolea usumbufu wa kutembea umbali mrefu (kutoka Masika hadi katikati ya mji na kutoka katikati ya mji hadi Misitu/maliasili/Simbaoil hasa wakati wa mvua na jua kali.)
Kumbuka wanaoumia ni wananchi wa kipato cha chini, wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wanaosoma shule za serikali ambao wanatoka kwenye familia duni, mathalani, mwanafunzi anaishi Kihonda, anasoma Sumaye Bigwa, Kola Hill, Lupanga na Kingalu anashushwa Masika, anatembea kwa miguu mpaka Manispaa akavizie usafiri wa Bigwa, au mwanafunzi huyo anatoka Sumaye Bigwa, Kola Hill, Lupanga na Kingalu, anatembea kwa miguu mpaka Misitu/maliasili/Simbaoil kwenda kusubiri usafiri wa Kihonda kwa sababu Masika wapo askari wanazuia mabasi kuchukua abiria.

  1. Kusema ukweli wananchi/wanafunzi wa kipato cha chini ndiyo wanateseka, lakini endapo wanaopanga hizo route na hivyo vituo vya kupakilia na kushushia abiria wangesafiri kwa public transport kwa angalau wiki moja huenda wangeelewa kinacholalamikiwa, lakini kwakuwa wao wako kwenye magari binafsi, hawatakaa waelewe.
  2. Kama viongozi husika wangekaa na wananchi wanaotumia daladala na kujadiliana nao, wachukue concerns zao na wazifanyie kazi ingekuwa jambo la busara zaidi kuliko kuwashinikiza wananchi kukabiliana na hali mbaya ya mfumo wa usafiri iliyoamriwa kwa interests zao binafsi.
nakubaliana na wewe juu ya kutokuwepo mipango thabiti tangu awali, hasa katika hatua iliyowafanya waamue mahala pa kuijenga hiyo stendi,
pengine walipaswa kuzingatia maoni ya wadau kwanza kabla ya hatua yoyote
 
Sio tu Morogoro hata Dar-es-Salaam vituo vya mabasi yakwenda Mikoani na nchi jiani.

Kujenga kituo kikuu cha mabasi kwenda mikoani Mbezi,wasiondoe vituo vingine katika maeneo mengine. Kwa mtu anaenda Lindi au Mtwara wajengewe maeneo ya kuelekea Kilwa Road.

Sana sana ikibidi kupitia Morogoro road kuelekea mikoani ndipo basi ipitie tu kama kituo kikuu tu.

Sisi wasafiri msitugeuze watumwa ,au mradi.Nimegundua vituo vingi vikubwa vilivyojengwa na serikali licha ya kuwa na maeneo makubwa na majengo yanayovutia lakini hawatilii maanani huduma kama Vyoo.

Vyoo mara nyingi having usafi wa kuridhisha,ni kero. Kama tungekuwa wakali kwa hilo karibu vituo vingi vingefungiwa.
wanaoenda lindi kituo chao kipo temeke sudan na mbagala kule na kuna mpango wa kuwapeleka vikindu
 
wanaoenda lindi kituo chao kipo temeke sudan na mbagala kule na kuna mpango wa kuwapeleka vikindu

Haidhuru kama watatengeneza link ya hizo stand ikibidi kuwe na trams connection maalumu kwa ajili ya kuhudumia stand hizo
 
Hata stendi ya Kisutu na Mnazi mmoja wakati zinahamishwa watu walipinga kama wanavyo pinga kuhamishwa stendi daladala ya Moro
 
Back
Top Bottom