Mradi wa LNG: Tukicheza Vizuri wakati huu ni hakika Umasikini tutausahau Tanzania na Samia anaweza kuwa Rais Bora zaidi kuwahi kutokea Tanzania

Mradi wa LNG: Tukicheza Vizuri wakati huu ni hakika Umasikini tutausahau Tanzania na Samia anaweza kuwa Rais Bora zaidi kuwahi kutokea Tanzania

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Amani iwe nanyi wadau,

Hali ya bara ya Ulaya na Asia sio nzuri kwa sasa, Urusi anaonesha ubabe wa waziwazi kwa kuanza kurudisha maeneo ya uliokuwa Umoja wa nchi za kisovieti.

Wiki hii imeanza kwa moto baada ya Rais Putin kutangaza kuyatambua maeneo ya Donesk na Luhansk kuwa nchi huru ikiwa ni harakati za kutwaa majimbo haya kutoka nchi ya Ukraine.

Haya yakiendelea inaonekana nchi za Marekani na Washirika wake wa Magharibi hasa NATO (Nchi za Ufaransa, Ujerumani, Uingereza na nyinginezo) hawataki vita zaidi ya kumdhoofisha Urusi kiuchumi ili afe kiuchumi

Njia kuu inayotumika na inayotarajia kutumika kwa sasa katika kumdhoofisha Urusi kiuchumi ni kwa kuacha utegemezi wa gesi ya Urusi na ikumbukwe kuwa Urusi ndo nchi inayotegemewa hasa na nchi za Ulaya kwa usambazaji wa gesi

Kwa Ulaya Gesi ndo hitaji kuu la nishati kwa sababu ya Baridi kali ambayo inawafanya wategemee zaidi Gesi kwa ajiri ya kupikia na mahitaji mengine.

Jana usiku Kansela wa Ujerumani ametangaza kusitisha mpango wa Bomba la Gesi kutoka Urusi kuingia Ujerumani na kwenda nchi zingine za Ulaya huku Mataifa mengine ya Ulaya na Marekani wakiweka vikwazo vikali dhidi ya Rais Putin na mabenki yake.

Kwa sasa inaonekana nchi za Ulaya zimeanza kutupa macho kwa Tanzania kwa sababu ndo imeonekana kuwa nchi yenye siasa nzuri na yenye hifadhi kubwa ya Gesi ambayo wanaweza kuinunua na kuitumia baada ya kuachana na Urusi

Jarida Maarufu la kiuchunguzi The African Report limeandika makala hii jana

Baada ya kuona hali hii niliyoielezea hapo juu naona sasa Wazungu wako serious mradi wa LNG uanze haraka hapa Tanzania ili waachane na Urusi mazima.

Taarifa iliyotolewa na kampuni iliyo kwenye mazungumzo na Serikali ya Tanzania katika mradi huu ya Shell kuwa wako kwenye sehemu nzuri kimazungumzo na Tanzania kwa ajiri ya mradi wa LNG kuanza naona imekaa ki strategy zaidi kwa ajiri ya kuwatuliza wananchi wa Bara la ulaya ambao hadi sasa hofu yao kuu ni Maisha yatakuwaje bila Gesi ya Urusi?

Napenda kuipongeza serikali ya Tanzania kwa hatua waliyofikia kwenye mazungumzo ya uwekezaji mkubwa wa Gesi huko Lindi na Mtwara na napenda kuwahusia tu kikubwa ni kuwa hakikisheni tu nchi yetu inafaidika massively kiuchumi kutokana na huu mradi.

Kwa Rais Samia napenda kusema unaanza kusomeka kwenye ramani ya Dunia. LNG ndo main legacy yako, ukicheza vizuri hapa umaskini itakuwa historia Tanzania na utakumbukwa milele kama The best President ever to happen in Tanzania!

Muwe na siku njema!
IMG-20220223-WA0000.jpg
 
Nimekusoma ulichoandika mpaka pale uliposema nchi yetu ina siasa nzuri, huu upofu wa makusudi unaojitia unajidanganya mwenyewe, ni kama unajitekenya na kucheka peke yako.

Kuhusu hiyo LNG mtazipata wapi $30mil zinazohitajika kwenye huo mradi?

Kwa utoto ulioandika hapa, vipi kuhusu Nyerere Dam ndio pesa imeshachezewa pale kwa hiyo iachwe ipotee?

Kama hiyo ndio akili yenu, kwanini nisiamini mnataka kuanzisha mradi mpya wa LNG ili nanyi mpate nafasi ya upigaji ili kama ikitokea msipoukamilisha kama wa Nyerere Dam muwe mmeshaiba mnachotaka?

Naona umejaza uzi wako na yanayotokea ulaya kama vile hao wazungu wanatupenda sana sisi, unajidanganya tu, kwenye maslahi hakuna taifa litakalokubali kuwa nyuma ya lingine hata kama kila siku mtaenda kwao miaka kumi mfululizo.

Tusidanganyane, sharti mradi wa Nyerere Dam ukamilike kwanza kama kweli mnataka kuokoa pesa za walipakodi masikini wa Tanzania, badala ya kujitutumua na miradi mipya ya bei ghali ambayo hamuwezi kuikamilisha wenyewe, huu ujinga wa kujiona wajanja kwasababu mnakopesheka utaangamiza vizazi vya hili taifa.
 
Hata wa gesi enzi za Kikwete walisema ukianza uzalishaji hakutakua na tatizo la umeme na nchi itapata faida za madola mengi mpaka waitu tukawa na matuamaini ya maisha mazuri.

Lakini mpaka sasa tunaugulia maumivu ya maisha magumu.

Hii ndo Tanzania ndugu.
 
Aisee kama ukisikia kukosa Busara na kutokufikiria mbali ndipo huku.

Kama kweli kilichoandikwa hapo kwamba anafikiri mgogoro wa Russia na Ukraine utamnufaisha kuuza gas (kufikiri sio kosa ila watu kujua fikra zako, hususan hizo fikra kama hazina ubinadamu basi ni kosa kubwa), Hujui kesho itakuwaje na nani..., atakuwa nani.... Alafu anajimarket kama mtaka Amani Duniani..., wakati matendo yanaonyesha ni mtafuta Fursa

Lesson from the Godfather; Never let anyone know what your are thinking
 
Aisee kama ukisikia kukosa Busara na kutokufikiria mbali ndipo huku.....

Kama kweli kilichoandikwa hapo kwamba anafikiri mgogoro wa Russia na Ukraine utamnufaisha kuuza gas (kufikiri sio kosa ila watu kujua fikra zako, hususan hizo fikra kama hazina ubinadamu basi ni kosa kubwa), Hujui kesho itakuwaje na nani..., atakuwa nani.... Alafu anajimarket kama mtaka Amani Duniani..., wakati matendo yanaonyesha ni mtafuta Fursa

Lesson from the Godfather; Never let anyone know what your are thinking
Kaka hakuna siri duniani
 
Huo mradi si mwendazake aliusimamisha
Hata wa gesi enzi za kikwete walisema ukianza uzalishaji hakutakua na tatizo la umeme na nchi itapata faida za madola mengi mpaka waitu tukawa na matuamaini ya maisha mazuli.
Lakini mpaka sasa tuna ugulia maumivu ya maisha magumu.

Hii ndo tanzania ndugu.
 
Hata wa gesi enzi za kikwete walisema ukianza uzalishaji hakutakua na tatizo la umeme na nchi itapata faida za madola mengi mpaka waitu tukawa na matuamaini ya maisha mazuli.
Lakini mpaka sasa tuna ugulia maumivu ya maisha magumu.

Hii ndo tanzania ndugu.
Wakati wa Kikwete hatukufikia hatua ya uzalishaji wa LNG
 
Upo sahihi kabisa...

Mwaka 2018 niliwahi kuandika haya...


mkuuwakaya,

Nitajitahidi kueleza kwa uchache sana manake kwenye issue ya gas kuna mengi sana ya kueleza!!

Mosi; FAILURE kubwa ya JPM katika issue ya kutozingaatia vipaumbele basi ni suala la gas!

Kama kweli JPM ana lengo la kuwaondolea Watanzania umaskini basi TOP PRIORITY yake ingekuwa kwenye gas na wala sio ndege na wala sio viwanda!

Angeweka priority kwenye gas... akazuia ufisadi kwenye gas; na akajenga uchumi mzuri wa gas; hayo ya ndege na viwanda yangekuja automatically tena at advanced level!

Wakati tunaenda mwaka wa 3 sasa na bado ndo kwanza kafanikiwa kupata vindege 3 kiasi cha kutokuwa threat hata kwa FastJet; endapo angejenga na uchumi wa gas angeweza kununua hata Airbus 100 kwa mpigo na kuyatisha hata mashirika makubwa kama Ethiopia Airline!

Gas ni uchumi

Gas ni viwanda

Gas ni fimbo ya diplomasia

Gas ni fimbo ya siasa za kimataifa

Kufafanunua yote hayo kunahitaji muda!

Lakini kwa ufupi tu ni kwamba; leo ukizalisha gas na kusambaza throughout East Africa... hizo nchi zote zitakuheshimu!

Zitakuheshimu kwa sababu zitafahamu uchumi wao unategemea gas ya Tanzania!!

Yule Kagame aliyekuwa anamkejeli JK ingekuwa ukimpigia kufuli koki inayopeleka gas Rwanda; siku ya pili angepanda ndege kuja Dar kusawazisha hali!

Hiyo ndiyo gas!

Hata byproducts zinazotokana na natural gas processing ni malighafi tosha ya viwanda!

I hate to say this but to be honest hata kwenye madini alikowekeza nguvu nako ni wastage of time!

Sisemi apuuze kwenye madini bali ile nguvu aliyowekeza kwenye madini ndo angewekeza kwenye gas basi impact yake ingekuwa kubwa zaidi ya mara 10!

Ngoja nikuulize swali moja:

Hivi wazungu wakigoma kununua ile Tanzanite na Gold; alternatively tutaifanyia nini?!

Swali lingine dogo: Unaweza kunitajia nchi 3 tu duniani zinazokula bata kwa kutegemea uchumi wa madini?!

Jiulize maswali sawa na hayo upande wa gas!

Panapo majaliwa; ningependa tujadili kwa mapana na marefu; with statistics and figures na subject iwe: "A Comparative Analysis of the Gas and Mining Economy"

To sum up... JPM bado hajaiangalia gas kwa jicho pana kiasi hicho! Pamoja na madhaifu yote ya JK lakini inaelekea yeye aliiangalia gas kwa jicho pana na ndio maana ilikuwa ndiyo priority yake!

Na ngoja nikutoe shaka!

Gas tunayoizungumza hapa na aliyokuwa anaisema JK na Muhongo wake sio hii iliyoanza kupita kwenye Bomba la Gas la Mtwara!

Gas yenyewe haijachimbwa bado! Ile ya kwenye bomba is just a fraction of 57 trillion cubic feet of discovered gas reserve!!

Gas yenyewe ni ile ambayo kiwanda cha kuichakata ndo kile kilitarajiwa kujengwa pale Lindi!

Mradi wa kile kiwanda peke yake ni zaidi ya Shilling Trilioni 65... narudia; sio Bilioni 65 bali TRILIONI 65... Bajeti yetu miaka 2 na chenji inabaki!

Kama kumbukumbu zangu zipo sawa, kiwango hicho ni takribani mara 2 ya Market Cap ya Barrick Gold!

Barrick Gold ndio kampuni kubwa kuliko zote za uchimbaji dhahabu duniani!

Cortez na Goldstrikes ni among top 10 mines duniani na yote hiyo ipo USA na inamilikiwa na Barrick Gold Mines!

Chukua mapato yote (not faida) ya mgodi wa Cortez na Goldstrikes kwa miaka 10 ndipo labda unaweza kufikia hiyo Trilioni 65.

Hiyo ndiyo gas tunayoisema! Investment ya kiwanda cha kuichakata tu ni Bajeti yetu ya miaka 2!!

JPM bado hajaona ikiwa mradi kama huo unahitaji priority!

Aidha nikujuze lingine! Achana na simulizi za kwamba gas yote imechukuliwa na Wachina!

Makampuni yaliyofanya exploration ni ya Ulaya na America! They invested billions of T Shilling kufanya exploration! Aidha zote hizo ni gas and oil companies!

That said; there's no way pamoja na energy yote waliyotumia halafu gas yote wamwachie Mchina wakati wao hiyo ndiyo biashara yao ambayo wapo tayari hata ku-initiate War for the sake of their business... gas and oil business!!

Gas and oil business iliyozalisha:
Etihad Airways
Emirates
Qatar Airways

Hivi umeshawahi fika Qatar ukaona wa-Qatar wanavyoishi kama Wafalme?!

Ni nchi pekee duniani ambayo zaidi ya 80% ya population yake ni wageni! Ni wageni walioenda kutafuta na kufanya kazi huku wenyewe wakifanya kazi kifalme! All that is because of the fvcking gas and oil business ambayo JPM ni kama bado sio priority kwake!

Tungechimba ile gas wala tusingehitaji tena Stigler's Gorge!

Stigler's tungeiacha iendelee kuhifadhi uoto wetu!!

What about Sheria ya Mafuta na Gas ya 2015 pamoja na ile ya Sheria ya Matumizi ya Mapato ya Mafuta na Gesi?!


mkuuwakaya,

Nitajitahidi kueleza kwa uchache sana manake kwenye issue ya gas kuna mengi sana ya kueleza!!

Mosi; FAILURE kubwa ya JPM katika issue ya kutozingaatia vipaumbele basi ni suala la gas!

Kama kweli JPM ana lengo la kuwaondolea Watanzania umaskini basi TOP PRIORITY yake ingekuwa kwenye gas na wala sio ndege na wala sio viwanda!

Angeweka priority kwenye gas... akazuia ufisadi kwenye gas; na akajenga uchumi mzuri wa gas; hayo ya ndege na viwanda yangekuja automatically tena at advanced level!

Wakati tunaenda mwaka wa 3 sasa na bado ndo kwanza kafanikiwa kupata vindege 3 kiasi cha kutokuwa threat hata kwa FastJet; endapo angejenga na uchumi wa gas angeweza kununua hata Airbus 100 kwa mpigo na kuyatisha hata mashirika makubwa kama Ethiopia Airline!

Gas ni uchumi

Gas ni viwanda

Gas ni fimbo ya diplomasia

Gas ni fimbo ya siasa za kimataifa

Kufafanunua yote hayo kunahitaji muda!

Lakini kwa ufupi tu ni kwamba; leo ukizalisha gas na kusambaza throughout East Africa... hizo nchi zote zitakuheshimu!

Zitakuheshimu kwa sababu zitafahamu uchumi wao unategemea gas ya Tanzania!!

Yule Kagame aliyekuwa anamkejeli JK ingekuwa ukimpigia kufuli koki inayopeleka gas Rwanda; siku ya pili angepanda ndege kuja Dar kusawazisha hali!

Hiyo ndiyo gas!

Hata byproducts zinazotokana na natural gas processing ni malighafi tosha ya viwanda!

I hate to say this but to be honest hata kwenye madini alikowekeza nguvu nako ni wastage of time!

Sisemi apuuze kwenye madini bali ile nguvu aliyowekeza kwenye madini ndo angewekeza kwenye gas basi impact yake ingekuwa kubwa zaidi ya mara 10!

Ngoja nikuulize swali moja:

Hivi wazungu wakigoma kununua ile Tanzanite na Gold; alternatively tutaifanyia nini?!

Swali lingine dogo: Unaweza kunitajia nchi 3 tu duniani zinazokula bata kwa kutegemea uchumi wa madini?!

Jiulize maswali sawa na hayo upande wa gas!

Panapo majaliwa; ningependa tujadili kwa mapana na marefu; with statistics and figures na subject iwe: "A Comparative Analysis of Gas and Mining Economy"

To sum up... JPM bado hajaiangalia gas kwa jicho pana kiasi hicho! Pamoja na madhaifu yote ya JK lakini inaelekea yeye aliiangalia gas kwa jicho pana na ndio maana ilikuwa ndiyo priority yake!

Na ngoja nikutoe shaka!

Gas tunayoizungumza hapa na aliyokuwa anaisema JK na Muhongo wake sio hii iliyoanza kupita kwenye Bomba la Gas la Mtwara!

Gas yenyewe haijachimbwa bado! Ile ya kwenye bomba is just a fraction of 57 trillion cubic feet of discovered gas reserve!!

Gas yenyewe ni ile ambayo kiwanda cha kuichakata ndo kile kilitarajiwa kujengwa pale Lindi!

Mradi wa kile kiwanda peke yake ni zaidi ya Shilling Trilioni 65... narudia; sio Bilioni 65 bali TRILIONI 65... Bajeti yetu miaka 2 na chenji inabaki!

Kama kumbukumbu zangu zipo sawa, kiwango hicho ni takribani mara 2 ya Market Cap ya Barrick Gold!

Barrick Gold ndio kampuni kubwa kuliko zote za uchimbaji dhahabu duniani!

Cortez na Goldstrikes ni among top 10 mines duniani na yote hiyo ipo USA na inamilikiwa na Barrick Gold Mines!

Chukua mapato yote (not faida) ya mgodi wa Cortez na Goldstrikes kwa miaka 10 ndipo labda unaweza kufikia hiyo Trilioni 65.

Hiyo ndiyo gas tunayoisema! Investment ya kiwanda cha kuichakata tu ni Bajeti yetu ya miaka 2!!

JPM bado hajaona ikiwa mradi kama huo unahitaji priority!

Aidha nikujuze lingine! Achana na simulizi za kwamba gas yote imechukuliwa na Wachina!

Makampuni yaliyofanya exploration ni ya Ulaya na America! They invested billions of T Shilling kufanya exploration! Aidha zote hizo ni gas and oil companies!

That said; there's no way pamoja na energy yote waliyotumia halafu gas yote wamwachie Mchina wakati wao hiyo ndiyo biashara yao ambayo wapo tayari hata ku-initiate War for the sake of their business... gas and oil business!!

Gas and oil business iliyozalisha:
Etihad Airways
Emirates
Qatar Airways

Hivi umeshawahi fika Qatar ukaona wa-Qatar wanavyoishi kama Wafalme?!

Ni nchi pekee duniani ambayo zaidi ya 80% ya population yake ni wageni! Ni wageni walioenda kutafuta na kufanya kazi huku wenyewe wakifanya kazi kifalme! All that is because of the fvcking gas and oil business ambayo JPM ni kama bado sio priority kwake!

Tungechimba ile gas wala tusingehitaji tena Stigler's Gorge!

Stigler's tungeiacha iendelee kuhifadhi uoto wetu!!

What about Sheria ya Mafuta na Gas ya 2015 pamoja na ile ya Sheria ya Matumizi ya Mapato ya Mafuta na Gesi?!

c.c Malcom Lumumba
Na kuna siku niliwahi kusema hapa kwamba, position ya Tanzania relative to Europe ni fursa kubwa sana kwa sababu Putin amekuwa akitumia sana fimbo ya gesi, na kwahiyo lau kama tungekuwa tumechangamka, basi ukanda huu wa Africa... yaani Tanzania and Mozambique ingekuwa ndo kimbilio la Europe ukiacha Middle East.
 
Nimekusoma ulichoandika mpaka pale uliposema nchi yetu ina siasa nzuri, huu upofu wa makusudi unaojitia unajidanganya mwenyewe, ni kama unajitekenya na kucheka peke yako.

Kuhusu hiyo LNG mtazipata wapi $30mil zinazohitajika kwenye huo mradi?

Kwa utoto ulioandika hapa, vipi kuhusu Nyerere Dam ndio pesa imeshachezewa pale kwa hiyo iachwe ipotee?

Kama hiyo ndio akili yenu, kwanini nisiamini mnataka kuanzisha mradi mpya wa LNG ili nanyi mpate nafasi ya upigaji ili kama ikitokea msipoukamilisha kama wa Nyerere Dam muwe mmeshaiba mnachotaka?

Naona umejaza uzi wako na yanayotokea ulaya kama vile hao wazungu wanatupenda sana sisi, unajidanganya tu, kwenye maslahi hakuna taifa litakalokubali kuwa nyuma ya lingine hata kama kila siku mtaenda kwao miaka kumi mfululizo.

Tusidanganyane, sharti mradi wa Nyerere Dam ukamilike kwanza kama kweli mnataka kuokoa pesa za walipakodi masikini wa Tanzania, badala ya kujitutumua na miradi mipya ya bei ghali ambayo hamuwezi kuikamilisha wenyewe, huu ujinga wa kujiona wajanja kwasababu mnakopesheka utaangamiza vizazi vya hili taifa.
Kwa iyo unapingana na wachambuzi mahiri The African Report?

Unaonekana hata Elimu yako ni mashaka, kuna uhusiano gani kati ya LNG na Umeme au Bwawa la Nyerere?

Nani kakwambia LNG inatumia pesa za serikali?
 
Kaka hakuna siri duniani
Nani kasema ni Siri...., Kuna Tofauti kubwa kuwaza kwamba rafiki yako amefariki huenda yule kimada wake atakuwa wako...., Na kusema hadharani kwamba sasa rafiki amefariki kuna uwezekano kimada atakuwa wangu...., unaweza kumkosa hata huyo Kimada kwa kuonekana una roho ya ajabu....
 
Amani iwe nanyi wadau,

Hali ya bara ya ulaya na Asia sio nzuri kwa sasa, Urusi anaonesha ubabe wa waziwazi kwa kuanza kurudisha maeneo ya uliokuwa Umoja wa nchi za kisovieti.

Wiki hii imeanza kwa moto baada ya Rais Putin kutangaza kuyatambua maeneo ya Donesk na Luhansk kuwa nchi huru ikiwa ni harakati za kutwaa majimbo haya kutoka nchi ya Ukraine.

Haya yakiendelea inaonekana nchi za Marekani na Washirika wake wa Magharibi hasa NATO (Nchi za Ufaransa, Ujerumani, Uingereza na nyinginezo) hawataki vita zaidi ya kumdhoofisha Urusi kiuchumi ili afe kiuchumi

Njia kuu inayotumika na inayotarajia kutumika kwa sasa katika kumdhoofisha urusi kiuchumi ni kwa kuacha utegemezi wa gesi ya Urusi na ikumbukwe kuwa Urusi ndo nchi inayotegemea hasa na nchi za Ulaya kwa usambazaji wa gesi

Kwa Ulaya Gesi bdo hitaji kuu la nishati kwa sababu ya Baridi kali ambayo inawafanya wategemee zaidi Gesi kwa ajiri ya kupikia na mahitaji mengine.

Jana usiku Kansela wa Ujerumani ametangaza kusitisha mpango wa Bomba la Gesi kutoka Urusi kuingia Ujerumani na kwenda nchi zingine za Ulaya huku Mataifa mengine ya Ulaya na Marekani wakiweka vikwazo vikali dhidi ya Rais Putin na mabenki yake.

Kwa sasa inaonekana nchi za Ulaya zimeanza kutupa macho kwa Tanzania kwa sababu ndo imeonekana kuwa nchi yenye siasa nuri na yenye hifadhi kubwa ya Gesi ambayo wanaweza kuinunua na kuitumia baada ya kuachana na Urusi

Jarida Maarufu la kiuchunguzi The African Report limeandika makala hii jana

Baada ya kuona hali hii niliyoielezea hapo juu naona sasa Wazungu wako serious mradi wa LNG uanze haraka hapa Tanzania ili waachane na Urusi mazima.

Taarifa iliyotolewa na kampuni iliyo kwenye mazungumzo na Serikali ya Tanzania katika mradi huu ya Shell kuwa wako kwenye sehemu nzuri kimazungumzo na Tanzania kwa ajiri ya mradi wa LNG kuanza naona imekaa ki strategy zaidi kwa ajiri ya kuwatuliza wananchi wa Bara la ulaya ambao hadi sasa hofu yao kuu ni Maisha yatakuwaje bila Gesi ya Urusi?

Napenda kuipongeza serikali ya Tanzania kwa hatua waliyofikia kwenye mazungumzo ya uwekezaji mkubwa wa Gesi huko Lindi na Mtwara na napenda kuwahusia tu kikubwa ni kuwa hakikisheni tu nchi yetu inafaidika massively kiuchumi kutokana na huu mradi.

Kwa Rais Samia napenda kusema unaanza kusomeka kwenye ramani ya Dunia. LNG ndo main legacy yako, ukicheza vizuri hapa umaskini itakuwa historia Tanzania na utakumbukwa milele kama The best President ever to happen in Tanzania!

Muwe na siku njema!
View attachment 2128208
Hivi ww upo Tanzania au nje ya Tanzania, unaambiwa hii gesi inayochibwa tanzania sio ya tanzania ni ya viongozi wachache na wawekezaji.

Taifa halina chake hapo umasikini ni wetu milele
 
Nchi hii bado ina vijana wa ovyo wengi. Naona mnaanza kujitengenezea mwanya wa kula national cake ili hali raia wanalia kwa maisha magumu. Mnataka mrudishe siasa za gas ya Mtwara zilizoacha watu wakiwa vilema na wengine kulazimika kuzikimbia familia zao.
 
Tanzania ni mbali sana kusafirisha Gesi mpaka Ulaya, Ulaya target yao ni Ukraine ambapo ni karibu gharama itakua ndogo ya usafirishaji
 
Nani kasema ni Siri...., Kuna Tofauti kubwa kuwaza kwamba rafiki yako amefariki huenda yule kimada wake atakuwa wako...., Na kusema hadharani kwamba sasa rafiki amefariki kuna uwezekano kimada atakuwa wangu...., unaweza kumkosa hata huyo Kimada kwa kuonekana una roho ya ajabu....
Acha kuongea nadharia, Samia alikuwa Ulaya wiki hii iliyopita, Mkuu wa Kampuni ya Shell kaongea na shirika kubwa la habari la Ulaya Reutres juzi na kasema juu ya maendeleo ya mazungumzo na serikali ya Tanzania

Wachambuzi wa nje wameona hilo na wanaliongelea wewe endelea tu kudhani ni siri
 
Na juzi juzi tu hapa nilimwambia ndugu yangu MALCOM LUMUMBA maneno haya:-
Ndugu yangu MALCOM LUMUMBA

....Long time no see!!

Kwa heshima ya ndugu Jinga la Zamani alienialika, wacha nami niseme machache.

Hapa wacha niende moja kwa moja kwenye JNHPP ili nisiifanye post yangu kuwa ndefu maradufu..

Kwa hapa tulipofikia, hatuwezi kuendelea na yale mambo ya ku-abandon miradi mikubwa wakati tayari imeshameza mabilion ya pesa! Kwa maana nyingine, JNHPP Must Continue kwa sababu tayari pesa nyingi imeshaingia!!

Hata hivyo, wakati mradi huu unaanza binafsi niliupinga! Sikuupinga kwa sababu za kimazingira wala kwamba ni unsustainable lakini mimi ni muumini mkubwa wa Economic Multiplier Effect na Optimal Resources Allocation.

Dhana hii ya Multplier Effect nishaieleza sana huko nyuma! Na kwavile I believe in Multiplier Effect, kama ningewekewa option ya either JNHPP or LNG Project (Gas Industry) kama source ya uzalishaji umeme, I'll ALWAYS be in favor of the Gas Industry kwa sababu huko kuna HIGHER multplier effect kulinganisha na umeme wa maji!!

There's no match between the two!

Bidhaa Kuu kutoka JNHPP ni UMEME PEKEE, and there's little (if any) to no by-products zinazoweza kuzalishwa kupitia JNHPP! Kinyume chake, Bidhaa Kuu ya LNG Project ni Gas na sio umeme lakini hapo hapo unaweza pia kupata UMEME + TAKATAKA ZINGINE!

Kumbe basi, 99% ya Multiplier Effect inayoweza kupatikana kupitia JNHPP pia inaweza kupatikana kutoka LNG Project. Kinyume chake, mengi unayoweza kupata kupitia LNG Project HUWEZI KUYAPATA kupitia JNHPP!

JNHPP itatupatia tu UMEME utakosaidia ku-boost sekta zingine za kiuchumi na labda kufanya Electricity Export but only regionally. Multiplier Effect tunayotarajia hapa inaweza kutokana na kuongezeka kwa uzalishaji kwa sababu tutakuwa na umeme wa uhakika.

Hata hivyo, YOTE hayo pia unaweza kuyapata kupitia LNG Project...

Wakati hali ni hiyo kwa KNHPP, LNG Project inaweza kukupatia AT LEAST yafuatayo:-

1. Umeme... Wakati Umeme sio Main Product from LNG Project, pale JNHPP umeme ndiyo MAIN PRODUCT itakayotokana na investment husika!

Kwa maana nyingine, faida yoyote ya kiuchumi INAYOWEZA kupatikana kwenye JNHPP Project ambayo umeme wake ndio Main Product, pia INAWEZA kupatikana, tena kwa ukubwa wa maradufu kutoka LNG Project kupitia umeme unaoweza kuzalishwa ingawaje sio Main Product!

Na kama tunasema LNG Project izalishe UMEME TU basi umeme huo unaweza kutumika kote Sub-Saharan Africa tena kwa miongo kadhaa wakati JNHPP Project haina uwezo hata ku-sustain hata uchumi kama wa South Africa!

In fact, hata Kenya ukiwaambia waachane na vyanzo VYOTE vya umeme walionao na watumie umeme kutoka JNHPP tena peke yao, bado umeme huo HUWEZI kuwatosha!!

Hapa ili nieleweke labda niseme hivi: Kwa sasa Umeme wa Gas uliopo kwenye Gridi ya Taifa ni almost 57% ya umeme WOTE huku hydropower ikichangia roughly 37%! Hata hivyo, 57% hiyo inatokana na less than 7.5 Trillion Cubic Feet of Gas ambazo ndizo zimeanza kuchimbwa kutoka Songongo, Mkoani Lindi na Madimba, mkoani Mtwara! U

Ukitoa hizo 7.5 Trillion Cubic Feet of gas ambazo zimeanza kuchimbwa, kuna almost 50 Trillion Cubic Feet of gas ambazo HAZIJAGUSWA! And remember, hiyo 57% ya umeme unaozalishwa sio unatokana na full capacity ya hizo 7.5 Trillion Cubic Feet za gas... hell no!

NInachotaka kusema ni kwamba, at full capacity, hizo 7.5 Trillion Cubic Feet zinaweza kuzalisha maradufu ya umeme utakaozalishwa na JNHPP na hapo bado zile 50 Trillion Cubic Feet HUJAZIGUSA!

2. Gas.. Hii ndiyo MAIN PRODUCT from the LNG Project. Hapo juu tumeshaona Umeme unavyoweza kuwa another product from the LNG Project, BUT...

(a) Gas For Export: LNG ni biashara kubwa sana duniani, na kwahiyo ni EXPORTABLE Product world-wide na sio tu regionally kama tunavyoweza kusafirisha the ONLY JNHPP Product!

Watu wanaposikia Lindi inataka kujengwa LNG Plant, akili yao wanadhani ni substitutes ya JNHPP! Kwamba, lengo ni tufanye gas processing kisha gas itumike kuzalisha umeme!

Kutokana na imani hiyo ndo maana unakuta Wafuasi wengi wa JPM wanapinga sana ule mradi kwa kile wanachodhani una lengo la kufuta JPM Legacy kwenye Bwawa la Nyerere!!!

Hapa ieleweke tu kwamba HAKUNA MJINGA ANAYEWEZA KUWEKEZA USD 30 BILLION for kwa ajili ya kuzalisha umeme kwa nchi maskini kama Tanzania! Hizo almost TRILLIONS 70 zinarudi rudi vipi ikiwa main product ni umeme?!

Hiyo investment inafanyika kwa sababu almost 50 Trillion Cubic Feet of UNDEVELOPED GAS ni Huge Opportunity for Export na sio eti kuzalisha umeme ili hatimae kuua Legacy ya JPM kwenye Bwawa la Nyerere!

(b) Gas For Domestic and Industrial Use:- Asikuambie mtu... this's a huge business opportunity!

Tuchukue mfano mdogo tu wa hii tenda ambayo ilitangazwa na TPDC...

View attachment 2113381

Kabla hata hatujaingia huko kwenye gesi yenyewe, hebu tutafakari hiyo project! Yaani tunahitaji kiwanda kitakachoweza kuzalisha vifaa vifuatavyo:- HDPE pipes, HDPE fittings, Domestic Gas Meters and associated fittings, Commercial Gas Meters and associated fittings, and PRMS.

Na kwavile hiyo inaangukia kwenye Local Content, hiyo kazi inatakiwa kufanywa na Watanzania as per Sheria ya Mafuta na Gesi ya 2015!

Now tujiulize!!

Kama tunaamua gas infrastructure zifike hadi wilayani, hapo atakayepata tenda atalazimika kuzalisha hivyo vifaa kwa wingi gani, na angetoa ajira za moja kwa moja ngapi, indirect employment ngapi, na Wauza Mama Lishe wangeuza sahani ngapi za ubwabwa, ugali, chapati and everything else?

That's what we call: ECONOMIC MULTPLIER EFFECT! Gesi ipo LIndi na Mtwara lakini effect yake inasababisha kujengwa kwa kiwanda cha kutengeneza vifaa vya kujengea miundo mbinu ya usambazaji gesi! Hapo zitazalishwa aina ya ajira kama nilivyotaja hapo juu!

LNG Project inayopelekea kujengwa kiwanda tajwa hapo juu, effect yake itamkuta hadi muuza Mama Lishe, Muuza Genge, Mangi na Mpemba na maharage unga na mchele wao dukani, mkulima aliyezalisha hizo bidhaa, n.k kwa sababu pesa itakayotokana na hizo shughuli itakuwa inaenda moja kwa moja kwa wananchi na pesa hizo kuambukiza sekta zingine za kiuchumi na kijamii!

Hapo umeshazalisha tu vifaa tajwa... what next?

Hivyo vifaa vikishazalishwa ina maana itabidi iwepo kampuni nyingine/zingine za kutandaza hizo infrastructure Tanzania mzima! Kampuni hiyo nayo itatoa ajira za moja kwa moja, kwa vibarua na wauza Mama Lishe ambao pia wataambukiza sekta zingine kama nilivyotaja hapo juu!

Aidha, projects zote mbili... za kuzalisha vifaa na kusambaza miundombinu pia zitazalisha PAYE na Kodi zingine kwenda serikalini, na hatimae kuleta direct effect kwenye public services zitolewazo na serikali!

THAT'S WHAT WE CALL MULTIPLIER EFFECT in the national economy ambayo inapatikana hata kabla gesi yenyewe HUJAIGUSA!

Gesi imeshazalishwa, and ready for different uses! Je, miundo mbinu itaweza kufika kila mahali? HELL NO! This HELL NO is another business opportunity kwa sababu hatimae kutakuwa na new opportunity to Gas Vendors! Wenye uwezo watajenga Gas Fuelling Stations!

That's what we call Multiplier Effect!!

3. Gas By-Products:-

Nimeshajaza server tayari kwahiyo hapa niongee kidogo tu ingawaje kuna mengi zaidi ya kuongea!

Mali Ghafi zinazotokana na uchakataji wa gesi zinaweza kutumika kutengeneza bidhaa mbalimbali! Hapa tusiende mbali! Tayari kuna project ya USD 1.9 Billion kwa ajili ya ujenzi wa Kiwanda cha Mbolea ambacho kinatarajia kutumia Gas By-Products!

Tanzania hii HAKUNA Kiwanda chenye thamani hata nusu ya hicho kiwanda!! Now tujuulize: Kiwanda kama hicho kinaweza kuzalisha direct and indirect employment to the company ngapi, Mama Lishe wangeuza kiasi gani kwa vibarua na wafanyakazi, PAYE and other taxes zingelipwa kiasi gani...

THAT'S WHAT WE CALL MULTIPLIER EFFECT!

Sio viwanda vya mbolea peke yake vinavyoweza kutumia Gas By-Products! Kuna at least 4 MORE products, including Plastic Products zinazoweza kuzalishwa kupitia Natural Gas By-Products!!!

FAIDA zote hizo nilizotaja hapo juu, HUWEZI KUZIPATA kupitia JNHPP!!

Sasa akina sisi tulikuwa tunapinga JNHPP kwa sababu tunaamini LNG Project inaweza ku-offer almost everything that can be offered by JNHPP but MANY MORE at much HIGHER VALUE than what JNHPP can offer!!!

Kwenye uchumi tunazungumzia dhana ya optimal allocation of resources!! Tunaambiwa resources, kwa muktadha huu pesa, ni SCARCE! Hivyo basi, kidogo utakachopata unatakiwa ku-allocate kule utakopata MAXIMUM RETURNS, and not just RETURNS!

LNG Project inaweza Kujenga JNHPP with our own money in less than 5 years lakini JNHPP KAMWE haiwezi kuwa na uwezo wa ku-fully finance LNG Project!! Kumbe basi, kama tunaamini Hydropower ni CHEAP source of electricity, bado tungeweza kujenga mradi huo kwa pesa zetu sisi wenyewe miaka michache tu baada ya kuanza kuzalisha gesi!

ALL IN ALL, should we expect CHEAP ELECTRICITY from JNHPP?!

Kwa maoni yangu, sioni hiyo cheap electricity inapatikana patikana vipi!!

Kwahiyo ndugu yangu Malcom, ule mpango wako wa kusambaza mashine za kusaga Tanzania mzima kwa sababu kuna umeme wa bei rahisi unakuja, man, ningekushauri pitia vizuri plans zako kwa sababu I strongly believe umeme wa bei rahisi HAUTAKUWEPO!!

WHY?

1. Mradi utatumia takribabi Sh 7 TRILLION. Hapo zijaweka riba za mabenki kwa sababu funding sources zingine zinatoka kwenye private banks!

Sasa kama tunadhani umeme utakuwa wa bei rahisi, who will pay hizo TZS 7 Trillions + Interests?! LAZIMA Watumiaji tulipe hizo gharama!!!

2. Watanzania tunadhani umeme utakaozalishwa pale ni MWINGI kweli kweli!!

Guys, kinachozalishwa pale sio kwamba Umeme Mwingi bali Umeme unazalishwa kwa ajili ya jamiii yenye Umaskini Mwingi!!

Kama nilivyosema hapo awali, Kenya ni nchi maskini tu! Lakini leo tuseme Kenya iachane na vyanzo vyote vya umeme inavyotumia hivi sasa na badala yake waanze kutumia umeme MWINGI utakazozalishwa pale JNHPP, katu Umeme huo HAUTAWATOSHA!!

Hata Tanzania kwenyewe, na umaskini wetu huu halafu tuseme tufunge vyanzo vyote vya umeme tulionao na tuanze kutumia tu Umeme MWINGI kutoka JNHPP... it'll take us less than 5 years kabla hatujaanza kuwa na uhaba wa kutisha wa umeme kwa sababu pale hakuna umeme mwingi bali tuna umaskini mwingi unaofanya less than 3000MW zionekane ni umeme mwingi!

Ninachojaribu kusema ni nini: Endapo uchumi wetu unaongeza kwa angalau 10% TU, umeme kutoka JNHPP + Available Sources HAUTAWEZA kuhimili uchumi huo ambao kimsingi na wenyewe utakuwa ni uchumi wa kimaskini tu!!!

Kwa maana nyingine, hata kabla hatujamaliza deni la TZS 7 Trillion za JNHPP basi kuna uwezekano mkubwa sana demand ya umeme nchini inaweza kuongezeka hapo mbeleni na kumeza umeme wote tulionao hivi sasa + Umeme wa JNHPP!

Demand ikiwa kubwa, watakachofanya TANESCO ni ku-DISCOURAGE Matumizi Makubwa ya Umeme! Una-discourage Matumizi Makubwa ya Umeme sio kwa kutoa elimu bubu watoazo kwenye ma-tv bali watafanya hivyo kwa kupandisha bei ya umeme ili hatimae muache matumizi holela ya umeme, kama mlivyoacha kutumia majiko ya umeme bila hata kutandikwa bakora!!

Na hapa tukumbushane kwamba, kama kweli tunaamini bei itakuwa ndogo basi ni hiyo bei ndogo ndiyo itakuwa chanzo cha kukaribisha bei kubwa! Umeme ukiwa nafuu, matumizi ya umeme yataongezeka! Watu watatupa majiko yao na pasi zao za mkaa kwa sababu umeme ni cheap!

Wafanyabiashara wataachana na mashine za kusaga zinazotumia mafuta na kuhamia mashine zinazotumia umeme kwa sababu umeme ni cheap!

Matumizi ya vifaa vya umeme yataongezeka kwa sababu umeme ni cheap!!! Huku Uswahilini ule ugomvi wa wapangaji kwamba tuwe tunazima mafriji na mafriza yetu, ugomvi huo utapungua kama sio kwisha kabisa kwa sababu umeme ni cheap, na watu watakuwa wanajiachia!!

OUTCOME?

Increased power consumption!! Njia ya kupambana na hilo? Nishasema hapo juu: discourage power consumption by increasing the price!!

IT'S SIMLE ECONOMY!

Is JNHPP White Elephant Project?

Yakitokea niliyosema hapo juu, HAIWEZI KUWA White Elephant Project lakini yasipotokea inaweza isiwe White Elephant Project lakini inaweza kuwa a STRUGGLING PROJECT!!

Tunahitaji uchumi mkubwa zaidi ili tuweze ku-consume hizo additional MW zitakazozalishwa! But don't forget, huo uchumi ukitokea itamaanisha NO MORE CHEAP ELECTRICITY kwa sababu power consumption itakuwa kubwa!!

Na isipotokea, ina maana Project Haitaweza kuzalisha pesa ya kutosha kulioa madeni yake, and hence becoming a STRUGGLING PROJECT!!

Yaani ndo ile inaitwa Ukichimama Nchale, Ukikimbia Nchale!! Sasa chagua mwenyee udungwe nchale wakati umesima au wakati unakimbia... MAUMIVU YAPO PALE PALE!!

Ndo vile tu umeme utaingizwa Grid ya Taifa lakini kama ingekuwa unakuwa distributed kipeke yake peke yake, watu wangeukimbia huo kama wanavyolikimbia Daraja la Kigamboni!!

Kwahiyo nakubaliana na wewe
 
Back
Top Bottom