Movement: Tunataka Katiba Mpya Tanzania

Movement: Tunataka Katiba Mpya Tanzania

Serikali ni watu na nahofia neno wananchi labda ungetumia neno umma. Ipo tofauti kati ya maneno umma na wananchi. Neno wananchi linaingia moja kwa moja kama mmiliki wa nchi na rasilimali zake. Umma unajumuisha asasi zote za kiraia, watawala na watawaliwa, walemavu na wasio walemavu, mashirika binafsi na yale ya serikali, dini zote na vyama vyote vya siasa vyenye usajili na visivyo na usajili. Unaposema serikali ni wananchi kupitia bunge, mimi nadhani si sahihi kwa kuwa huu ni mgawanyo wa madaraka uliopo katika mihimili yetu mitatu ya uongozi nchini. Katika mchakato huu wa katiba mpya, bunge lina nafasi yake katika kufanya maamuzi, watawala wana sehemu yao, vile vile mahakama nayo ina nafasi yake.

Lengo la mchakato tunataka kuwa na katiba inayotaja mambo yote,toa uhuru kati ya mihimili yetu 3 na umma uachiewe uwe na maamuzi ya mwisho juu ya muundo wa katiba. Tatizo lililopo ni pale serikali inapotaka kuhodhi madaraka yote kikatiba au katiba ile kuwa muundo wa kutetea chama au kikundi Fulani cha watu au kumpa mtu Fulani madaraka na mamlaka zaidi. Hapa tutakuwa tunaingia kwenye utawala wa kifalme au tunamfanya mtu Fulani kuwa dikteta.

Tatizo linacholewesha maendeleo Tanzania ni kuwa hatuna committed leaders ambao wanaingia madarakani kwa ajili ya kutumikia umma wa mtanzania. Tulionao kwa kipindi cha miaka taklibani 50 ni wale wenye kujali matumbo yao binafsi, mtanzania baadaye. Japo wengi huthibitika bado tuna mfumo ule wa kuleana au kikingiana kifua, na hii ndiyo inayofanya maendeleo yaonekane kama agenda isiyowezekana.

Viongozi wetu wanasafiri kwa dhana ya kutanua na kuficha mali nje tu na si kujifunza toka kwa mataifa yaliyoendelea. Ipo haja ya madaraka ya rais kupunguzwa katika katiba yetu ijayo na ipo haja pia ya kuwa na serikali tatu ambazo lazima zilindwe kwa mujibu wa katiba.
 
Nimeisoma vizuri na kwa makini kabisa katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na nimeielewa vyema ipasavyo. Hakika hii si katiba inayowafaa wananchi wa Tanzania katika karne hii ya 21. Ina mambo mengi ya upotofu na udanganyifu wa hali ya juu na kwa hivyo inapaswa kurekebishwa kama si kutungwa kwa katiba mpya
 
Ndugu Wanajamii Wasomi na Wasiowasomi,Salam,

Mimi kwa hili lakuhitaji Katiba Mpya naliunga Mkono mia kwa mia,Lakini tatizo langu kwa wasomi wengi hapa Tanzania ni waoga sana,Kwa upande mwingine wapo upande wa Serikali,ndio maana wanashindwa kutoa maoni na mwongozo wa jinsi ya kuunda Katiba.Kwa nini ninasema hivyo hawa jamaa muda wao mwingi wanakua katika kuandika machapisho mbali mbali,kwa hiyo nilidhani hawa wangekuwa mstari wa mbele kudai Katiba mpya,lakini hoja ya katiba mpya ilitoka kwa vyama vya upinzani,baada ya kushiriki kwenye chaguzi mbali mbali na kugundua kuwa kushindwa kwao tatizo ni Katiba,napenda kuuliza hawa Wasomi walikuwa hawalioni hilo siku zote,au ni woga wa kupoteza ajira,Ninasema sio wasomi wote waoga,lakini wengi wetu tunaogopa vyombo vya dola hata katika kutoa hoja zetu.

Kwa hiyo hawa wasomi wanatakiwa wakatoe elimu ya uraia kule vijijini na sio tu kujificha kwenye makongamano kwenye vyuo vikuu,Na kama utakumbuka hawa wanachuo hata mwaka jana kwenye uchaguzi mkuu hawakupiga kura,Na waalimu wao hawa kuwatetea,kuwa ile ilikuwa ni haki yao ya Kikatiba,Mimi hili linanipa wasiwasi juu ya Wasomi wetu,Mimi kwa uelewa wangu Chuo Kikuu ni Sehemu huru ya kutoa mawazo,kukosoa serikali,kuishauri kwa kupitia tafiti ambazo zina majibu yaliyofanyiwa uchambuzi wa kisayansi.Na kuwaelimisha wananchi wa vijijini ambao hata hawajawahi kuiona Katiba licha ya Kuisoma,waulize ni wanachuo wangapi waliokuwa wanajua Katiba Miaka kumi nyuma kabla ya Hoja hii kuingia.Kwa hiyo ni makundi yote yanatakiwa kudai katiba Mpya.

Lakini kuna Makundi yanatakiwa kuongoza umma na kuuelimisha,Wenzetu Kenya walienda kuelimisha wananchi Kaya hadi kaya.Na sio kujicha kwenye vioyoyozi eti unadai Katiba.No easy Tasks by Nelson Mandela.
 
Senior member,mchango wako ni mzuri lakini umesahau kwamba mikataba mibovu ktk nchi hii haikuanzia wakati wa serikali ya awamu ya 4, ila nimuendelezo wa serikali awamu wa tatu,kwa kufuata na kuzingatia matakwa ya IMF na WB(SAP) bila kujali na kuzingatia maslahi ya watanzania,ndipo hapo serkali ya awamu ya 4 ikamua kufanya marekebisha na kuangalia upya mfumo wa uakezaji kwa kurekebisha mirahaba chini ya tume ya rais iliongozwa na naibu katibu mkuu chadem na mbunge Kgm kaskazini.

Kimsingi mi sio msemaji wa serikali lakini lengo langu nikutaka kuweka wazi ukweli mbele ya watanzania wenzangu. Sasa nini kifanyike ili kuondoa dhuluma hii,moja tutoe mapendekezo muafaka wakati utakapofika kupendekeza katiba mpya, pili watanzania tumepewa dhamana mikononi mwetu ya kuchagua chama na watu watakaye tufaa kuongoza vita hivi mwisho tusipige kura kwa maslahi ya udini,ukabila,umaeneo na pesa au aina yeyote ya ubaguzi.
 
Mimi nafikiri tatizo ni letu sisi wananchi,
1. Tuko waoga tunaogopa CCM na dola yake, kama tunajua maovu yanayotendeka kwa nini tusiandamane hadi kikaeleweka? Ikiwa kundi dogo tu la wanafunzi wa vyuo wanaweza kuleta changes kwa migomo itakuwa nchi nzima? Lets wake up
2.
 
Ni vizuri kwa mitazamo yenu wanajamii lkn kwa nini kila kitu ni vigumu kukipata Tz na ni nani aliyetupandia hofu Wa Tz ? Mm nafikiri ni sahihi kabisa kuwa wale waliotoa masomo ya siasa, uraia, pamoja na sheria kuanzia chini ndio wenye makosa kwa sababu watu hatujiamin tunacho kidai na hao wachache ndio wanaojua kinachoendea ndo wanaopiga kelele na mpaka wa Tz tuelewe ni mda sana na kwa sababu wa Tz wengi tatizo liko kwenye ubongo ni tatizo sana
 
kuwe na kikomo cha umiliki wa ardhi kwenye katiba..............miaka ya karibuni tumekuwa tukiona watu hasa wenye nafasi na madaraka serikalini,na wenye uwezo wa kifedha wakijilimbikizia ardhi kubwa ambayo wakati mwingine hata huwa hawaitumii kitu ambacho kinasababisha migogoro ya ardhi,kwani ardhi yote yenye rutuba imetwaliwa na watu hao,wazawa wakiacha bila ardhi kwa kisingizio cha kutokuwa na hati.
 
Kuwe na maelekezo rasmi ya madaraka na mamlaka ambayo yule atakaekaimu nafasi ya rais anakua nayo pindi rais anapokua nje ya nchi.

Hili nalisema kutokana na mkanganyiko uliotokea pale rais aliposubiriwa kutoa maamuzi juu ya Jairo ilhali kulikua na mtu ameachiwa ukaimu.
 
Capitalism is not the best way to organise our society. It is an oppressive system which is seen as normal but in reality is very unfair. Like now look at how much the CEO of TANESCO in an year then look at what the poor labourer on the street earns and finally look at how much there are willing to charge customers it is so unfair.

The worst thing about capitalism is individualism because it fragments the social relationships and leads to a lot of mental health problems! How many jails the west created before the realised money is not everything?

We should create our system better than capitalism by blending in the various systems such as communism and socialism and also we should be creative to come up with original systems. I believe we can do far much better than the west.
 
Tunachohitaji sisi walalahoi ni mabadiliko ya katiba ambayo yatatuwezesha kuwashitaki mahakamani wezi na wahujumu uchumi wetu wote bila kujali sura ya mtu wala madaraka aliyonayo.
 
Capitalism is not the best way to organise our society. It is an oppressive system which is seen as normal but in reality is very unfair. Like now look at how much the CEO of TANESCO in an year then look at what the poor labourer on the street earns and finally look at how much there are willing to charge customers it is so unfair.

The worst thing about capitalism is individualism because it fragments the social relationships and leads to a lot of mental health problems! How many jails the west created before the realised money is not everything?

We should create our system better than capitalism by blending in the various systems such as communism and socialism and also we should be creative to come up with original systems. I believe we can do far much better than the west.

Lakini kuna hii bias watanzania tukiwaangalia westerners... In their totality European countries are more extreme to socialism than are to the capitalism. Most of their public services are subsdiesed wakati huo huo sisi kila siku tunasema westerners in generocity.

Who are these westerners je America na Uk ndiyo ambao wana create hii bias tunayojipa? Hakuna uchumi/serikali duniani ambayo iko pure capitalist ila extremes zina vary kutoka moja kwenda nyingine na kwa ujumla serikali nyingi duniani ni more extreme to the socalism scale than to capitalism with quite few of them ambo capitalism ni dominant system.
 
Lakini kuna hii bias watanzania tukiwaangalia westerners... In their totality European countries are more extreme to socialism than are to the capitalism. Most of their public services are subsdiesed wakati huo huo sisi kila siku tunasema westerners in generocity. Who are these westerners je America na Uk ndiyo ambao wana create hii bias tunayojipa? Hakuna uchumi/serikali duniani ambayo iko pure capitalist ila extremes zina vary kutoka moja kwenda nyingine na kwa ujumla serikali nyingi duniani ni more extreme to the socalism scale than to capitalism with quite few of them ambo capitalism ni dominant system.

Mkuu nimekusoma vizuri ok, let us say now that Tanzanians are up in arms about wanting a new constitution, I am just wondering if they know what exactly they want written down. I think it would be prudent to know what was in the old one first and identify the issues that caused it to fail, and then decide what ammendments to make otherwise we Tanzanians might be duped by some know-it-all politicians who labour for their stomachs day in and day out and are only interested to push for ammendments that would empower them even more and enable them to rob Tanzania blind!

My people are destroyed for lack of knowledge
Hosea 4:6
 
  • Thanks
Reactions: Ame
As a keen student of history I can testify to you all that constitution making in any country is not as easy as many of you seem to think. Many great countries have had to go through the shenanigans and commotion we are now expriencing in our dear country. Some countries have had to go through bloody revolutions and civil wars to get that most important document that establishes the foundation and source of the legal authority.

If the proposed draft in Tanzania didn't have any opposition I would be very very worried. We need such healthy debate on such an important document that will be used for many generations to come. No constitution in any country is ever perfect, even the US one that was adopted in 1787 was never perfect and has been amended 27 times. The French one which was adopted in 1958 has been amended 18 times.

Tanzania is at the moment ahead in Africa when it comes to making its own constitution since nearly all African countries still have colonial laws. So if this current referendum goes through it may usher in a wind of change in the continent. Let us appreciate what is going on in Tanzania, these are truly monumental times in our country. Whether you like it or not, let's all have healthy and productive debates, without some in here being insultive or over emotional. What we do this year will be the bench mark for ever lasting peace and development in our great country. WE ARE ALL IN THE RIGHT SIDE OF HISTORY.
 
Sababu kuu za msingi kwa Tanzania kuondokana na katiba ya sasa na kuundwa katiba mpya si kupinga mamlaka aliyonayo Raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Pekee bali ni kutaka kuondoa kabisa katiba ya sasa inayoshabihiana na ukandamizaji wa Demokrasia Nchini.

Tanzania hadi leo haitambuliki kama ni nchi ya kibepari au ya comunisti kutokana na misingi ya katiba iliyopo. Tunachokiamini wengi ni kuwa Tanzania ni Nchi ya Kijamaa jambo ambalo halipo kwa sasa.

Vijiji vilivyoundwa kwa misingi ya Kijamaa, sasahivi ni maeneo ambayo yanafanyiwa vitendo vya kikatili. Leo hii tunaambiwa mtu yeyote hana haki ya kukampeni juu ya mswada wa sheria ya Kuunda tume itakayosimamia ukusanyji maoni kwa ajili ya kuundwa katiba mpya, je Usiri huo una maana gani kwa watu wengi wasiokuwa wabunge?

:lock1:Hapa kunadalili zote kuwapo kwa uvunjifu wa uhuru na Haki kwa Watanzania (tumefungwa).:lock1:
 
Me nafukiri huu mjadala wa katiba unge kaa kwa wana nchi,waelimishwe vya kutosha haswa kama DAWA MSETO YA MALERIA AU MATANGAZO YA MITANDAO YA CMU na cyo ku uparaza kama chai ya rangi!!!
Me naona chenga tupu chadema nao cjui walipewa juice wakalewa wakaruhus jamaa aka mwaga wino!!!
 
Hello, Mimi ni mgeni kwenye forum hii ila ni raia wa Tanzania. Kwa umuhimu wa topic hii ninaomba kuwasilisha mawazo yangu. Jambo ambalo ninaomba wadau tujadili kuhusu Katiba mpya ni mfumo wa uchumi ambao Katiba yetu tunayoitaka iuainishe.

Katiba ya sasa ina ruhusu Mfumo wa Uzalishaji wa Kijamaa. Nina dhani tuna haja ya kujadili kwa kina juu ya mfumo wa uzalishaji mali kwanza kabla ya kuangalia vipengele vingine kwa sababu mahusiano ya kiuchumi katika jamii ndiyo yanayopangilia mahusiano maengine katika jamii. Nionavyo mimi mfumo wa uzalishaji wa kijamaa hauakisi jamii tuliyonayo sasa.

Nawasilisha
 
Tutakapokubaliana juu ya mfumo wa uzalishaji tutajibu maswali kama kwanini mtu mmoja anaweza kumiliki mabilioni na mwingine chakula cha siku moja ni issue na nchi bado ikawa tulivu. ni falsafa rahisi tu.
 
Back
Top Bottom