Mrejesho: Biashara ya Nyumba za Kupangisha Vs Nyumba za Kulala Wageni

Mrejesho: Biashara ya Nyumba za Kupangisha Vs Nyumba za Kulala Wageni

Uzi nzuri Sana ..naomba kuongezea...

Kuhusu wizi tumia technology..nenda jukwaa la IT wakueleze kuhusu vitasa vya card. Na software zake iwe chumba kikipata Tu mgeni unapata notifications hapo hapo...hata kama wa short time.....

Kwingine since wewe ni mpya kwenye biashara nashauri Fanya research ya lodge zilizo kufa au kukosa soko ikiwezekana uzi Kodi upige hela ..

Wengi wanashindwa maintenance Tu...sasa badala ya wewe kutumia hela nyingi kujenga zingine ...jaribu kukodi Kwa mkataba mrefu ..itakusaidia vitu viwili....kwanza utapunguza competition since competition umeinunua...pili utantumia hela ndogo for expansion...

Unaweza amini kkoo kuna hotel inakodishwa Kwa milioni 4 Tu Kwa mwezi wakati ni jengo la ghorofa 8..?

kisa muasisi kafa na watoto wanakula hela yote hawafanyi maintenance..

All in all nakutakia all the best miaka miachache kutoka sasa uwe na lodge hata tano...
Hiyo lodge ya ghorofa nane utaikodi na kuipangisha bila ukarabati?
 
Poa, kwa uzoefu wangu nimeona mikoa flani kupata logde ya maana ni shida, ikifika saa flani zote zimejaa. Kwahiyo ndio kusema kuna wateja wengi kuliko vyumba.

Nimeona pia wengine ukibook siku tano unapewa discount kidogo au ukipanga vyumba vingi as group siku moja.

Vingine ndani vina vitanda viwili, makochi, friji ndogo, breakfast nk. Hapo unachaji pesa nzuri.

Pia nimeona wengine uk-book inadvance kwa siku kadhaa bei inapungua.

Kuna mikakati mingi ya kuvutia wateja kama kuwa na generator, umeme usiokatika.

Nje kama una eneo unauza supu, nyama za kila aina, pombe, chakula, hata wapita njia na marafiki wa waliopanga, majirani wanakuja kula hapo.
Hiyo line yako ya mwisho kuna wengine wateja hawapendi pulukushani za kelele sasa ukishaanza kuuza Pombe, supu, chakula hiyo sasa inakua sio lodge hata mazingira wateja wanaweza kimbia wale wastaarabu. Alafu ukiweka hivo vitu inakua lodge ya wahuni shortime, uchafu. Labda aweke ki bar nje ya lodge huko ambapo mteja akiitaji chakula inakua sio mbali kukifata na kelele za watu/miziki haziingii lodge.

Maana kuna logde zingine zenye bar ni kelele sana likipigwa "IN DA CLUB" la 50 cent unaweza hisi umo ndani chumbani kitanda kina dance imagine mziki huo mpaka saa saba au nane usiku huko na unataka kulala.

Lodge wewe weka vitu vya kawaida pale reception kama miswaki, maji, dawa ya mswaki, vitu vile vitakavomvutia mteja maana ni wa kulala na kuondoka.

Ukianza kuweka sijui chakula, pombe, mziki e.t.c hiyo sio lodge ni bar wateja utakaopata ni wahuni na kukuharibia lodge yako.
 
Hiyo line yako ya mwisho kuna wengine wateja hawapendi pulukushani za kelele sasa ukishaanza kuuza Pombe, supu, chakula hiyo sasa inakua sio lodge hata mazingira wateja wanaweza kimbia wale wastaarabu. Alafu ukiweka hivo vitu inakua lodge ya wahuni shortime, uchafu. Labda aweke ki bar nje ya lodge huko ambapo mteja akiitaji chakula inakua sio mbali kukifata na kelele za watu/miziki haziingii lodge.

Maana kuna logde zingine zenye bar ni kelele sana likipigwa "IN DA CLUB" la 50 cent unaweza hisi umo ndani chumbani kitanda kina dance imagine mziki huo mpaka saa saba au nane usiku huko na unataka kulala.

Lodge wewe weka vitu vya kawaida pale reception kama miswaki, maji, dawa ya mswaki, vitu vile vitakavomvutia mteja maana ni wa kulala na kuondoka.

Ukianza kuweka sijui chakula, pombe, mziki e.t.c hiyo sio lodge ni bar wateja utakaopata ni wahuni na kukuharibia lodge yako.
Kuna lodge moja njombe niliipenda sana mm nikisafiri napenda kulala lodge wanazolala wasafiri au wafanyabiashara sio wenyeji wanaokuja kufanya ngono na ulevi lodge zenye bar mzik mnene kelele nyingi sipendi, napenda nikanywe bar ya karibu na nitakapolala, ile lodge wameweka bango kubwa juu ya paa "hauruhusiwi kuingia na mwanamke asiye mke wako, pombe,kelele,sigara haziruhusiwi" nilipapenda ni pa tulivu sana mashuka mablanket masafi sana, hata majina ya vyumba ni majina ya vitabu vya biblia na panajaa sana watu wanaopenda utulivu wapo wengi.
 
Mwishoni mwa Mwaka 2022 nilianza Ujenzi wa nyumba ya Kulala Wageni.

Ni Moja ya biashara niliyokuwa naifikiria Kwa muda mrefu. Nilianza Ujenzi Kwa kudunduliza kama ilivyo desturi ya Wajasirimali wengi Nchini. Nilikuwa na akiba ya shilingi 35M wakati naanza, ambapo nilianza Kwa kununua Kiwanja ambacho kilikuwa kipo katikati ya Makao Makuu ya Wilaya. Kiwanja kina Ukubwa wa mita 35 Kwa 43.5.

Kilinigharimu kiasi cha shilingi 11.8M kukinunua.

Bahati nzuri nilisanifu mwenyewe ramani niliyodhani ingefaa kujenga nyumba ya Wageni pamoja na mahitaji muhimu ya mashimo ya Maji machafu/Parking n.k

Niliweza kupata ramani ya vyumba 10 pamoja na Chumba cha Mhudumu/stoo/Public Toilet n.k

Baada ya kukamilisha taratibu za Vibali kutoka Halmashauri nikaanza Ujenzi. Nilitafuta Mafundi Kwa makundi kadri ya mahitaji.

Ujenzi uliweza kuchukua miezi 12 hadi kukamilika kwake. Hii ilitokana na Changamoto ya Fedha.

Nashukuru Mungu Mwaka Jana Mwezi September, 2023 nilikamilisha Mradi wangu wa Lodge ikiwa na accessories zote tayari Kwa kuanza kutoa huduma.

Jumla ya gharama nilizotumia zimefika shilingi 110,787,700TShs.

Baada ya kuanza huduma trend ya Mapato ghafi ilikuwa shilingi millioni 3.6 Kwa Mwezi.

Ambapo nimekadiria kuweza kukusanya shilingi 43,200,000 Kwa Mwaka ambapo nimechukulia kuwa Kila Siku watalala Wageni 4 kati ya Vyumba vyote 10.

Ikitokea wamelala wateja 10 itasaidia kufidia Siku ambazo hakutakuwa na mteja aliyelala ama walipolala pungufu ya Idadi tarajiwa.

Hata hivyo ninatumia kiasi cha shilingi 987,000 Kwa Mwezi kwaajili ya Mishahara pamoja na gharama nyingine za Uendeshaji sawa na shilingi 11,844,000 Kwa Mwaka.

Ili kujua kama fedha niliyowekeza itarudi ama itapotea nilijaribu kufanya tathmini Kwa kuangalia;

~Muda wa Kurejesha kiasi cha fedha nilichowekeza (Payback Period on investment)

Ambapo nilichukua kiasi cha Mtaji nilichowekeza÷Kiasi cha Faida ninachokadiria kupata kama Faida

=110,787,700/31,356,000
PBP= 3.53Years

Utaona naweza Kurejesha kiasi nilichotumia kwenye Uwekezaji wangu Kwa kipindi cha miaka 3 na nusu hivi.

VIPI KAMA INGEKUWA NYUMBA YA KUPANGISHA?

Gharama ningetumia hizo hizo ama zingepungua kidogo Kwa kuondoa gharama za Kununua TV/Magodoro/Vitanda/Ving'amuzi n.k ambapo pengine ingepungua labda 16M kutoka kwenye gharama za awali ya shilingi 110,787,700 na kuwa 94,787,700

Hivyo kupata muda wa kurudisha fedha uliyotumia kuwekeza ukizingatia bei ya Chumba self chenye hadhi hiyo hutozwa shilingi 60,000 Kwa Mwezi

Hivyo ningezalisha kiasi cha shilingi 600,000 Kwa Mwezi Kwa Vyumba vyote 10 na shilingi 7,200,000 Kwa Mwaka.

Hivyo Payback Period yetu ingekuwa = 94,787,700÷7,200,000
Miaka 13.2 hivi

Kwa kuifanya Nyumba ya Kupangisha ingenichukua miaka 13.2 hivi kuweza kurudisha Mtaji wangu wote niliyowekeza.

Kwa Kuhitimisha utaona Biashara ya Lodge ina unafuu Mkubwa kwenye Uwekezaji hasa Kwa kuangalia muda mchache wa kurudisha fedha uliyotumia kuwekeza (3.5yrs) kuliko Biashara ya Nyumba za Kupangisha(13.2yrs).

Nimeambatisha mchanganuo wa gharama nilizotumia,Mapato na Matumizi niyafanyayo (O&M).

Changamoto nilizopitia kwenye Biashara hii ni;
....Kutoaminika na Mabenki hasa kwenye start up project. Mabenki hayakopeshi Kwa biashara inayoanza ila Kwa biashara inayoendelea.

.....Wizi Kwa Wahudumu, licha ya kufunga CCTV Camera bado Mhudumu anaiba Kwa kuharibu Camera isifanye kazi.

All in all Biashara ya Lodge ni nzuri sana hasa Ukipata eneo lenye Mzunguko Mkubwa wa Watu.
Uko sahihi
Pia ukiweza kuwekeza kwenye njia kuu....kwa kulenga malori
 
Watu wanalala makanisani/misikitini na wamekufa vibaya zaidi ya hivyo.

Watu wamefanya anasa zote na bado wanadunda tu.

I don't condone madanguro/umalaya ila sababu yako ni ya kijinga sana (excuse my language).

Huu Uzi ni wa biashara your why or why not inabidi ziwe sababu za kibiashara sio habari za kufikirika.
Bila shaka wewe ni mkristo ndio maana hauelewi hicho nilichokiandika na uzito wake pia, kwahiyo ni ngumu sana mimi na wewe kuelewana
 
Mkuu wale wa Malori wanalalaga lodge kweli? Naonaga kama wanapark na kulala seat za magari yao akijilngeza sana anataka guest za short time apinguze usingizi aendelee mbele
Hulala bei ya wastani ili wapate bafu....
 
Kuna lodge moja njombe niliipenda sana mm nikisafiri napenda kulala lodge wanazolala wasafiri au wafanyabiashara sio wenyeji wanaokuja kufanya ngono na ulevi lodge zenye bar mzik mnene kelele nyingi sipendi, napenda nikanywe bar ya karibu na nitakapolala, ile lodge wameweka bango kubwa juu ya paa "hauruhusiwi kuingia na mwanamke asiye mke wako, pombe,kelele,sigara haziruhusiwi" nilipapenda ni pa tulivu sana mashuka mablanket masafi sana, hata majina ya vyumba ni majina ya vitabu vya biblia na panajaa sana watu wanaopenda utulivu wapo wengi.
Kabisa mkuu! Sio unaenda lodge watu wanapishana pishana sana kwenye korido.Mimi kiukweli lodge zenye bar kwa nje sio choice zangu kabisa.Nenda kale/kunywa kwingine ukirudi ni kulala tu.
Kuna moja nililala ifakara inaitwa clifton lodge ina vyumba vina majina ya wanyama, ukitaka kuna chef pale unaweka oda anakupikia chakula chochote kuna jiko lao zuri, safi hapo reception aiseeh yule chef ni fundi kwenye kukaangiza aiseeh😀
 

Attachments

  • images.jpeg
    images.jpeg
    59.8 KB · Views: 21
Mwishoni mwa Mwaka 2022 nilianza Ujenzi wa nyumba ya Kulala Wageni.

Ni Moja ya biashara niliyokuwa naifikiria Kwa muda mrefu. Nilianza Ujenzi Kwa kudunduliza kama ilivyo desturi ya Wajasirimali wengi Nchini. Nilikuwa na akiba ya shilingi 35M wakati naanza, ambapo nilianza Kwa kununua Kiwanja ambacho kilikuwa kipo katikati ya Makao Makuu ya Wilaya. Kiwanja kina Ukubwa wa mita 35 Kwa 43.5.

Kilinigharimu kiasi cha shilingi 11.8M kukinunua.

Bahati nzuri nilisanifu mwenyewe ramani niliyodhani ingefaa kujenga nyumba ya Wageni pamoja na mahitaji muhimu ya mashimo ya Maji machafu/Parking n.k

Niliweza kupata ramani ya vyumba 10 pamoja na Chumba cha Mhudumu/stoo/Public Toilet n.k

Baada ya kukamilisha taratibu za Vibali kutoka Halmashauri nikaanza Ujenzi. Nilitafuta Mafundi Kwa makundi kadri ya mahitaji.

Ujenzi uliweza kuchukua miezi 12 hadi kukamilika kwake. Hii ilitokana na Changamoto ya Fedha.

Nashukuru Mungu Mwaka Jana Mwezi September, 2023 nilikamilisha Mradi wangu wa Lodge ikiwa na accessories zote tayari Kwa kuanza kutoa huduma.

Jumla ya gharama nilizotumia zimefika shilingi 110,787,700TShs.

Baada ya kuanza huduma trend ya Mapato ghafi ilikuwa shilingi millioni 3.6 Kwa Mwezi.

Ambapo nimekadiria kuweza kukusanya shilingi 43,200,000 Kwa Mwaka ambapo nimechukulia kuwa Kila Siku watalala Wageni 4 kati ya Vyumba vyote 10.

Ikitokea wamelala wateja 10 itasaidia kufidia Siku ambazo hakutakuwa na mteja aliyelala ama walipolala pungufu ya Idadi tarajiwa.

Hata hivyo ninatumia kiasi cha shilingi 987,000 Kwa Mwezi kwaajili ya Mishahara pamoja na gharama nyingine za Uendeshaji sawa na shilingi 11,844,000 Kwa Mwaka.

Ili kujua kama fedha niliyowekeza itarudi ama itapotea nilijaribu kufanya tathmini Kwa kuangalia;

~Muda wa Kurejesha kiasi cha fedha nilichowekeza (Payback Period on investment)

Ambapo nilichukua kiasi cha Mtaji nilichowekeza÷Kiasi cha Faida ninachokadiria kupata kama Faida

=110,787,700/31,356,000
PBP= 3.53Years

Utaona naweza Kurejesha kiasi nilichotumia kwenye Uwekezaji wangu Kwa kipindi cha miaka 3 na nusu hivi.

VIPI KAMA INGEKUWA NYUMBA YA KUPANGISHA?

Gharama ningetumia hizo hizo ama zingepungua kidogo Kwa kuondoa gharama za Kununua TV/Magodoro/Vitanda/Ving'amuzi n.k ambapo pengine ingepungua labda 16M kutoka kwenye gharama za awali ya shilingi 110,787,700 na kuwa 94,787,700

Hivyo kupata muda wa kurudisha fedha uliyotumia kuwekeza ukizingatia bei ya Chumba self chenye hadhi hiyo hutozwa shilingi 60,000 Kwa Mwezi

Hivyo ningezalisha kiasi cha shilingi 600,000 Kwa Mwezi Kwa Vyumba vyote 10 na shilingi 7,200,000 Kwa Mwaka.

Hivyo Payback Period yetu ingekuwa = 94,787,700÷7,200,000
Miaka 13.2 hivi

Kwa kuifanya Nyumba ya Kupangisha ingenichukua miaka 13.2 hivi kuweza kurudisha Mtaji wangu wote niliyowekeza.

Kwa Kuhitimisha utaona Biashara ya Lodge ina unafuu Mkubwa kwenye Uwekezaji hasa Kwa kuangalia muda mchache wa kurudisha fedha uliyotumia kuwekeza (3.5yrs) kuliko Biashara ya Nyumba za Kupangisha(13.2yrs).

Nimeambatisha mchanganuo wa gharama nilizotumia,Mapato na Matumizi niyafanyayo (O&M).

Changamoto nilizopitia kwenye Biashara hii ni;
....Kutoaminika na Mabenki hasa kwenye start up project. Mabenki hayakopeshi Kwa biashara inayoanza ila Kwa biashara inayoendelea.

.....Wizi Kwa Wahudumu, licha ya kufunga CCTV Camera bado Mhudumu anaiba Kwa kuharibu Camera isifanye kazi.

All in all Biashara ya Lodge ni nzuri sana hasa Ukipata eneo lenye Mzunguko Mkubwa wa Watu.
Hongera sana mkuu, uwekezaji mzuri pia nimejifunza kitu
 
Mwishoni mwa Mwaka 2022 nilianza Ujenzi wa nyumba ya Kulala Wageni.

Ni Moja ya biashara niliyokuwa naifikiria Kwa muda mrefu. Nilianza Ujenzi Kwa kudunduliza kama ilivyo desturi ya Wajasirimali wengi Nchini. Nilikuwa na akiba ya shilingi 35M wakati naanza, ambapo nilianza Kwa kununua Kiwanja ambacho kilikuwa kipo katikati ya Makao Makuu ya Wilaya. Kiwanja kina Ukubwa wa mita 35 Kwa 43.5.

Kilinigharimu kiasi cha shilingi 11.8M kukinunua.

Bahati nzuri nilisanifu mwenyewe ramani niliyodhani ingefaa kujenga nyumba ya Wageni pamoja na mahitaji muhimu ya mashimo ya Maji machafu/Parking n.k

Niliweza kupata ramani ya vyumba 10 pamoja na Chumba cha Mhudumu/stoo/Public Toilet n.k

Baada ya kukamilisha taratibu za Vibali kutoka Halmashauri nikaanza Ujenzi. Nilitafuta Mafundi Kwa makundi kadri ya mahitaji.

Ujenzi uliweza kuchukua miezi 12 hadi kukamilika kwake. Hii ilitokana na Changamoto ya Fedha.

Nashukuru Mungu Mwaka Jana Mwezi September, 2023 nilikamilisha Mradi wangu wa Lodge ikiwa na accessories zote tayari Kwa kuanza kutoa huduma.

Jumla ya gharama nilizotumia zimefika shilingi 110,787,700TShs.

Baada ya kuanza huduma trend ya Mapato ghafi ilikuwa shilingi millioni 3.6 Kwa Mwezi.

Ambapo nimekadiria kuweza kukusanya shilingi 43,200,000 Kwa Mwaka ambapo nimechukulia kuwa Kila Siku watalala Wageni 4 kati ya Vyumba vyote 10.

Ikitokea wamelala wateja 10 itasaidia kufidia Siku ambazo hakutakuwa na mteja aliyelala ama walipolala pungufu ya Idadi tarajiwa.

Hata hivyo ninatumia kiasi cha shilingi 987,000 Kwa Mwezi kwaajili ya Mishahara pamoja na gharama nyingine za Uendeshaji sawa na shilingi 11,844,000 Kwa Mwaka.

Ili kujua kama fedha niliyowekeza itarudi ama itapotea nilijaribu kufanya tathmini Kwa kuangalia;

~Muda wa Kurejesha kiasi cha fedha nilichowekeza (Payback Period on investment)

Ambapo nilichukua kiasi cha Mtaji nilichowekeza÷Kiasi cha Faida ninachokadiria kupata kama Faida

=110,787,700/31,356,000
PBP= 3.53Years

Utaona naweza Kurejesha kiasi nilichotumia kwenye Uwekezaji wangu Kwa kipindi cha miaka 3 na nusu hivi.

VIPI KAMA INGEKUWA NYUMBA YA KUPANGISHA?

Gharama ningetumia hizo hizo ama zingepungua kidogo Kwa kuondoa gharama za Kununua TV/Magodoro/Vitanda/Ving'amuzi n.k ambapo pengine ingepungua labda 16M kutoka kwenye gharama za awali ya shilingi 110,787,700 na kuwa 94,787,700

Hivyo kupata muda wa kurudisha fedha uliyotumia kuwekeza ukizingatia bei ya Chumba self chenye hadhi hiyo hutozwa shilingi 60,000 Kwa Mwezi

Hivyo ningezalisha kiasi cha shilingi 600,000 Kwa Mwezi Kwa Vyumba vyote 10 na shilingi 7,200,000 Kwa Mwaka.

Hivyo Payback Period yetu ingekuwa = 94,787,700÷7,200,000
Miaka 13.2 hivi

Kwa kuifanya Nyumba ya Kupangisha ingenichukua miaka 13.2 hivi kuweza kurudisha Mtaji wangu wote niliyowekeza.

Kwa Kuhitimisha utaona Biashara ya Lodge ina unafuu Mkubwa kwenye Uwekezaji hasa Kwa kuangalia muda mchache wa kurudisha fedha uliyotumia kuwekeza (3.5yrs) kuliko Biashara ya Nyumba za Kupangisha(13.2yrs).

Nimeambatisha mchanganuo wa gharama nilizotumia,Mapato na Matumizi niyafanyayo (O&M).

Changamoto nilizopitia kwenye Biashara hii ni;
....Kutoaminika na Mabenki hasa kwenye start up project. Mabenki hayakopeshi Kwa biashara inayoanza ila Kwa biashara inayoendelea.

.....Wizi Kwa Wahudumu, licha ya kufunga CCTV Camera bado Mhudumu anaiba Kwa kuharibu Camera isifanye kazi.

All in all Biashara ya Lodge ni nzuri sana hasa Ukipata eneo lenye Mzunguko Mkubwa wa Watu.

Hongera kwa uwekezaji Mkuu.
Somo hili pia tumelichukua, Asante…
 
Kabisa mkuu! Sio unaenda lodge watu wanapishana pishana sana kwenye korido.Mimi kiukweli lodge zenye bar kwa nje sio choice zangu kabisa.Nenda kale/kunywa kwingine ukirudi ni kulala tu.
Kuna moja nililala ifakara inaitwa clifton lodge ina vyumba vina majina ya wanyama, ukitaka kuna chef pale unaweka oda anakupikia chakula chochote kuna jiko lao zuri, safi hapo reception aiseeh yule chef ni fundi kwenye kukaangiza aiseeh😀
Pazuri asee gharama ni ngapi kwa usiku mmoja?
 
Hiyo line yako ya mwisho kuna wengine wateja hawapendi pulukushani za kelele sasa ukishaanza kuuza Pombe, supu, chakula hiyo sasa inakua sio lodge hata mazingira wateja wanaweza kimbia wale wastaarabu. Alafu ukiweka hivo vitu inakua lodge ya wahuni shortime, uchafu. Labda aweke ki bar nje ya lodge huko ambapo mteja akiitaji chakula inakua sio mbali kukifata na kelele za watu/miziki haziingii lodge.

Maana kuna logde zingine zenye bar ni kelele sana likipigwa "IN DA CLUB" la 50 cent unaweza hisi umo ndani chumbani kitanda kina dance imagine mziki huo mpaka saa saba au nane usiku huko na unataka kulala.

Lodge wewe weka vitu vya kawaida pale reception kama miswaki, maji, dawa ya mswaki, vitu vile vitakavomvutia mteja maana ni wa kulala na kuondoka.

Ukianza kuweka sijui chakula, pombe, mziki e.t.c hiyo sio lodge ni bar wateja utakaopata ni wahuni na kukuharibia lodge yako.
Sio purukushani hapo ndio watu wanafanya dili za maana. Hakuna mziki kabisa kuna utulivu sana ila kuna chakula, vinywaji.

Lodge ya viwango mswaki, dawa ya mswaki, taulo mpya, makobazi mapya yote unawekewa chumbani.

Mara nyingi nimona kuhusu breakfast, lodgers na wageni wao walipewa breakfast bure asubuhi.

Inaleta kuaminika. Ujue kitu cha kwanza wateja wako ni kina nani? Sio maskini wanahitaji mazingira rafiki kufanya kazi zao. Uaminifu, utulivu, huduma za viwango ndio wanacholipia.
 
Sio purukushani hapo ndio watu wanafanya dili za maana. Hakuna mziki kabisa kuna utulivu sana ila kuna chakula, vinywaji.

Lodge ya viwango mswaki, dawa ya mswaki, taulo mpya, makobazi mapya yote unawekewa chumbani.

Mara nyingi nimona kuhusu breakfast, lodgers na wageni wao walipewa breakfast bure asubuhi.

Inaleta kuaminika. Ujue kitu cha kwanza wateja wako ni kina nani? Sio maskini wanahitaji mazingira rafiki kufanya kazi zao. Uaminifu, utulivu, huduma za viwango ndio wanacholipia.
Umesema sahihi, Mimi nilishauriwa pia niweke Vinywaji kwamaana beer.

Nilikataa as Kuna watu wakishalewa wataanza kupiga kelele bila kuangalia Kuna mtu amelala kesho alfajiri anawahi kikao/usafiri hivyo angehitaji utulivu.

Hizo huduma za miswaki/dawa n.k wanavipata kule vyumbani
 
Kabisa mkuu! Sio unaenda lodge watu wanapishana pishana sana kwenye korido.Mimi kiukweli lodge zenye bar kwa nje sio choice zangu kabisa.Nenda kale/kunywa kwingine ukirudi ni kulala tu.
Kuna moja nililala ifakara inaitwa clifton lodge ina vyumba vina majina ya wanyama, ukitaka kuna chef pale unaweka oda anakupikia chakula chochote kuna jiko lao zuri, safi hapo reception aiseeh yule chef ni fundi kwenye kukaangiza aiseeh😀
Sure

Mimi pia huwa sipendi kelele hivyo na pale ofisini sijaweka hiyo biashara ya Vinywaji.

Vinywaji vinaenda sambamba na Muziki, hivyo itakuwa usumbufu Kwa mteja aliyeko ndani amejipumzisha
 
Asante Mkuu

Watanzania wengi sio waaminifu

Baada ya kuichezea Camera saivi analeta hela anayojisikia maana anasema Leo wamelala wateja 7 kumbe wamelala 9

Nimetengeneza mara 3 lakini baada ya muda inaharibika Tena.

Nina hakika ningekuwa nakaa mwenyewe huenda Payback period ingeshuka hadi miaka 2

Maana nahisi napoteza Mapato mengi Kwa Wizi wao Hawa Vijana
Tatizo huoni CCTV upande wako, weka na WIFI uwe waona au mtoe weka mwingine
 
Back
Top Bottom