Mradi wa SGR umeendeshwa vibaya na utalitia Taifa hasara kizazi hadi kizazi

Mradi wa SGR umeendeshwa vibaya na utalitia Taifa hasara kizazi hadi kizazi

Tutenganishe kwanza biashara na siasa. Tatizo ni kwamba hata watendaji wakuu wa miradi kama hiyo wanateuliwa. Kibaya zaidi wanateuliwa kisiasa, ni makada ambao unakuta mara nyingi hawana sifa, wao wakishaingia maofisini ndo kuidhinisha pesa za kampeni za chama, wanajijenga wao kuja kugombea baadae badala ya kusimamia maendeleo.

Hatuwezi kwenda huku tunajiibia wenyewe, lazima tuonekane matahira tu.
 
Wakati serikali inaamua kusimamia baadhi ya bishara,kuna watu walipiga kelele mno kwamba hakuna serikali inafanya biashara duniani.

Wacha niwakumbushe,serikali haifanyi biashara ya aina yeyote bali inajenga miundombinu na kuisimamia itoe huduma na kuongeza speed ya utafutaji kukuza uchumi.

Umetoa mfano wa mwendokasi,na hasara zake,ila sijui kama unajua bado ujenzi unaendelea!!unadhani ni bahati mbaya??lengo ni huduma sio biashara.

Kesho reli ikikamilika,ni wewe utaamua ukasafirishe mitumba yako ktk train kwa masaa manne ulipe laki tano,au kwa roli masaa 12 ulipe laki 8?

Reli ya kati imetoa huduma muda mrefu sana, mpaka ilipokuja kuachwa na mabadiliko ya tech na huduma kwa ujumla,train unalipa elfu 8 unasafiri siki 2,basi unalipa elfu 24 unafasiri masaa 12.hapa uchumi wa mtanzania mwenyewe utaamua train iendelee kuishi au ife jumla.

Kuliko kuwa watu wa kulalamika kila siku kama chadema,ni heri tukawa washauri na watu wa kupiga kelee tunapohisi kuna uzembe na hujuma ktk mali za uma.
 
LOooh, mkuu 'William Mshumbusi', umeweka bonge la mada hapa, lakini najua, kama kawaida yetu siku hizi hapa JF, tutaigusagusa tu na kwenda zetu kwenye utani wetu wa CCM na CHADEMA!

Umeanza na mfano mzuri sana wa TAZARA, jinsi reli ile ilivyojengwa haraka na kwa ufanisi na wachina. Madhumuni wa ujenzi wa reli ile ulijulikana bayana, kuondokana na utegemezi wa nchi za mstari wa mbele katika ukombozi kuwategemea makaburu katika maswala yao ya uchukuzi na usafirishaji wa mizigo yao.
Kabla ya mchina kujenga ile reli, wafadhiri wa nchi za Magharibi waliombwa kusaidia kuijenga, wakang'aka, huku wakisema reli eneo hilo haina faida. Hao hao, walipoona mchina anaijenga reli, haraka wakawa mbioni kwenye ujenzi wa barabara. Unaweza kutafsiri mwenyewe maana ya hayo yote.

Reli, kama ulivyoeleza ilifanya kazi vizuri mwanzoni mwa utumikaji wake, na umeeleza kwa nini kadri miaka ilivyoendelea, ndio ufanisi wake ulivyozidi kufifia hadi sasa.
Binafsi ningependa sana ukazie hapa, penye udhoofu wa ufanisi. Ueleze sababu hasa ni zipi, pamoja na kwamba umegusia kama kawaida yetu sote siku hizi, lawama za kwamba serikali haiwezi kufanya biashara. Mimi sikubaliani na jibu hilo jepesijepesi hivyo. Serikali inaweza sana kufanya mambo yake kwa ufanisi iktaka kufanya hivyo. Nyakati hizi haifanyi hivyo kwa sababu mbalimbali, ikiwemo hiyo ya sekta binafsi unayoipigia chapuo hapa, ikiwa ndio kikwazo kikubwa sana katika kudhoofisha shughuli za serikali.

Wenye malori bila shaka hawawezi kulaza damu wakiona shughuli za reli zinafana huku zikiwapunguzia wao wanachokitafuta. Tunaweza sana kulijadili hili, hata kama hatuwezi kukubaliana.

Matatizo yanayojitokeza ndani ya mashirika ya umma, yanaanzia huko huko kwenye sekta binafsi, na ukosefu wa usimamizi bora ndani ya mashirika yenyewe. Hii haimaanishi kwamba udhaifu huo hauwezi kudhibitiwa kama serikali ikiamua na kuwa na nia ya kufanikisha shughuli zake. Kusema serikali haiwezi kufanya biashara, ni sawa pia na kusema serikali haiwezi kufanya shughuli yoyote kwa ufanisi. Kwa hiyo tuondoe serikali tubinafsishe shughuli zote zinazofanywa na serikali?

Tusifanye uwekezaji ndio uwe muarobaini wa matatizo yetu, kila mara tunaposhindwa kwa uzembe tu, eti tukimbilie kwenye uwekezaji.
Tatizo aliloezea kwa mafumboni conflict of interest. Hii ndiyo inaua sekta nyingi za umma. Mkurugenzi mtendaji Sema wa tazara, Ana malori - 100 (mfano tu huo) amepata mzigo kwenda Zambia, je ataupeleka kwa malori au kwa reli? Mwingine Ana daladala 50 kila route, haya ya mwendokasi atayapa muda mwingi WA kuyashughulikia? Mwanzoniwamiaka Ile, viongozi WA umma hawakuwa na ruksa ya kushughulika na kitu nje ya kazi Ile aliyopewa. Mageuzi yaliyofanywa pale Mbeya yalileta haya tunayolalamikia Leo. HATA BABA WA TAIFA ALILISEMA NA KUOMBA AONYESHWE UBAYA WA YALE WIYOKUBALIANA KABLA YA MBEYA CONFERENCE.
 
Kwa hiyo mwendo kasi ni huduma au biashara? Ukiniambia shule za msingi ni huduma nitakuelewa, sio hayo mabasi yanayojaza abiria wanaolipa nauli mpaka mlango inakuwa shida kuufunga.
Yaani mpaka iwe bure kabisa ndo ujue ni huduma kwa jamii?
 
LOooh, mkuu 'William Mshumbusi', umeweka bonge la mada hapa, lakini najua, kama kawaida yetu siku hizi hapa JF, tutaigusagusa tu na kwenda zetu kwenye utani wetu wa CCM na CHADEMA!

Umeanza na mfano mzuri sana wa TAZARA, jinsi reli ile ilivyojengwa haraka na kwa ufanisi na wachina. Madhumuni wa ujenzi wa reli ile ulijulikana bayana, kuondokana na utegemezi wa nchi za mstari wa mbele katika ukombozi kuwategemea makaburu katika maswala yao ya uchukuzi na usafirishaji wa mizigo yao.
Kabla ya mchina kujenga ile reli, wafadhiri wa nchi za Magharibi waliombwa kusaidia kuijenga, wakang'aka, huku wakisema reli eneo hilo haina faida. Hao hao, walipoona mchina anaijenga reli, haraka wakawa mbioni kwenye ujenzi wa barabara. Unaweza kutafsiri mwenyewe maana ya hayo yote.

Reli, kama ulivyoeleza ilifanya kazi vizuri mwanzoni mwa utumikaji wake, na umeeleza kwa nini kadri miaka ilivyoendelea, ndio ufanisi wake ulivyozidi kufifia hadi sasa.
Binafsi ningependa sana ukazie hapa, penye udhoofu wa ufanisi. Ueleze sababu hasa ni zipi, pamoja na kwamba umegusia kama kawaida yetu sote siku hizi, lawama za kwamba serikali haiwezi kufanya biashara. Mimi sikubaliani na jibu hilo jepesijepesi hivyo. Serikali inaweza sana kufanya mambo yake kwa ufanisi iktaka kufanya hivyo. Nyakati hizi haifanyi hivyo kwa sababu mbalimbali, ikiwemo hiyo ya sekta binafsi unayoipigia chapuo hapa, ikiwa ndio kikwazo kikubwa sana katika kudhoofisha shughuli za serikali.

Wenye malori bila shaka hawawezi kulaza damu wakiona shughuli za reli zinafana huku zikiwapunguzia wao wanachokitafuta. Tunaweza sana kulijadili hili, hata kama hatuwezi kukubaliana.

Matatizo yanayojitokeza ndani ya mashirika ya umma, yanaanzia huko huko kwenye sekta binafsi, na ukosefu wa usimamizi bora ndani ya mashirika yenyewe. Hii haimaanishi kwamba udhaifu huo hauwezi kudhibitiwa kama serikali ikiamua na kuwa na nia ya kufanikisha shughuli zake. Kusema serikali haiwezi kufanya biashara, ni sawa pia na kusema serikali haiwezi kufanya shughuli yoyote kwa ufanisi. Kwa hiyo tuondoe serikali tubinafsishe shughuli zote zinazofanywa na serikali?

Tusifanye uwekezaji ndio uwe muarobaini wa matatizo yetu, kila mara tunaposhindwa kwa uzembe tu, eti tukimbilie kwenye uwekezaji.

Serikali ya Tanzania haina uwezo wa kuendesha mradi wowote kwa faida.

Siyo kweli kuwa eti sekta binafsi ndiyo inayosababisha serikali ishindwe kuendesha miradi ya biashara kwa faida. Kusema kwamba sekta binafsi inaihujumu miradi ya serikali ili sekta binafsi ipate biashara ni uwongo mkubwa:

1) TANESCO haijawahi kutengeneza faida hata mwaka mmoja, inashindana na nani?

2) ATCL haijawahi kupata faida hata mwaka mmoja. Waliiondoa Fastjet kwa mizengwe. Je, sasa wanapata faida?

3) Serikali ilikiwa inamiliki viwanda vya bia kabla ya kubinafsishwa, haikuwahi kutengeneza faida hata mwaka mmoja. Ilikuwa inashindana na nani wakati huo?

4) Serikali ilikuwa inamiliki kiwanda cha sigara, haikuwahi kutengeneza faida, ilikuwa inashindana na nani?

5) Serikali ilikuwa inamiliki viwanda vya zana za kilimo, kampuni ya simu na posta, na mengine mengi, lakini ilishindwa.

Serikali, kama ilivyo kwenye taasisi nyingine, imejaza watu wa ajabu, watu wenye uwezo mdogo, wanaoteuliwa kuendesha miradi hiyo wanateuliwa kwa mtazamo wa kisiasa, watu ambao uwezo na maarifa yao ni duni sana. Watu kama Sabaya, Mwigulu, Kalemani, Biteko, unategemea wanaweza kuendesha mradi wowote ukapata faida? Watu wa namna hiyo, ndiyo wamejaa kwenye taasisi za Serikali ambazo zilistahili kuongozwa na watu kwa kuangalia weledi na siyo siasa za ulimbukeni.

Nani atumie usafiri wa TAZARA, wakati ukitaka kusafirisha mizigo yako, mlolongo wa kupitia ni kama umeenda kuomba msaada. Watendaji wengi wa sekta ya umma wanachojua ni kuabudiwa, siyo time sensitive. Vivyo hivyo itakuwa kwa SGR.
 
Kuna Watu wa janja Watanzania wana hujumu hizi reli ndo maana hazifanikiwa.

Mtu ananunua magari 100, 200 ya mizigo au Abiria ni watu wenye fedha na majina makubwa wakati Mwingine wanashirikiana na watu wa Serikali anategemea kutumia barabara ya Lami hauwezi kuunga mkono reli.

Reli ikifika itaharibu biashara yake
 
Duniani kote ni nadra sana kupata serikali inayoweza kufanya biashara yoyote kwa faida. Biashara ni uwanja wa sekta binafsi, serikali iache kufanya biashara badala yake itengeneze mazingira mazuri ya biashara kufanyika na yenyewe ikusanye kodi.

Serikali ya Marekani hadi sekta nyeti kama ya Ulinzi imetoa fursa kubwa ya sekta binafsi kufanya kazi. Sekta binafsi inatengeneza silaha zote zinazotumika na jeshi la Marekani, zinazouzwa na kutolewa misaada nje ya nchi. Karibia vinu vyote vya nyuklia Marekani vinamilikiwa na makampuni binafsi, sisi bado tumebaki na mawazo ya kijima ya karne za giza ya serikali kumilik hadi ng'ombe kwenye ranchi!
LOooh, mkuu 'William Mshumbusi', umeweka bonge la mada hapa, lakini najua, kama kawaida yetu siku hizi hapa JF, tutaigusagusa tu na kwenda zetu kwenye utani wetu wa CCM na CHADEMA!

Umeanza na mfano mzuri sana wa TAZARA, jinsi reli ile ilivyojengwa haraka na kwa ufanisi na wachina. Madhumuni wa ujenzi wa reli ile ulijulikana bayana, kuondokana na utegemezi wa nchi za mstari wa mbele katika ukombozi kuwategemea makaburu katika maswala yao ya uchukuzi na usafirishaji wa mizigo yao.
Kabla ya mchina kujenga ile reli, wafadhiri wa nchi za Magharibi waliombwa kusaidia kuijenga, wakang'aka, huku wakisema reli eneo hilo haina faida. Hao hao, walipoona mchina anaijenga reli, haraka wakawa mbioni kwenye ujenzi wa barabara. Unaweza kutafsiri mwenyewe maana ya hayo yote.

Reli, kama ulivyoeleza ilifanya kazi vizuri mwanzoni mwa utumikaji wake, na umeeleza kwa nini kadri miaka ilivyoendelea, ndio ufanisi wake ulivyozidi kufifia hadi sasa.
Binafsi ningependa sana ukazie hapa, penye udhoofu wa ufanisi. Ueleze sababu hasa ni zipi, pamoja na kwamba umegusia kama kawaida yetu sote siku hizi, lawama za kwamba serikali haiwezi kufanya biashara. Mimi sikubaliani na jibu hilo jepesijepesi hivyo. Serikali inaweza sana kufanya mambo yake kwa ufanisi iktaka kufanya hivyo. Nyakati hizi haifanyi hivyo kwa sababu mbalimbali, ikiwemo hiyo ya sekta binafsi unayoipigia chapuo hapa, ikiwa ndio kikwazo kikubwa sana katika kudhoofisha shughuli za serikali.

Wenye malori bila shaka hawawezi kulaza damu wakiona shughuli za reli zinafana huku zikiwapunguzia wao wanachokitafuta. Tunaweza sana kulijadili hili, hata kama hatuwezi kukubaliana.

Matatizo yanayojitokeza ndani ya mashirika ya umma, yanaanzia huko huko kwenye sekta binafsi, na ukosefu wa usimamizi bora ndani ya mashirika yenyewe. Hii haimaanishi kwamba udhaifu huo hauwezi kudhibitiwa kama serikali ikiamua na kuwa na nia ya kufanikisha shughuli zake. Kusema serikali haiwezi kufanya biashara, ni sawa pia na kusema serikali haiwezi kufanya shughuli yoyote kwa ufanisi. Kwa hiyo tuondoe serikali tubinafsishe shughuli zote zinazofanywa na serikali?

Tusifanye uwekezaji ndio uwe muarobaini wa matatizo yetu, kila mara tunaposhindwa kwa uzembe tu, eti tukimbilie kwenye uwekezaji.
 
Hata kusipokuwepo na conflict of Interest, watu walioajiriwa serikalini sio rahisi kufanya biashara kwa ufanisi kwa sababu nyingi sana.
Meneja wa masoko wa TAZARA, Meli za Serikali au ATCL watalipwa mishahara yao tu pasipo kujali kuna faida au hasara ya miaka 10 katika shirika, hali ikizidi kuwa mbaya watahamishiwa sehemu nyingine na wataendelea kulipwa kama kawaida huku mshahara wao ukipanda kila mwaka.

Meneja masoko wa Precision Air, Azam Marine au Basi la Saul utakuwa na bahati sana kama kampuni itapata hasara kwa miezi 6 mfululizo na ukaendelea "kusavaivu" ofisini.
Tatizo aliloezea kwa mafumboni conflict of interest. Hii ndiyo inaua sekta nyingi za umma. Mkurugenzi mtendaji Sema wa tazara, Ana malori - 100 (mfano tu huo) amepata mzigo kwenda Zambia, je ataupeleka kwa malori au kwa reli? Mwingine Ana daladala 50 kila route, haya ya mwendokasi atayapa muda mwingi WA kuyashughulikia? Mwanzoniwamiaka Ile, viongozi WA umma hawakuwa na ruksa ya kushughulika na kitu nje ya kazi Ile aliyopewa. Mageuzi yaliyofanywa pale Mbeya yalileta haya tunayolalamikia Leo. HATA BABA WA TAIFA ALILISEMA NA KUOMBA AONYESHWE UBAYA WA YALE WIYOKUBALIANA KABLA YA MBEYA CONFERENCE.
 
Reli muhimu kuliko zote nchi hii ni reli ya TAZARA na hiyo ndiyo serikali ilapaswa ifufue miondombinu yake iwe ya kisasa na sekta binafsi ipewe fursa ya kufanya bishara ya usafiri huko.
Nafikiri kwa uwekezaji, unaofanywa kwenye Reli,ni lazima lengo.liwe n biashara.
Nina mashaka makubwa na hii miradi ya Mwendazake!
Kuna kila dalili tutakujakulia huko mbeleni.
Nafikiri kinachoendelea Kenya kwenye SGR ya Nairobi Mombasa ni mfano.mzuri ,sana!
Haiwezekani nchi ikajiingiza kwenye miradi mikubwa hivi ,bika mjadala wa kutosha!
 
Reli ya Tazara ilipingwa vikali na WB/IMF kwa sababu za nguvu kwamba was not economically viable na mbaya zaidi feasibility study haikufangika hivyo wakakataa kutoa mkopo kwa Nyerere.

Hapo sasa ikabidi mwalimu akajisalikishe kwa beberu mpya China matokeo yake reli ikajengwa ndio hadi leo hii ni hasara kwa kwenda mbele.

Jiulize kama Tazara inakula hasara na 70% za mzigo wa bandara ya Dar unakwenda Sadc region unadhani hiyo sgr ya TRC itakuaje?

Kwa miaka yote TRc inakula hasara mara wafanye wao mara walete wawekezaji lakini ni loss loss loss na zero kila wakati.Sasa subiria sgr ikamilike loss yake Atcl na Tanesco watasoma.

Hii nchi tutaendelea kula hasara na maisha magumu kwa mda wote kutokana na maamuzi yasiyo na tija hayakuzingatia weledi bali hisia za kikanda na kisiasa.

As for me muda wa kujenga sgr ulikuwa bado Sana ilitakiwa tuimarishe barabara na tusubirie Congo drc iwe na stability huku mashariki kwake na biashara yake iwe vizuri ndio Tujenge hiyo sgr .

Hakuna shirika la serikali linapata faida halipo labda mabenki ambako ina hisa,hata huo mwendokasi ni bora wafanye private sector au njia hizo ziwe za daladala tuu.Kila siku nawaambia mtu wa serikali anaepokea salary hawezi leta tija Serikalini hata siku moja,kinachofanyika private sector Ili mambo yaende ukileta Serikalini watu wataacha Kazi na wengi watafukuzwa.
 
Hata kusipokuwepo na conflict of Interest, watu walioajiriwa serikalini sio rahisi kufanya biashara kwa ufanisi kwa sababu nyingi sana.
Meneja wa masoko wa TAZARA, Meli za Serikali au ATCL watalipwa mishahara yao tu pasipo kujali kuna faida au hasara ya miaka 10 katika shirika, hali ikizidi kuwa mbaya watahamishiwa sehemu nyingine na wataendelea kulipwa kama kawaida huku mshahara wao ukipanda kila mwaka.

Meneja masoko wa Precision Air, Azam Marine au Basi la Saul utakuwa na bahati sana kama kampuni itapata hasara kwa miezi 6 mfululizo na ukaendelea "kusavaivu" ofisini.
Pamoja na hilo lakini kubwa kabisa ni kuruhusiwa viongozi Tena kule juu kabisa kujiingiza kwenye biashara, wakati huo huo TAIFA halikuwa na mwongozo wa kushughulika mambo kama haya yakitokea. Kungekuwa na sheria kuwa kama ni biashara basi a ha u director General wa TPA au TRC, fanya biashara yako.

TAIFA lilikuwa bado changa wakati huo na wakaruhusu viongozi kuwa ndumila kuwili. Je inategemewa nini. Makampuni ya biashara makubwa yalifukuzwa, elimu ya biashara ndiyo kwanza inaanza, kesho mtu Ana cheti toka cbe wakati huo au chuo cha ushirika moshi anakabidhiwa rtc mkoa au kampuni ya usafirishaji mkoa, unategemea nini.
 
Miradi ni ya mhimu ,tatizo lipo kwenye usimamizi this why miradi inaonekana ni ya hovyo
Usimamizi umefanyaje? Utasimamia nini ikiwa sgr unajenga sehemu isiyokuwa na mzigo kama njia ya Mwanza au central corridor nzima?

Tazara,mwendokasi na masoko yamewashinda ndio huko wataweza?
 
Umeandika jambo kubwa lakini bila vielelezo na uthibitisho mfano umeandika serikali inatoa fedha kwenye mradi wa mwendokasi ilitakiwa useme inatoa kiasi gani na mradi unapata hasara kiasi gani na kwanini unashindwa kujiendesha.Umeandika kuhusu SGR lakini sijaona facts kuthibitisha mradi utashindwa.
Kumbuka viongozi wote waliotembelea bwawa la Nyerere pamoja na waandishi wa habari waliwasifu wajenzi! Sasa kauli ya makamu wa Rais aliyoitoa juzi kuhusu ujenzi tuisemeje!
 
Wewe hufai kuwepo katika jukwaa hili. Unachojua ni chuki kwa chadema na matusi ya aibu. Nadhani hii ni reflection ya malezi mabovu uliyopitia . Mada ni nzuri na fikirishi, wewe unaingiza uvyama na matusi tu basi. Huwezi kuhimili nguvu ya hoja pita kimya.

chadema ni chama kimejaa watu wa ajabu wasioitakia nchi hii jema la aina yoyote,sababu tu wamekosa nafasi ya uongozi.

bisha nikuonyeshe ni kwa namna gani watu hawa hawaitakii nchi hii aina yoyote jema.
 
Mwaka 1970-1974 mchina alijenga reli ya Tazara ya kisasa kwa wakati huo na watanzania waliaminishwa makubwa Sana juu ya faida ya mradi husika. Miaka 25 tu baada ya mradi kukamilika reli ikachoka, ikakosa wateja, usimamizi mbovu. Zile hadithi na simulizi tamu za manufaa ya mradi huo walioaminishwa watanzania hakuna Tena na njia kuu ya uchukuzi Tanzania to Zambia kubaki NI barabara ya Rami.

Pia Serikali ililithi reli ya Kati kutoka kwa mkoloni. Na reli ilibaki njia kuu ya uchukuzi Hadi miaka ya 90s katikati. Lakini shirika liliendeshwa kihuni Sana. Shirika liliuza tiketi chache Sana. Zaidi ya 80% ya abilia walilipa Ela keshi zilizoishia mikononi mwa walinzi na wafanyakazi wa shirika lenyewe.

Mpaka leo reli haikujiendesha. Inakula Kodi zetu kila siku kukarabatiwa lkn maingizo hakuna NI hasara tu.
Nisiwachoshe kabisa. Sizungumzii kbs mradi wa Mabasi ya mwendokasi unavyoumiza taifa ikiwa NI chini ya miaka kumi tu uanshwe. Serikali inamwaga fedha kuuokoa Ila watachoka tu. Mabasi kibao yameharibika yakatelekezwa na kuoza.
Ndege zipo kwaajili ya kujisifu lkn hakuna faida ya kipato.

Ambao wanachukulia Mambo kirahisi hawataelewa. Wataamini propaganda na hadidhi za bulicheka na ndoto za abunuasi za kuvuka bahati kwa kugeuza meza na kupanda juu yake.

Ukweli NI kuwa mradi utakausha kau fedha mtaani,

Serikali ingejitoa kabisa kwenye ujenzi na uendeshaji ikakaa kusubili kodi.
Ila Kama Serikali itafanya biashara nk hatari kwake. Haina ubunifu. Usimamizi mbovu.
Kwa jinsi tulivyo

Tunaitaji reli nzuri lkn bila kupitiachito reli.

Tukubali tu tungevutia mwekezaji binafsi. Serikali ikiuchukua usimamizi na hivi haijui ubunifu, Itapiga marufuku maroli ya mizigo ili wao wapate mzigo.

Hayo matilioni yatapotea Kama mradi usio na uhakika.

kwan mwendokasi umeharibu biashara ya daladala?
 
Kwa muundo, mifumo na desturi za serikali inaweza kuwekeza na kuendesha miradi hiyo kibiashara kweli? Nina mashaka. Katika mazingira ya soko huru na ushindani sidhani ,huko nyuma tulishindwa leo tutaweza kweli. Tungeenda na utaratibu wa PPP ingewezekana.

unajua kama hujawahi fanya biashara ni rahisi sana kutoa ushauri kwa anaefanya biashara! nchi nyingi sana znategemea reli kama njia ya usafiri ila malori yapo kama kawa, hata hapa daladala zililalamika sana mwendokasi ulivokuja, hizo daladala zmekufa?
 
Back
Top Bottom