Mpango mauaji ya Wayne Derek Lotter ulivyosukwa na kutekelezwa jijini Dar

Mpango mauaji ya Wayne Derek Lotter ulivyosukwa na kutekelezwa jijini Dar

Rahma na dereva bodaboda wameonewa,kupika chakula watu wanaoukuja nyumbani kwa kakaake sidhan kama wamehusika na mauaji,hata kama alificha silaha ni ktk hali ya kawaida ya kujihami,anahitaji mwanasheria mzuri,kuna watu wanastahili kunyongwa ila siyo rahma na dereva wa bodaboda,halafu hajasema hizo milion 58 zilitoks kwanani na zilienda kwa lengo gani ikiwa huyo mrundi alipewa milioni 20 na myu mwingine
... Rahma alijihami dhidi ya nini boss? Siku hizi utaratibu ni kwenda kuzika silaha makaburini na sio kutoa taarifa polisi? Huyo bodaboda umesoma vizuri role yake kwenye hili sakata? Tena huyo ndio muuwaji haswa!
 
Tatizo ni chain kuwa kubwa sana lilikuwa swala la hitman mmoja tu getini mchezo unaisha, hawa wapuuzi wanaenda na IST, Bodaboda
... eti walishirikisha hadi bodaboda! Huyu si alienda simulia wenzie kijiweni muda ule ule baada ya tukio kuonesha sifa.
 
Hao watu waliosome na kubobea kufanya uchunguzi hawawezi kutumiwa na majambazi ili kuondoa traces zote?
Kwa teknolojianya kibongo mi naona ni rahisi sana, na majambazi wengi tu wanaua na kudunda mtaani.
Apo itategemea wamemuua nani! Huyu mzungu unazan kwao mngewambia nn ?? Ety tumeshindwa wabain wauwaji?? Weee thubutuuu ndio maana ikabidi ata small fish wahusike Ili kupoteza maboya
 
Sio mtaa wa majengo alikuwa karibu kabisa na stand kubwa, hata mimi nilikuwa na duka mitaa hiyo, Dah namuonea huruma kijana wa watu maana bado umri mdogo tu ule
Ukiachana na Ile majengo ya Kule chini sakon hicho kimtaa hapo karibu na pab Norberto pia ndio maarufu kwa jina Hilo. Ni kimtaa chenye biashara Haram nyingi sana
 
Walioplot haya mauwaji ni mandezi tu na hata aliye recruit assasin anafanya mambo locally sana na bahati analindwa na mamlaka thats why case imeishia mabegani tu!
Hapa ni dhahiri mfadhiri wa mauwaji wauaji walimtaja, sema mpelelezi/wapelelezi wameufyata kumuunga.

Walichobugi ni kuwahusisha madereva na kuua mtu mmoja tu hiyo imewapa syndicate nyepesi kwa mpelelezi kuunganisha nukta.
Halafu usikute wametumia mawasiliano kwa namba za simu zinazo tambulika.
Kwa professional killer angehusisha mtu mmoja tu halafu yy angetoka nao kia then angemuweka mtu na gari pale JNIA na targeted area ya kumaliza mchezo.
Nawe ni muuaji?
 
Ukiachana na Ile majengo ya Kule chini sakon hicho kimtaa hapo karibu na pab Norberto pia ndio maarufu kwa jina Hilo. Ni kimtaa chenye biashara Haram nyingi sana
Namuonea huruma kaka wa watu kaacha mke na watoto. Maana nakumbuka huo mwaka hao wasiojulikana walimfuata hapo dukani wakamchukua ndo hadi leo hajarudi mtaani na kwa maana hiyo hatorudi tena mtaani
 
Mpango umeshirikisha watu wengi mno Lazima mkamatwe

Mrundi nae alipomaliza kazi ana 2m mfukoni kwa nini asiondoke
 
Namuonea huruma kaka wa watu kaacha mke na watoto. Maana nakumbuka huo mwaka hao wasiojulikana walimfuata hapo dukani wakamchukua ndo hadi leo hajarudi mtaani na kwa maana hiyo hatorudi tena mtaani
Makoi na machips Walikamatwa the some year.

tuwaombee akina Machips na Makoi kwenye rufaa yao washinde.
 
Kuna watu walisomea na kubobea kufanya uchunguzi.

Huezi fanya mauaji watu wasikukamate. Lazima utaacha trace ambayo ndo itasababisha wewe kukamatwa.

Labda uue mbuzi wa jirani yako.
Tatizo hapa utumiaji wa simu kwenye mipango inatakiwa kutumika karatasi tu
 
Kuna kazi ukifanya au nyadhifa flani ukiwa nayo inapaswa uishi kimafya, kiroho mbaya ile hucheki na nyani, gari tinted, ukiwa unakwenda nyumbani mita 100 unapiga simu geti ifunguliwe, ukiwa unatoka ni 80km/h, glock imekaa kiunoni na magazine ipo full, nyumbani cctv mpaka bafuni, ratiba zako hata mkeo hazielewi.. Mzungu alikua anafanya kazi ya kuhatarisha usalama wake hakupaswa kujiachia hivyo, RIP kamanda, may be alihisi majangili ndio adui zake, kumbe hao hao wa karibu yake ndio maadui, halafu na huyo jamaa alikuwa nae kwenye gari wambane kende how comes aachwe asipigwe hata panga? Jambazi ili kulinda usalama wake anapoondoka eneo la tukio lazima akuache hoi ushindwe hata kupiga simu polisi... Kuna kitu hakipo sawa...
 
Bunduki, bomu vilivyofukuliwa makaburini (2)

Jumatano, Desemba 14, 2022

By Daniel Mjema
Mwandishi mwandamizi
Mwananchi Communications Ltd (MCL)

Muktasari:

Katika sehemu ya kwanza tuliona Agosti 16, 2017, mwanaharakati wa mapambano ya ujangili, Wayne Dereck Lotter Wayne akiwa na mkurugenzi mwenza wa Pams, walisafiri kutoka Arusha kwenda Dar es Salaam kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).
Baada ya kuwasili Dar es Salaam tuliona jinsi madereva teksi ambao waliaminiwa na mwanaharakati huyo kwa zaidi ya miaka 10 walivyoshiriki kusuka mipango ya kumuua tajiri huyo aliyekuwa raia wa Afrika Kusini. Endelea..

Katika sehemu ya pili, tunaendelea kukuletea ushahidi wa mashahidi wa Jamhuri ambao kwa njia moja ama nyingine walishiriki katika kushuhudia tukio au kufanya upelelezi uliofanikisha kujulikana ukweli wa mauaji ya Wayne.

Shahidi wa pili wa upande wa Jamhuri aliyetambuliwa kama AB, ambaye ni mmoja wa wakurugenzi watano wa Pams Foundation, alisema siku ya tukio alijulishwa na mkurugenzi mwenzake kwamba wamevamiwa eneo la Masaki.

Mkurugenzi huyo ndiye aliyekuwa amesafiri pamoja na Wayne kutoka Arusha hadi KIA na baadaye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), alisema walivamiwa eneo hilo wakitokea uwanja wa ndege na baadaye alikwenda haraka hospitali ya Sally International.

RELATED

Simulizi mauaji mtetezi wa tembo yalivyopangwa (1)

Kitaifa 3 hours ago

Shahidi huyo aliithibitishia mahakama kuuona mwili wa Wayne pale Sally International, lakini wakati huo ilikuwa tayari imethibitishwa kuwa amefariki dunia na ndiye pia aliyeutambua mwili wa Wayne katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kabla ya kufanyika uchunguzi (post mortem).

Shahidi wa tatu, nne na tano

Shahidi wa tatu ambaye kama waliomtangulia naye alipewa kifupisho cha AC na ni mtaalamu wa uchunguzi wa kisayansi kutoka Forensic Bureau, yeye aliieleza mahakama kuwa Desemba 13, 2017 alipokea vitu vinne avifanyie kazi.

Vitu hivyo ni silaha mbili, risasi ndogo 162, risasi kubwa moja na bomu la kurushwa kwa mkono na vitu hivyo viliambatana na barua kutoka ofisi ya RCO Kinondoni ikimtaka achunguze kama silaha hizo zilikuwa zinafanya kazi sawa sawa.

Barua ya pili ilikuwa na sampuli za maganda mawili ya risasi yaliyotumika kutoka silaha aina ya Uzi-Gun na kichwa kimoja cha risasi na ilimtaka kuchunguza sampuli hizo zilifyatuliwa kutoka kwenye silaha gani kati ya Uzi-Gun au Riffle Marker 4.

Baada ya uchunguzi wa kina, aliiambia mahakama kuwa aligundua silaha zile zilikuwa zinafanya kazi barabara na hata lile bomu la kurushwa kwa mkono na kwamba maganda na kichwa cha risasi vilifyatuliwa kutoka silaha aina ya Uzi-Gun.

Vitu hivyo pamoja na nyaraka vilipokelewa kama vielelezo namba 2 hadi 15.

Shahidi wa nne kama AD ambaye ni Ofisa wa Polisi aliieleza mahakama kuwa ndiye polisi wa kwanza kwenda eneo la tukio na huko alikutana na dereva teksi (Kwavava-mshtakiwa wa 14) ambaye alikuwa amewabeba wazungu hao.

Akiwa hapo aliona gari alilokuwa akiendesha dereva teksi huyo na alipata nafasi ya kumuuliza dereva nini kilichotokea, na baadaye alikwenda Hospitali ya Sally International lakini alipofika huko alielezwa Wayne alishafariki.

Baada ya hapo alirudi eneo la tukio ambako katika uchunguzi alifanikiwa kupata maganda mawili ya risasi yaliyotumika, moja aliliokota ardhini na lingine likiwa ndani ya teksi iliyokuwa imembeba Wayne na mkurugenzi mwenza wake.

Pia alisema baada ya kufanya yote hayo, Agosti 19, 2017 alishiriki na kushuhudia uchunguzi wa mwili wa Wayne katika Hospitali ya Muhimbili na akiwa kizimbani alimtambua mshtakiwa wa 14, Kwavava aliyekuwa dereva teksi.

Shahidi wa tano aliyetambuliwa kama AE ambaye anafanya kazi katika Dry Clearner ya Isnashir iliyopo mtaa wa Bibi Titi, Kinondoni na anakumbuka Septemba 19, 2017 wakimuomba ashuhudie upekuzi katika makaburi ya Ngazija.

Hapo makaburini anakumbuka kumuona msichana ambaye baadaye alikuja kumtambua mahakamani kama mshtakiwa wa pili, Rahma na mtu mwingine aliyemtaja kama Mzee Maganga ambaye ni mhudumu wa makaburi.

Akiwa hapo alimsikia mshtakiwa huyo wa pili akiulizwa na polisi ni wapi walipochimbia silaha na baada ya kuonyesha kwa ishara, ndipo Mzee Maganga aliwaambia polisi walihamisha mzigo huo hadi eneo la kona makaburini.

Anasema Mzee Maganga alichukua jembe na kuchimba ambapo alishuhudia mfuko wa kiroba ulitolewa na ndani yake kulikuwa na begi jeusi na lilipofunguliwa kulikutwa silaha mbili na bomu na birika yenye rangi ya bluu bahari.

Birika hiyo ilipofunguliwa kulikutwa soksi zilizokuwa na risasi na zilikuwa risasi kama 160 baada ya kuhesabiwa na alikiri kusaini hati ya ukamataji mali na akiwa hapo alimuona polisi mmoja akipiga picha vitu vyote vilivyopatikana hapo.

Ushahidi wa shahidi wa sita

Shahihi huyu, Ofisa wa Polisi aliyepewa utambulisho AF, aliieleza mahakama kuwa Septemba 16, 2017 kati ya saa 6:00 na saa 6:30 mchana alipata taarifa kutoka kwa msiri kuwa mmoja wa washukiwa wa mauaji yuko Kasoro Guest House.

AF ambaye anafanya kazi katika kikosi kazi cha makosa makubwa Polisi Chang’ombe, Dar es Salaam anasema alikwenda katika nyumba hiyo ya kulala wageni na kufanikiwa kumkamata mshukiwa ambaye katika kesi hiyo ni Rahma.

Shahidi huyo alieleza kuwa alimkuta na pasi ya kusafiria yenye jina la Rahma Almasi na kumpeleka kituo cha Polisi Oysterbay, lakini baadaye aliitwa tena aungane na timu ya makachero kwamba Rahma amekiri na yuko tayari kuonyesha silaha.

Wakiwa katika makaburi ya Ngazija, kulifukuliwa mfuko wa kiroba ambao ndani yake kulikuwa na begi jeusi na ndani yake kulikuwa na vitu vitatu ambavyo ni kitenge, mfuko mweusi na birika (thermos) yenye rangi ya bluu bahari.

Ndani ya vitu hivyo kulikutwa silaha aina ya Uzi-Gun yenye namba 084912 na bunduki aina ya Rifle ambayo haikuwa na namba za utambulisho na pia kulikuwa na bomu la kurusha kwa mkono na risasi 167 huku 162 zikiwa za Uzi-Gun.

Katika maswali ya dodoso (cross examination), shahidi huyo aliieleza mahakama kuwa alikuwa na taarifa kuwa mshtakiwa huyo wa pili, Rahma alikuwa mbioni kuondoka nchini kwenda Comoro kulingana na taarifa alizopewa na msiri wake.

Itaendelea
 
Basi kuyafahamu yote hayo, fuatilia mfululizo wa matoleo ya makala katika gazeti hili ambapo tutakuletea mwanzo mwisho wa tukio hilo, kesi ilivyoendeshwa hadi kufikia uamuzi wa washtakiwa 11 kuhukumiwa kunyongwa hadi kufa.

Katika sehemu hii ya kwanza, tutaangalia tangu marehemu ambaye ni mkurugenzi wa taasisi ya Protected Area Management System (PAMS) na mkurugenzi mwenza walivyoondoka Arusha hadi anauawa Dar es Salaam.

Usiku wa Agosti 16, 2017, Wayne akiwa na mkurugenzi mwenza wa Pams walisafiri kutoka Arusha kwenda Dar es Salaam kupitia uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) pasipokujua kuna kifo kinamsubiri.

Hakufahamu kama dereva aliyemchukua kutoka Arusha mjini kwenda KIA ambaye wamemfahamu kwa miaka mingi na dereva teksi atakayewapokea uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jullius Nyerere (JNIA), Jijini Dar es Salaam, wamekula njama ya kumuua.

Baada ya kutua JNIA, walipokelewa na dereva teksi wa siku zote anayewapokea aitwaye Michael Daud Kwavava ambaye wamemfahamu kwa zaidi ya miaka 10, aliwachukua kuelekea Babao Village ambako ndipo walipokuwa wakielekea.

Wakiwa njiani walipofika katika njiapanda ya Barabara ya Kaole na Haile Selassie katika eneo la Masaki, walizuiwa kwa mbele na gari lingine na kwa mshtuko ndani ya gari hiyo walishuka watu walioonekana ni majambazi.

Majambazi wawili walilisogelea gari lao na mmoja akachukua kompyuta mpakato (laptop) zao na baadhi ya nyaraka ambazo walikuwa wakizifanyia kazi, mmoja alikuwa na silaha na alimfyatulia risasi mwanaharakati huyo. Baadaye majambazi hao waliokuwa na gari aina ya Toyota IST, walitokomea kusikojulikana na Wayne alikimbizwa hospitali ya Sally International ambayo haikuwa mbali na eneo la tukio, lakini tayari alikuwa amefariki dunia.

Baada ya tukio hilo, Jeshi la Polisi lilianza upelelezi kuwabaini nani wanaoshukiwa kuhusika na mauaji hayo na washukiwa 18 walikamatwa wakiwamo raia wawili wa Burundi na mwanamke Rahma Mwinyi. Watuhumiwa hao walifikishwa mahakamani na katika usikilizwaji wa shauri hilo Mahakama Kuu walipangwa kuanzia mshtakiwa wa kwanza Khalid Mwinyi au Banyata, hadi mshtakiwa wa 18, Almas Swedi maarufu kwa jina la Malcom.

Wengine kuanzia namba mbili walikuwa ni Rahma Mwinyi au Baby, Nduimana Ogisye ambaye ni raia wa Burundi, Godfrey Salamba, Chambie Ally, Allan Mafue, Ismail Mohamed au Machips, Leonard Makoi na Ayoub Seleman Kiholi.

Mbali na washtakiwa hao, walikuwepo Joseph Lukoa, Gaudence Matemu, Abuu Mkingie, Habonimana Nywandwi au Ogistee ambaye ni raia wa Burundi na Michael Kwavava aliyekuwa dereva teksi aliyewabeba Wayner kutoka JKIA.

Wengine katika orodha hiyo ni Emannuel Sonde, Kelvine Soko, Samia Hujat na Almas Swedi au Malcom na wote walikanusha mashtaka matatu ya kula njama kufanya mauaji na kumuua kwa kukusudia Wayne.

Kabla ya kuanza kusikilizwa kwa kesi hiyo na Jaji Leila Mgonya, Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), akawasilisha maombi kwa njia ya chemba ambayo yalikubaliwa, kwamba kesi iendeshwe faragha ili kulinda mashahidi.

Kutokana na ombi hilo ambalo lilikubaliwa na Jaji Lameck Mlacha katika uamuzi wake wa Desemba 8, 2020, mashahidi wote 32 waliotoa ushahidi walitambuliwa kwa vifupisho vya maneno AA hadi AZ na BA hadi BF 32.

Katika ushahidi huo, upande wa Jamhuri ulikuwa na mawakili wa Serikali saba wakiongozwa na wakili wa Serikali mkuu, Yamiko Mlekano na mahakama ilipokea pia vielelezo 43 yakiwamo maelezo ya ungamo ya baadhi ya washtakiwa.

Mathalan katika mahojiano yaliyorekodiwa, mshtakiwa wa tatu ananukuliwa akieleza namna alivyoelezwa kuwa mzungu (Wayne) angekuja na usafiri wa ndege siku hiyo huku mwingine akinukuliwa akielezea mgawo wa fedha ulivyokuwa.

Ni katika maelezo hayo ya ungamo, unakuta simulizi za mshtakiwa wa nne, Salamba anavyoeleza walivyokwenda JNIA baada ya mauaji na mshtakiwa wa tatu aliyemfyatulia risasi marehemu, alikabidhiwa mgawo wake wa Sh20 milioni.

“Huyo Allan Mafue alitoa Sh20 milioni ambazo alikabidhiwa Zebedayo kama mgawo wake katika nafasi yake ya uuaji kama alivyoahidiwa, baada ya hapo tulimrudisha Zebedayo Temeke nyumbani kwa Fahami Karama,” anaeleza. Maelezo mengine ni ya mshtakiwa wanane, Makoi anayesema katika maelezo yake “Ni kwamba mwaka 2017 mwezi wa saba tarehe sikumbuki alinipigia simu mzee mmoja anayeitwa Machips jina kamili silifahamu akaniambia kuna biashara.

“Nilimuuliza ni kazi gani akaniambia kuna mzungu anayehusika na meno ya tembo anatakiwa auawe. Akaniambia kama kuna watu wanaweza kufanya hizo kazi niongee nao, ili tukubaliane kazi ifanyike,” ananukuliwa Makoi akisema.


Shahidi wa kwanza

Shahidi wa kwanza aliyetambulika kama AA ambaye ni daktari anayefanya kazi Hospitali ya Taifa ya Muhimbili anasema Agosti 19, 2017 alisaidiana na daktari mwenzake ndio walioufanyia uchunguzi mwili wa Wayne.

Katika uchunguzi huo walibaini marehemu alikuwa na jeraha karibu na mdomo na walipochunguza zaidi ndani waliona kipande cha chuma ambacho waliamini ni risasi ilipenya hadi mkono wa kushoto wa marehemu. Kutokana na risasi hiyo, mfumo wa upumuaji ulizibwa na damu na kwamba sababu za haraka za kifo ilisababishwa na kukosa hewa katika mfumo wa upumuaji kutokana na kuganda kwa damu.

Baada ya uchunguzi huo aliandaa ripoti ya uchunguzi ambayo ilipokelwa mahakamani kama kama kielelezo namba moja.

Itaendelea kesho
 
Back
Top Bottom