Hizo 1.5b aliingiza kwenye account yake binafsi au "alitohoa" matumizi?
Tofautisha ufisadi unaopigiwa kelele sasa na kubadilisha "mfumo" wa manunuzi ama matumizi lakini fedha zikawa zimefanya kazi zile zile za umma kwa mtindo mwingine.
Mimi niseme tu kwamba haitakuja kunitokea hata siku moja kum'rank' Magufuli tofauti, kwa maelezo yoyote mabaya anayozuliwa kwayo hivi sasa baada ya kifo chake.
Ujue, sababu kubwa hasa inayofanya watu kuanza kulalamika na kukufuru baada ya kifo chake ni zile tabia za kuleana zilizomo kwenye damu, wizi na janja janja walizozoea waTz.
Uhalifu ulishakuwa ni utamaduni wa jamii, ndiyo maana hata ufisadi unaofanywa sasa, hakuna anayeshangaa wala kujali.
Alivyofukuza watumishi wa umma wenye vyeti ghushi, viongozi wasiowajibika nk nk, tunajua hakuna ulimi wala vinywa vyao ama vya wahalifu wengine vinavyoweza kumsema vyema pamwe kutambua mchango wake mkubwa alioutoa kwa Taifa hili na kuacha alama za kudumu kwa kipindi chake kifupi.
Mwenyezi Mungu amuweke mahali pema peponi, amina.