Mrejesho: Biashara ya Nyumba za Kupangisha Vs Nyumba za Kulala Wageni

Mrejesho: Biashara ya Nyumba za Kupangisha Vs Nyumba za Kulala Wageni

Kuuza dhamana siyo lengo la kwanza la mkopeshaji ;sababu kuna usumbufu wa kuiuza dhamana.Mabenk wanataka kujiridhisha na uwezo wako wa kuingiza mapato.Waone angalau mtiririko wa kipato chako cha muda mrefu kutoka kwenye hiyo biashara,ndiyo wajue watakavyo kukakata.vinginevyo uweke dhamana halafu ukope nusu ya thamani ya dhamana ya soko.ili ukishindwa wauze kirahisi.
Umeshauri vizuri sana Mkuu

Iwapo Mamlaka zikafanyia kazi Ushauri wako, utaleta tija sana Kwa ma-hustler wengi Nchini
 
Mwishoni mwa Mwaka 2022 nilianza Ujenzi wa nyumba ya Kulala Wageni.

Ni Moja ya biashara niliyokuwa naifikiria Kwa muda mrefu. Nilianza Ujenzi Kwa kudunduliza kama ilivyo desturi ya Wajasirimali wengi Nchini. Nilikuwa na akiba ya shilingi 35M wakati naanza, ambapo nilianza Kwa kununua Kiwanja ambacho kilikuwa kipo katikati ya Makao Makuu ya Wilaya. Kiwanja kina Ukubwa wa mita 35 Kwa 43.5.

Kilinigharimu kiasi cha shilingi 11.8M kukinunua.

Bahati nzuri nilisanifu mwenyewe ramani niliyodhani ingefaa kujenga nyumba ya Wageni pamoja na mahitaji muhimu ya mashimo ya Maji machafu/Parking n.k

Niliweza kupata ramani ya vyumba 10 pamoja na Chumba cha Mhudumu/stoo/Public Toilet n.k

Baada ya kukamilisha taratibu za Vibali kutoka Halmashauri nikaanza Ujenzi. Nilitafuta Mafundi Kwa makundi kadri ya mahitaji.

Ujenzi uliweza kuchukua miezi 12 hadi kukamilika kwake. Hii ilitokana na Changamoto ya Fedha.

Nashukuru Mungu Mwaka Jana Mwezi September, 2023 nilikamilisha Mradi wangu wa Lodge ikiwa na accessories zote tayari Kwa kuanza kutoa huduma.

Jumla ya gharama nilizotumia zimefika shilingi 110,787,700TShs.

Baada ya kuanza huduma trend ya Mapato ghafi ilikuwa shilingi millioni 3.6 Kwa Mwezi.

Ambapo nimekadiria kuweza kukusanya shilingi 43,200,000 Kwa Mwaka ambapo nimechukulia kuwa Kila Siku watalala Wageni 4 kati ya Vyumba vyote 10.

Ikitokea wamelala wateja 10 itasaidia kufidia Siku ambazo hakutakuwa na mteja aliyelala ama walipolala pungufu ya Idadi tarajiwa.

Hata hivyo ninatumia kiasi cha shilingi 987,000 Kwa Mwezi kwaajili ya Mishahara pamoja na gharama nyingine za Uendeshaji sawa na shilingi 11,844,000 Kwa Mwaka.

Ili kujua kama fedha niliyowekeza itarudi ama itapotea nilijaribu kufanya tathmini Kwa kuangalia;

~Muda wa Kurejesha kiasi cha fedha nilichowekeza (Payback Period on investment)

Ambapo nilichukua kiasi cha Mtaji nilichowekeza÷Kiasi cha Faida ninachokadiria kupata kama Faida

=110,787,700/31,356,000
PBP= 3.53Years

Utaona naweza Kurejesha kiasi nilichotumia kwenye Uwekezaji wangu Kwa kipindi cha miaka 3 na nusu hivi.

VIPI KAMA INGEKUWA NYUMBA YA KUPANGISHA?

Gharama ningetumia hizo hizo ama zingepungua kidogo Kwa kuondoa gharama za Kununua TV/Magodoro/Vitanda/Ving'amuzi n.k ambapo pengine ingepungua labda 16M kutoka kwenye gharama za awali ya shilingi 110,787,700 na kuwa 94,787,700

Hivyo kupata muda wa kurudisha fedha uliyotumia kuwekeza ukizingatia bei ya Chumba self chenye hadhi hiyo hutozwa shilingi 60,000 Kwa Mwezi

Hivyo ningezalisha kiasi cha shilingi 600,000 Kwa Mwezi Kwa Vyumba vyote 10 na shilingi 7,200,000 Kwa Mwaka.

Hivyo Payback Period yetu ingekuwa = 94,787,700÷7,200,000
Miaka 13.2 hivi

Kwa kuifanya Nyumba ya Kupangisha ingenichukua miaka 13.2 hivi kuweza kurudisha Mtaji wangu wote niliyowekeza.

Kwa Kuhitimisha utaona Biashara ya Lodge ina unafuu Mkubwa kwenye Uwekezaji hasa Kwa kuangalia muda mchache wa kurudisha fedha uliyotumia kuwekeza (3.5yrs) kuliko Biashara ya Nyumba za Kupangisha(13.2yrs).

Nimeambatisha mchanganuo wa gharama nilizotumia,Mapato na Matumizi niyafanyayo (O&M).

Changamoto nilizopitia kwenye Biashara hii ni;
....Kutoaminika na Mabenki hasa kwenye start up project. Mabenki hayakopeshi Kwa biashara inayoanza ila Kwa biashara inayoendelea.

.....Wizi Kwa Wahudumu, licha ya kufunga CCTV Camera bado Mhudumu anaiba Kwa kuharibu Camera isifanye kazi.

All in all Biashara ya Lodge ni nzuri sana hasa Ukipata eneo lenye Mzunguko Mkubwa wa Watu.

Hongera mkuu,
Kama mzee pia ninayepambana, umenipa motisha sana.
 
Najuta kujenga Apartment ya kupangisha,ni jana tu nimetoka kugombana na wapangaji wawili ambao mmoja hajanilipa tangu mwezi April na mwingine tangu Mei kila siku sound tu!!ningejenga Lodge nisingepata usumbufu kama huu. Cha kushangaza hawa wapangaji wangu wanaonisumbua Kodi wameshawajaza wake zao mimba,najiuliza nguvu na hamu za kutomba wanazipata wapi ilihali Kodi hawalipi. Nimewapa notisi mwisho wa mwezi huu wawe wameondoka
 
Najuta kujenga Apartment ya kupangisha,ni jana tu nimetoka kugombana na wapangaji wawili ambao mmoja hajanilipa tangu mwezi April na mwingine tangu Mei kila siku sound tu!!ningejenga Lodge nisingepata usumbufu kama huu. Cha kushangaza hawa wapangaji wangu wanaonisumbua Kodi wameshawajaza wake zao mimba,najiuliza nguvu na hamu za kutomba wanazipata wapi ilihali Kodi hawalipi. Nimewapa notisi mwisho wa mwezi huu wawe wameondoka
Hahaha........pole Mkuu Kwa kadhia unayopitia.

Biashara ya nyumba za Kupangisha, ina adha kubwa ya baadhi ya wapangaji kushindwa kulipa Kodi zao Kwa wakati.

Mimi pia nimelazimika kubadirisha kitasa Kwa mmoja wa wapangaji wangu baada ya kushindwa kulipa Kodi yake Kwa miezi 5 sasa, bahati mbaya hata simu hapokei.

Kama utaweza jipange uwekeze kwenye biashara ya Lodge ambayo walau ina unafuu kuliko nyumba za Kupangisha
 
Hahaha........pole Mkuu Kwa kadhia unayopitia.

Biashara ya nyumba za Kupangisha, ina adha kubwa ya baadhi ya wapangaji kushindwa kulipa Kodi zao Kwa wakati.

Mimi pia nimelazimika kubadirisha kitasa Kwa mmoja wa wapangaji wangu baada ya kushindwa kulipa Kodi yake Kwa miezi 5 sasa, bahati mbaya hata simu hapokei.

Kama utaweza jipange uwekeze kwenye biashara ya Lodge ambayo walau ina unafuu kuliko nyumba za Kupangisha

Pole sana mkuu ila ndio hivyo, sometimes hawa wapangaji wanatuona wenye nyumba muda wote tuna fedha.
Mimi mwenyewe kuna sehemu nina viapartment nimevipanga kimkakati ili nivibadilishe kuwa lodge hapo baadae
All in all biashara ya nyumba inalipa sana inspite of changamoto ndogondogo.
 
Pole sana mkuu ila ndio hivyo, sometimes hawa wapangaji wanatuona wenye nyumba muda wote tuna fedha.
Mimi mwenyewe kuna sehemu nina viapartment nimevipanga kimkakati ili nivibadilishe kuwa lodge hapo baadae
All in all biashara ya nyumba inalipa sana inspite of changamoto ndogondogo.
Asante Mkuu

Nafikiri ni suala la kukosa uungwana.

Baba mwenye nyumba Mimi ni muelewa Kwa mtu ambaye anaweza kutoa taarifa ya kuchelewa kutoa hela yake ya Kodi, nipo tayari kumsubiria hata miezi 6 lakini akiwa ametoa taarifa.

Huyo Kijana nimelazimika kubadiri kitasa baada ya kuona simu zangu hapokei, kingine ni tabia yake ya kuingia usiku mnene na kuwahi kutoka saa 11 alfajiri.

Nikajua huyu anataka kunikimbia bila kunilipa Kodi yangu.
 
Asante Mkuu

Nafikiri ni suala la kukosa uungwana.

Baba mwenye nyumba Mimi ni muelewa Kwa mtu ambaye anaweza kutoa taarifa ya kuchelewa kutoa hela yake ya Kodi, nipo tayari kumsubiria hata miezi 6 lakini akiwa ametoa taarifa.

Huyo Kijana nimelazimika kubadiri kitasa baada ya kuona simu zangu hapokei, kingine ni tabia yake ya kuingia usiku mnene na kuwahi kutoka saa 11 alfajiri.

Nikajua huyu anataka kunikimbia bila kunilipa Kodi yangu.
Mkuu Ile ushauri wa kufungua kampuni kwa ajili ya unafuu wa Kodi umefikia wapi..?
 
Najuta kujenga Apartment ya kupangisha,ni jana tu nimetoka kugombana na wapangaji wawili ambao mmoja hajanilipa tangu mwezi April na mwingine tangu Mei kila siku sound tu!!ningejenga Lodge nisingepata usumbufu kama huu. Cha kushangaza hawa wapangaji wangu wanaonisumbua Kodi wameshawajaza wake zao mimba,najiuliza nguvu na hamu za kutomba wanazipata wapi ilihali Kodi hawalipi. Nimewapa notisi mwisho wa mwezi huu wawe wameondoka
Ndio maana ni muhimu sana kuuliza ajira au shughuli ya mtu ambaye unataka kumpangishia
 
Najuta kujenga Apartment ya kupangisha,ni jana tu nimetoka kugombana na wapangaji wawili ambao mmoja hajanilipa tangu mwezi April na mwingine tangu Mei kila siku sound tu!!ningejenga Lodge nisingepata usumbufu kama huu. Cha kushangaza hawa wapangaji wangu wanaonisumbua Kodi wameshawajaza wake zao mimba,najiuliza nguvu na hamu za kutomba wanazipata wapi ilihali Kodi hawalipi. Nimewapa notisi mwisho wa mwezi huu wawe wameondoka
Polee sana mkuu.. Biashara yoyote ile haikosi changamoto, ukisema lodge bila shaka wenye lodge wapo uku watatupa uzoefu ..usimamizi wa lodge ni mgumu sana. Alot of variables to handle.

Changamoto ya wapangaji kutolipa kodi inatokana na kutokuwa na mfumo mzuri wa malipo. Usikubali mtu aishi kwenye nyumba yako in advance, yaani aishi atalipa akijiskia.. nyumba umetengeneza kwa gharama sana, pengine umekopa.. upangishe kwa mkopo!
Kodi ni miezi mi 3, 6 au 12, kulingana na ubora na location ya nyumba, ..na mteja analipa mwanzo kabla hajaishi.

Tafuta mwanasheria akutengenezee mkataba na kipindi cha kusainishana awepo.. (sikuiz wako wengi sana mtaani wana mihuri hawana kazi). mkataba uweke wazi grace period, unayotoa kodi inapoisha.

Kuna level ukifika huitaji kujuana na mpangaji kabisa, yeye atapambana na mwanasheria wako.
Hii itakusaidia pia kutunza ubora wa nyumba yako, kuna wapangaji wanachafua sana ukuta, wanavunja vioo, masink chooni.. kwenye mkataba inabidi kipengele cha utunzaji wa mali kiwepo.. vitakavyoharibika nyumba ikiwa chini yake atalipa..

Kuna gharama ambazo utazikwepa na kuziona sio muhimu, zikagharimu investment ya millions of money.
Mfano mzuri, ni Bima ya gari sio muhimu ad litakapopata ajali.
.
 
Polee sana mkuu.. Biashara yoyote ile haikosi changamoto, ukisema lodge bila shaka wenye lodge wapo uku watatupa uzoefu ..usimamizi wa lodge ni mgumu sana. Alot of variables to handle.

Changamoto ya wapangaji kutolipa kodi inatokana na kutokuwa na mfumo mzuri wa malipo. Usikubali mtu aishi kwenye nyumba yako in advance, yaani aishi atalipa akijiskia.. nyumba umetengeneza kwa gharama sana, pengine umekopa.. upangishe kwa mkopo!
Kodi ni miezi mi 3, 6 au 12, kulingana na ubora na location ya nyumba, ..na mteja analipa mwanzo kabla hajaishi.

Tafuta mwanasheria akutengenezee mkataba na kipindi cha kusainishana awepo.. (sikuiz wako wengi sana mtaani wana mihuri hawana kazi). mkataba uweke wazi grace period, unayotoa kodi inapoisha.

Kuna level ukifika huitaji kujuana na mpangaji kabisa, yeye atapambana na mwanasheria wako.
Hii itakusaidia pia kutunza ubora wa nyumba yako, kuna wapangaji wanachafua sana ukuta, wanavunja vioo, masink chooni.. kwenye mkataba inabidi kipengele cha utunzaji wa mali kiwepo.. vitakavyoharibika nyumba ikiwa chini yake atalipa..

Kuna gharama ambazo utazikwepa na kuziona sio muhimu, zikagharimu investment ya millions of money.
Mfano mzuri, ni Bima ya gari sio muhimu ad litakapopata ajali.
.
Marekani kule ukihamia kwenye nyumba ya mtu unaweka deposit ambayo kwa kawaida huwa ni kodi ya mwezi mmoja. Ukiondoka kwenye hiyo apartment ni lazima uiache kama ulivyoikuta. Ukiondoka nyumba ikiwa salama deposit yako unarudishiwa. Vinginevyo itatumika kwenye matengenezo yote ambayo mwenye nyumba itabidi afanye kabla mpangaji mwingine hajaingia. Hii huwa inasaidia wapangaji kutoharibu vitu makusudi mbali na tear and wear za kawaida.

Na ukienda kupanga kwingine lazima useme ulikopanga kwa mara ya mwisho na lazima watawasiliana naye. Akisema kuwa huyo mpangaji ni bomu aisee hupangishwi. Na ikitokea ukabadilishiwa kitasa hiyo inaingia kwenye rekodi moja kwa moja na itakuwia vigumu sana kupata sehemu ya kupanga maana kila mtu atakuwa anakukimbia.

Mifumo kama hii huwa inasaidia. Sisi huku mtu anaharibu nyumba makusudi na hakuna kitu utamfanya!
 
Marekani kule ukihamia kwenye nyumba ya mtu unaweka deposit ambayo kwa kawaida huwa ni kodi ya mwezi mmoja. Ukiondoka kwenye hiyo apartment ni lazima uiache kama ulivyoikuta. Ukiondoka nyumba ikiwa salama deposit yako unarudishiwa. Vinginevyo itatumika kwenye matengenezo yote ambayo mwenye nyumba itabidi afanye kabla mpangaji mwingine hajaingia. Hii huwa inasaidia wapangaji kutoharibu vitu makusudi mbali na tear and wear za kawaida.

Na ukienda kupanga kwingine lazima useme ulikopanga kwa mara ya mwisho na lazima watawasiliana naye. Akisema kuwa huyo mpangaji ni bomu aisee hupangishwi. Na ikitokea ukabadilishiwa kitasa hiyo inaingia kwenye rekodi moja kwa moja na itakuwia vigumu sana kupata sehemu ya kupanga maana kila mtu atakuwa anakukimbia.

Mifumo kama hii huwa inasaidia. Sisi huku mtu anaharibu nyumba makusudi na hakuna kitu utamfanya!
Very right! 👍, hela yake ikiwa rehani atatunza nyumba tu!
 
Mkuu Ile ushauri wa kufungua kampuni kwa ajili ya unafuu wa Kodi umefikia wapi..?
Nipo kwenye Process, nimeshaenda baadhi ya Taasisi za Serikali ikiwemo TRA kwaajili ya kupata miongozo yao.

Hopefully Mwakani panapo Majaaliwa itakuwa tayari.

Bila kutumia mbinu hiyo, TRA hawana utani kwenye Kodi zao 🙌
 
Ndio maana ni muhimu sana kuuliza ajira au shughuli ya mtu ambaye unataka kumpangishia
Sahihi, nimewahi kupata tukio moja Mwaka Juzi.

Kuna Kijana mmoja alikuja kumpangia nyumba binti mmoja kwenye apartment yangu, alimlipia Kodi ya miezi 8, baadaye akaja kuongeza Kodi ya miezi 4. Jumla miezi 12.

Ilipobaki miezi 3 Kodi yao kuisha, nilifanya kuwakumbusha (Nina kawaida ya kumjulisha Mpangaji kwamba Kodi yao inakaribia kuisha Kila ikibaki miezi 3).

Yule binti amekaa, hadi Kodi ikaisha, nikampa wiki moja awe amenilipa Kodi yangu ama ahame.

Binti hana hela, na kumbe yule Boyfriend yake aliyekuwa anamlipia Kodi ameachana naye 🙌

Usumbufu ukawa mwingi pamoja na Kiswahili, baada ya wiki 2 nikamtolea Vyombo vyake Kwa nguvu.

Hii ni changamoto za kuwa na Wapangaji Wasumbufu wasio na Kipato cha kueleweka
 
Marekani kule ukihamia kwenye nyumba ya mtu unaweka deposit ambayo kwa kawaida huwa ni kodi ya mwezi mmoja. Ukiondoka kwenye hiyo apartment ni lazima uiache kama ulivyoikuta. Ukiondoka nyumba ikiwa salama deposit yako unarudishiwa. Vinginevyo itatumika kwenye matengenezo yote ambayo mwenye nyumba itabidi afanye kabla mpangaji mwingine hajaingia. Hii huwa inasaidia wapangaji kutoharibu vitu makusudi mbali na tear and wear za kawaida.

Na ukienda kupanga kwingine lazima useme ulikopanga kwa mara ya mwisho na lazima watawasiliana naye. Akisema kuwa huyo mpangaji ni bomu aisee hupangishwi. Na ikitokea ukabadilishiwa kitasa hiyo inaingia kwenye rekodi moja kwa moja na itakuwia vigumu sana kupata sehemu ya kupanga maana kila mtu atakuwa anakukimbia.

Mifumo kama hii huwa inasaidia. Sisi huku mtu anaharibu nyumba makusudi na hakuna kitu utamfanya!
Sio vibaya kujifunza vitu vizuri, nadhani hii idea yako ni nzuri.

Ukipata Mpangaji, unamsainisha Mkataba wa namna hiyo ili kulinda nyumba yako Incase akaiharibu kwa namna moja ama nyingine
 
Polee sana mkuu.. Biashara yoyote ile haikosi changamoto, ukisema lodge bila shaka wenye lodge wapo uku watatupa uzoefu ..usimamizi wa lodge ni mgumu sana. Alot of variables to handle.

Changamoto ya wapangaji kutolipa kodi inatokana na kutokuwa na mfumo mzuri wa malipo. Usikubali mtu aishi kwenye nyumba yako in advance, yaani aishi atalipa akijiskia.. nyumba umetengeneza kwa gharama sana, pengine umekopa.. upangishe kwa mkopo!
Kodi ni miezi mi 3, 6 au 12, kulingana na ubora na location ya nyumba, ..na mteja analipa mwanzo kabla hajaishi.

Tafuta mwanasheria akutengenezee mkataba na kipindi cha kusainishana awepo.. (sikuiz wako wengi sana mtaani wana mihuri hawana kazi). mkataba uweke wazi grace period, unayotoa kodi inapoisha.

Kuna level ukifika huitaji kujuana na mpangaji kabisa, yeye atapambana na mwanasheria wako.
Hii itakusaidia pia kutunza ubora wa nyumba yako, kuna wapangaji wanachafua sana ukuta, wanavunja vioo, masink chooni.. kwenye mkataba inabidi kipengele cha utunzaji wa mali kiwepo.. vitakavyoharibika nyumba ikiwa chini yake atalipa..

Kuna gharama ambazo utazikwepa na kuziona sio muhimu, zikagharimu investment ya millions of money.
Mfano mzuri, ni Bima ya gari sio muhimu ad litakapopata ajali.
.
Very right, japo unaweza kuonekana Mnoko Kwa Wapangaji lakini inasaidia kulinda asset yako.

Kodi zenyewe hazifanani hata na hela uliyotumia kujengea 🙌
 
Back
Top Bottom