Mpeni Mungu yaliyo ya Kimungu na Kaisari yaliyo ya Kaisari! Hiki kinachofanywa na Baraza la Maaskofu Katoliki, sio kuchanganya dini na siasa?

Hakuna kingine wanaogopa influence ya mwarabu,wanajua uislam ulifika Tanganyika kupitia mwarabu,bila ujio wa mwarabu pasingekua na uislam,wanajua mwarabu ana pesa,pesa zitaleta miradi Kama shule na hospital ambazo wao wametumia kuvuna waamini
Nyie waswahili mnasitahili misikiti tu. Mbeya tayari ujenzi unaendelea
 
Dini na siasa huwezi kuzitenganisha, Yesu mwenyewe alisulubiwa na wanasiasa. Na alikuwa anapambana nao sana Kila mara alikuwa anawaita wanafiki.
Mwaka 312 mfalme Constantino ndo iliingiza dini kwenye siasa ambayo ilizaa Roman Catholic mwaka 612
 
Haya yanayofanyika ni ya Kaisari ?!!!!

Kwanini wana-mpango wa kwenda kubadilisha vipengele Bungeni viendane na uozo utakaokuja (hapo ni kwamba haya sio ya Kaisari - Kulingana na sheria zetu) haya ni ya kwao na magenge yao...
 
Pascal Mayalla Fanya hima kama kweli wewe ni mkatoliki huende kwenye sala ya kitubio haraka sana.

Nimesoma tamko la baraza la maaskofu ambalo linaundwa na maaskofu 37.

Walikaa kwa siku kadhaa na kuomba kabla ya Mungu kuwaongoza kutowa tako hili, nimesoma kwa makini vipengele vyote walivyotaja inaonekana hawa maaskofu kipindi cha ukimya wao wametumia resources zao zote kuuchimbuwa huu mkataba na kufikia conclusion kwamba wanasimama na umma.

Wewe Pascal ni mpagani wala usijibanze kwenye ukatoliki, tafsiri halisi ya Askofu ndio kanisa, na Askofu ni mwakilishi wa Yesu Kristo duniani hiyo ndio tafsiri sahihi ya Askofu mpakwa mafuta wa Roman Catholic Church, sasa wewe ni nani wa kuwadhiaki maaskofu 37? Shensana.

Kwa kifupi kwa bandiko lako hili kwanza umekufuru, Pili umeikana imani yako mwenyewe kwa tamaa za kidunia kama walivyoelezea maaskofu kwenye Waraka wao kuhusu wanaopigia debe mkataba huu wa kipuuzi.

Unasikitisha sana angalau wenzako kina Kitenge wameambulia maokoto wewe umekuja kujiunga na machawa too late.

Ila nakuhakikishia hili, Rais Samia hayuko tayari kwenda kinyume na umma kwa maslahi ya machawa kama nyinyi.

Roma Locuta, Causa Finita Est.
 
Kwa maana hiyo wote tunajua kuwa kuna tatizo lakini ni lazima tunyamaze kwa kuwa Rais siyo Mkatoliki.... This is too Low my Bro!
 

Paskal nadhani wewe si mkatoliki, au waweza kuwa mkatoliki jina. Waraka wa kulaani mauji 2017 ulitolewa wakati wa nani? Waraka wa Kwaresma 2019 ulitolewa rais akiwa nani? Uwe mwenye kumbukumbu sahihi.

Demokrasia yenyewe unayodhani waijua imelelewa kanisani, au hujui?

TEC ana haki ya kuhoji mambo yanayoigusa jamii yake-wakristu wake. Kumbuka kanisa linamkomboa mtu kiroho na kimwili! Mengine ni umbeya wako!
 
Pascal.
Tambua nafasi yako na unaheshimika pia kama mkatoliki acha upoyoyo!
Haya mapungufu ni mengi na Taifa linapukutika Wayne wanavyotafuna wewe unataka wakae kimya.
Acha Uchawa.
 
Umesahau waraka wa TEC wa Kwaresma kipindi cha JPM?

Nenda tena kafungue archives zako!
 
Msema kweli ni mpenzi wa Mungu 🙏🙏
 
Tuongee ukweli tu bila kupepesa macho hizi kelele zote hizi drama zote toka awali, sababu DP World ni Waarabu.

Hakuna uchungu wa rasilimali za nchi wala nini issue ni Uarabu wa DP World. Period!
According to you. Shida mnataka kila mtu awe chawa Kama nyie. Kwani mwarabu kaja Leo?. Mbona mturuki kapewa SGR, Kuna mtu kalalamika.
 
Hakuna kingine wanaogopa influence ya mwarabu,wanajua uislam ulifika Tanganyika kupitia mwarabu,bila ujio wa mwarabu pasingekua na uislam,wanajua mwarabu ana pesa,pesa zitaleta miradi Kama shule na hospital ambazo wao wametumia kuvuna waamini

Baba umevuta ya Meru au Musoma? Kwani uislamu hauko Tanzania? Upo Tanzania muda mrefu zaidi ya ukristu. Nani anawazuia kufanya miradi kama wafanyayo wenzao? Pamoja na pesa alizonazo, nani anamzuia mwarabu kujenga shule za maana na mahospitali na vyuo vikuu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…