kwa unafki grade one kama huu kuna kaukweli flani unakaongea na huyo mkandarazi kweli ni feki kwa ushahidi wa kumpa kazi Mchina nae kutupiga percent ya malipo bila jasho na pia yaonesha mwangalizi mkuu wa hapo yaani Waziri wa Nishati ni feki kama ilivyokuwa enzi za Mwalimu alihangaika mpaka akakonda kila mradi kama hakuna upigaji basi hakuna usimamizi!!Nyerere alitamani kuwa waziri wa kila kitu alipoona kachoka kuzuia maji kwa mikono nchi nzima imejaa majizi akamtupia kijiti Mzee Ruksa na kukimbilia Butiama kutuliza kichwa chake!!
Mradi huu ni mkubwa wenye maslahi makubwa kwa raia wote yafaa kuvunja mkataba na Watu wa Egypt na kuwapa mkataba hao wachina wanaojenga ili tupunguze costs na bureaucracy na kumuondoa mtu wa kati ili mradi uishe kwa wakati, yafaa Mkulu apewe activity plan yote ikiwa na dates za kila stage of implementation na awe kila three months anaenda mwenyewe kukagua kama reality ina reflect what is on the paper!! akikuta karatasi na reality ni tofauti hiyo ni kigezo cha kuvunja mkataba, heri nusu shari kuliko shari kamili!! huu ni mradi mkubwa wa kimkakati uliomshinda Nyerere na wengine waliomfuatia , ni mradi utakaoacha alama ya Mkulu na Chato kwa karne nyingi! Mkulu asione aibu kuwaita mawaziri na kuwakaripia na kubadilisha wasimamizi wa mradi , Nyerere aliwachekea kina Kambona akavuna mabua!!
Wakati huu mawaziri wake Mkulu wote wamepagawa na majimbo yao wanahangaika kuhonga huko vijijini warudi bungeni ni muda miradi yote itavurugika na kukosa usimamizi Mkulu awe makini!! ni ngumu Mkulu kushtuka kuwa serikali iko likizo kwa mawaziri wake kuhangaikia urais na ubunge sababu yeye Mkulu sote tunajua hana upinzani kwenye kiti chake kupitia kazi bora aliyowafanyia watanzania na systemic threat kwa kila mwana CCM anaetaka kupimana nae ubavu , vitisho vilivyopo ni grade one wanafki wote wa sisiem wanaotaka kugombea urais bara wamekunja mikia, wengine wametupiliwa mbali kina Maembe!! Mkulu for five months from now needs to create a small taskforce kuangalia miradi mikubwa kwakuwa mawaziri wake hawamsikilizi na hawatulii now wanasaka kura!!na kama wachumia tumbo wengine nchi hii ni haki yao kuhangaika majimboni kusaka ugali wa familia zao!! Mkulu needs to be waziri wa kila kitu temporarily!!