Movement: Tunataka Katiba Mpya Tanzania

Movement: Tunataka Katiba Mpya Tanzania

Sasa nadhani umefika wakati muafaka kwa wananchi kuungana pamoja kuhakikisha kwamba Viongozi wetu na hasa hao wa CCM kuelewa kwamba wao ni waajiriwa!...

Kama kweli serikali ya CCM imefikia kukataa kwa kauli moja kuhusu KATIBA basi hakuna haja ya kuendelea na mijadala inayohusu mustakabali wa nchi yetu.
Vyama vya Upinzani kwa pomoja viungane na viandike barua nzito kwa vyombo vya kimataifa ambavyo mapema iwezekanavyo na watoe msimamao wao kuhusu Uchaguzi unaofuata. Bungeni kusiweko na amani tena bila serikali kubadilisha kauli hiyo na wala msidanganywe na uchache wenu bungeni ila mnaweza kukataa vikao vya Bunge kwa pamoja hadi kieleweke. Dunia nzima itawasikia hata kama mtakuwa watu wawili!...

Na wasikomee hapo ila waingie Mikoani hadi ktk vyuo vyetu vikuu kutoa hotuba zinazohusiana na mapungufu ya Katiba ya nchi. UMoja wao utasikilizwa na wananchi ambao wengi wao hawafahamu ni kitu gani hasa wapinzani wanakitaka. Wakumbuke tu kwamba kuhitaji katiba mpya hakueleweki kwa Watanzania walio wengi hasa wa vijijini ambao kwao maisha ni yao yanategemea rehma za Mungu.

Pasiwepo na lugha nyingine zaidi ya Katiba!..
 
Kitila acha bwana! Ruksa usimlinganishe na Mugabe kabisaa!Ni kweli alikuwa ni Rahisi (Rais)mwenye mamlaka kamili lakini alikuwa na ubavu huo wa kukataa kama Mugabe? Mtu ambaye ofisi 'takatifu' kama ile anaigeuza kijiwe cha wafanyabiashara na mashemeji anaweza kuwa na roho nya paka kama Mugabe? Sikatai anasifa za ziada kuliko wengi ndani ya CCM lakini kwenye suala hili NO.

Kwanza isiwe ni 'kuirekebisha' katiba kirasharasha tu! It is a major overhaul. Anatakiwa a reputable and respectected individual ambaye hana maslahi katika mchakato mzima wa kuibadili katiba hiyo; preferably awe na background ya law, especially constitutional law. Kama hakuna mtu kama huyo, watu kama Prof. Shivji anaweza kutufanyia kazi nzuri ya kusimamia zoezi hilo.
 
Mimi nasema yeyote yule ambaye hataonyesha upendeleo maalum kwa walio madarakani au CCM. Mwinyi, SAS na Warioba wote nawakubali. Tuwaombe watembelee Tanzania nzima kukusanya maoni ya Watanzania kuhusu katiba na kisha kuyakabidhi kwa walio madarakani hata kama hawakupata baraka zao katika hili. Lakini kama mnavyowajua viongozi wetu kama wasipopata go ahead toka kwa walio madarakani, basi wataingia mitini.
 
Nakubaliana na Overhaul ya Katiba, lakini naomba tufanye baada ya muda mzuri.

Kwa nini, kwa sababu nchi hii bwana kila siku kunatafutwa kitu cha kuwapa wanasiasa excuse;

East Africa Federation Fast track, ilikuwa mbinu ya kutu-derail Tanzania baada ya mkapa angalau kuirudisha kwenye mstari... sasa JK ndio anaanza kufahamu nchi vizuri mwataka kumtwisha mzigo mwingine,,, ili kesho na kesho kutwa aseme sijafanya hili na lile kwa sababu ya issue nzito ya kuangalia mambo ya katiba yanaendelea je...

Ukweli kuhusu the need for new constitution hilo liko wazi,,, lakini
1. Punguza munkari wa Maalim Seif na CUF Kwanza, maana msijetuletea mambo ya Rwanda hapa.
2. Tupeane timeframe nzuri, hatuhitaji kukimbia kwenye hili, si watani wetu pia yaliwashinda. a good timeframe is mandatory ili msiwaogopeshe waliokuwa na vitumbua jamani. sisi si ndio tutakuwa tayari ku-implement katiba mpya, wahakikishieni tu kwamba ninyi hamtaadhirika.
3. Wariomba is my first choice... asaidiwe na Jaji mkuu mstahafu. Na scholars watulivu...sio kama akina Senkondo Mvungi!!!


Naomba Kutoa hoja.

Kitila:
Ulishawahi kugombea UVCCM, naomba unijibu kaka? naona ulinikweba kwenye thread nyingine... ninakufuata hata huku kidali po! kidali po!!!!mpaka unijibu kaka!!!
 
Naliunga mkono hilo la vyama vya upinzani kuandika barua ya pamoja na kuipeleka katika vyombo vya habari vya kimataifa, IMF, UN, WB, na balozi za nchi za magharibi ili kuishinikiza sirikali katika kupata katiba mpya.

Pia ile article inayohusu kuwanyima wanahari uhuru wa kuandika kuhusu rushwa ipelekwe kote huko.

Watu wanaomba kistaarabu kwamba katiba yetu ina mapungufu mengi hivyo tuijadili na kuifanyia mabadiliko kwa faida ya Watanzania wote lakini wanene hawaoni umuhimu wa hilo.

Sasa ni kupeleka manung'uniko ya Watanzania katika vyombo vya kimataifa ambavyo labda vinaweza kuwashtua hawa jamaa kwamba wananchi hawaridhiki na mengi katika uongozi wenu ikiwemo la rushwa na katiba.

Inaelekea wakishinikizwa na vyombo hivyo basi huwa wanasikiliza. Si tunaona uundwaji wa tume ya kuchunguza kashfa ya BOT, usingefanyika bila IMF kutia sauti yake.
 
Katiba ina mapungufu? jibu ni Ndiyo!.. ja mapungufu hayo yanamdhuru nani zaidi na nani anafaidika nayo? Jibu, mapungufu yanawadhuru wapinzani zaidi na yanawanufaisha CCM zaidi. Now, kama CCM ndio wananufaika zaidi na Katiba iliyopo (pamoja na mapungufu yake) kwanini waamue kuibadilisha? Je, kwa mtazamo wao, kama nchi imeweza kwenda jinsi ilivyo sasa na Katiba iliyopo why change? Wapinzani wanapodai kuandikwa katiba mpya ni kwa sababu wanataka Katiba itakayowanufaisha wao na kuwajengea mazingira mazuri ya kuweza kushinda (licha ya kwamba wameweza kushinda majimbo kadhaa kupitia Katiba iliyopo). Hivyo wanapolalamika kuhusu Katiba CCM wanacheka kwa sababu wanauliza, yaani "tuwatengenezee mazingira ya wao kushinda, ili watuondoe madarakani?". Hapo ndipo tatizo lilipo.

Kwa maoni yangu ni mpaka suala la Katiba mpya lionekane katika mwanga wa kitaifa kwamba mabadiliko au Katiba mpya vitawafaa CCM na Wapinzani na kwa ujumla vitaifaa nchi yetu hapo ndipo tutaweza kuanza mjadala wa Katiba.

Nawapa Home Work:

Imagine mimi ni sehemu ya Kamati Kuu ya CCM ambao wamekuomba wewe uje uzungumze nao kuwaeleza kwanini nchi inahitaji Katiba Mpya, na kwanini Katiba hiyo mpya itamfaa kila mhusika na haitakuwa tailored kwa ajili ya wapinzani. Utasema nini kwetu? Convince the NEC why Tanzania (not opposition parties) need new Constitution?
 
Mabadiliko ya katiba ni haki ya wananchi wote. Kama viongozi wa serikali (CCM) hawataki kutupa haki yetu, basi itabidi tujichukulie. Ninadhani huu ni wakati muafaka wa kufanya hivyo.
 
Mbunge ni mtunga sheria na serikali ni mtekelezaji, mahakama pia ni mtekelezaji.

Serikali kwa makusudi inakwenda kinyume na maamuzi ya mahakama kwa sababu ina bunduki.

Serikali ya Tanzania iko juu ya Sheria, vivyo hivyo hii ina maana watendaji wote wa serikali wako juu ya sheria.

Maana yake ni hii waendao jela Tanzania kwa maamuzi ya mahakama ni walala hoi tu.


Serikali by Definition ni Legal entity inayojiendesha kwa sheria si kwa kujisikia.

Kwa uchungu kabisa kama kuchomwa mshale mbavuni nasema;

Serikali ya Tanzania inatekeleza maamuzi yake kwa kujisikia na si kwa sheria.

Tutafika tuendako?!
 
Mzee Mwanakijiji,

Ndugu yangu hawa jamaa wa nje hawajaisoma hiyo katiba yetu vizuri na kutazama vipengele ambavyo hawa Wapinzani wanavipigia kelele. Ukivitazama kwa makini vinawahusu wananchi moja kwa moja na hsa kuifanya serikali yetu kuwa - Above the law!

Nimesoma report kibao ambazo wataalam wamezunguzia kuhusu bunge na mahakama zetu kutokuwa huru. Wamezungumzia mambo mengi mazito ambayo sisi kama tunataka kuendelea ni lazima tuyabadilishe ili mikakati yao iweze kufanya kazi lakini wameshindwa kuelewa kwamba, matatizo ya nchi yetu yameanzia kwenye katiba.

Nadhani unakumbuka wakati tulipokuwa tukijadili jinsi ya Tanzania kuondokana na Umaskini na kila mmoja wetu alikuja na Idea tofauti bila kuzingatia kwamba hayo yote ni hadithi ya tamthilia ikiwa katiba yenyewe ni tungo la Usanii ambalo lina Starring mmoja tu - CCM. Hao wengine ni majambazi co-Stars ambao siku zote watacheza nafasi zao.

Siku ambayo hawa jamaa watakuja soma na kutazama madai ya Wapinzani kwa pamoja na hasa vyama hivi vikubwa vinne, hayo madai yetu ya kuwepo kwa demokrasia watapigwa na Butaa... Na pengine wanaelewa isipokuwa wameacha wazi kwa sababu wananchi na vyama vya Upinzani wamekaa kimya! why bother ikiwa wananchi wenyewe wanaridhika.
Ujuwe demokrasia kwa akili ya Mdanganyika ni kuwepo kwa vyama vingi! kwa hiyo wanapoulizwa kuhusu demokrasia yetu wenyeji wengi watasema - Oooh Tanzania tuna vyama karibu ishirini na vyote hujiandikisha wakati wa kura!. That's all they wonna hear!..

Niamini kuna vipande kibao aliviweka J.J. Mnyika ktk ile mada ya Katiba, mimim hapa sikuweza kuamini maneno yale, nilifikiria kaongezea chunvi kidogo. Pamoja na shule yangu ya Madrasa ilikuwa shock kwangu na nikauliza kama kweli tunaipenda nchi yetu.
Katiba yetu bado kabisa imelenga kuboresha chama kimoja na viongozi wa chama hiki ni untouchables!...Wee hata wabunge wanaambiwa wakae kimya wasiulize swali linahusu kitu fulani?...why kwa sababu anayezungumza bungeni ni waziri mkuu na hao wabunge mawaziri ni waajiwa wake yaani hapa tumeshatoka bungeni.. who is the master!.
Ebu jiulize kweli naibu waziri anaweza kusimama bungeni na kudai hakuna mjadala wa Katiba na Spika wetu asiwe na nguvu ya kusema - wait a minute hakuna kitu hakiwezi kujadiliwa hapa hadi mimi nitakapo sema - NO!
 
Hawa mawaziri wanajiona wao ndio sheria, we ngoja tu iko siku watalipa ufedhuli wao.
 
Katiba ina mapungufu? jibu ni Ndiyo!.. ja mapungufu hayo yanamdhuru nani zaidi na nani anafaidika nayo? Jibu, mapungufu yanawadhuru wapinzani zaidi na yanawanufaisha CCM zaidi. Now, kama CCM ndio wananufaika zaidi na Katiba iliyopo (pamoja na mapungufu yake) kwanini waamue kuibadilisha? Je, kwa mtazamo wao, kama nchi imeweza kwenda jinsi ilivyo sasa na Katiba iliyopo why change? Wapinzani wanapodai kuandikwa katiba mpya ni kwa sababu wanataka Katiba itakayowanufaisha wao na kuwajengea mazingira mazuri ya kuweza kushinda (licha ya kwamba wameweza kushinda majimbo kadhaa kupitia Katiba iliyopo). Hivyo wanapolalamika kuhusu Katiba CCM wanacheka kwa sababu wanauliza, yaani "tuwatengenezee mazingira ya wao kushinda, ili watuondoe madarakani?". Hapo ndipo tatizo lilipo.

Kwa maoni yangu ni mpaka suala la Katiba mpya lionekane katika mwanga wa kitaifa kwamba mabadiliko au Katiba mpya vitawafaa CCM na Wapinzani na kwa ujumla vitaifaa nchi yetu hapo ndipo tutaweza kuanza mjadala wa Katiba.

Nawapa Home Work:

Imagine mimi ni sehemu ya Kamati Kuu ya CCM ambao wamekuomba wewe uje uzungumze nao kuwaeleza kwanini nchi inahitaji Katiba Mpya, na kwanini Katiba hiyo mpya itamfaa kila mhusika na haitakuwa tailored kwa ajili ya wapinzani. Utasema nini kwetu? Convince the NEC why Tanzania (not opposition parties) need new Constitution?

Mzee Mkjj
Mimi binafsi, dai langu la katiba mpya halipo polarised kama ulivyoliweka hapo juu: watawala versus upinzani. Badala yake nasema nataka katiba mpya itakayowawezesha wananchi kusikilizwa na kutekelezewa madai yao. Na wananchi hawa huwakilishwa na wabunge.

Naamini wewe, kama mimi, umeisoma katiba ya Tanzania. Sitanukuu vipengele. Lakini kwa ujumla wake rais/serikali(the executive branch) ana madaraka makubwa ya kupindukia. Mpaka bunge liko chini yake, hata mahakama. Hii ina maana wale wote walioko serikalini ndio wenye nchi hii; na sio wananchi, wanaowakilishwa na wabunge. Checks and balances hatuna katika katiba yetu.

Kwa nini serikali/CCM iandae katiba mpya, kama hii ya sasa inawafaa? (swali lako hapo juu). Jibu lake nadhani ni kwamba inawafaa wao kama chama kinachotawala at the expense of people's welfare. Kama wewe unaamini kwamba maendeleo ni watu(wananchi-centered); katiba yetu inaenda kinyume.....watawala's wishes centered.

Dai la katiba mpya lilitakiwa litoke kwa wananchi, liwe la kitaifa. Lakini ukiona hali halisi nchini.....walalahoi wengi hawawezi kuona uhusiano wa katiba iliyopo na ustawi wa demokrasia na maendeleo yao. Nyinyi wachache mliokuwa enlightened ndio mnaelewa hili. Kwa hivi ni sawa tu kwa wapinzani wakidai katiba mpya. Naamini ni kwa niaba ya wale wengi; na sio ubinafsi wao. Wao wadai katiba mpya; ila sio wao pekee waiandike. Uwakilishi kutoka kwa watanzania wote unahitajika.

Kwa kumalizia: wewe Mzee Mkjj kama upo NEC au CC ya CCM, na unahitaji usadikishwe juu ya hitaji la katiba mpya: Jibu lake ni checks and balances kwa maendeleo ya nchi: Viongozi wawajibike kwa wananchi. Wasipofanya hivyo, wawajibishwe.
 
Mimi sioni sababu za kukusanya maoni ndio kuchelewesha mambo, ni watu kuka wawe wanasiasa wastaafu, pamoja na Magwiji wa Sheria inatosha.
Kwa sababu vifungu vyenye utata vinaeleweka, au vilivyo wekwa ktk kudumaza Demokrasia vinajulikana.

Alternatively wanasiasa waje na vision yao na wanasheria waje na ya kwao zipigiwe kura basi. Katika Kamati Hizo wato wote waliopendekezwa hapo Juu Kama Alhaji Ali Hassan Mwinyi, SAS, Warioba, Shivji na Samatta ni Vizuri wawepo.
 
Inawezekana aliyekosea hapo mwanzo ameisha jirudi au alikosea wakati ule kwa sababu yeye mwenyewe alikuwa na maslahi na hiyo katiba mbovu.
 
Haki haotolewi kama sadaka, hupiganiwa.
Hata wakoloni hawakupenda kutupa Uhuru wetu, ni pressure dio iliowafanya wakubali.
so ni kazi kwetu kutoa hiyo pressure in different forms
 
Kila siku kwenye maisha yangu nikishindwa kumshawishi mtu kitu ambacho naamini kwa asilimia mia moja (100&#37😉 kwamba ni sawa, najiuliza maswahili haya:-

1. Je nimekifikisha/kiwasilisha kama kilivyotakiwa kiwe kwa maana niliongea au niliwasiliana (communication). hili ni muhimu sana mara nyingi tunalaumu wengine kumbe mbinu zetu za kuwasilisha ujumbe ndio dhaifu.
Kwa mfano njia nzuri zaidi (effective strategy) ya kuwasilisha ujumbe wa kupata katiba mpya ni kuwatumia kwa kuwaelimisha nia, madhumuni na namna ya kufanya ujumbe ufike kwa urahisi zaidi bila upinzani mkubwa kwa wale wenye mamlaka ya sheria (Bunge) na ki-halisia (CC, NEC ya CCM). Ukiweza kulifanya hili utakuwa umewasiliana, na sio umeongea tu na kupiga kelele...

2.Nimetumia mbinu kuhakikisha ninapata upinzani mdogo sana kutoka kwa wale ninaotaka wabadilike,,, ni muhimu kujua kwamba popote duniani na kwenye maisha yetu yakawaida binadamu wanaogopa changes... hii ipo kwenye makapuni na n.k... lakini (changes are inevitable) the issue is how do you make the changes,,, change will always be there in our life... (Kwa hiyo again) mbinu gani mmetumia kutuweza kufuta concern za hao wanaotaka kulindwa (CCM, Viongozi walioko madarakani etc.

Majumuisho:
Kwa maoni yangu basi, siitupii CCM mzigo yenyewe bali jamii ya scholars na pia vyama vya upinzania.
(a)Scholars:
Hawajatumia mbinu rahisi za kuwaelimisha wananchi, wadau na suspect wa kuadhirika na katiba mpya, ili kuwaeleza faida za katiba mpya kwa makundi yote.

(b)Vyama vya Upinzani:
we meant to believe wao ndio wazuri kuliko chama tawala, hata hivyo ni jambo lililowazi at least kwangu kwamba namna wanavyo-deliver/communicate kuhusu kubadili katiba kunawafanya wapate upinzani zaidi kuliko kuelekea kwenye suluhisho la kupata katiba yenyewe... kwa kuwa ukishatanguliza na neno ninyi wa chama tawala hamna akili sisi ndio twajua,,, umejijenga upinzania mwenyewe...

Mwisho:-
Tujifunze namna nzuri za ku-communicate ili hatimaye tuweze kufanikiwa kufikia malengo(objectives)

Mpaka leo naona mapungufu makubwa sana katika namna tunapoongelea kubalishwa kwa katiba kwa kuwa kila anayekuja anajifanya much know zaid...(JF) include na wale wanaobezwa wanasema balisha basi kama waweza!!!

Kwa maana nyingine kwa kutumia route ya vyama vya upinzani na strategy ninazoziona sasa,,, nadhani tutakesha, kwanza ndio wanawaamsha CCM waongeze kiraka kingine kwenye katiba, kuziba ufa kidogo kidogo; potential driver changers, should be scholars lakini sio wa mrengo wa kushoto kama akina Senkondo.

Mheshimiwa Moderator, sina nia ya kutoa shilingi lakini hata hivyo....

Mh. moderator naunga mkono hoja mia kwa mia...
 
Kilitime,

Mimi sidhani kama kuna haja kubwa ya kutafuta mbinu ya ku- communicate na mtu ama CCM ambayo ni chama cha wananchi. Hatuombi upya Uhuru wetu hapa kiasi kwamba inatakiwa tunanze somo Aalif kwa ujiti kujipanga kuomba Uhuru wetu.

CCM ni chama cha wananchi kilichoundwa na wananchi sio kwa sababu ya kubadilisha mtawala toka mtu mweupe kuwa mweusi. Hakuna njia ya mawasiliano zaidi ya Bunge letu na ikiwa wapo watu wanaoweza kulinyamazisha Bunge basi hapo hakuna haki tena wala mjadala wa Communication ndani ya nchi. CCM sio kundi fulani la watu watawala against wananchi hata kidogo na sidhani kama kuna sababu ya kutafuta kuwasiliana kama vile Hamas na Waisrael!

Samahani kidogo lakini sidhani kama kuna mtu humu anayesema hawa Wapinzani ni wazuri kuliko chama tawala... Hapana hakuna mtu anayesema wao ni wazuri lakini at least wao wameweza kuona Ubaya wa mwongozo wetu KATIBA na wameweza kuwakilisha madai haya panapohitajika!

Tatizo kubwa ni pale Mtawala anaposhindwa kuona mapungufu ndani ya sheria ya nchi kwa kutukuza Ubinafsi. Utaweza vipi kuzungumza na mtu ambaye kisha amini KUTAWALA watu badala ya KUWAONGOZA kuwa ndio njia pekee ya kudumisha Utawala wao.

Je, umeweza kujiuliza hasa nini malengo ya vyama vyetu nchini?..Na hasa pale CCM anaposema kuhakikisha Ushindi ktk chaguzi zake!

Statement hii ni scary thing bob kwa sababu chama kipo kuwakilisha wananchi na sio kuhakikisha Ushindi kwa njia zote. Hii dhahiri ina maanisha wao Kutawala ndio agenda ya kwanza ya chama na sio kuwakilisha wananchi wake kwa matakwa yatokanayo na wananchi.
 
Je, umeweza kujiuliza hasa nini malengo ya vyama vyetu nchini?..Na hasa pale CCM anaposema kuhakikisha Ushindi ktk chaguzi zake!

Tunarudi pale pale, je vyama vyote vya upinzani vinqvyosema hoja number moja ya kuungana kwa mfano ni ili kuitoa CCM madarakani,,, kwangu mimi it is also wrong and upuuzi mtu!!! I don't which party will be rulling and which will be in opposition side, what i care is is there enough opposition to make sure important thing are not passed while MPs are asleep in the assemply.

Ni a vyama vingi ni check and balance tu na kuhakikisha haki zinatendeka na makosa hayatokei, uharamia hautokei...

However in multiparty democracy at any time (t), there will be always a rulling party and opposition parties, so to me kusema nia ni kuiondoa CCM madarakani naona ni Upumbavu, though it should be a long run

They were just supposed to measure how many idea of theirs has been implemented and provided relieves or prosperity to the community period
 
Kila siku kwenye maisha yangu nikishindwa kumshawishi mtu kitu ambacho naamini kwa asilimia mia moja (100%) kwamba ni sawa, najiuliza maswahili haya:-

1. Je nimekifikisha/kiwasilisha kama kilivyotakiwa kiwe kwa maana niliongea au niliwasiliana (communication). hili ni muhimu sana mara nyingi tunalaumu wengine kumbe mbinu zetu za kuwasilisha ujumbe ndio dhaifu.
Kwa mfano njia nzuri zaidi (effective strategy) ya kuwasilisha ujumbe wa kupata katiba mpya ni kuwatumia kwa kuwaelimisha nia, madhumuni na namna ya kufanya ujumbe ufike kwa urahisi zaidi bila upinzani mkubwa kwa wale wenye mamlaka ya sheria (Bunge) na ki-halisia (CC, NEC ya CCM). Ukiweza kulifanya hili utakuwa umewasiliana, na sio umeongea tu na kupiga kelele...

2.Nimetumia mbinu kuhakikisha ninapata upinzani mdogo sana kutoka kwa wale ninaotaka wabadilike,,, ni muhimu kujua kwamba popote duniani na kwenye maisha yetu yakawaida binadamu wanaogopa changes... hii ipo kwenye makapuni na n.k... lakini (changes are inevitable) the issue is how do you make the changes,,, change will always be there in our life... (Kwa hiyo again) mbinu gani mmetumia kutuweza kufuta concern za hao wanaotaka kulindwa (CCM, Viongozi walioko madarakani etc.

Majumuisho:
Kwa maoni yangu basi, siitupii CCM mzigo yenyewe bali jamii ya scholars na pia vyama vya upinzania.
(a)Scholars:
Hawajatumia mbinu rahisi za kuwaelimisha wananchi, wadau na suspect wa kuadhirika na katiba mpya, ili kuwaeleza faida za katiba mpya kwa makundi yote.

(b)Vyama vya Upinzani:
we meant to believe wao ndio wazuri kuliko chama tawala, hata hivyo ni jambo lililowazi at least kwangu kwamba namna wanavyo-deliver/communicate kuhusu kubadili katiba kunawafanya wapate upinzani zaidi kuliko kuelekea kwenye suluhisho la kupata katiba yenyewe... kwa kuwa ukishatanguliza na neno ninyi wa chama tawala hamna akili sisi ndio twajua,,, umejijenga upinzania mwenyewe...

Mwisho:-
Tujifunze namna nzuri za ku-communicate ili hatimaye tuweze kufanikiwa kufikia malengo(objectives)

Mpaka leo naona mapungufu makubwa sana katika namna tunapoongelea kubalishwa kwa katiba kwa kuwa kila anayekuja anajifanya much know zaid...(JF) include na wale wanaobezwa wanasema balisha basi kama waweza!!!

Kwa maana nyingine kwa kutumia route ya vyama vya upinzani na strategy ninazoziona sasa,,, nadhani tutakesha, kwanza ndio wanawaamsha CCM waongeze kiraka kingine kwenye katiba, kuziba ufa kidogo kidogo; potential driver changers, should be scholars lakini sio wa mrengo wa kushoto kama akina Senkondo.

Mheshimiwa Moderator, sina nia ya kutoa shilingi lakini hata hivyo....

Mh. moderator naunga mkono hoja mia kwa mia...

Utatumia 'communication skills'kwa mtu aliyeweka pamba masikioni, sijui kama mta-communicate hapo! Lugha za mizungusho ndio zinazozidi kutudidimiza katika nyanja mbalimbali za kimaendeleo, hata katika mikataba yetu na mataifa au makampuni mbalimbali. Mtu unataka kusema "hapana" kwa jambo, badala yake unaanza ku-beat in the bush; why? Kama hutaki, mwambie mtu sitaki.

Kama katiba iliyopo haikidhi mahitaji yetu, ni kwa nini tuendelee kuzungushana na kubembelezana, eti kwa 'communication skills! Wewe unadhani wale waPalestina wale hawajui au hawana communication skills ya kuwasaidia? Wata-communicate hadi lyamba, hakuna kitakachotokea. Unatafuta anayekuonea huku akifaidi akuonee huruma? Hilo halitokei!
 
Kalamu,

Mapambano yoyote ni kutumia mbinu mbalimbali na ukitumia Akili zaidi unawini kama kumsukuma mlevi vile, kule kutumia makele kama yakina Mrema,

Mfano kama tungepigana vita ya Uganda tukifikiri tuko fit kwa maguruneti tungezidiwa lakini tulitumia mbinu tofauti,,, eventually tulishinda vita...

Lakini hatukushinda kumimina B52 kama za Bush kule Afghkanistan, that was my message
 
Back
Top Bottom