Mpaka sasa uongozi wa Lissu na Heche umeshindwa kufanya mambo ya msingi yafuatayo

Mpaka sasa uongozi wa Lissu na Heche umeshindwa kufanya mambo ya msingi yafuatayo

Namba Tatu hapo ni suala lake binafsi halihusiani na nafasi yake ya uenyeketi wake, kwani aliwalazimisha mchangie, ndio maana huwa sichangii michango ya kijinga.
 
Sasa kama huyasomi inanihusu nini? Unapata faida gani kunijibu ili kuniambia tuu kuwa haunisomi? Mimi nilijua hausomi chochote ninachoandika. Kwa kweli nilifurahi kwa sababu nilijua utaniweka katika "ignore list" yako nisikuchoshe. Lakini sishangai, maana uko hapa unamtetea Lissu lakini hautaki kukubali kuwa unakipenda chama chake. Au na wewe ni follower wa Lissu, sio chama chake?
Btw naandika maneno mengi kwa sababu najua wengi ni wavivu wa kusoma.

Amandla...
Ukiandika kwa uchache hivi ninakusoma; ukiandika gazeti sisomi.
Kama unataka kujuwa mimi ni" follower" wa nani, jibu ni rahisi sana. Ni mfuasi wa TANZANIAmchana na usiku na siku zote za uhai wangu.
Kiongoz au chama chochote kikionyesha kuwa na maslahi kwa Tanzania, sina haya/aibu yoyote kukiunga mkono; kama nilivyo kuwa na matarajio na Bwana Mbowe wakati fulani kabla hajatekwa na ulaghai wa Samia. Sasa hivi matumaini yapo kwa CHADEMA, Lissu na viongozi wenzake. Lakini na wao wakionyesha dalili za kutetereka, hasa kuungana na kuikwamisha nchi, tutawaponda mawe vile vile kama wasaliti wa nchi yetu wengine wote.
 
mtoa mada naomba kuuliza pesa ya kukodisha bandari kwa warabuu. ipo. Wapi


Ennewei. Watu wametooa pesa. Kwa mapenzi. Yao binafsi. Kwa kiongozii wao so. Unapataje nguvu ya kuhoji

Alafu waulize ccm pesa ambayo hutolewa na jumuiya zake Za kumchangia samia pesa ya fomu huwa zinaendaga wapi?
 
Ukiandika kwa uchache hivi ninakusoma; ukiandika gazeti sisomi.
Kama unataka kujuwa mimi ni" follower" wa nani, jibu ni rahisi sana. Ni mfuasi wa TANZANIAmchana na usiku na siku zote za uhai wangu.
Kiongoz au chama chochote kikionyesha kuwa na maslahi kwa Tanzania, sina haya/aibu yoyote kukiunga mkono; kama nilivyo kuwa na matarajio na Bwana Mbowe wakati fulani kabla hajatekwa na ulaghai wa Samia. Sasa hivi matumaini yapo kwa CHADEMA, Lissu na viongozi wenzake. Lakini na wao wakionyesha dalili za kutetereka, hasa kuungana na kuikwamisha nchi, tutawaponda mawe vile vile kama wasaliti wa nchi yetu wengine wote.
Kwa vile sikuandikii wewe bora uni "ignore" kabisa. Nitaendelea kuandika ninavyotaka na sio unavyotaka.
Mtu uliyemtaka ndio ameshinda. Na kokote atakakokipeleka chama chenu ni juu yenu. Mbowe hahusiki.
FAFO.

Amandla...
 
Kwa vile sikuandikii wewe bora uni "ignore" kabisa. Nitaendelea kuandika ninavyotaka na sio unavyotaka.
Mtu uliyemtaka ndio ameshinda. Na kokote atakakokipeleka chama chenu ni juu yenu. Mbowe hahusiki.
FAFO.

Amandla...
Majibishano na mimi kama unavyo fanya hapa ni kuniandikia mimi, na hilo ndilo nililo maanisha nilipo andika kuwa "sisomi gazeti". Sina sababu ya kukuweka kwenye "ignore list"; na wala sina kizuizi cha kutojibu hoja zako kama zipo, unapoziweka humu.
Hakuna mahali popote nilipo kuzuia kuandika unavyotaka; kama wewe usivyo kuwa na uwezo wa kunizuia nisiyatolee maoni maandishi yako.
Sasa unasubiri huyo aliyeshinda kwa demokrasia uliyokuwa ukiiimba ashindwe na chama kisambaratikeili upate nafasi ya kuja hapa kutueleza ulivyojuwa hayo yote yangetokea hata kabla ya "demokrasia"!
"...Mbowe hahusiki"? Wewe sasa umekuwa msemaji wa Mbowe wakati kote umejitangaza kuwa ulicho kuwa ukipigania ni "demokrasi"?
 
Majibishano na mimi kama unavyo fanya hapa ni kuniandikia mimi, na hilo ndilo nililo maanisha nilipo andika kuwa "sisomi gazeti". Sina sababu ya kukuweka kwenye "ignore list"; na wala sina kizuizi cha kutojibu hoja zako kama zipo, unapoziweka humu.
Ni jambo jema kama ni hivyo. Kwa vile wewe ndie uliingiza suala la kutosoma nilichoandika bado naamini itakurahisishia kama utaniweka katika "ignore list" yako. Lakini ni uamuzi wako. Siwezi kukulazimisha.
Hakuna mahali popote nilipo kuzuia kuandika unavyotaka; kama wewe usivyo kuwa na uwezo wa kunizuia nisiyatolee maoni maandishi yako.
Sawa.
Sasa unasubiri huyo aliyeshinda kwa demokrasia uliyokuwa ukiiimba ashindwe na chama kisambaratikeili upate nafasi ya kuja hapa kutueleza ulivyojuwa hayo yote yangetokea hata kabla ya "demokrasia"!
Kwa vile inaelekea umekuwa unanifuatilia kwa muda mrefu, nipe mfano wa mahali nilipomuombea Lissu ashindwe na CDM isambaratike. Mimi nilisema hafai lakini pamoja na hayo nikasema bora ashinde maana angeshindwa asingekubali matokeo na hivyo kuzidisha mpasuko katika chama chake.
"...Mbowe hahusiki"? Wewe sasa umekuwa msemaji wa Mbowe wakati kote umejitangaza kuwa ulicho kuwa ukipigania ni "demokrasi"?
Uchaguzi umepita na uongozi wa juu wote wa CDM ni Team Lissu. Mbowe anahusika vipi katika muelekeo wa sasa wa CDM? Demokrasia ilifanyika pale alipoweza kugombea, kushindwa na kukubali matokeo. Sasa hii inahusika vipi na uendeshaji wa sasa wa CDM? Au hamuamini kuwa kweli mlishinda na mmeshika hatamu?

Amandla...
 
Mimi nilisema hafai lakini pamoja na hayo nikasema bora ashinde maana angeshindwa asingekubali matokeo na hivyo kuzidisha mpasuko katika chama chake.
Sasa wewe hilo la Tundu Lissu "asingekubali matokeo" umelitoa wapi; wewe mwenyewe hata hapa unaonyesha ni kiasi gani unavyo subiri CHADEMA chini ya Tundu Lissu isambaratike; halafu nataka nikupe mfano wa maneno uliyo andika kuhusu hili kuonyesha ushahidi?
Uchaguzi umepita na uongozi wa juu wote wa CDM ni Team Lissu
Una maana Wenje naye ni timu Lissu, na yule mama wa BAWACHA aliyetangaza kumuunga mkono Mbowe, pia ni timu Lissu?
Naona hata subira tu ya kuiona CHADEMA ikisambaratika imekuwa ngumu kwenu?
 
Sasa wewe hilo la Tundu Lissu "asingekubali matokeo" umelitoa wapi; wewe mwenyewe hata hapa unaonyesha ni kiasi gani unavyo subiri CHADEMA chini ya Tundu Lissu isambaratike; halafu nataka nikupe mfano wa maneno uliyo andika kuhusu hili kuonyesha ushahidi?
Lissu hakuwahi kusema kuwa atakubali matokeo ya uchaguzi. Kabla ya uchaguzi mkaanza kupenyeza taarifa za watu kuhongwa na watu wa Mbowe ( kumbe walikuwa wanalipwa posho zao). Usiku wa kabla ya uchaguzi Lema akatoa taarifa kuwa kuna wapiga kura wao ambao wananyimwa vitambulisho. Waandishi wa habari walipoenda katika kituo husika wakakuta watu wanaendelea kupewa vitambulisho na hamna aliyenyimwa. Zote hizo zilikuwa ni kutayarisha uwanja kwa ajili ya kupinga matokeo kwa sababu waliisha jiaminisha kuwa Mbowe ni king'ang'anizi na atafanya kila namna abakie madarakani.
Tuache kudanganyana, hauna ushahidi wowote wa Fundi Utumbo akiombea CDM isambaratike.
Una maana Wenje naye ni timu Lissu, na yule mama wa BAWACHA aliyetangaza kumuunga mkono Mbowe, pia ni timu Lissu?
Naona hata subira tu ya kuiona CHADEMA ikisambaratika imekuwa ngumu kwenu?
Uongozi wa juu ni Mwenyekiti, naMakamu Wenyeviti. Katibu Mkuu na wenzake ni watendaji na wanatekeleza maagizo ya viongozi wa juu. Kamati Kuu sio uongozi wa juu. Humo utawakuta sio tu hao uliowataja bali watu kama Boni Yai, Sugu, Sharifa na Freeman Aikaeli Mbowe. Hawa hawahusiki katika uendeshaji wa siku kwa siku wa chama. Kama hata hilo hauelewi basi iko namna.

Amandla...
 
Lissu hakuwahi kusema kuwa atakubali matokeo ya uchaguzi. Kabla ya uchaguzi mkaanza kupenyeza taarifa za watu kuhongwa na watu wa Mbowe ( kumbe walikuwa wanalipwa posho zao). Usiku wa kabla ya uchaguzi Lema akatoa taarifa kuwa kuna wapiga kura wao ambao wananyimwa vitambulisho. Waandishi wa habari walipoenda katika kituo husika wakakuta watu wanaendelea kupewa vitambulisho na hamna aliyenyimwa. Zote hizo zilikuwa ni kutayarisha uwanja kwa ajili ya kupinga matokeo kwa sababu waliisha jiaminisha kuwa Mbowe ni king'ang'anizi na atafanya kila namna abakie madarakani.
Tuache kudanganyana, hauna ushahidi wowote wa Fundi Utumbo akiombea CDM isambaratike.
Wewe inaonekana unayasema yote haya kwa sababu ulikuwa ni sehemu ya wahusika wa karibu katika mchakato huo, mimi sijui; kwa sababu sipo huko ulipokuwa wewe. Ila niliwahi kumsikia Mbowe akijigamba kuwa hana shaka na ushindi kwa sababu pesa ya kutosha ipo, na watu wa kumwezesha kufanya hivyo anao! Sasa maana ya majingambo hayo kabla ya uchaguzi mimi siijui.
Sijui kama ulitarajia Tundu Lissu akubali matokeo hata kama ni matokeo batili!
Uongozi wa juu ni Mwenyekiti, naMakamu Wenyeviti.
Sasa sikuelewi. Hawa hawakuchaguliwa kidemokrasia kama ulivyo taka wewe. Tatizo lipo wapi?
 
Wewe inaonekana unayasema yote haya kwa sababu ulikuwa ni sehemu ya wahusika wa karibu katika mchakato huo, mimi sijui; kwa sababu sipo huko ulipokuwa wewe. Ila niliwahi kumsikia Mbowe akijigamba kuwa hana shaka na ushindi kwa sababu pesa ya kutosha ipo, na watu wa kumwezesha kufanya hivyo anao! Sasa maana ya majingambo hayo kabla ya uchaguzi mimi siijui.
Umewahi kumsikia mgombea yeyote akiingia katika mpambano na kusema kuwa anategemea kushindwa. Hata Heche alitangaza wazi kuwa wanaenda kumshinda Mbowe ingawa wanamheshimu. Hizo pesa ni kweli zilikuwepo na ndio maana alitoa milioni 250 kuwezesha mkutano ufanyike. Watu alikuwa nao ndio maana Bawacha walimchagua Sharifa pamoja na Lissu kumfanyie kampeni mshindani wake. Uo ndio ukweli wenyewe kama ulivyo ukweli kuwa Mbowe alishindwa kutetea nafasi yake.
Sijui kama ulitarajia Tundu Lissu akubali matokeo hata kama ni matokeo batili!
Sasa sikuelewi. Hawa hawakuchaguliwa kidemokrasia kama ulivyo taka wewe. Tatizo lipo wapi?
Unaposema nitakubali tu matokeo kama nitashinda. Hapo ni kuweka njia ya kuyabatilisha kama akishindwa.
Huwezi kunielewa kwa sababu unataka tubishane tu. Lissu na Heche wamechaguliwa kidemokrasia kwa sababu ushindi wao ulipatikana kwenye boksi la kura. Nyinyi mlitaka Mbowe ajitoe ili mtu wenu awe coronated. Hiyo ni pamoja na Mbowe kuonyesha kuwa anataka kugombea. Kwa maneno mengine mlitaka kubaka demokrasia. Na darsa la mwisho alilowapa Mbowe ni kuwa uchaguzi huru
na wa haki unawezekana kama kuna nia ya dhati. Aidha, kushindwa katika uchaguzi sio dhambi. Kwenye hili anastahili shukrani zetu wote.

Amandla...

Hii hapa ndefu nyingine.
 
Back
Top Bottom