Mrejesho: Biashara ya Nyumba za Kupangisha Vs Nyumba za Kulala Wageni

Mrejesho: Biashara ya Nyumba za Kupangisha Vs Nyumba za Kulala Wageni

Biashara ya Uchimbaji ina changamoto nyingi sana hasa Kwa small scale Mining.

Nilijaribu wakati fulani, lakini Kila nikifanya tathmini mwisho wa mwaka naona napata hasara tu za vibarua na materials

Hivyo nili- quit

Shukrani Kwa mchango wako Chanya, nitafanyia kazi hili.

Barikiwa 🙏🙏🙏
Ila mkuu kwa mtu ambae anataka kuwekeza kwenye uchimbaji kwa kiwango cha kati unamshauri awe na nini na nini ?
 
Airbnb ni unapangisha chumba/ nyumba kwa muda wowote kuanzia siku, wiki, mwezi, hadi miezi mitatu nk. Unafanya haya kupitia platform/ mtandao wa Airbnb.

NI hivi badala ya mfano wewe mwenye ku-advertise nyumba yako kupitia dalali, unaiweka kwenye website ya Airbnb unalipa pesa kidogo mpangaji anakutafuta pale mnakutana moja kwa moja hapo sokoni mpangaji anachagua ayatoka analipia unapata pesa zako chap.

Kiufupi inarahisisha sana mambo mfano una watoto saba unataka kwenda holiday au wewe na washkaji zako wanne mmeamua kwenda morogoro kwa siku tatu mnapangisha nyumba moja badala ya kuchukua hotel na vyumba tofauti. Kiufupi unapata huduma zote utakazopata nyumbani kama jiko, washing machine, na vingine.

Siyo kama hotel, lodge, hostel, guest ni kama unahamia nyumba nyingine kwa muda mchache kutoka nyumbani kwako sababu inatokana na wewe mwenyewe.

Sasa ukiondoka unaacha review, rate, marks ulipapenda, usalama, usafi, facilities nk. Na yeye mwenye nyumba anaacha review kuhusu wewe ni msafi, hukufanya fujo na kuvunjavunja TV, hukuacha, bangi na gongo kila chumba nk.

Hizo review ni ukiwa nazo nyingi positives (chanya) unaweza ku-kodi nyumba yako kwa urahisi. Zikiwa negatives. (hasi) nyingi kupata wateja itakuwa vigumu.

Vivyo hivyo kwa mpangaji na yeye kwenye profile yake kuna hasi na chanya. Kama hasi ni nyingi, kupata nyumba itakuwa vigumu sababu wenye nyumba wanangalia kwanza feedback historia yako kwanza kabla hawajakukubali. Umeelewa?

Shukrani Kwa Elimu hii Mkuu

Kuna jamaa angu anataka kuwekeza Kigoma huko.

Nimemshauri aache, Kigoma haina muingiliano Mkubwa wa Wageni zaidi ya wale jama zetu wa Burundi
 
Ila mkuu kwa mtu ambae anataka kuwekeza kwenye uchimbaji kwa kiwango cha kati unamshauri awe na nini na nini ?
Muhimu upate kitalu ambavyo vinauzwa/Kukodishwa na Ofisi za Madini za Wilaya, ambapo huwa ni surveyed plots

Andaa kiasi cha shilingi almost 12M kwaajili ya kununua Karasha kwaajili ya kusaga mawe yatakayokuwa yanachimbwa na vibarua wako

Upate vifaa vya kusaidia kuchimba kwamaana ya sululu, kamba, tochi n.k

Vifaa vya kubebea mawe kule Chini ya maduara

Fedha kwaajili ya Uendeshaji i.e mishahara, unga, mboga n.k

Hii ni Kwa small scale

Ukitaka kufanya Kwa Ukubwa ingiza Mtaji Mkubwa Kwa

Kununua excavator kwaajili ya kusaidia kuchimba

Matipper ya kubebea udongo kwaajili ya kupeleka kuozesha

Jenga mashimo Yako ya kuozeshea udongo na kukamata dhahabu

Ama ukishindwa unaweza kupeleka Kwa jamaa wenye hivyo vitendea kazi ambapo baada ya process zote utapewa dhahabu Yako ikiwa tayari kwaajili ya kupeleka sokoni
 
Mimi nafikiria kufungua danguro kama yule jamaa wa Riverside

Malaya wanamlipa nadhani kwa siku 5,000 ana vyumba kama 20 hivi

Na kuna vyumba utakuta malaya hata 3 wanashare kwa hiyo jumla analipwa 15,000

Tuseme tu kila chumba malaya 1 ina maana 5000× vyumba 20= 100,000

Uzuri wa malaya wako kazini kila siku

100,000×365=36,500,000

Meneja ukilimpa 450,000 si haba ukitoa na gharama nyingine za uendeshaji kama umeme, maji, maintenance hukosi kitu

Nafikiria maeneo yenye migodi ya wachimba madini kama Chunya, Mererani na Geita inaweza kulipa au miji mikubwa ya Tanzania
Usijaribu hiyo biashara ina laana mno hapa mtwara kuna ndugu yetu Alhaji Lipaja alienda mpaka kuhiji mji mtakatifu wa maka na siku zote biashara yake ni hiyo yeye ana chumba kama 40 hivi na malaya wakimlipa 80000 kwa mwezi sasa zidisha 80000x40.... Aliporudi kuhiji alishauriwa mno aache hiyo biashara akawa anajibu kijeuri kuwa yeye kawapangisha tu hajui kinachofanyika vyumbani baada ya muda aliumwa sana akakatwa miguu yote miwili na mikono yote miwili kiufupi tumemzika hana mikono wala miguu je unadhani atamjibu nini Allah?
 
Usijaribu hiyo biashara ina laana mno hapa mtwara kuna ndugu yetu Alhaji Lipaja alienda mpaka kuhiji mji mtakatifu wa maka na siku zote biashara yake ni hiyo yeye ana chumba kama 40 hivi na malaya wakimlipa 80000 kwa mwezi sasa zidisha 80000x40.... Aliporudi kuhiji alishauriwa mno aache hiyo biashara akawa anajibu kijeuri kuwa yeye kawapangisha tu hajui kinachofanyika vyumbani baada ya muda aliumwa sana akakatwa miguu yote miwili na mikono yote miwili kiufupi tumemzika hana mikono wala miguu je unadhani atamjibu nini Allah?
Hiko kisa mbona kinatia huzuni sana

Pole sana Kwa huyo Mzee.

Ila mbona ni kama huyo Mzee alikuwa na Kisukari kutokana na hayo unayosimulia.

Anyways utafutaji una mambo mengi Mkuu
 
Usijaribu hiyo biashara ina laana mno hapa mtwara kuna ndugu yetu Alhaji Lipaja alienda mpaka kuhiji mji mtakatifu wa maka na siku zote biashara yake ni hiyo yeye ana chumba kama 40 hivi na malaya wakimlipa 80000 kwa mwezi sasa zidisha 80000x40.... Aliporudi kuhiji alishauriwa mno aache hiyo biashara akawa anajibu kijeuri kuwa yeye kawapangisha tu hajui kinachofanyika vyumbani baada ya muda aliumwa sana akakatwa miguu yote miwili na mikono yote miwili kiufupi tumemzika hana mikono wala miguu je unadhani atamjibu nini Allah?
Ndugu yangu ukianza kufuatilia maisha ya wafanyabiashara mambo meusi ni mengi

Huyo jamaa siyo kwamba biashara hiyo ndiyo imemsababishia mtu yeyote anaweza kupatwa na magonjwa na kufa
 
Hiko kisa mbona kinatia huzuni sana

Pole sana Kwa huyo Mzee.

Ila mbona ni kama huyo Mzee alikuwa na Kisukari kutokana na hayo unayosimulia.

Anyways utafutaji una mambo mengi Mkuu
Nikweli alikuwa na kisukari ila dakika za mwisho alikuwa analia sana anamuomba Allah amsamehe kwasababu hakukuwa na msaada mwingine kwake au kimbilio jingine zaidi ya huyo aliyeziumba Mbingu na nchi...kaka ni pesa tu mimi nakushauri achana na kuwaza hiyo biashara ya pombe jiulize swali dogo je unapenda mwanao aje kuwa mlevi?
 
Mimi nafikiria kufungua danguro kama yule jamaa wa Riverside

Malaya wanamlipa nadhani kwa siku 5,000 ana vyumba kama 20 hivi

Na kuna vyumba utakuta malaya hata 3 wanashare kwa hiyo jumla analipwa 15,000

Tuseme tu kila chumba malaya 1 ina maana 5000× vyumba 20= 100,000

Uzuri wa malaya wako kazini kila siku

100,000×365=36,500,000

Meneja ukilimpa 450,000 si haba ukitoa na gharama nyingine za uendeshaji kama umeme, maji, maintenance hukosi kitu

Nafikiria maeneo yenye migodi ya wachimba madini kama Chunya, Mererani na Geita inaweza kulipa au miji mikubwa ya Tanzania
Bonge la biashara Mkuu

Kule kwenye machimbo Kuna Hela nyingi sana Mkuu, Tena nyingi ipo kwenye vinywaji/Pombe na Malaya.

Maana hawaoni shida kumgharamia Mwanamke kutoka DSM kwenda kule kwaajili ya kustarehe nao.

Imagine kama na wewe utakuwa umewasogezea huduma 😜🏃🏃🏃
 
Ndugu yangu ukianza kufuatilia maisha ya wafanyabiashara mambo meusi ni mengi

Huyo jamaa siyo kwamba biashara hiyo ndiyo imemsababishia mtu yeyote anaweza kupatwa na magonjwa na kufa
Shida ya huyo mzee sio kufa ila shida ni kuwa bidii zote za hospital zilifeli ikawa kimbilio lake yeye na nafsi yake ilikuwa ni kwa Allah pekeyake hiki kisa nikikusimulia kinatisha sana hakika huyo mzee amefariki huku anatoka machozi ya majuto
 
Nikweli alikuwa na kisukari ila dakika za mwisho alikuwa analia sana anamuomba Allah amsamehe kwasababu hakukuwa na msaada mwingine kwake au kimbilio jingine zaidi ya huyo aliyeziumba Mbingu na nchi...kaka ni pesa tu mimi nakushauri achana na kuwaza hiyo biashara ya pombe jiulize swali dogo je unapenda mwanao aje kuwa mlevi?
Nimekuelewa Mkuu, ila hata kama hutauza wewe lakini wengine wanauza
 
Shida ya huyo mzee sio kufa ila shida ni kuwa bidii zote za hospital zilifeli ikawa kimbilio lake yeye na nafsi yake ilikuwa ni kwa Allah pekeyake hiki kisa nikikusimulia kinatisha sana hakika huyo mzee amefariki huku anatoka machozi ya majuto
Kwenye utafutaji hutakiwi kuangalia hivyo vitu.

Ukiendekeza sana hizo habari unaweza kupishana na mafanikio
 
Nikweli ndio maana kila nafsi itahukumiwa kivyake...
Ukifatilia sana hizo habari utagundua hata nyumba za Kupangisha ni dhambi pia.

Mimi nilikuwa na mpangaji Binti wa kama miaka 22 hivi, kumbe alikuwa anajiuza maana wanaume walikuwa wanaingia mule ndani Kwa kupishana.

Zile ndiyo wanaitaga huduma za short time eeh?
Maana Kila baada ya nusu saa ama saa Moja anaingia mtu mwingine

Niliamua kumwondoa baada ya kujua anayoyafanya
 
Shukrani Kwa Elimu hii Mkuu

Kuna jamaa angu anataka kuwekeza Kigoma huko.

Nimemshauri aache, Kigoma haina muingiliano Mkubwa wa Wageni zaidi ya wale jama zetu wa Burundi

Kule labda guesthouses and very cheap lodges. Mwambie asogee Mwanza hapo kuna uhaba mkubwa wa Lodges zenye viwango vya kuridhisha. Chache ziliizopo nyingi zimejaa muda wote.

Masasi, Tunduma kuna uhaba mkubwa wa Lodges zenye viwango ila ni sehemu zilizochangamka.
 
Kule labda guesthouses and very cheap lodges. Mwambie asogee Mwanza hapo kuna uhaba mkubwa wa Lodges zenye viwango vya kuridhisha. Chache ziliizopo nyingi zimejaa muda wote.

Masasi, Tunduma kuna uhaba mkubwa wa Lodges zenye viwango ila ni sehemu zilizochangamka.
Yeah umesema sahihi kuhusu Mwanza, kule pana shida sana ya Lodge zenye viwango

Tunduma nimefika mara kadhaa, pana Lodge chache sana licha ya mwingiliano Mkubwa wa Watu.

Kuna jamaa alitaka kuniuzia Kiwanja pale Mpemba ila pana shida sana ya Maji nisije kukosa hata ya kujengea
 
Ukifatilia sana hizo habari utagundua hata nyumba za Kupangisha ni dhambi pia.

Mimi nilikuwa na mpangaji Binti wa kama miaka 22 hivi, kumbe alikuwa anajiuza maana wanaume walikuwa wanaingia mule ndani Kwa kupishana.

Zile ndiyo wanaitaga huduma za short time eeh?
Maana Kila baada ya nusu saa ama saa Moja anaingia mtu mwingine

Niliamua kumwondoa baada ya kujua anayoyafanya

Kuna rafiki alipangisha nyumba yake sehemu flani eneo la kishua kwa mwanadada mmoja mrembo anamtajia bei ya kupanga ambayo wengi wanaikimbia yeye hana wasiwasi kabisa na ataka kulipa kwa Mwaka. Akaona poa huyu atamfaa.

Baada ya muda alikuja kugundua anafanyia massage yeye na wenzake wawili humo ndani. Na nje ameweka kibao kabisa. Alipogundua alimuongezea kodi na akampa notice mkataba ulipokaribia kuisha, ulipoisha akabadilisha matumizi ikawa office.
 
Kuna rafiki alipangisha nyumba yake sehemu flani eneo la kishua kwa mwanadada mmoja mrembo anamtajia bei ya kupanga ambayo wengi wanaikimbia yeye hana wasiwasi kabisa na ataka kulipa kwa Mwaka. Akaona poa huyu atamfaa.

Baada ya muda alikuja kugundua anafanyia massage yeye na wenzake wawili humo ndani. Na nje ameweka kibao kabisa. Alipogundua alimuongezea kodi na akampa notice mkataba ulipokaribia kuisha, ulipoisha akabadilisha matumizi ikawa office.
Wajanja sana hao mabinti.

Huyu wa kwangu alijitambulisha kwamba anafanya kazi Duka la dawa, kumbe anafanya biashara ya kuuza mwili

Kwasasa sipangishi Binti Single
 
Back
Top Bottom