Mradi wa Bagamoyo: Hujuma Tanzania na ushindi kwa Kenya na Rwanda

Mradi wa Bagamoyo: Hujuma Tanzania na ushindi kwa Kenya na Rwanda

Zitto

Former MP Kigoma Urban
Joined
Mar 2, 2007
Posts
1,562
Reaction score
10,888
Nasubiri Bandari Kubwa ya Lamu izuie Bandari Ndogo za Dar na Mombasa: Namna Maarifa Madogo Yanavyoiua Bandari ya Bagamoyo na Kuifaidisha Kenya

Kumekuwa na mijadala mikali kuhusu Mradi wa Eneo la Kiuchumi la Bagamoyo. Mjadala huo wenye malumbano ya kurushiana shutuma umekuwa mjadala mbovu sana kwenye jambo nyeti la kiuchumi Kama vile Mradi wa Bagamoyo SEZ. Wanaounga mkono wanaona fursa za maendeleo katika Mradi, wanaopinga wakiona hasara nchi itapata. Wanaopinga wanawashutumu wanaounga mkono kuwa wanataka kuuza Nchi.

Kundi la wanaopinga linaongozwa na Rais John Magufuli, Spika wa Bunge ndg. Ndugai mwanzoni alikuwa kinara wa kuunga mkono Mradi kwa hoja nzito zenye nguvu. Lakini baadaye alisalimu amri kwa hoja dhaifu sana na hivyo kujisalimisha kwa Rais Magufuli kwenye hoja nyepesi zilizojaa woga na zisizo na tafakuri yenye mwono mpana wa Uchumi wa Jiografia.

Sasa inadhihirika kuwa Rais Magufuli anatumika dhidi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa maslahi ya Jamhuri ya Kenya. Nitafafanua.

Kila nchi ina picha kubwa katika mambo inayotaka kuwa (a grand vision). Picha hiyo kubwa inapaswa kuzingatia mazingira ya nchi husika (context) na namna ya kuyatumia mazingira hayo kufikia hiyo picha kubwa. Tanzania na Kenya ni nchi ndugu ndani ya familia ya Afrika Mashariki. Nchi hizi pia ni Nchi shindani kiuchumi. Ni nchi pekee za Afrika Mashariki ambazo zote zina pwani ya Bahari (access to the sea). Lakini Tanzania ina Pwani ndefu zaidi kuliko Kenya na hivyo kuipa fursa kubwa zaidi.

Nchi zote mbili zinapakana na nchi ambazo hazina pwani. Kenya inapakana na Ethiopia, Sudani Kusini na Uganda. Tanzania inapakana na Uganda, Malawi, Zambia, Kongo DRC, Burundi na Rwanda. Tanzania ina fursa zaidi kuliko Kenya kutokana kupakana na Nchi nyingi zaidi. Kenya kwa muda mrefu imekuwa ikishika biashara ya nchi inazopakana nazo na isizopakana nazo pia. Tanzania imekuwa ikisuasua kufaidika na nafasi yake kijiografia katika kushika biashara ya eneo hili la maziwa makuu. Miji inayoongoza ushindani wa Biashara wa nchi hizi ndugu ni Mombasa na Dar es Salaam. Ni miji ya Bandari, yote ikitawaliwa na Sultan wa Zanzibar wakati fulani na baadaye wababe wa Vita za Dunia Uingereza na Ujerumani kugawana miji hiyo - Mombasa kwa Waingereza na Dar es Salaam kwa Wajerumani.

Hata hivyo Bandari zote hizi 2 zimekuwa ni Bandari za mizigo inayopita (transit goods) kwa kuwa vina vyake ni vidogo hivyo kuweza kupokea Meli ndogo tu. Meli kubwa kutoka China hufika Singapore na kupakua mizigo kuweka kwenye Meli ndogo zinazokuja kutia nanga Mombasa au Dar es Salaam. Meli kubwa kutoka Ulaya hushusha mizigo kwa Meli ndogo huko Bandari ya Salalah, Oman. Ili kuwezesha Meli kubwa kufika Pwani ya Afrika Mashariki, Nchi ndugu za Kenya na Tanzania zikaanza kuwaza na kuwazua miradi ya kufanya ili kuwa Kituo Kikubwa cha Biashara ya Bahari Eneo la Afrika Mashariki (transshipment hub). Mzozo wa kimkakati ulianzia hapo katika ya Nchi rafiki Kenya na Tanzania.

Jamhuri ya Kenya ilitumia diplomasia ya Hali ya Juu kuunganisha Nchi za Rwanda, Uganda, Ethiopia na Sudan ya Kusini kwenye Mradi wa picha kubwa wa Bandari ya Lamu. Ikazaliwa kinachoitwa ‘Northern Corridor’. Tanzania ikatengwa katika Afrika Mashariki (EAC) kikaanzishwa kitu kinaitwa ‘Coalition of the Willing’. Kenya wakazindua kwa fujo Mradi wa Bandari ya Lamu ili kuwa Bandari ya Meli kubwa za Afrika Mashariki. Marais wa nchi zote za coalition of the willing za EAC na nje ya EAC walikusanyika huko Lamu kuanzisha Mradi huo.

Uongozi wa Awamu ya Nne wa Tanzania chini ya Rais Jakaya M Kikwete nao wakaamua kutumia mtaji mkubwa wa diplomasia aliouacha Mwalimu Nyerere kujibu mapigo. Mapigo ya Lamu ni Bagamoyo. Rais Kikwete akafanikiwa kuwashawishi Rais Xi Jinping wa China na Sultan Qabos Bin Said wa Oman kuisadia Tanzania katika mpambano wa kuishika Bahari ya Hindi. China na Oman wakakubali kuanzisha Mradi mkubwa wa kituo cha Meli katika Afrika na Eneo Huru la Uchumi pale Bagamoyo. Mradi wenye thamani ya Dola za Marekani Bilioni 10.

Rais Jakaya Kikwete alifanya kosa analolijutia, naamini, mpaka sasa. Aliondoka madarakani bila kutia saini Mkataba wa Ujenzi wa Mradi. Makosa haya yanaigharimu Nchi sasa kwani ushindi wa kuimiliki na kuitawala Biashara ya Bahari ya Hindi upande wa Magharibi umekwenda Kenya bila hata risasi moja kurushwa. Mradi wa Bagamoyo umehujumiwa. Umekufa.

Baada ya Utawala wa Awamu ya Tano kuingia madarakani waliokuwa ‘coalition of the willing’ wakajisogeza karibu. Rwanda ikatangaza kuegemea Central Corridor. Tanzania ikabadili mpango wake wa Kujenga Reli kutoka Dar es Salaam kupitia Uvinza mpaka Musongati nchini Burundi na sasa ikaamua kuielekeza reli Isaka kwenda Rwanda. Badala ya Uvinza kuwa Kituo cha Biashara na Mizigo kwa Nchi za Maziwa Makuu, Sasa itakuwa Kigali, Rwanda.

Rwanda tayari imefungua Kigali Logistics Platform na Bandari huru ya Masaka (Kigali) yenye thamani ya Dola za kimarekani milioni 35. Bandari hiyo itaendeshwa na Kampuni kubwa duniani ya kuendesha Bandari iitwayo Dubai World. Kwa mkakati huu Rwanda itabeba mzigo wote kutoka DRC na kuhudumiwa kupitia Kigali, na hivyo Uvinza (Kigoma) kujifia kwa kukosa Biashara. Tanzania imepoteza kwa Rwanda.

Kenya kwa upande wake ilianza vibaya mahusiano yake na Tanzania ya utawala mpya. Katika hali ya kuweka maslahi ya nchi yao mbele wanasiasa wa Kenya waliamua kuungana katika kile kinachoitwa ‘handshake’, na ndugu Raila Amolo Odinga akapewa rasmi kazi ya kuhakikisha anasimamia hiyo diplomasia ya Kenya inafanikiwa. Propaganda kali dhidi ya Bagamoyo zikaanza na safari za Raila kuja kuonana na Magufuli zikawa nyingi pengine wakikutana Chato na pengine kwa Siri.

Baadhi ya watendaji wakanyweshwa sumu za ubovu wa mkataba wa Mradi wa Bagamoyo (ambapo hapakuwepo na Mkataba). Serikali ya Awamu ya Tano ikatamka rasmi kuwa hawataki Mradi ule kwa sababu za kitoto kabisa, kwani walitumia nyaraka za majadiliano na Mwekezaji. Spika wa Bunge alipoinua sauti yake akanyamazishwa. Vyombo vya Habari vikalishwa sumu na Mradi ukanuka. Msemaji wa Mradi wa Bagamoyo siku zote ni Wizara ya Viwanda na Biashara, lakini ghafla Mamlaka ya Bandari Nchini (TPA) ndio ikawa ndio Msemaji badala ya Wizara. Na baadhi ya Watendaji wa Serikali wenye mwono wa mbali walipotoa mawazo yao wakaondolewa kwenye nafasi zao.

Baada ya mradi wa Bagamoyo kuuawa, Waziri Mkuu mstaafu wa Kenya Raila Odinga akapewa tuzo na nchi yake kwa kuifanya Kenya kuwa mtawala wa Bahari ya Hindi, tuzo ya ‘Maritime Champion of the Indian Ocean’. Na Rais Kenyatta akawa rafiki ya karibu ya Rais Magufuli. Nchi yetu ikiwa imepoteza miaka minne sasa bila kutekeleza mradi wa Bagamoyo.

Ujenzi wa Bandari yenye kina kirefu ya Lamu sasa kuzinduliwa rasmi Novemba, 2019. Sasa Lamu itapokea Meli kubwa za 4th Generation kama vile Suezmax, Neo-Panamax na Chinamax. Mizigo kutoka Meli kubwa itashushwa Lamu na kupakiwa kwenye Meli ndogo kuja Bandari ya Dar es Salaam na kwenda Bandari nyengine za Afrika kama Beira na Durban. Hii ndio kazi ilikuwa ifanywe na Bandari ya Bagamoyo - Mradi ambao umehujumiwa. Pia Kenya wameamua kuchukua mpango mzima wa Bagamoyo na kuutekeleza Lamu kwa kuanzisha Eneo Maalumu la Uchumi. Hapo kabla ilikuwa iwe Lamu Port Pekee.

Watawala wetu wameonyesha uwezo mdogo sana wa kung’amua mambo na kujikuta kuwa sehemu ya Hujuma kwa Nchi yetu. Faida ya kijiografia ya nchi yetu ambayo Mungu alitupa tumeipoteza. Baadhi ya watu wanashangilia ujinga huu wa kiuchumi ambao tumeufanya bila kujua. Shida kubwa ya watu wenye mamlaka ya Dola katika nchi yetu hawasomi kujiongezea MAARIFA ili kuepuka hujuma dhidi ya nchi yetu, hujuma ambazo zitaathiri vizazi na vizazi.

Tumepoteza fursa ya nchi kwa sababu za kitoto, zisizo na maana na za kipropaganda tu. Kuendesha bandari miaka 99 mara tunataka miaka 33 haiwezi kuwa sababu kwa mtu mwenye akili timamu wakati Mradi ni Joint Venture na Serikali ni mbia mwenye hisa zinazotokana na ardhi yake. Kuna mwekezaji atabeba ardhi ya Tanzania kuipeleka China au Oman? Eti Bagamoyo itaua Bandari ya Dar es Salaam, kwa hiyo Ujenzi wa Bandari ya Lamu utaua Bandari ya Mombasa? Nasubiri kuona Bandari ya Dar ikifa kwa sababu ya ujenzi wa Bandari ya Lamu.

Biashara ya Bandari ya Bagamoyo ingekuwa kwa Meli kubwa kuleta mizigo na Meli ndogo kuja kubeba kupeleka Bandari za Afrika nzima kazi ambayo haifanywi na Dar es Salaam na wala haitaweza kufanywa kwa sababu Eneo la Bandari ya Dar ni dogo. Kazi ambayo sasa itafanywa na Bandari ya Lamu.

Hujuma hii kwa Jamhuri ya Muungano haipaswi kupita bila kulipiwa. Rais Magufuli na Serikali yake wanapaswa kulipa gharama ya hujuma hii kwa Nchi yetu. Wasipolipia watakuja Viongozi wengine kuhujumu nchi yetu kama hawa. Wakiadhibiwa itakuwa somo kwa wengine. Kwa uelewa mpana kuhusu Uchumi wa Bahari soma Gazeti la The East African la October 26 - November 1, 2019:
Inside Kenya’s plan to rule EA Coast.



Kabwe Z. Ruyagwa Zitto

Mbunge - Kigoma Mjini

Kiongozi wa Chama, ACT Wazalendo

Oktoba 28, 2019
 
Sawa mkuu nimekuelewa. Nadhani uzi huu uendelee na nondo nyingine zaidi kama; Expected return from Investment ya Bagamoyo port ili tujue tungeanza kuneemeka baada ya miaka mingapi ya uwekezaji.

Pia Sikubaliani sana na wewe kwenye suala zima la kuamini kuwa uamuzi wa kusitisha Bagamoyo Economic zone ni uamuzi wa Rais peke yake. Bila shaka majasusi wa kiuchumi waliokuwa kazini kabla ya kusaini mkataba huu ndio chanzo cha kuukataa.

China ni rafiki yetu hilo sikatai, lakini China wa enzi za baba wa taifa (Socialist China) sio huyu China wa sasa (capitalist China).
 
Nimesoma bandiko lako Zitto, lakini umeshindwa kumuelewa Rais Magufuli.

Ni kwamba Mh Magufuli hajakataa maradi wa bandari ya Bagamoyo. Alichokikataa Magufuli ni mkataba haujakaa kwa maslahi ya watanzania. Umekaa kwa maslahi ya wanaoujenga. Kitu ambacho hata sisi watanzania tunamuunga mkono kama mkataba umekaa kiunyonyaji hauna maslahi kwetu kuna haja gani kuendelea nao?

Mradi gani huo ambao serikali haitapata kodi, mradi gani huo ambao kama nchi haturuhusiwi kuendeleza au kujenga bandari nyingine yoyote kwa karne nzima hivi tumelogwa au?

Hapana tuendeleze tu bandari yetu ya Dar, Tanga na nyinginezo taratibu kwa maslahi yetu, badala ya kuwa na miradi feki isiyo na tija kwa nchi.

Huu ni ukoloni kama ukoloni mwingine tu, kama tutauza nchi kirahisi hivi. Kwa hili tumuunge mkono Rais Magufuli kwa maslahi ya nchi yetu. Huu ukoloni mamboleo tuukatae, chochote ambacho hakina maslahi kwetu tukatae.., hivyo hivyo watatuelewa tu.

Mambo ya kuuza rasilimali zetu tunajikuta tu watumwa hapana, hatutaki ya Zambia hapa..

Zitto kwa hii hoja yako itakushushia heshima na malengo yako ya mbeleni. Washauri wenye huo mradi uwe kwa maslahi ya wote. Kama haipo win win hiyo siyo biashara tena ni unyonyaji.
 
ZZK anatueleza mkakati wa Bandari ya Bagamoyo kuwa ni gateway ya imports.

Kwa mchumi yeyote ningetegemea angekuwa na in-depth analysis ya how do we strengthen production ya mazao ghafi na processing ili kuwa na certain ya exports.

JK toka 2013 mpaka 2015 anatoka madarakani alisita kusaini a go ahead. Unadhani kwanini year 1 imepita hakusaini,
Year 2 imepita hakusaini.

Year 3 anatoka madarakani early November bila kusaini. Nini alikiona kama sio favourable clauses ya mkataba mpaka 3 years zikakatika hakutia mkono.

Dr. Mpango waziri wa Fedha alikuwa mkuu wa Tume ya Mipango wakati wa JK; bila shaka alikuwa sehemu ya walimshauro JK asiwe "fasta" kusaini.

ZZK uliponda sana initiative za JPM na Prof. Kabudi kukaa na Barick na kushikilia makanikia in the name of tutashitakiwa. Leo hii uongo wako umeonekana wazi mchana peupe.

By the way, show by numerical projections namna gani Bagamoyo port could make a difference kwenye kuongeza revenues ambapo Mtwara, Tanga na Dar zime-fail ili ku-justify hoja yako.
 
Kwanza hiyo bandari ni white elephant, waliijenga ili kuhudumia shehena ya Ethiopia na Sudan ndio maana mradi unaitwa lapsset lakini cha kushangaza Ethiopia imejenga railway to Djibouti.

Wangefaidi kama kipindi kile Ethiopia ilivyokua haina mahusiano mazuri na Djibouti lakini baada ya kusameeana na kuungana mpaka Rais wa Ethiopia kapewa nobel maana yake hiyo Lamu haitapata hata container moja la Ethiopia.

Bandari Ya Mombasa ni kubwa na haijatumika yote kiasi cha kuhitaji bandari nyingine ya ziada.
 
Djbout bandari yao inaweza pokea Meli kubwa? Umemuelewa Zitto kwamba Lamu itahudumia hadi South Africa? Kwani South Africa haina Bandari?

Inazungumziwa Bandari ya kuwezesha meli kubwa kutia nanga kitu ambacho hakipo kabisa kwenye bandari karibia zote za Africa@Naton Jr,
 
Majasusi gani? Ndiyo hao walio mshauri kwamba Serikali ikanunue korosho kwa kutumia Jeshi? Kama ndiyo hao basi tuna shida kubwa na majasusi wetu.
Sawa mkuu nimekuelewa. Nadhani uzi huu uendelee na nondo nyingine zaidi kama; Expected return from Investment ya Bagamoyo port ili tujue tungeanza kuneemeka baada ya miaka mingapi ya uwekezaji. Pia Sikubaliani sana na wewe kwenye suala zima la kuamini kuwa uamuzi wa kusitisha Bagamoyo Economic zone ni uamuzi wa raisi peke yake. Bila shaka majasusi wa kiuchumi waliokuwa kazini kabla ya kusaini mkataba huu ndio chanzo cha kuukataa.
China ni rafiki yetu hilo sikatai, lakini China wa enzi za baba wa taifa (Socialist China) sio huyu China wa sasa (capitalist China).
 
Djbout bandari yao inaweza pinea Meli kubwa? Umemyelewa Zitto kwamba Lamu itahudumia hadi south Africa? Kwani South Africa haina Bandari?

Inazungumziwa Bandari ya kuwezesha meli kubwa kutia nanda kitu ambacho hakipo kabisa kwenye bandari karibia zote za Africa
Kuna Meli gani kubwa duniani kwa sasa ambayo haziwezi kutia nanga kwenye bandari ya Dar?

Sikiliza hiyo video, kina cha bandari ya Dar Ni kikubwa zaidi na kinao uwezo wa kuhudumia meli ya ukubwa wowote duniani
 
Mipasho ndo mbayo weza hakuna kitu kingine. Ndo uwezo unapo kita kwenye mipasho.

Msha lemazwa akili myu ana leta hoja ntia mnaanza tukana.

Pangua hoja kwa hoja kama unaweza. Ingawa najua huwezi kitu
Mbona wewe ndio unaweka mipasho na ushabiki zaidi?
 
Mtukufu Magufuli ameahidiwa vingi na Kenya kwa ajili ya uchaguzi wa 2020 lakini China siyo wajinga wapo kimya wanamhadaa kama wapo pamoja nae lakini moshi wa Ruangwa waliuona na hawapo mbali na ule moshi na pia wanajua kila kitu hata Spika ndungai mpaka leo anaumia moyoni.

Kwa kifupi Bandari ya Bagamoyo ingeleta mapinduzi makubwa kiuchumi na kuipelekea Tanzania kupiga hatua kubwa kimaendeleo, wapinzani wengine wa Bandari ya Bagamoyo ni msumbiji na Bandari ya Darban ambayo pia ina uwezo wa kupokea meli kubwa.
 
Majasusi gani? Ndo hao walio mshauri kwamba Serikali ikanunue korosho kwa kutumia Jeshi? Kama ndo hao basi tuna shida kubwa na majasusi wetu.
Mkuu, kumbuka mkataba wa Bandari ya Bagamoyo ni mkataba mkubwa na wa muda mrefu. Hata Jakaya mwenyewe hakutaka kuharakisha mkataba ule, huwezi kulinganisha mkataba wa Bandari na manunuzi ya korosho ambayo hata hivyo makubaliano ya ununuzi yamebatilishwa ndani ya muda mfupi (Chini ya mwaka mmoja).
 
Moja ya mambo ambayo nimeandika hadi vidole vimegoma kuandika ni suala la bandari!!! Na eneo ambalo Magufuli nimeamini ni muongo wa kupindukia ni suala la Bandari ya Bagamoyo!

Eti serikali haitapata chochote na mazuzu wanamshangilia!

Eti hata kodi hatutakusanya wakati duniani kote inafahamika kodi ni mali ya serikali!

Na kama alivyosema Zitto, hoja ya ardhi ni hoja ya kijinga!! Sheria ya ardhi inatamka wazi kwamba hati miliki inaweza kutolewa kwa miaka 33, au miaka 66 au 99!!!

Sasa mradi mkubwa kama wa bandari na economic zone hau-qualify hatimiliki ya miaka 99, ni mradi gani tena unaoweza ku-qualify?! Kama mradi mkubwa kama Bandari ya Bagamoyo stahili yake ni miaka 33, ni miradi ya aina gani tena itakayokuwa na sifa ya kuwa na hati miliki ya angalau miaka 66?

Ukweli ni kwamba, Magufuli anapenda sifa... angependa sana aonekane yeye ndie mwanzilishi wa ule mradi! Na hicho ndicho kinachomfanya akimbilie miradi mingi mikubwa ili apate hiyo status kwamba kama isingekuwa Magu, basi xyz usingekuwepo kama ambavyo amekuwa akitamba kwamba kama sisi yeye, ATCL isingekuwa na ndege!
 
Back
Top Bottom