Kweli Kiongozi. Shida iko hapo.Wapo busy na bongo fleva..
Sasa b17 unabakiaje bongo tena?
Wala haihusiani na utawala mkuu,kumtia mtu hatiani tena case kama hizi sio kazi rahisi,ndio maana unaona hata wazee wa Escrow waliitwa mezani tu wakayaongea maana battle ya kisheria one on one mahakamani serikali ingepigwa tu..Huyu mr kuku labda wafanye nae plea bargain la sivyo akiwa na lawyer makini na hela anayo anashinda fresh tu..Labda utawala mwengine sio huu! Ukae ukijua kampeni ni mwezi wa 10 hapo, 3 months ahead! Na nimesikia tetesi bureau de change zinafunguliwa.
Anashindaje? Wakati vipengele vya wazi kabisa kavivunja.Wala haihusiani na utawala mkuu,kumtia mtu hatiani tena case kama hizi sio kazi rahisi,ndio maana unaona hata wazee wa Escrow waliitwa mezani tu wakayaongea maana battle ya kisheria one on one mahakamani serikali ingepigwa tu..Huyu mr kuku labda wafanye nae plea bargain la sivyo akiwa na lawyer makini na hela anayo anashinda fresh tu..
Ili wataifishe pesa nyingi za waliotapeliwa, kwakuwa hawarudishiwi waliozichanga, kwakuwa nao pia wanamakosa.Kijana amebuni njia yake yakujipatia cake ya Taifa, jamaa wa Taifa wameona amezikusanya wameamua kufanya yao.Kwanini wasingemzingua kabla hazijafika kiasi hicho?
Sheria zina mambo na technicallities nyingi, Zombe alitoka kwenye kesi ya wazi kabisa.Anashindaje? Wakati vipengele vya wazi kabisa kavivunja.
Hela jinsi unavyozipata utamu unaongezeka kuzitafuta zaidi. Pia kama ni kuexit labda kuepuka tu mkono wa dola ila asingeweza kutoka na huo mpunga wote. Cha muhimu kama alijua ni kitu haramu anafanya angestop baada ya kufika point flani na kusepa mapema.Hakujua yani, angejua angekuwa ame exit mapema sana. Inaonekana ni wale machalii much know wakishika hela. Inaonesha hakuwa benet na wanasheria!
Kinachofanya ushinde sio wingi/uzito wa tuhuma mkuu,ni case proceedings(mwenendo wa kesi).Kina rugemalila walipewa tuhuma kibaao mwanzo ila kadri muda unavyoenda zina drop moja moja tu,mwisho serikali ikaomba plea bargain...Unawakumbuka wale jamaa wa EFD walikuwa wanapiga 7M per day?,Sidhani kama wapo gerezani sasa hivi..Plea bargain.Anashindaje? Wakati vipengele vya wazi kabisa kavivunja.
Vere turuu!! Hivi sijui ni nini huwa kinatupumbaza kiasi ambacho huwa tunasahau kufikiria. Benki zenyewe zinatoa interest ya 16% average maximum (Sijui kama inazidi hapo) kwa mwaka, na zinaendeshwa kitaalamu; halafu kuna ngómbe moja inakuja inawaaminisha watu kwamba unaweza kupanda leo ukavuna mara tatu ya ulichopanda ndani ya miezi sita!!!Hivi bado tuna watu wajinga kiasi hichi wanaoamini kuna hela rahisi kiasi hicho? yani mtu anakwambia uweke laki 5 upate 5m na wewe unaamini kweli?
Poleni sana! ingekua rahisi hivyo kila mtu angekua bilionea na tungekua uchumi wa juu....Mo angeweka bilioni mia ili apate trilioni kumi!
The end doesn't justify the means. Nchi inaendeshwa kwa sheria na taratibu; so hakutakiwi kuwa na excuse yoyote ya kufanya uhalifu; kosa liitwe kosa - kusiwe na lakini.... otherwise kila mtu atakuwa anavunja sheria akijua kuwa kuna mahali atasamehewa makosa yake ikiwa ataleta matokeo mazuri. Vipi kama akisababisha madhara kwa hicho anachofanya? Utasikia kila mtu anailalamikia serikali kuwa ilikuwa wapi kumchukulia hatua huyo mtu. Kwahiyo kwamba ameajiri watu, amelipa kodi, amenyoosha maisha ya watu bado haiondoi ukweli kuwa amefanya uhalifu. Hata wauza madawa ya kulevya wanaajiri watu, wanalipa kodi na wanawafanya watu watoboe... lakini madhara yake ni makubwa kuzidi faida.Watanzania hatutatoboa kwa majungu. Mtu ameanza kidogo kodogo, sasa ametoboa na anasaidia wengi, badala umfanyie promo watu wainuke, unamwekea vikwazo.
Ameajiri wangapi?
Kodi kiasi gani kinalipwa?
Maisha ya wangapi yamenyooka kwa juhudi zake?
Kama halipi kodi ipasavyo, aelimishwe alipe kodi hizo siyo kumfunga.
Ujinga na kukomoana. Halafu sisi watumishi wa serikali tunaotegemea mishahara na rushwa za wananchi hatuwawazii mema wahangaikaji. Wakitoboa tunanuna.
Tuanzishe kazi za mikataba tu, nadhani tutaheshimiana
Unapata fedha kwa Njia haramu ka kutapeli au kuuza madawa ya Kulevya then unatumia hizo Pesa kufungua Biashara Halaliii ili ionekane zile pesa unazipata toka kwenye hiyo biashara kumbe ni UongooIvi kutakatisha pesa ni nn??????
The end doesn't justify the means. Nchi inaendeshwa kwa sheria na taratibu; so hakutakiwi kuwa na excuse yoyote ya kufanya uhalifu; kosa liitwe kosa - kusiwe na lakini.... otherwise kila mtu atakuwa anavunja sheria akijua kuwa kuna mahali atasamehewa makosa yake ikiwa ataleta matokeo mazuri. Vipi kama akisababisha madhara kwa hicho anachofanya? Utasikia kila mtu anailalamikia serikali kuwa ilikuwa wapi kumchukulia hatua huyo mtu. Kwahiyo kwamba ameajiri watu, amelipa kodi, amenyoosha maisha ya watu bado haiondoi ukweli kuwa amefanya uhalifu. Hata wauza madawa ya kulevya wanaajiri watu, wanalipa kodi na wanawafanya watu watoboe... lakini madhara yake ni makubwa kuzidi faida.
Kwa mfano huyu bwana angeamua kusepa na mipunga ya watu... mngesemaje? Well, tuseme jamaa ni mwaminifu hawezi kusepa na mipunga ya watu; vipi kama akiamka siku moja akakuta kuku wote wamekufa, atawalipa nini wawekezaji wake? Is he insured? Kama unafikiri napiga porojo kamuulize Ontario atakusimulia kilichowakuta na TMT yao. Mpaka leo kuna watu wanatamani wamrarue Ontario - lakini na yeye aliajiri watu, alilipa kodi na aliwafanya baadhi ya watu watusue.
Na vipi kama watu wanamtumia yeye kutakatisha pesa = yaani wanafanya mishe haramu (Mfano kuuza madawa ya kulevya) halafu mapato wanayopata wanaenda kuwekeza kwa jamaa. How does he screen them? Hapo ndipo serikali inaposisitiza kuwa lazima uwe na leseni, kwasababu leseni hupewi kizembe - lazima wawe na uhakika kuwa hakuna janja janja utafanya kwenye pesa za watu, wala hutapokea pesa zilizotokana na mishe za kijanja janja.
Jamani, mnataka watapeliwe angalau watu wangapi ndo hili somo liwaingie? Tujifunze kutokana na makosa, lakini hayo makosa sio lazima tuyafanye sisi.