Mpasuko mkubwa wa Ardhi watokea Mbagala Saku. Baadhi ya nyumba za watu zaripotiwa kubomoka

Mpasuko mkubwa wa Ardhi watokea Mbagala Saku. Baadhi ya nyumba za watu zaripotiwa kubomoka

Serikali na idara zake za ardhi na hali ya hewa hawajulikani walipo, madiwani , wabunge au madiwani wao hawana number zao? mbunge anaweza kumpigia waziri Moja Kwa Moja wakapata usaidizi wa haraka
 
Watu wamejega juu ya madampo juu ya makaburi juu ya mito kwenye mashimo ya michanga ili mradi vurugu hiyo mimomonyoko lazima itokee kipindi flani!
 
Hii sijui ni tetemeko au ni kitu gani, wataalamu tunaomba mfuatilie na mtupatie majibu, Ardhi inapasuka na nyumba zinabomoka, eneo ni Saku Mwisho DSM
---

View attachment 3001336
Taharuki imeibuka kwa wakazi wa Mbagala Saku baada ya kutokea kwa mpasuko mkubwa wa ardhi na kusababisha kubomoka kwa nyumba nyingi za wakazi wa eneo hilo na kuacha nyingine zikiwa zimeathirika kwa kiasi kikubwa

Wakazi wa eneo hilo wameiomba serikali kwenda kufanya uchunguzi juu ya chanzo cha tatizo hilo na kugundua endapo ni salama kwa wao kuendelea kuishi katika eneo hilo pamoja na kuwapatia msaada kwa wale walio athiriwa zaidi na tatizo hilo
Tanzania hatuna wataalamu wanaoweza kupima chini ya ardhi, tukumbuke tukio la tope Kunduchi mpaka leo hakuna jibu mpaka leo, wataalamu wa Chuo Kikuu cha Ardhi waliingia mitini.
 
Watu waache kuchimba visima vya maji, kwa kutoa maji ardhini wanafanya ardhi kuwa dhaifu
 
Nadhani mvua iliyonyesha imesavabisha udongo kubeba maji mengi. Hiyo ilitokea pia maeneo ya Tabata Bonyokwa, maji yalikuwa yanatokea mlimani kama chemchem, na ukikanyaga hiyo sehemu unatitia. Maji yalikauka wiki 2 baada ya mvua kukatika. Uzuri eneo hilo lina miti na majani. Kuna ukuta wa nyumba moja ulishuka sababu ya hiyo chemchem.
 
Hapa kwa hesab za haraka haraka ni kwamba hifadhi ya maji ardhini imekua disturbed na unstable, pengine kutokana na kuzidisha uvunaji wa maji-ardhi, uchimbaji madini au vifusi nk. cha msingi serikali iingilie kati wataalam husika wafanye mapping ili kuwaelekeza wananchi waondoke kwenye maeneo yote hatarishi. ni vyema pia ikawapa nyumba au viwanja maeneo mbadala.
 
Back
Top Bottom