Mpira wa Tanzania unaendeshwa na wahuni, lililotokea Yanga Magoma yupo sahihi!

Mpira wa Tanzania unaendeshwa na wahuni, lililotokea Yanga Magoma yupo sahihi!

Cha kushangaza kila taasisi ina utaratibu na msemaji wake baada ya vikao lakini vijiwe vya wahuni kila mmoja ni msemaji sasa haji anahusikaje na ni nani ndio vibaka wenyewe hao!
Timu ina wasemaji kila mtaa..yani huyo nae anatoa tamko lake kama nani..na Ally Kamwe nae afanye nini...
 
Manara eti anamtishia huyo mzee...😃😃😃hivi Manara anajikuta nani pale Yanga..eti mm nimezaliwa Yanga..familia yangu imefanya makubwa kuliko familia zingine pale Yanga..yani huyo baba yake kucheza Yanga ndo kumfanye avimbe kuwa Yanga ni yake..wakati yupo Simba aliwadharau Yanga na kuwaita hawana akili na kusema yy akichanjwa damu yake ni Simba tupu...eti mtoto wa mjini sema watu wana mstahi tu kwa ule ulemavu wake..aache kubwabwaja...kina GSM kina Hersi wamenyamaza wamemuacha huyo mzee na ishu zake ila eti yeye huyo mzungu pori ndo kujiona mwamba...
Manara ana penda jazba na fujo sana,ni mtu wa ugomvi,hana busara kabisa
 
Mpira wa bongo umejaa wahuni ndio maana vilabu vinaongozwa na vibaka tu, wenye uwezo wa kununua suti na kupata sapoti ya watu wenye pesa kuongoza hivyo vilabu.

Juzi kati Simba watu wamebadishana uongozi kama vile wachezaji wanabadishana jezi au mbio za vijiti, hapo akitokea mtu mwenye kichaa akienda mahakamani kwa viongozi kutokufuata katiba na kuvunja kanuni.mahakama inampa ushindi kichaa.

Kibaka mmoja akishachaguliwa na klabu huteuwa vibaka wenzie wa kumlinda madarakani sio wale wenye klabu yao hapana, mfano Eng Hersi sijui kama ana washauri wazuri ni mambo yale yale badala ya kukaa chini akatafakuri hili jambo limetokea wapi .

Tunaona kila kibaka na muhuni anatoa tamko lisilo na mashiko wote wanamzodoa Magoma kwenye vyombo vya habari badala ya kuijibu mahakama kwa makaratasi, kila muhuni anajibu kivyake vibaka wanajibu barua ya mahakama kishabiki.

Msemaji kibaka anajibu pumba mwanasheria kibaka anajibu kihuni bila kufuata sheria mwisho wa siku waandishi vibaka wamekuwa wapotoshaji kuisemea klabu badala ya kumshauri kiongozi atulie afuatilie sakata liliopoanzia na kulimaliza!

Tufikie mahali vilabu visiendeshwe na wahuni kuepuka haya yanayotokea kisa wanachama na mashabiki ni njaa kali wanafikiri tajiri hawezi kushitakiwa.

N:B Magoma ni mtanzania shabiki na mwanachama yanga anayo haki ya kufungua kesi mahakama yeyote nchini tanzania na akasikilizwa kama mambo hayaendi sawa!
muombe sana Mungu akuzidishie akili hapo ulipo sipo
 
Manara ana penda jazba na fujo sana,ni mtu wa ugomvi,hana busara kabisa
Ana shida ya kisaikolojia sio bure...na wanao muunga mkono na kumpa kichwa ni wale ambao pia hawajiamini na wamejikatia tamaa...wanaona wanapata faraja kupitia mdomo mchafu wa huyo mtu..
 
Siifahamu, maneno ya kichawi hayo.

Labda alimaanisha "kulu juan", linamaanisha "wote njaa ". Wazee wa zamani walikuwa wana msemo wa "muombee adui yako njaa".

Huyo poyoyo kalisikia tu hilo neno kwenye vijiwe vya kahawa wala hajuwi linaaminisha nini na hata kulitamka hajuwi.
Akirusha hilo kombora hata humu JF kutakuwa ni vilio vitupu maana jana kapewa kila aina ya tusi. Yanga itashuka hadi ligi daraja la 3, ikacheze na Bom Bom FC.
 
Mpira wa bongo umejaa wahuni ndio maana vilabu vinaongozwa na vibaka tu, wenye uwezo wa kununua suti na kupata sapoti ya watu wenye pesa kuongoza hivyo vilabu.

Juzi kati Simba watu wamebadishana uongozi kama vile wachezaji wanabadishana jezi au mbio za vijiti, hapo akitokea mtu mwenye kichaa akienda mahakamani kwa viongozi kutokufuata katiba na kuvunja kanuni.mahakama inampa ushindi kichaa.

Kibaka mmoja akishachaguliwa na klabu huteuwa vibaka wenzie wa kumlinda madarakani sio wale wenye klabu yao hapana, mfano Eng Hersi sijui kama ana washauri wazuri ni mambo yale yale badala ya kukaa chini akatafakuri hili jambo limetokea wapi .

Tunaona kila kibaka na muhuni anatoa tamko lisilo na mashiko wote wanamzodoa Magoma kwenye vyombo vya habari badala ya kuijibu mahakama kwa makaratasi, kila muhuni anajibu kivyake vibaka wanajibu barua ya mahakama kishabiki.

Msemaji kibaka anajibu pumba mwanasheria kibaka anajibu kihuni bila kufuata sheria mwisho wa siku waandishi vibaka wamekuwa wapotoshaji kuisemea klabu badala ya kumshauri kiongozi atulie afuatilie sakata liliopoanzia na kulimaliza!

Tufikie mahali vilabu visiendeshwe na wahuni kuepuka haya yanayotokea kisa wanachama na mashabiki ni njaa kali wanafikiri tajiri hawezi kushitakiwa.

N:B Magoma ni mtanzania shabiki na mwanachama yanga anayo haki ya kufungua kesi mahakama yeyote nchini tanzania na akasikilizwa kama mambo hayaendi sawa!
Nothing will change.
 
Back
Top Bottom