Movement: Tunataka Katiba Mpya Tanzania

Movement: Tunataka Katiba Mpya Tanzania

Jamani CHADEMA kama wanahitaji suport ya wananchi waseme tu sie tunasubiri kauli yao tu.
 
Safi sana, Walidhani wanaweza kufukiafukia madudu yao??
Sasa ulimwengu mzima unajua jinsi walivyochakachua, Na bado!!!
 
WAKUU HESHIMA MBELE.
Kwa heshima zote nawaombeni kama kuna mkuu yeyote mwenye KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA kwa mfumo wa kieletroniki anisaidie kuipata kupitia uwanja wetu wa GREAT THINKERS. Natanguliza shukrani.
 
WAKUU HESHIMA MBELE.
Kwa heshima zote nawaombeni kama kuna mkuu yeyote mwenye KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA kwa mfumo wa kieletroniki anisaidie kuipata kupitia uwanja wetu wa GREAT THINKERS. Natanguliza shukrani.

Sina link ila nina copy itakufafaa mkuu?
 
WAKUU HESHIMA MBELE.
Kwa heshima zote nawaombeni kama kuna mkuu yeyote mwenye KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA kwa mfumo wa kieletroniki anisaidie kuipata kupitia uwanja wetu wa GREAT THINKERS. Natanguliza shukrani.

Na wewe uisambaze kadiri utakavyoweza ama kwa kui-print au ku-forward kama email kwani ni mali ya kila mtanzania.
 
The search engine function of the world wide web is very useful, and they say Google is your friend. Google

Ukizoea kuomba sana hata hiyo link utatuambia huwezi kufungua, au ukaomba kusomewa.
 
sina link ila nina copy itakufafaa mkuu?
wakuu wote heshima mbele.

Nawashukuru wote mliofanikisha maelekezo ya kupata katiba ya jamhuri ya muungano wa tanzania. Nawashukuru sana sana. Na tayari nimesharudufu nakala kumi na kuwapa watanzania wengine ambao walikuwa wanahitaji. Nawashukuru sana, licha ya baadhi ya wana jamvi wengine kunikebehi. Wakuu woooooteeeeeeeeee asanteni.

Nawasilisha.
 
Jamani soft copy ya katiba yetu hiyo hapo! Akina Jayfour mnaulizia katiba muidownload. Naiweka kama attachment
 
Ninaamini katiba iliyopo ilitungwa zamani, Hivyo ni dhahiri kwamba hata baadhi ya mambo yaliyopo ndani yake hayawezi work effectively kwa kizazi hiki.Ndio maana nchi nyingi dunianizilikwisha badili katiba zao.Kwa hiyo ni
vema wadau tukajulishana baadhi ya mambo ili nikajua na watu wote wakajua ili tuone/waone kama kuna umuhimu wa reconstruct au tuache hii iendelee.
 
Katiba lazima ibadilike, mfano inasema nchi hii ni ya ujamaa na kujitegema, je ni kweli badu sisi ni wajamaa, au wabepari wa kutupwa ??:embarrassed:
 
Suala la umhimu wa kuwa na Katiba mpya naliunga mkono. ila kwamba vyama vya upinzani wanajiandaa kuandika rasmi ya katiba mpya linanitia shaka kidogo. Hii ina maana vyama vya upinzani wanataka kuleta katiba mbadala ambayo kwa maoni yao ni nzuri kuliko iliyopo? Rasmi hiyo ya katiba ya vyama vya upinzani itakuwa katika sura gani? Itawakilisha maslahi ya kisiasa ya vyama vya upinzani au maslahi ya watu? Kama vyama vya upinzani wameshindwa kukaa pamoja na kuunda kambi ya upinzani bungeni wataweza kukaa pamoja na kuandika rasmu ya katiba itakayo kubalika kwa vyama vyote vya upinzani achilia mbali watu wote?

Kwa maoni yangu suala la mabadiliko ya katiba ni suala la watu wote. Linahitaji kuwashilikisha watu wote ili kuweza kupata maoni yao ya namna wanavyotaka katiba yetu iwe. Na kama tunataka mabadiliko ya Katiba yenye manufaa ya kudumu kwa Taifa letu tukubali kwamba suala hilo linahitaji muda wa kutosha sio la kuharakisha tu. Awali ya yote, wananchi ambao wengi wetu hatujui katiba ni nini na katiba yetu ya sasa hivi ikoje tunapaswa kupewa elimu ya kutosha ya katiba na uraia kabla hatujatakiwa kutoa maoni yetu juu ya mabadiliko ya katiba. Nionavyo mimi, ili wananchi tuwe katika nafasi nzuri kuyabainisha mapungifu ama mazuri yaliyomo katika katiba yetu tunapaswa kuwa na ufahamu kiasi kuhusiana na katiba. Vinginevyo, wengi kati yetu tunaweza kufata mkumbo bila kujua tunafanya mabadiliko gani na kwa sababu gani?

Ni ukweli usiopingwa kwa wale wenye ufahamu kwamba katiba yetu inayo mapungufu ya msingi na ya kawaida. Jambo la kujadili baada ya kuwapa mwanga wananchi juu ya katiba ni namna mapungufu katika katiba yetu yanavyoweza kuondolewa ima kwa kuifuta katiba iliyopo na kuandika katiba mpya au kuifanyia marekebisho ya msingi. Yoyote kati njia hizi inaweza kutumika ili mradi wananchi wanashirikishwa vya kutosha ili kuwafanya waione katiba kama zao lao na sio zao la viongozi wa kisiasa. Hilo litawafanya wananchi kuipa hadhi katiba inayofaa zaidi na kuyaheshimu na kuwa tayari kuyatetea yaliyomo katika katiba kwa kuwa yanatokana na wao.

Ni wazi kabisa kutokana na historia ya nchi kwamba ushirikishwaji wa wananchi katika uandikaji na urekebishaji wa katiba tuliyo nayo ulikuwa mdogo sana. Bila shaka hilo lilichangiwa pia na uchanga wetu wa demokrasia pamoja na mambo mengine.

Kutoshirikishwa kwa wananchi katika utungwaji wa katiba toka mwanzo kumeifanya nafasi ya wananchi katika maamuzi kuishia zaidi katika kuchagua viongozi. Marekebisho ya katiba bila kujali ni vifungu gani yamebaki kwa wabunge kwa taratibu mbalimbali kulingana na vifungu vya katiba vinavyotaka kubadilishwa. Kutokana na katiba iliyopo wabunge wana uwezo hata wa kuamua kujiongezea muda wao wa kuwa bungeni kutoka miaka mitano hata kumi au zaidi. Nani atawazuia kama kura zao zikitosha? Kwa maoni yangu, ilikuwa ni mhimu kuwa na vifungu katika katiba ambavyo haviwezi kurekebishwa bila kuwa na maoni ya wananchi. Vifungu kama vya ukomo wa bunge, ukomo wa ofisi ya raisi, haki za msingi za binaadamu, uhusiano wa mihimili mitatu ya dola, usekula wa dola yetu, mfumo wa vyama vingi, muungano, tume huru ya uchaguzi yawe ni baadhi ya mambo ambayo hayawezi kurekebishwa bila kuwepo referandum.

Mabadiliko katika masuala hayo yanaweza kufanyika kwa marekebisho au kutunga katiba mpya. Mhimu ni kwamba hayo mamabo yawemo katika katiba na mamlaka ya wananchi yawekwe wazi na kupewa nguvu za kisheria. Kwa sasa mamlaka ya wanachi katika maamuzi yanatamkwa tu kinadhalia katika ibara ya 8 ya katiba ambayo inaangukia katika Maelekezo ya Sera za Dola ambayo kitaalamu hayana nguvu za kisheria wala hayawezi kutekelezeka mahakamani.

Masuala mengine ya msingi ambayo yanapaswa kutizamwa vizuri ni haki ya kumiliki mali na kunufaika katika rasilimali za taifa. Hilo linahitaji maoni mengi kutoka kwa wananchi na ulinzi makini wa kikatiba.

Kuna hili suala la matokeo ya uchaguzi kupingwa mahakamani. Suala hilo lilizua mjadala mzito wakati tunaingia katika mfumo wa vyama vingi. Ni vizuri wananchi wakajulishwa mazuri na mabaya ya kuwepo kwa haki hiyo. Kwa maoni yangu binafsi suala la matokeo ya uchaguzi wa raisi kutopingwa mahakamani lingebaki hivyo hivyo ila nguvu zaidi zikapelekwa katika kuifanya tume ya uchaguzi na utaratibu wa kutangaza matokeo ya uraisi kuwa huru zaidi. Angalia kilichotokea Ivory Coast ambako haki hiyo imetamkwa katika katiba.

Mabadiliko ya katiba yasifanyike kwa njia ya zima moto. Tunaweza kuandika katiba mpya kwa kipindi kifupi na ikawa haina tofauti na hii tuliyonayo. Wananchi wanapaswa kuandaliwa, kuelimishwa na kushilikishwa vya kutosha katika mabadiliko ya katiba. Washiriki bila kuwa na upendeleo wa maslahi yao binafsi ya kivyama vya siasa wala ya kidini bali watizame maslahi ya kitaifa.


Yapo mengi ya kuchangia lakini ningependa kusikia kwa wengine pia.
 
Kwa maoni yangu.
Tunahitaji elimu zaidi kwenda kwa wananchi,hasa kwa kupitia nakala ya katiba iliyopo nakuelezea mapungufu yaliyopo.Wengi wetu Katiba iliyopo hata kuiona kwa macho bado, sembuze kuisoma.Inafaa zaidi nakala za katiba iliyopo kusambazwa nchi nzima kadri inavyowezekana na kama inawezekana itolewe bure.
Kuna mambo mengi kwenye katiba iliyopo ambayo bila kuyapitia kipengele kwa kipengele tutakuwa tunafanya kosa kubwa katika kujenga hoja ya ubovu wa Katiba yenyewe.
Mimi na anzaa;
1.MISINGI YA KATIBA​
Sheria ya 1984
Na.15 ib.3​
KWA KUWA​
SISI Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania tumeamua rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi
yetu jamii inayozingatia misingi ya uhuru, haki, udugu na

amani:
KWA HIYO, BASI, KATIBA HII IMETUNGWA NA BUNGE
MAALUM LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA,
kwa niaba ya Wananchi, kwa madhumuni ya kujenga jamii
kama hiyo, na pia kwa ajili ya kuhakikisha kwamba Tanzania
inaongozwa na Serikali yenye kufuata misingi ya demokrasia​
na ujamaa.

Sheria ya 1992
Na.4 ib.3​
2.​
-(1) Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la
Tanzania Bara na eneo lote la Tanzania Zanzibar, na ni
pamoja na sehemu yake ya bahari ambayo Tanzania
inapakana nayo.
(2) Kwa ajili ya utekelezaji bora wa shughuli za Serikali
ya Jamhuri ya Muungano au Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar, Rais aweza kuigawa Jamhuri ya Muungano katika
mikoa, wilaya na maeneo mengineyo, kwa kufuata utaratibu
uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria iliyotungwa na
Bunge:
Isipokuwa kwamba Rais atashauriana kwanza na Rais
wa Zanzibar kabla ya kuigawa Tanzania Zanzibar katika
Mikoa, Wilaya au maeneo mengineyo.

Hapo juu kwenye nyekundu utaona tayari kuna mapungufu,JMT imeundwa na nini ,wabunge wamepata wapi mamlaka ya kuwatungia wananchi katiba na Serikali ndani ya Serikali inatoka wapi (Serikali ya Zanzibar)?.
Ukisoma Katiba kipengele kwa kipengele utagundua kuwa 60% ya katiba nzima inafaa isiwepo kabisa.

Wana Jf kwa maoni yangu bado hatujachelewa tutafufe namna nzuri ya kupitia Katiba mzima wakati huo huo tukianza Mchakato wa Rasimu ya Katiba Mpya.
Naelewa kabisa kuna watu wanadai kazi hii lazima ifanywe na wataalamu wa Sheria tunasema sawa, lakini kazi yao itakuwa katika hatua fulani fulani,maana mawazo ya nini sisi wananchi tunataka hayawezi kubebwa na kundi fulani kama tunavyoona hapo juu jinsi wa Bunge wa wakati huo walivyo tutwisha mzigo huu wa katiba mbovu.


 
Toleo hili la Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ya Mwaka 1977,
limezingatia na kuweka pamoja mabadiliko yote yaliyofanywa katika Katiba
ya Muungano tangu ilipotungwa mwaka 1977 hadi tarehe 30 Aprili, 2000.

Dar es Salaam,
A.J. CHENGE
1 Novemba, 2000

hii sio katiba iliyo in force sasa hivi, ni ya zamani.

katiba ya mwisho ni version yenye amendments za 2005

tukijadili Katiba tuanze na kuwa na Katiba
 
Back
Top Bottom