Mrejesho: Biashara ya Nyumba za Kupangisha Vs Nyumba za Kulala Wageni

Mrejesho: Biashara ya Nyumba za Kupangisha Vs Nyumba za Kulala Wageni

Hongera mkuu!

UUjenzi unachosha sana akili,mwili Hadi mifupa!

Hasa ujenzi wa kudunduliza ni hatari sana!!!

Nimejenga mchangangiko aiseh weka mbali na watoto!!

Yaani nyumba vyumba vitatu na sebule inaweza kukuchezesha sebene Hadi machozi yakakutoka!!

Big up sana aiseh!!
Kwa kweli Ujenzi unachosha sana kama ulivyosema.

Binafsi napenda kujenga

Nipo radhi Kwa Mwaka nisinunue shati jipya lakini site niwe nina Ujenzi unaendelea.

Ukiwa una nafasi Jenga mdogomdogo hata Vyumba single single upangishe
 
Hii iko Wilaya na Mkoa gani ndugu? Kutoka million 35 hadi zaidi ya 100millions, hizi nyingine hujasema ziliparikanaje ? All in all hongera sana kwa kazi nzuri!
Kihasibu inashauriwa hata kama Hela ya Kuwekeza ulipewa zawadi basi ihesabie kama Mikopo.

Kwa kufanya hivyo itasaidia kufanya maamuzi ya Uwekezaji wako.

Fedha nyingine nilizipata kwenye vyanzo vyangu vingine vya Uwekezaji na nilipofika asilimia 90 ya Mradi nilienda kuyajenga na watu wa Benki

Japo Benki hawatoi Mikopo Kwa startup business lakini nilifanikiwa kupata kukamilisha Mradi
 
Tufungueni macho nasi ni kitu gani hii
Airbnb ni unapangisha chumba/ nyumba kwa muda wowote kuanzia siku, wiki, mwezi, hadi miezi mitatu nk. Unafanya haya kupitia platform/ mtandao wa Airbnb.

NI hivi badala ya mfano wewe mwenye ku-advertise nyumba yako kupitia dalali, unaiweka kwenye website ya Airbnb unalipa pesa kidogo mpangaji anakutafuta pale mnakutana moja kwa moja hapo sokoni mpangaji anachagua ayatoka analipia unapata pesa zako chap.

Kiufupi inarahisisha sana mambo mfano una watoto saba unataka kwenda holiday au wewe na washkaji zako wanne mmeamua kwenda morogoro kwa siku tatu mnapangisha nyumba moja badala ya kuchukua hotel na vyumba tofauti. Kiufupi unapata huduma zote utakazopata nyumbani kama jiko, washing machine, na vingine.

Siyo kama hotel, lodge, hostel, guest ni kama unahamia nyumba nyingine kwa muda mchache kutoka nyumbani kwako sababu inatokana na wewe mwenyewe.

Sasa ukiondoka unaacha review, rate, marks ulipapenda, usalama, usafi, facilities nk. Na yeye mwenye nyumba anaacha review kuhusu wewe ni msafi, hukufanya fujo na kuvunjavunja TV, hukuacha, bangi na gongo kila chumba nk.

Hizo review ni ukiwa nazo nyingi positives (chanya) unaweza ku-kodi nyumba yako kwa urahisi. Zikiwa negatives. (hasi) nyingi kupata wateja itakuwa vigumu.

Vivyo hivyo kwa mpangaji na yeye kwenye profile yake kuna hasi na chanya. Kama hasi ni nyingi, kupata nyumba itakuwa vigumu sababu wenye nyumba wanangalia kwanza feedback historia yako kwanza kabla hawajakukubali. Umeelewa?

 
Kiufupi inarahisisha sana mambo mfano una watoto saba unataka kwenda holiday au wewe na washkaji zako wanne mmeamua kwenda morogoro kwa siku tatu mnapangisha nyumba moja badala ya kuchukua hotel na vyumba tofauti. Kiufupi unapata huduma zote utakazopata nyumbani kama jiko, washing machine, na vingine.

Siyo kama hotel, lodge, hostel, guest ni kama unahamia nyumba nyingine kwa muda mchache kutoka nyumbani kwako sababu inatokana na wewe mwenyewe.
Nakushukuru sana kiongozi umenipa jambo zuri sana hili
 
Back
Top Bottom