Mpambano wa Freeman Mbowe na Tundu Lissu: Wajue wagombea hawa wawili

Mpambano wa Freeman Mbowe na Tundu Lissu: Wajue wagombea hawa wawili

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,358
Ilikuwa kama utani na ilianza tetesi kwamba Tundu Lissu ameamua kupambana na Mwenyekiti wake ili kumpata kiongozi mpya atakayekiongoza chama hicho kwa miaka mitano ijayo

Sasa ni rasmi mafahali hawa wawili wameingia ulingoni ili kuamua ugomvi wao kupitia sanduku la kura.

Freeman Mbowe amekiongoza chama hicho kwa mafanikio makubwa mpaka zasa kiasi kwamba hata washindani wake wanakosa hoja ya msingi sana ya kushindana naye badala yake zimebaki tu propaganda za hapa na pale.

Freeman Mbowe mwanasiasa mfanyabiashara mwenye ukwasi mkubwa mpaka sasa anaungwa mkono na wenyeviti 9 wa Kanda kati ya 10 waliopo huku pia akiungwa mkono na wenyeviti wa mikoa 24 kati ya 30 iliyopo

Freeman Mbowe amekuwa mwanasiasa na kiongozi mtulivu zaidi, anayesikiliza, anayeshaurika na ambaye hana maneno mengi sana bali vitendo kwa wingi.

Freeman Mbowe ni kiongozi anayesimamia na kuliamini jambo lililopitishwa na vikao hata kama baadhi ya watu watalipinga na mfano mzuri ni maridhiano kati ya chama chake na serikali ya CCM.

Tundu Lissu msanaharakati na mtetezi wa haki za binadamu kwa muda mrefu ametangaza kugombea uenyekiti Chadema miezi mitatu tu tangu kutangaza kugombea Makamo Mwenyekiti wa chama hicho.Hajaweka wazi kwanini ghafla amebadili uamuzi wake

Tundu Lissu mwanasheria aliyebobea ni kiongozi ambaye ana misimamo mikali na ambaye haamini katika maridhiano.

Baadhi ya wapinzani wa Tundu Lissu wanamuona kama ni mtu anayeungwa mkono zaidi na makundi yaliyo nje ya Chadema hasa wanaharakati na watanzania waishio nje ya nchi.

Kingine ambacho wapinzani wa Tundu Lissu wanamwandama nacho ni tabia yake ya kupenda sana kuzungumza sana na vyombo vya habari hasa mitandao ya kijamii kama vile Club House, Spaces, Digital channels nk ambapo imedaiwa amekuwa akizungumza wakati mwingine mambo ya ndani ya chama.

Yote kwa yote msema kweli ni tarehe 21/1/2025 ambapo Mkutano Mkuu utachagua Mwenyekiti mpya kati ya miamba hii miwili ya siasa za Chadema na Tanzania kwa ujumla.

Sisi wa Molemo Media Tutawabarisha mambo mbalimbali kuhusu wagombea hawa kuelekea Januari 21 inayosubiriwa kwa hamu na Watanzania kwa ujumla.
 
Yote kwa yote msema kweli ni tarehe 21/1/2025 ambapo Mkutano Mkuu utachagua Mwenyekiti mpya kati ya miamba hii miwili ya siasa za Chadema na Tanzania kwa ujumla
Tarehe 21 haiamui mwenyekiti ila inaamua hatma ya kifo au uhai wa chadema. Mkimchagua huyo CCM B ndio mjue wapinzani halisi wote wataacha kupiga kura wala kuhudhuria matukio ya chama.

Freeman Mbowe mwanasiasa mfanyabiashara mwenye ukwasi mkubwa mpaka sasa anaungwa mkono na wenyeviti 9 wa Kanda kati ya 10 waliopo huku pia akiungwa mkono na wenyeviti wa mikoa 24 kati ya 30 iliyopo
Najua Mbowe alifanya utafiti wa nani anakubalika kati ya wanachama, na yeye anajua kabisa hayuko popular kuliko Lissu sasa mkidhani hao wenyeviti 24 ndio watatupangia mwenyekiti wao kisa kuhonhwa basi mnajidanganya. Wasiposikiliza maoni yetu wanachama; tutawaachia hiko chama kama Lipumba anaongoza chama hewa tu.
 
Freeman Mbowe amekiongoza chama hicho kwa mafanikio makubwa mpaka zasa kiasi kwamba hata washindani wake wanakosa hoja ya msingi sana ya kushindana naye badala yake zimebaki tu propaganda za hapa na pale.

Freeman Mbowe mwanasiasa mfanyabiashara mwenye ukwasi mkubwa mpaka sasa anaungwa mkono na wenyeviti 9 wa Kanda kati ya 10 waliopo huku pia akiungwa mkono na wenyeviti wa mikoa 24 kati ya 30 iliyopo

Freeman Mbowe amekuwa mwanasiasa na kiongozi mtulivu zaidi, anayesikiliza, anayeshaurika na ambaye hana maneno mengi sana bali vitendo kwa wingi.


Tundu Lissu msanaharakati na mtetezi wa haki za binadamu kwa muda mrefu ametangaza kugombea uenyekiti Chadema miezi mitatu tu tangu kutangaza kugombea Makamo Mwenyekiti wa chama hicho.Hajaweka wazi kwanini ghafla amebadili uamuzi wake
Hongera tumejua unayemuunga mkono
Kingine ambacho wapinzani wa Tundu Lissu wanamwandama nacho ni tabia yake ya kupenda sana kuzungumza sana na vyombo vya habari hasa mitandao ya kijamii kama vile Club House, Spaces, Digital channels nk ambapo imedaiwa amekuwa akizungumza wakati mwingine mambo ya ndani ya chama.
Kwanini msiseme nyie kama Malemo Media mko tayari kuelezea mafinikio ya Mbowe kwa miaka 20 mkiwa katika zoezi la kumfanyia kampeni?
Sisi wa Molemo Media Tutawabarisha mambo mbalimbali kuhusu wagombea hawa kuelekea Januari 21 inayosubiriwa kwa hamu na Watanzania kwa ujumla.
 
Tarehe 21 haiamui mwenyekiti ila inaamua hatma ya kifo au uhai wa chadema. Mkimchagua huyo CCM B ndio mjue wapinzani halisi wote wataacha kupiga kura wala kuhudhuria matukio ya chama.
Hii nimeisema sana 2015 alisamehewa japo ilipunguza hari na nguvu ya chama kwa kiasi kikubwa , 2025 will not be a walk in the park
Najua Mbowe alifanya utafiti wa nani anakubalika kati ya wanachama, na yeye anajua kabisa hayuko popular kuliko Lissu sasa mkidhani hao wenyeviti 24 ndio watatupangia mwenyekiti wao kisa kuhonhwa basi mnajidanganya. Wasiposikiliza maoni yetu wanachama; tutawaachia hiko chama kama Lipumba anaongoza chama hewa tu.
Mbowe asipoangalia atakuwa kama Lipumba nani aliwahi kujua Lipumba wa ngangari miaka 19 iliyopita atapata watu kama hawa?

Hawa kama hawajui nguvu ya umma inamshusha mtu vipi wakaangalie account ya Kigogo 2014 aliyesaliti watu.
20241226_175613.jpg
 
Sisi wa Molemo Media Tutawabarisha mambo mbalimbali kuhusu wagombea hawa kuelekea Januari 21 inayosubiriwa kwa hamu na Watanzania kwa ujumla.
Nyinyi wa "Molemo" hamna la ziada la kuwajulisha watu, kwa vile majibu tayari mnayo; kama mlivyo yaweka hapo juu.

Kwa hiyo hakuna sababu ya kuwatafuta tena nyinyi kupata majibu ambayo tayari mmekwisha yaweka bayana kwa maoni yenu.
 
Tarehe 21 haiamui mwenyekiti ila inaamua hatma ya kifo au uhai wa chadema. Mkimchagua huyo CCM B ndio mjue wapinzani halisi wote wataacha kupiga kura wala kuhudhuria matukio ya chama.


Najua Mbowe alifanya utafiti wa nani anakubalika kati ya wanachama, na yeye anajua kabisa hayuko popular kuliko Lissu sasa mkidhani hao wenyeviti 24 ndio watatupangia mwenyekiti wao kisa kuhonhwa basi mnajidanganya. Wasiposikiliza maoni yetu wanachama; tutawaachia hiko chama kama Lipumba anaongoza chama hewa tu.
Sahihi kabisa, kama wanategemea watu wachache ndio wataaamua mapenzi ya wengi, basi watajua kuwa hakuna kitu cha kuheshimu maishani kama mahitaji ya nyakati.
 
Back
Top Bottom