Mradi wa Bagamoyo: Hujuma Tanzania na ushindi kwa Kenya na Rwanda

Mradi wa Bagamoyo: Hujuma Tanzania na ushindi kwa Kenya na Rwanda

Man, kwenye hili la bandari unatakiwa ukajipange upya manake maelezo yako yana mapungufu kadhaa!!!

Unachotakiwa kufahamu ni kwamba, kupitia China's Belt & Road Initiative, Mchina alijipanga kuwekeza kwenye miundombinu sehemu kadhaa duniani. Hili nalifahamu vizuri kwa sababu nilikuwa mbeba mikoba wa Beberu moja la Kimarekani wakati wa kufanya research, na moja ya case study ni Bandari ya Bagamoyo!!!

Katika kufikia hilo, Mchina akawa ameigawa dunia kwa mafungu... kule Ulaya akawekeza pesa ya kutosha kwenye Bandari ya Piraeus nchini Greece!!!

Kama alivyo beberu langu lile la Kimarekani linavyopinga hii miradi including mradi wa Bagamoyo, Mabeberu ya Ulaya yakaanza kumwekea figisu figisu Mchina kwenye Bandari ya Piraeus! Kuna wakati EU, huku Italy wakiwa ndi viherehere zaidi, wakaanza kusema kwamba China inaitumia Bandari ya Piraues kufanya biashara haramu!!

Cha ajabu, miezi kadhaa baadae, Italy ile ile ikaingia mkataba wa kibiashara na bandari ile ile!! Na bandari ile ile ambayo walikuwa wanaisemanga, leo hii imeingia kwenye Top 10 of largest terminal ports in Europe wakati uendelezaji wala hujafika ukingoni!!

Hilo ni la Ulaya! Mchina huyo huyo akataka kwenda kumchezea sharubu Marekani kwa kutaka container terminal ya South California! Hadi mara ya mwisho nafuatilia, Senate likaanza kutoa povu hawataki Mchina achukue terminal pale South Port!!

Hilo ni la Marekani!!

Tukija Africa sasa, Mchina anafahamu fika kwamba Africa ni emerging market.Strategy yake ikawa kuigawa Afrika kwa blocks! Kwenye Horn of Africa, akawekeza Djibouti ili hatimae mizigo yake itakayoenda ukanda wa Horn of Africa ipitie Djbouti!

Afrika Mashariki tukawa na competition kati ya Kenya na Tanzania huku Kenya akimkaribisha Mchina ajenge Lamu!!! Kenya walitoa incentives kibao lakini Mchina akachomoa na kuchagua Bagamoyo!

Unlike Djibouti na sehemu zingine Africa, Mchina alitaka kuifanya Bagamoyo iwe ndo central unit! I wish ungeiona ile plan, ambayo in the long run, makao makuu ya mkoa wa pwani yangehamishwa kutoka Kibaha to Bagamoyo!!

Ili kuifanya Bagamoyo kuwa Central Unit kwa kufuata mfumo ule ule wa Shenzhen Uchina, ikapangwa kujengwa not just a port but a megaport! Pamoja na hii megaport, pia na industrial complex pamoja na railway network to connect Bagamoyo na nchi zingine za ukanda wa maziwa makuu pamoja na kusini... Malawi, and Zambia in particular!!

Awamu ya 4 ya nne watu wamekula posho na kusafiri hadi Shenzhen kujifunza jinsi Shenzhen ilivyogeuzwa kuwa a fishing village like Bagamoyo!!

So, what was the idea?! Mega ships kutoka China zingekuwa zinafaulisha mzigo Bagamoyo na mzigo huo kuchukuliwa na meli za kawaida na kusambazwa sehemu zingine za Africa, na mali zingine zingetumia reli kwenda landlocked countries.

Pale Industrial Complex kungetokea mambo mawili!! Hivi sasa Uchina labor cost inapanda kila uchao! Kutokana na hilo, kulikuwa na uwezekano mkubwa Mchina akaifanya Bagamoyo Free Economic zone kama sehemu ya kuzalisha baadhi ya bidhaa zake za kulisha Afrika na maeneo mengine!

Kutokea Bagamoyo, bidhaa hizo zingesafirishwa kwa meli na zingine kwa reli kwenda landlocked countries!!!

Sasa unadai kwamba Kenya hatapata mizigo... man, unajidanganya!!! Salama yetu ni Mchina kurudi Bagamoyo vinginevyo, ile plan ya Bagamoyo anaweza kuihamishia Lamu ambako Kenyatta tangia mwanzo alisema msipojenga, tutajenga wewe!!!

Yule Beberu wangu kwavile sawa na mabeberu wenzake wanaipinga hii miradi ya Uchina, Bagamoyo Port included, moja ya hoja yake ilikuwa eti Bagamoyo Port will be too big for Tanzania's Economy, na kwahiyo Bandari ya Dar es salaam inatosha sana!!

Nilipomuuliza ikiwa na umaskini wetu wote huu pamoja na majirani zetu bado wakati mwingine Bandari ya Dar es salaam huwa inaelemewa! What if uchumi wa Tanzania na majirani zake ukipanda angalau kwa mara mbili tu hasa tukizingatia hata ukipanda mara mbili bado tutakuwa maskini!!
Ukisoma ramani ya kwanza ya Belt-Road Initiative utaona kwamba njia ni Pakistani hadi Lamu na siyo Bagamoyo. Hivyo ina maana Uchina alikuwa na mpango wa kujenga Mega-Port Lamu na siyo Bagamoyo, lakini Jakaya Kikwete akafanya yake.

Wanasemaga hivi, One man's poison is another man's meat: Sisi tumegoma, Wakenya washachangamkia dili mapema. Sasa sijui tumlaumu nani ???
 
Brother umeongea point.

Shenzhen ilikuwa ni pilot project ya Deng Xiaoping katika move yake ya kuibadiri China kutoka uchumi ule uliofeli wa Mao Tse Tung kuwa Uchumi wa kisasa ambao tunauona leo hii wachina wakinufaika nao.

Lazima Tuelewe, Kama Mababeru walivyokuwa wakipinga miradi ya nishati ya umeme ndivyo hivyo hivyo watakavyopinga maendeleo ya bandari, sababu ni mbili, Moja Afrika isijitegemee, pili Kuicontain China

China mwenyewe alipokuwa akitafuta uwekezaji kwa makampuni ya Mabeberu alijishusha kinyama, akakubali hata watu wake walipwe kiduchu ili kusustain investment. Leo hii mchina ana mihela mingi hadi anawakopesha hao mabeberu mapesa.

Just Imagine leo hata nchi ya Israel kwa kuona umuhimu wa investment ya wachina nao wameipa Uchina eneo ijenge bandari kama ambavyo Walitaka kujenga bandari nchini.

Tumepoteza nafasi hii kwa sababu ya EGO, EGO ya Jiwe badala ya kuangalia picha nzima za Tanzania ya miaka 100 ijayo yeye anaangalia Kampeni za uchaguzi za mwaka 2020

Suala si kujenga tu bandari, bali masharti ya uwekezaji huo. Tusingekuwa makini tungeenda kama wenzetu wa Zambia na Sri Lanka walivyofikia. Walifurahia bandari, lakini kilichotokea ni majuto, hawakuweza kulipia deni na kilichotokea waChina ikabidi wachukue bandari kwa muda wa miaka 100. Yaani wachina wana maarifa kuliko wakoloni waliokutana na akina Chief Mangungo.
 
Nimesoma bandiko lako Zitto, lakini umeshindwa kumuelewa Rais Magufuli.

Ni kwamba Mh Magufuli hajakataa maradi wa bandari ya Bagamoyo. Alichokikataa Magufuli ni mkataba haujakaa kwa maslahi ya watanzania. Umekaa kwa maslahi ya wanaoujenga. Kitu ambacho hata sisi watanzania tunamuunga mkono kama mkataba umekaa kiunyonyaji hauna maslahi kwetu kuna haja gani kuendelea nao?

Mradi gani huo ambao serikali haitapata kodi, mradi gani huo ambao kama nchi haturuhusiwi kuendeleza au kujenga bandari nyingine yoyote kwa karne nzima hivi tumelogwa au?

Hapana tuendeleze tu bandari yetu ya Dar, Tanga na nyinginezo taratibu kwa maslahi yetu, badala ya kuwa na miradi feki isiyo na tija kwa nchi.

Huu ni ukoloni kama ukoloni mwingine tu, kama tutauza nchi kirahisi hivi. Kwa hili tumuunge mkono Rais Magufuli kwa maslahi ya nchi yetu. Huu ukoloni mamboleo tuukatae, chochote ambacho hakina maslahi kwetu tukatae.., hivyo hivyo watatuelewa tu.

Mambo ya kuuza rasilimali zetu tunajikuta tu watumwa hapana, hatutaki ya Zambia hapa..

Zitto kwa hii hoja yako itakushushia heshima na malengo yako ya mbeleni. Washauri wenye huo mradi uwe kwa maslahi ya wote. Kama haipo win win hiyo siyo biashara tena ni unyonyaji.
Swala la mkataba ni tata naamini hata ww hujauona na kuusoma ili kusiwe na lawama ni bora mkataba huo ukapelekwa bungeni uchambuliwe ili kila mta aelewe ni nn kilichomo kuliko kuambiwa tu ni nani kati yao yupo sahihi kutokana na mkataba? Weka mambo hadharani kila mtu achambue
 
"Pale Industrial Complex kungetokea mambo mawili!! Hivi sasa Uchina labor cost inapanda kila uchao! Kutokana na hilo, kulikuwa na uwezekano mkubwa Mchina akaifanya Bagamoyo Free Economic zone kama sehemu ya kuzalisha baadhi ya bidhaa zake za kulisha Afrika na maeneo mengine"

Tumekosa tu viongozi makini ili kutatua hali ya uchumi wetu ila Tz ingekua industrial superpower katika Africa hi Ndege flyover zingekuja kama mahitaji ya industriazation
Labor Cost ya Uchina ni ya bei ya chini duniani, lakini Afrika ndiyo chini zaidi. Wanasema Technician au Fundi Mchundo wa Tanzania, Kenya na Ethiopia mwenye kiwango kilekile na yule wa Uchina, analipwa mshahara mdogo mara kumi ya yule wa Uchina.

Gharama za uzalishaji zinaanza kumzidia Uchina maana watu wa kipato cha kati wameanza kuwa wengi. Sehemu rahisi ya kukimbilia ni Afrika ambako ndiyo kuna Cheap Labor. Sasa wahafidhina watakwambia Wachina watakimbilia Afrika ili kukwepa hilo.

Lakini wanasahau jambo la msingi kwamba idadi ya watu wa Uchina inazeeka au The Population is Aging na hivyo nguvu kazi kubwa ya vijana wa Uchina itahitajika kule kwao zaidi ya kuwaleta huku Afrika. Hapa Afrika watafanya waafrika wenyewe ili kupunguza gharama za uzalishaji.

Sasa sijui kwanini huwa tunaangalia mambo ya miaka 10 au 20 mbele tu. Tunakwama wapi......???
 
Tatizo kubwa ni kwamba watu wengi hata ZK hajui return ya bandari, na risk ya Bagamoyo kuwa chini ya muwekezaji yeyote yule; awe China, USA, UK, France.

Serikali ya Tanzania hasa taasisi rais wamefanya jambo la msingi kuliko mtu yeyote anavyoweza kueleza na kuandika.

Mfano, Hapo Bagamoyo pakijengwa kwa China kumiliki atakachokifanya ni sabotage to Dar Port hapo Tanzania inakosa mapato yote ya Tanga, Mtwara na Dar Ports.

Viva Taasisi ya Rais, TISS na wote waliohusika kupindua meza.

Kwa hili naipongeza sana Tanzania.
Mkuu unataka kusema kwamba Lamu nayo itaivuruga bandari ya Mombasa si ndiyo ???

Hivi Chige umewahi kusikia nini kilitokea wakati reli ya TAZARA inajengwa: Unajua kampeni iliyopigwa na Marekani ili kuzuia ile kitu isijengwe ??? Basi kuna injinia mchina alikuwa ni mzee anasimulia hadi walivyopigana ngumi na wamarekani wakati wanatengeneza reli ile.
 
Kikwete hakusita kusaini bali alikuwa akisubiria upembuzi yakinifu ukamilike vizuri na ukaja kukamilika akiwa katoka ikulu na sasa aliyepo ikulu yeye kawapa Dili Bandari ya Lamu hataki meli kubwa kuja Tanzania


Huu?

 
Dah hapa ndo naamini watanzania tuna minyoo kichwani.

1. Hivi wachina wajenge afu wasilipe kodi hata cent lakini wawe huru kufanya biashara.
2. Wakae kwenye ardhi yetu miaka 99
3. Haturuhusiwi kuendeleza bandari yeyote zilizopo
4. Wasimamie wao for the whole period kweli. Ndugu zangu hawa hawa


Wanapinga miradi kama
1. Stiglers gorge
2. Reli
3. Ndege
I ambayo hii unakwenda kwa mwananchi wa kawaida moja kwa moja.
Sijui watanzania tunataka nini


Sisi hatukuwa tayari kupata uhuru au tunatakiwa kutawaliwa kidikteta for while hadi hadi tupate akili
Kwani walikataa kufanya mazungumzo upya?

Alichotaka bwana mkubwa ni yeye kuleta wawekezaji wengine ili tu achukue ujiko na si kitu kingine.
 
Suala si kujenga tu bandari, bali masharti ya uwekezaji huo. Tusingekuwa makini tungeenda kama wenzetu wa Zambia na Sri Lanka walivyofikia. Walifurahia bandari, lakini kilichotokea ni majuto, hawakuweza kulipia deni na kilichotokea waChina ikabidi wachukue bandari kwa muda wa miaka 100. Yaani wachina wana maarifa kuliko wakoloni waliokutana na akina Chief Mangungo.
Bandari ya Bagamoyo haijengwi kwa mkopo kama Sri-Lanka na Zambia. Hela zote za mradi wanatoa Uchina na Oman: hapa mnaogopa nini ???
 
Hoja nzima ya ZZK inamalizwa na hoja rahisi kwamba tukiamua kuijenga bandari ya Bagamoyo hata leo kwa mkataba unaofaa kwa maslahi ya umma shida itakua wapi? Kwa position yetu kijiografia tutaiua hiyo bandari ya Lamu haraka sana
 
Zitto asitulishe matango pori. Asijifanye ana uchungu sana na nchi wakati ni mchumia tumbo. Anamjua anayemtumikia. Apeleke njaa zake huko. Bandari ya Bagamoyo tutaijenga wenyewe siku tukiamua au siku tukimpata mbia ambaye na sisi tutanufaika. Zitto siyo mchumi pekee nchi hii. Nchi hii ina wachumi wengi tena mahiri kuliko yeye na njaa zake.
 
Story ndeefu wkt lengo la thread yako ni hapa tu ulipoandika.

'Tanzania ikabadili mpango wake wa Kujenga Reli kutoka Dar es Salaam kupitia Uvinza mpaka Musongati nchini Burundi'

Reli kutopitishwa Kigoma imekua Nongwa.
Umetisha...
 
Bandari ya Bagamoyo haijengwi kwa mkopo kama Sri-Lanka na Zambia. Hela zote za mradi wanatoa Uchina na Oman: hapa mnaogopa nini ???
Kweli akili ni nywele kila mtu ana zake. Ati fedha ni za wachina na wa omani sisi tusiogepe? Are you serious pal? Something very wrong is happening in your brain!
 
Zitto asitulishe matango pori. Asijefanye ana uchungu sana na nchi wakati ni mchimia tumbo. Anamjua anayemtumikia. Apeleke njaa zake huko. Bandari ya Bagamoyo tutaijenga wenyewe siku tukikaa sawa, lakini siyo kwa maslahi ya wache na Wachina.

Magufuli amesamehe Trilion 424 (Dola bilion 190) kwa ACACIA ambazo thamani yake ni kubwa kiasi kwamba tungeweza kujenga bandari ya bagamoyo bila kukopa wala kupata msaada wa nchi yoyote na kisha mapesa mengi tu yakabaki
 
Kweli akili ni nywele kila mtu ana zake. Ati fedha ni za wachina na wa omani sisi tusiogepe? Are you serious pal? Something very wrong is happening in your brain!

Mkuu point ya jamaa ni hii, Mchina na Muoman wanajenga everything kwa gharama zao.. Operation na usimamizi wa kila kitu ni wao ili warejeshe gharama zao kwa hiyo 90yrs baada ya hapo wanasurrender kwetu tunaendelea wenyewe... Zambia na Sri-lanka walikopa wajenge kwa maana ya kulipa, SGR ya Kenya anaiendesha Mchina kurudisha gharama zake nafikiri pia Kenya hawakukopa..
 
Dr. Mpango waziri wa Fedha alikuwa mkuu wa Tume ya Mipango wakati wa JK; bila shaka alikuwa sehemu ya walimshauro JK asiwe "fasta" kusaini

Philip Mango hakuwa na guts kumshauri Mkwere asisaini ule mkataba; mkwere ule mradi ndio ilikuwa lala salama yake ya kuendeleza kwao hivyo asingekubali kuacha kusaini!! Hii ndio ilikuwa kati ya ile mikataba alipokuwa anasaini MOUs hata bila kusoma hivyo bila shaka ulipofika wakati wa implementation machale yalimcheza.
 
Ukiwasikiliza wengi wa wanaojiita viongozi Tanzania ni wenye ufinyu wa akili na wasioweza kupambanua mambo
matokeo yake ndio kama hayo, wako radhi wanunue ndege au kujenga SGR na kuacha miradi sahihi kwa maslahi ya nchi na wananchi.

mimi nasubili nije nione SGR na ndege zitakavyoleta faida mwisho nchi ina 80pct ya electricity accessibility na ina ziada ya MGWT 300 out of 1500. Investments ya mgwt 2100 ya nini kwa sasa au hata miaka 20 ijayo tutakuwa na consumption ya chini ya mgwt 2500 mpaka hapo hatuna optimal resources allocation.Wachumi na wenye akili kubwa watanielewa logic yangu
Nafikili uwekezaji kwenye umeme ni jmabo la maana sana,,Huwezi kuwa na viwanda vikubwa vya Chuma bila umeme wa Uhakika,
 
Kwanza hiyo bandari ni white elephant, waliijenga ili kuhudumia shehena ya Ethiopia na Sudan ndio maana mradi unaitwa lapsset lakini cha kushangaza Ethiopia imejenga railway to Djibouti

Wangefaidi kama kipindi kile Ethiopia ilivyokua haina mahusiano mazuri na Djibouti lakini baada ya kusameeana na kuungana mpaka Rais wa Ethiopia kapewa nobel maana yake hiyo Lamu haitapata hata container moja la Ethiopia

Bandari Ya Mombasa ni kubwa na haijatumika yote kiasi cha kuhitaji bandari nyingine ya ziada
Wewe unaambiwa bandari zenye kupokea meli kubwa,sio bandari kubwa.
Ki ukweli nchi hii tuna safari ndefu mno maana vilaza walio soma wapo wengi mno,
Akina zidumu fikra za mwalimu hata kama si sahihi.
 
Mkuu point ya jamaa ni hii, Mchina na Muoman wanajenga everything kwa gharama zao.. Operation na usimamizi wa kila kitu ni wao ili warejeshe gharama zao kwa hiyo 90yrs baada ya hapo wanasurrender kwetu tunaendelea wenyewe... Zambia na Sri-lanka walikopa wajenge kwa maana ya kulipa, SGR ya Kenya anaiendesha Mchina kurudisha gharama zake nafikiri pia Kenya hawakukopa..
Mkuu sasa si bora kukopa kuliko kujitoa ufahamu namna hii? Hapa ni kama umeuza moja kwa moja. Sasa kulikuwa na mantiki gani ya kudai uhuru na kuwafukuza wakoloni wakati nao walikuwa wanajenga na kuendesha nchi yetu? Huoni Afrika Kusini ilivyojengwa? Lakini pamoja na kujengwa kote wananchi wake walikuwa hawana raha. Kwa nini tujiweke kwenye hali ngumu kama hii wakati kuna mambo mengi basic tunaweza kufanya yakanufaisha wananchi zaidi? Waje tuwekeze kwenye kilimo. Mazao yakivunwa tunagawana kulingana na makubaliano.
 
Mkuu sasa si bora kukopa kuliko kujitoa ufahamu namna hii? Hapa ni kama umeuza moja kwa moja. Sasa kulikuwa na mantiki gani ya kudai uhuru na kuwafukuza wakoloni wakati nao walikuwa wanajenga na kuendesha nchi yetu? Huoni Afrika Kusini ilivyojengwa? Lakini pamoja na kujengwa kote wananchi wake walikuwa hawana raha. Kwa nini tujiweke kwenye hali ngumu kama hii wakati kuna mambo mengi basic tunaweza kufanya yakanufaisha wananchi zaidi? Waje tuwekeze kwenye kilimo. Mazao yakivunwa tunagawana kulingana na makubaliano.
Duu, umepewa mfano wa HONGKONG, ilivyokuwa chini ya UINGEREZA kwa miaka 100, Leo imerudi CHINA na kuinufaisha China Kimaendeleo.
 
Natamani Bandari hii, ingelikuwepo Zanzibar kitambo lakini Tanganyika wakatuwekea kauzibe,
Eti nduguzetu wa damu.

Hapa ndo ninapoona kuwa CCM ni adui si wa Tanzania bara tuu bali Zanzibar pia.
Maana Inatumiwa na majirani kwa maslahi ya wengine si Tanzania.

Tumejitolea sana Majeshi yetu kuilinda serikali ya Kongo, sijui kwa maslahi ya nani? Majeneza kila mara yanarudi Nyumbani.

Msumbiji, Angola na sasa Rwanda inapaa kwa mgongo wetu na Kenya ndo hiyo.
Sijui hawa jamaa wanatuwekea Maraisi mamluki?
 
Back
Top Bottom