Moshi: Yanayojiri katika Kongamano la BAWACHA Siku ya Wanawake Duniani Machi 3, 2023; Rais Samia mgeni rasmi

Moshi: Yanayojiri katika Kongamano la BAWACHA Siku ya Wanawake Duniani Machi 3, 2023; Rais Samia mgeni rasmi

Ni Asubuhi tulivu siku ya Jumatano tarehe 8 March ikiwa ni kilele Cha Siku ya Wanawake Duniani.

Macho na masikio ya Watanzania leo yanaelekezwa katika mji maarufu wa Moshi mkoani Kilimanjaro.

Chama kikuu Cha Chadema chenye wafuasi takribani Milioni 10 nchini kupitia Baraza lake la Wanawake Bawacha linafanya Kongamano kubwa la kuadhimisha siku hii ya Wanawake Kitaifa katika Ukumbi wa KURINGE.

Kinachovutia kwenye Kongamano hili la Bawacha mwaka huu ni mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ambaye atakuwa mgeni Rasmi kwenye Kongamano hilo.

Kukubali kwa Rais Samia Suluhu Hassan kuwa mgeni Rasmi kwenye Kongamano la Chadema kumevuta hisia za mamilioni ya Watanzania na hata Jamii ya Kimataifa.

Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe ndiye atakayekuwa mwenyeji wa Rais Samia na anatarajia kumpokea kuanzia saa 3 asubuhi.

Rais Samia kuhutubia Jukwaa moja na Chama kikuu Cha Upinzani Chadema kinaonyesha kilele Cha mafanikio ya Maridhiano ya kisiasa yaliyoasisiwa na Rais pamoja na Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe.

Rais Samia Suluhu Hassan amesikika mara kadhaa akitangaza hadharani kwamba wapinzani nchini siyo maadui wake tofauti na mtangulizi wake John Magufuli aliyejiapiza kuangamiza upinzani nchini na hatimaye kuuvuruga uchaguzi mkuu wa mwaka 2020

Mji wa Moshi ambao ni Kati ya ngome kuu za Chadema nchini umepambwa na bendera nyingi za chama hicho kikuu Cha Upinzani huku mazungumzo katika mikusanyiko mbalimbali ikiwa ni tukio hili la kihistoria.

Molemo Media tunatarajia kuwaletea mubashara matukio yote muhimu yatakayoendelea hapa ukumbini mjini Moshi kabla na wakati wa Kongamano hilo

Karibuni Sana
Tuko tayari makada woote wa ccm na chadema Mh Molemo.
 
sisi washabiki wa vyama tunapaswa tutambue na tuelewe kuwa siasa sio uadui wala kuchukiana.

RAIS Dr. Samia ni Rais wa watanzania wote bila kujali unachama au huna
Hakika Rais anaonyesha demokrasia ya kweli kwa vitendo hivyo hatuna budi kufuata nyayo zake, haswa kwa viongozi wa vyama vya upinzani,
Ukionyeshwa wema tenda wema tuache unafiki.
Wacha ikae hivyo hivyo Ndugu Zendrano
 
Mama yetu mpendwa akianza kuhutubia mni-tag. Asante mama wa taifa kwa kutufundisha upendo

 
Hizi kura za hawa wanachama huwa zinakwendaga wapi?!.

Ni ulikuwa ngome enzi zile, sasa Chadema haina tena mbunge hata mmoja!, hii ni ngome gani?.
P
Wewe mwenyewe unafahamu ni kwanini hawana Mbunge hata mmoja.
 
I'm sure Mbowe anaenda kutamgaza chama kuwasamehe wale wabunge walio kengeuka.
Kisha atamponda sana Rais wa awamu iliyopita na Spika, alafu atamalizia kumsifia mama na kisha kutangaza kwamba siasa za chuki zimekwisha.
hao mtawasamehe uvccm.
 
Msije kutuambia mme wasamehe covid 19. Hawa ni wezi, wa kuaminika. Msimamo wa chama uendelee kubaki kuwa hamtambui ubunge wao.
 
Hizi kura za hawa wanachama huwa zinakwendaga wapi?!.

Ni ulikuwa ngome enzi zile, sasa Chadema haina tena mbunge hata mmoja!, hii ni ngome gani?.
P
Sitakujibu maana unauliza kwa kunijaribu

Kwa akili yako ya kawaida tu kulikuwa na uchaguzi 2020? Au unazungumzia uharamia wa Rafiki yako aliyetangulia mbele ya haki?
 
Mitaa ya Moshi imefulika wakina mama wa chadema kutoka kona mbalimbali za nchi
IMG-20230308-WA0015.jpg
IMG-20230308-WA0014.jpg
IMG-20230308-WA0013.jpg
 
Video wamama wa chadema wakiwa na shangwe siku ya wanawake duniani
 
Back
Top Bottom