Mradi wa Stieglers: Mwarabu anaharibu mradi hana utaalam wala ujuzi wa kujenga bwawa, italeta hasara kubwa kwa taifa na ubora hafifu

Mradi wa Stieglers: Mwarabu anaharibu mradi hana utaalam wala ujuzi wa kujenga bwawa, italeta hasara kubwa kwa taifa na ubora hafifu

Ni kweli kabisa. Mradi ulijengwa kwa utaalam wa hali ya juu na mifumo ya kisasa. Hasa katika kituo cha jangwani ambacho kina mifumo ya kitaalam ya kudhibiti maji muda wa mvua. Pia mfumo wa kisasa wa kadi za kukatisha tiketi uliowekwa ni wa utaalam wa hali ya juu. Pamoja na mbinu za kisasa za kisasa za kubanana kwenye gari. Kwa kweli ni utaalam wa hali ya juu. Inawezekana anabisha kwa kuwa hana utaalam wowote.

[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Tanzania ndo nchii pekee kila mtu mjuaji na ana ujuzi wa kila kitu, mradi hata hujakamilika tayari tuhuma! upinzani kazi kwel kwel
 
Mimi sioni tatizo,sio lazima mkurugenzi wa hiyo kampuni ajue kutumia sululu katika kuchimba hilo bwawa,,atatumia subcontractor
 
Tanzania ndo nchii pekee kila mtu mjuaji na ana ujuzi wa kila kitu, mradi hata hujakamilika tayari tuhuma! upinzani kazi kwel kwel
hahaha. mkuu umenikumbusha mbali, wakati daraja la kigamboni lizinduliwa kuna watu humu walisema halina viwango na litavunjika mda wowote
 
Hiyo kampuni mbona nilisikia huko kwao ilikuwa ni kitengeneza chemba za choo na nyingine inashughulika na stetionary
 
Yeye alishauri kama wachina ndo wanafanya hiyo kazi vizuri, basi wapewe huo mradi ili wae committed na kama wakala.
Kimkataba sio Jambo jepesi hivyo, mwarabu Amepewa kandarasi ya kutengeneza bwawa,yeye ndio atajua anaajiri makampuni gani ktk vipande gani ili kumaliza kazi aliyopewa kwa ubora na kwa wakati.
 
Sijui kama taifa lini tutaacha usiri ktk kuingia mikataba mikubwa ya nchi yetu. Kukosekana kwa uwazi, tamaa ya kupata sifa binafsi kama kiki ya kisiasa, na pia tamaa ya kunufaika binafsi na kificho kutokana na fedha ya umma kwa njia za kifisadi ndizo sababu kubwa kila siku tunapigwa na wajanja.

Kabla ya utekelezaji wa miradi yote mikubwa inatotaka kuingiwa na serikali; Je! Ni kwa nini isijadiliwe kwanza bungeni ili kuweza kuzungumziwa kwa upana zaidi? Hivi ni kwa nini serikali hupenda sana kuingia mikataba kama hii kwa usiri mkubwa?

Mimi nafikiri tuelekeapo ktk uchaguzi mkuu, hapa napo panahitajika kuhojiwa na hata kupata majibu ya uhakika. Serikali imefanikiwa kuleta sheria nyingi kandamizi, matokeo yake tunakosa vyombo makini vya habari za kiitelejensia vyenye kuweza kuibua madudu ndani ya awamu hii ya tano, kwa ama kuogopa vitisho vya vyombo vya dola au hata kukabiliana na mkono wa sheria.
 
Hahaahahahhahaahahaahahahah unakuta naitwa Dr Mubarak Ni mfagizi wa kampuni nimekuja kuleta barua ya maombi kwenye huu mradi
Mkuu wengi mno ,nakambuka huko Chuo kikongwe huko Alexandria Egypt mwaka 1987 alikuwepo mwalinu mmoja kijana ana Phd mbili za Engineering kutoka UK,USA akisaka PHD ya tatu.
 
Wabongo kwa nongwa hatujambo walisema mradi utaharibu mazingira mara hakuna pesa za ujenzi sasa ujenzi unaendelea wanasema mwarabu hana uwezo ukweli ni kwamba mradi utafanikiwa na umeme utapatikana
 
Usimlaumu mwarabu, huyo alijaribu bahati yake kwenye tender ilivyotangazwa akashinda, mlaumu aliempa kazi mwarabu, huyo ndie tatizo haswa, huwezi jua huyo mwarabu alitoa nini mpaka akapewa hiyo kazi.
Kumbe basi mwaarabu ni mjanja ametumia fursa vizuri 'opportunity seeker' He is using other people's skillsets
 
Kabudi aitaja Timu ya "Taifa" ya wahandisi wa kiTanzania Stiegler's Gorge

Mhandisi Robert Kabudi msimamizi wa mkataba wa ujenzi wa JNHPP mwenye miaka 20 ya kusimamia miradi mikubwa ya ujenzi nje ya Tanzania pamoja na wahandisi wengine mahiri wazalendo wapo ktk mradi wa ujenzi wa Bwawa la Umeme la Rufiji linatotegemewa kuzalisha 2115 MW wa umeme Tanzania. Mhandisi Robert anaitaja timu hiyo ya watu 21, kikosi anacho kibainisha kama timu ya kutizamwa duniani.



Timu hiyo ya wahandisi wa kiTanzania walio na ujuzikazi kwa vitendo, kuna mhandisi aliyepata kusimamia mradi wa kiwanja cha ndege cha Dubai kilichokuwa na bajeti ya zaidi ya US$ 3.5Bn. Miradi mikubwa ya Qatar, Abu Dhabi, Botswana , World Cup Africa Kusini wahandisi wake wakiTanzania wazalendo walishiriki ktk ujenzi huko ughaibuni.

Wahandisi hao chini ya kitengo cha Tanroads Engineering Consultanting Unit TECU wana kiu ya kuongeza CV zao ktk mradi huu wa Rufiji wenye bajeti kubwa kuliko iliyotumika ktk ujenzi wa Uwanja Mkubwa Mpya wa Ndege Dubai na hivyo si tu kuitambulisha Tanzania bali hata wahandisi wazalendo waTanzania kwa ulimwengu, kukitokea mradi wowote mkubwa nje ya Tanzania watapata kuitwa.
 
Kwani hiyo project bei gani?

Nachojua katika project kama hizo lazima awepo main contractors na sub hata katika ujenzi wa SGR wapo sub contractors kibao
 
Naona wengi humu mnakuja na negativity kwa kutoa taarifa. Naishia hapo sina haja ya vijembe vya kijinga na ushabiki wa kipuuzi
Itakuwa umehubiriwa kanisani leo. Nawe mbio ukaleta humu bila utafiti.
 
kwa unafki grade one kama huu kuna kaukweli flani unakaongea na huyo mkandarazi kweli ni feki kwa ushahidi wa kumpa kazi Mchina nae kutupiga percent ya malipo bila jasho na pia yaonesha mwangalizi mkuu wa hapo yaani Waziri wa Nishati ni feki kama ilivyokuwa enzi za Mwalimu alihangaika mpaka akakonda kila mradi kama hakuna upigaji basi hakuna usimamizi!!Nyerere alitamani kuwa waziri wa kila kitu alipoona kachoka kuzuia maji kwa mikono nchi nzima imejaa majizi akamtupia kijiti Mzee Ruksa na kukimbilia Butiama kutuliza kichwa chake!!

Mradi huu ni mkubwa wenye maslahi makubwa kwa raia wote yafaa kuvunja mkataba na Watu wa Egypt na kuwapa mkataba hao wachina wanaojenga ili tupunguze costs na bureaucracy na kumuondoa mtu wa kati ili mradi uishe kwa wakati, yafaa Mkulu apewe activity plan yote ikiwa na dates za kila stage of implementation na awe kila three months anaenda mwenyewe kukagua kama reality ina reflect what is on the paper!! akikuta karatasi na reality ni tofauti hiyo ni kigezo cha kuvunja mkataba, heri nusu shari kuliko shari kamili!! huu ni mradi mkubwa wa kimkakati uliomshinda Nyerere na wengine waliomfuatia , ni mradi utakaoacha alama ya Mkulu na Chato kwa karne nyingi! Mkulu asione aibu kuwaita mawaziri na kuwakaripia na kubadilisha wasimamizi wa mradi , Nyerere aliwachekea kina Kambona akavuna mabua!!

Wakati huu mawaziri wake Mkulu wote wamepagawa na majimbo yao wanahangaika kuhonga huko vijijini warudi bungeni ni muda miradi yote itavurugika na kukosa usimamizi Mkulu awe makini!! ni ngumu Mkulu kushtuka kuwa serikali iko likizo kwa mawaziri wake kuhangaikia urais na ubunge sababu yeye Mkulu sote tunajua hana upinzani kwenye kiti chake kupitia kazi bora aliyowafanyia watanzania na systemic threat kwa kila mwana CCM anaetaka kupimana nae ubavu , vitisho vilivyopo ni grade one wanafki wote wa sisiem wanaotaka kugombea urais bara wamekunja mikia, wengine wametupiliwa mbali kina Maembe!! Mkulu for five months from now needs to create a small taskforce kuangalia miradi mikubwa kwakuwa mawaziri wake hawamsikilizi na hawatulii now wanasaka kura!!na kama wachumia tumbo wengine nchi hii ni haki yao kuhangaika majimboni kusaka ugali wa familia zao!! Mkulu needs to be waziri wa kila kitu temporarily!!
Utakuwa muathirika wa yule mtetezi wa ushoga aliyepo Ubelgiji
 
Naongea kama mwananchi na kushauri kuwa kumwendekeza huyu mwarabu wa Egypt's ni hasara kwa taifa na uharibifu wa mradi na uasili wake wa stiegler's gorge unapotea kwa sababu zifuatazo.

1. Hawa waarabu wa Misri kutoka Elsewedy electric na Arab contractors kutoka Misri hawana utaalamu wowote wa ujenzi wa bwawa kubwa kama la mwalimu nyerere wanatembelea nyota ya mchina waliyempa almost 90% ya mradi. Huyu mwarabu hata idea ya mining kwa manpower aliyokuja nao ni zero kabisa. Wazawa ndio wanaowafundisha kazi hawa wanaojiita maengener toka misri.

Ulipuaji wa miamba inafanyika kama vile hakuna site plani ya kujua kazi inatokea hapa inaenda kule wao kila siku wanakuja na plan mpya yaani haijulikani kesho itafanyika kazi gani.

2. Walio wengi wanahusika security kuhakikisha nani kaingia site, katoka na nini na kuandaa vibali pia administration na accomodation ambapo nadhani hii kazi wazawa kupitia suma jkt wanaweza kuifanya.

3. Wafanyakazi wengi wazawa mikataba yao na maslai yao sio mazuri na mahusioano kati ya mwarabu na mtanzania yako kibaguzi utadhani enzi za utumwa, wana mentality za kitumwa sana na kutomjali mwafrika.

4. Kazi inayoonekana inafanyika anafanya mchina toka kampuni ya Sinohydro akiwa na kampuni zake kama CBRC ndio wanafanya kazi na unaona kazi ya mchina inatoka hapa kwenda kule na sio mwarabu ambaye kama kama dalali.

5. Uongozi wa tanesco kama mwenye mradi pamoja na teku inaonekana hakuna umakini na ufatiliaji either wanajua na wasafikisha ila hakuna maamuzi au kuna kuwindana na uwoga kutoka juu.

Ushauri wangu
1. Kama hakuto athiri napendekeza huu mradi angepewa mchina utaisha kwa wakati ila huyu mwarabu hasara iliyo mbele ni kubwa sana katika pesa na wakati.

Wewe umesema kampa mchina 90% sasa wasiwasi wako upo wapi kama kazi hiyo bado inafanywa mchina?
Sema wapi pana mapungufu ili pafanyiwe kazi.
 
Wewe umesema kampa mchina 90% sasa wasiwasi wako upo wapi kama kazi hiyo bado inafanywa mchina?
Sema wapi pana mapungufu ili pafanyiwe kazi.
cha kuangalia ni time frame kwa kila stage na ubora wa vifaa vinavyotumiwa! lazima work plan yao iwe shared ili wafanyiwe tathmini kupitia hiyo plan!
 
Back
Top Bottom