Mpina: Kifungu kilichotumiwa na Spika Tulia kunituhumu na kunihukumu hakipo!

Mpina: Kifungu kilichotumiwa na Spika Tulia kunituhumu na kunihukumu hakipo!

Technically ilipaswa Spika amuachie naibu wake alisimamie lile swala, maana yeye tayari alikuwa ni mlalamikaji. Sasa mlalamikaji kapeleka malalamiko yake kwenye kamati na akaielekeza kamati cha kufanya, akapokea taarifa ya kamati na kuendesha kikao cha kutoa hukumu ya dhidi ya mtuhumiwa huku yeye akiwa ni mlalamikaji.
 
Sikiliza dakika 59 na sekunde 39 utaelewa nani anahitaji kupgwa spana.
usijaribu kuleta uongo, Bashe kashindwa hata kujitetea kwa zile hoja zilizotolewa, na hapa tena anaenda kuwavua nguo. Bunge zima Hakuna mtu aliyesimama kujibu zile hoja zaidi ya kuongea upumbavu, spika Tulia ndio kabisa ni kama Likwidi tu wa pale kurasini.
Wewe unaweza kujibu hoja za mpina?
 
Wakuu,

Luhaga Mpina alipewa adhabu na Bunge Juni 24, 2024 baada ya kwenda kinyume kwa kuwasilisha taarifa yake kwa wananchi mara baada ya kuikabidhi katika Kamaati ya Bunge. Zaidi soma - Bunge lajadili juu ya adhabu ya Mbunge Luhaga Mpina. Laamua kumfungia vikao 15

Usiku huu tukio linarushwa live mpina akiongelea suala hilo kwa mara ya kwanza baada ya adhabu yake kuanza rasmi. Fuatilia uzi huu kwa updates zaidi.


====


Kamati iliongeza mashtaka tofauti za aliyoagiza Spika - kwenda kinyume na kufungu cha 29 D na E na kifungu cha 34(1) G cha Sheria na Kinga, Haki na Madaraka ya Bunge sura ya 296 na siyo tuhuma zilizokuja kuongezwa baadaye kwamba ni kifungu Kifungu cha 26 D na E na Kanuni ya 84(1) J na K.

Kifungu cha 29 D na E cha Sheria na Kinga, Haki na Madaraka ya Bunge sura namba 296 ambacho Spika alirejea kumtuhumu nayo hakiendani na maudhui ya tuhuma zilizotolewa katika taarifa ya Spika, kifungu hicho kinazungumzia makosa ya Waandishi wa Habari wanapoingia katika vikao vya Bunge bila kufuata utaratibu!

Kifungu hicho hakitengenezi kosa la kijinai wala kinidhamu kwa Mpina, hivyo haikuwa sahihi kwa Spika kumtuhumu kwa makosa yaliyokwa kwaajili ya waandishi wa habari akijiua fika Mpina ni Mbunge.

Hivyo kifungu hicho alichotumia Spika kumtuhumu na kumhumuku hakipo na kwa makosa ya nidhamu ambayo hayapo!

Vilevile Kifungu cha 34(1) G nacho hakihusiani na machapisho ya kila taarifa bali kinahusu kosa la kuchapisha kwa umma taarifa zilizoandaliwa mahususi kwaajili ya kuwasilishwa bungeni. Kifungu hiki hakihusiani na kosa la kinidhamu bali ni kosa la jinai kwa mtu yoyote atakayechapisha taarifa hizo tajwa ambapo ni taafira/nakala mahususi/rasmi kwaajili ya kupelekwa bungeni.

Wasilisho la Mpina kwa Spika alilotoa kuwasilisha vielelezo vya ushahidi kikanuni haliwezi kuwa taarifa rasmi ya bunge, ni mawasiliano ya kawaida ambayo yanawezwa kufanywa kati ya mbunge na mbunge, Rais au taasisi nyingine.

Kwa mujibu wa Kanuni ya 70, toleo la 223 inabainisha kuwa uthibitisho wa uongo siyo jambo la siri, linaweza kutolewa bungeni ambapo vyombo vya habari vipo na wananchi wanafuatilia. Hakikatazi kama Spika atatoa muda zaidi wa uwasilishaji huo, kwa Mpina kuongea na wanachi kabla au baada ya uwasilishaji huo kwa Spika.

Lakini pia upo ushahidi wa Wabunge ambao wamewahi kutoa ushahidi huo ndani ya bunge mbele ya waandishi wa habari na mijadala kuendelea hata nje ya bunge lakini hawajahi kushughulikiwa kinidhamu kwa kuliingilia bunge! Mfano tar 3 Juni, 2024 Mbunge Ole Sendeka alitoa ushahidi bungeni na kwenda mbali zaidi na kusoma baadhi ya barua bungeni ambapo waandishi wa habari walichukua tukio hilo, lakini hakuchukuliwa hatua zozote za kinidhamu.

Mpina anaujulisha umma kuwa hakutenda kosa lolote au kuvunja kipengele chochote cha kanuni ya 70 toleo la 223 ambacho ndiyo msingi wa agizo la Spika la la tar 14, Juni 2024.

Hata hivyo vielelezo ambavyo Mpina aliwasilisha kwa Spika hakuvitoa na kuvichapisha kwenye vyombo vya habari kwakuwa alijua huenda baadaye vitatumika kwaajili ya Kamati, Mahakamani au Bungeni.

Misingi ya mabunge yote Duniani imejegwa kwa uwazi, ukweli, uwajibikaji na Demokrasia, Mpina anasema inashangaza kuona Spika ambaye anasisitiza mambo kufanyika gizani

Kanuni ya 83(2) toleo la 2023 Taarifa ya spika imeeleza adhabu iliyopo katika kanuni ya 83(1) - wakati spika anaongea alisema apewa adhabu katika kanuni ya 83(2)
a) Kumuonya mbunge na kutaka ajirekebishe
b) Kumuamuru mbunge huyo kutoka nje ya ukumbi mara moja au abaki huko kwa muda wa kikao uliyosalia
c) Kumsimamisha kuhudhuria vikao visivyozidi 10 mfululizo

Kwa Spika kuruka adhabu za mwanzo na kwenda moja kwa moja kwenye adhabu ya 3, inaleta tafsiri kuwa Spika alikuwa akielekza kamati adhabu gani iamuliwe. Kaulli hiyo inafanya kamati ikose uhuru wa aina gani ya adhabu itolewe kutemea na ukubwa wa makosa.

Katika taarifa ya Spika hakuna mahala popote alipoweka rejea ya Mpina kuvunja kanuni yoyote ile ya bunge wakati akitoa taarifa yake bungeni.

Kifungu cha 26(D) na (E) sura 296 kilichoongezwa, kinatumika tu pale ambapo wasilisho la Mpina lingekuwa linamlenga Spika. Lakini je, wasilisho la Mpina dhidi ya waziri Bashe lililoisha kwa pongezi kwa Spika kwa uzalendo wake linahusika vipi vipi na kumvunjia heshima Spika?

Kitendo cha Mpina kufichua Waziri waliyekuwa amevunja Sheria za Bunge ilikuwa ni kitendo cha kulinda Heshima za Bunge, na siyo kubadilisha aliyefichua kuwa ndiyo mwenye makosa kwa kulidhalilisha bunge.

Spika alisema kosa lizingatie kanuni ya 83 lakini kamati ikazingatia kanuni ya 84, na hivyo kuleta kosa jingine ambalo Spika hakulitaja kwenye taarifa yake.

Kwa Spika kupeleka mashtaka na kutoa hukumu haikuwa sawa, kwa kufanya hivyo amesababisha haki isitendeke. Ambapo Mpina alihukumiwa bila kusikilizwa jambo ambalo linaenda kinyume na Katiba ya nchi.

Mbunge Mpina anasema alitegemea Spika angechukizwa Waziri Bashe pamoja na Waziri Mwigulu kutokana na ushahidi uliyopelekwa mbele yake, ambapo angetoa msimamo wa bunge, badala yake akachukiwa yeye aliyepeleka ushahidi.

Kasoro zilizojitokeza katika mjadala wa azimio la bunge 24 June, 2024
1. Taarifa ya Kamati ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge haikuwa sehemu ya shughuli za bunge (order paper) ya 24 June, 2024 hivyo kufanya wabunge wengi kutokuwa na taarifa ya kuwasilishwa kwa hoja hiyo.

2. Spika hakutoa utaratibu wa mwongozo wa namna ya kuchangia taarifa ya Kamati ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge badala yake alisema anayo orodha ya majina ya wabunge watakaochangia bila kueleza orodha hiyo ameipataje.

3. Spika aliwaruhusu baadhi ya wabunge kutumia maneno ya kutweza utu na lugha zisizo ruhusiwa bungeni kinyume na kanuni ya 71(1) I na J ya kanuni za kudumu za bunge toleo la 2023, wabunge waliopata nafasi ya kuchangia waliacha hoja ya msingi na kumshambulia Mpina huku Spika akiacha hali hiyo iendelee na kushindwa kutoa uamuzi kinyume na kanuni ya 78 ya kanuni za kudumu za bunge huku akijua ni kinyume na kanuni.

4. Spika hakumpa Mpina nafasi ya kuchangia hoja hiyo na kutolea ufafanuzi hata kwa baadhi ya mambo ambayo yalikuwa yakipotoshwa

5. Wabunge waliochangia hawakuwa na taarifa za kutosha kuweza kutoa maoni yao, sababu taarifa ilitolewa kwa kifupi bila kuwa na upande wa mpina pamoja na vielelezo alivyowasilisha.

6. Baadhi ya wabunge walisema wao ni Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa CCM na kwamba watenda kumshtaki kwenye vikao vya NEC kwa kutoa uthibitisho wa ulaghai na rushwa pamoja na uvunjifu wa sheria, badala ya waziri husika kuchukuliwa hatua. Waliingiza mambo ya chama kwenye mambo ya kiserikali huku wakijua ajenda za vikao vya NEC huwa ni za siri

7. Kitendo cha kumsimamisha mbunge vikao 15 mfululizo ilipaswa kujiridhisha pasi na mashaka ama bunge kuziona kasoro hizo zilizosababishwa na mbunge

Mpina awahakikishia wananchi kuwa haya yote yaliyotokea na aliyotendewa hayawezi kumtoa kwenye mstari wala kumrudisha nyuma katika harakati za kuhakikisha kwamba maendeleo yanapatitaka

Mpina aazimia yafuatayo;
- Kupeleka malalamiko yake ya kuondolewa bungeni kwa uonevu na kutokutendewa haki na Spika wa Bunge kwenye vyombo vya sheria ili vikapime na kutoa haki kwa mujibu wa katiba ya Tanzania na sheria za nchi

- Kumpeleka mahakamani waziri wa kilimo ndg Hussein Bashe na bodi ya sukari chini ya ibara ya 26 na 27 ya katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa kitendo cha kutoa idhini ya vibali vya kuagiza sukari kinyume cha sheria na kulisababishia taifa hili hasara kubwa

- Kuyafikisha hakamani makampuni yote yaliyojihusisha na ungizaji wa sukari nchini kinyume cha sheria.

====

Pia soma: Mpina kuwapelea Mahakamani Waziri Bashe na Bodi ya Sukari kwa kutoa idhini ya vibali vya kuagiza sukari kinyume cha Sheria

Mheshimiwaspika waBunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bi Tulia Amemuonea Msheshimiwa mpina kwa maelezo aliyoyatowa Mpina ana ahaki ya kusema ukweli ingawa ukisema ukweli ndio unapigwa vita Mheshimiwa Bache amefanya makosa kama anavyosema Mheshimiwa mpina na kusababisha bei ya sukari kuwa juu. Hakutendewa Haki Mheshimiwa mpina Ameonewa na Spika pamoja na kamati ya maadili ya bunge na wabunge wote waliounga mkono. Mheshimiwa Mpina ni mtetezi wa Wanyonge wananchi walala hoi hongera zake tuko pamoja nae siku zote asivunjike moyo awe mstari wa mbele kutetea maslahi ya Wananchi.
 
Ana maana kwa lipi zaidi?

Eti spika amaemtuhumu, wakati spika kamwambia apeleke ushahidi kama yu mkweli, ni takwa la kisheria za bunge unapomtuhumu kuwa ni muongo.

Huyu sasa nimeamini maneno ya Msukuma, ana matatizo binagsi, tazameni hata macho yake yanaashiria ni mwehu fulani.
Umeangalia Kikao Kizima???
Uliona alipotoa Taarifa akasema kama kazuiwa Kwnda bungeni wala kusogea Karibu na Bunge "aliuliza atawezaje kupeleka Ushahidi wake na utetezi wake?"
 
Umeangalia Kikao Kizima???
Uliona alipotoa Taarifa akasema kama kazuiwa Kwnda bungeni wala kusogea Karibu na Bunge "aliuliza atawezaje kupeleka Ushahidi wake na utetezi wake?"
kazuiliwa baadaya kupeleka kitu chake cha ushahidi na baada ya kusikilizwa kwa siku kadhaa na kamati.

Hukumu ya kuondoilewa bungeni imetolewa na bunge lote. Kila mtu kashuhudia.

zingine zote ni porojo zake tu.
 
Viva Luhaga Mpina ; uishi maisha marefu .
 
Huyo mpina anafikiri kamati iliwekwa ya nini? Kuchunguza na kupitia yasiyokuwepo?

Anacheza na akili za wajinga tu.
 
Katika maisha kila mwanadamu ni chawa kwa yule anaye mshabikia. Nawe ERoni ni chawa wa Luhaga Mpina


Wewe kwa akili yako tu hata kama ni cha wa mama na mama yake na mama yake mzaa mama yake unaona kuwa ni kweli sukari iliingizwa tani Elfu 60 isiyo na kodi tena imeagizwa kwa dharura halafu imeingia mtaani iuzwe zaidi ya sh. 2000/- Sukari kutoka Brazil haiwezi kuuzwa zaidi ya sh. 1800 iliwa na kodi . Sasa iweje sukari iliyofutiwa kodi iendelee kuuzwa sh . 3500/ - mpaka 5000/ - Ni wazi kuwa sukari haikuingizwa nchini bali walidanganya kama kawaida . Na mchezo huo unafanywa sana na hizo bodi zikishirikiana na Mawaziri na watendaji wengine kwenye wizara . Meli ilifika bandarini na kuegesha pale documents zikatolewa meli aikasepa na sukari yake . Ni meli tu iliokotezwa njiani na kuambiwa hebu njoo simama hapa kidogo halafu chukua mpunga wako kidogo sepa .

Kama kweli walikua wana nia ya kuondoa adha ya sukari nchini hawa wageni na sukari yao ya kigeni kwa Watangayika basi wangeruhusu Sukari toka Zanzibar ambayo ni washirika wa Muungano iingie kwa dharura.
Zanzibar ambayo mpaka mwaka jana sukari ilikua haijawahi kuvuka sh. 2000/- Kwanza wangeinua sasa Soko la Sukari Zanzibar na kuongeza kipato cha wananchi wa Zanzibar na kiwanda chao na wakulima wao.
Hili ina maana hawakuliona hao wazamagendo na sio Wazalendo wenu ?

Kenya kwa miaka yote wananunua mahindi Tanganyika kama ujirani mwema ! Lakini kama kweli palikua na nia ya dhati ya kuingiza sukari kwa nini tusiingize sukari toka Malawi?
Kama ni dharura kwa nini wasiruhusu wafanyabiashara wa Mbeya na Tunduma kuvuka Boda na kununua sukari ya Malawi kwa dha9iii0rura na kuwanufaisha watanzania wenye mitaji ya kawaida kama yule mfanyabishara wa makava ya Simu?

Kwa nini iwe ni dharura halafu iletwa na muuza Makava ya Simu asiyejua hara ubora wa sukari na hana hata Magodown ya kuhifadhi ani Elf 30 za Sukari?
Je , anaweza kutuonyesha walipohifadhi hiyo Sukari na aliisafirisha kwa fuso au IST au Boda boda au Kirikuu kwenda kwenye magodaoni ya mengine?

Ni wazi mchezo huu ndio uliomwondoa Kangi Lugola enzi za JPM japo Kangi hakuhusika na hakujua kua kuna mchezo kama huo wa kuagiza vitu hewa na pesa inapigwa na wajanja.

Serikali imeshajitoa kwenye uzalishaji wa sukari na haina kiwanda sasa haya mabodi bodi ya nini kama sio kufuja fedha za umma na kufanya michongo ya kishetani kwenye fedha za umma!!

Eti bodi ya Korosho inaundwa na Rais wakati serikali haina hata eka moja ya Shamba la korosho .
Bodi ya Kahawa wakati hakuna mashamba ya Umma. Ni wizi mtupu .

Basi wateue vijana wasio na ajira kwenye hizo bodi la hasha wanateua watu walioshindwa na kufilisi makampuni mengine.

Enyi CCM na watawala wake Msipotubu na kubadilika yanayotokea Huko kwingine huko yatawafikia na mali mnazizozivuna bila jasho zitachukuliwa bila jasho.

Mungu amechoka kusikia vilio vya watu wa nyonge kwenye nchi aliyoiumba na kuipa utajiri mkubwa ambao sio mali yenu wenyewe na familia zenu bali ni mali ya Watanzania mil. 65 pasiwe na anayekosa chakula wala dawa wala maji wala choo shuleni.
 
Back
Top Bottom