Mrejesho: Mke wangu anataka kuandika jina lake nyumba niliyoijenga

Zingatia hili
 
Zingatia haya
 
Yafuatayo wanaume tubadilike

1---mtoto watoto hawana Chao kwetu wazazi(Mali zetu tunazochuma sisi sio zawatoto nizetu sisi wazazi wao). Kivuli hicho kiondolewe na ni ujinga wa hali ya juu


2---mwanume unajengaje katika kiwanja Cha mwanamke au mwanamke unajengaje kwenye kiwanja Cha mwanaume
**Kwenye SHERIA kunakitu kinaitwa kuchumwa Mali pamoja unapokuja kujenga nyumba kwenye kiwanja alijinunulia mtu kabla ya ndoa huo ni ujuha mkubwa Sana ,kwakweli TUBADILIKe

Mleta mada ,bomoa tofali zako kwenye hiyo nyumba uza maisha yaendelee kabla hamjua MSIISHIE kuPima UKIMwI tu , Jaribuni kusoma SHERIA ya ndoa na mchakato wa TALAKa kupata ufumbuzi wa mambo
 
Kwanza nikupe pole ingawa ni jambo jepesi kwa mwanaume aliekamilika na kujitambua. It's a very minor case.

Pili usitegemee km utapata majibu muafaka kutoka kwa jinsia ya KE maana muda wote lao huwa moja na kuona km wanaume wanawaonea.

Tatu, nimesoma msitari kwa mstari, neno kwa neno, kuna sentensi umesema mkeo aliwahi kukutamkia kuwa "anajuta kuolewa na wewe". Hapo wewe km kidume huoni maneno hayo yana maanisha zaidi ya yale yaliyopo moyoni mwake usio yaona? Ukizingatia inaonesha wewe unaishi mbali na familia yako kwa namna ulivyoelezea humu. Hapo mzee ukiona manyoa jua keshaliwa, na dalili za mvua ni mawingu lakini heri kuziba ufa kuliko kujenga ukuta.

USHAURI
Simamia hapohapo ulipo hivi sasa vinginevyo utajikuta siku moja unatupiwa virago km ambavyo wewe mwenyewe tayari umeshitukia.

Akikataa wazo lako la kumrudishia pesa za kiwanja, basi wewe pindua meza, mwambie yeye akurudishie pesa za ujenzi ulizotumia ili ukanunue kiwanja kingine na kujenga nyumba ya familia. Hiyo ya kwake atajua mwenyewe km atapangisha, kuuza, kumilikisha watoto au kuhonga.

Mwisho, kwa maelezo yako mkeo ni mbinafisi sana na anapenda kuwa juu Yako, na kuna watu wamemshikia akili ndio maana akasema ngoja akae ajifikirie juu ya maamuzi yako. Hivi ukimtongoza mwanamke akakwambia "ngoja nikajifikirie nitakupa jibu" hapo unadhani anaenda kufanya nini km sio kuulizia na kusimulia marafiki.

Kaza Jamba wewe ni mtoto wa kiume hata akienda kushitaki kwa ndugu zako kushitaki, wewe baki na msimamo wako maana familia ni yako na future ya watoto Iko mikononi mwako kwa sasa ambapo bado upo hai.
 
Kiwanja na hati ni chake mwanamke, anakaa na watoto wako humo ndani na anaonekana selfish, nyumba ni vyumba viwili tuu (sio madharau), na watoto wako salama inaonekana, vitu vingine kama mwanaume unaachia tuu ili maisha yaendelee, labda mwenzetu unataka kuvunja nyumba uchukue tofali maana kiwanja sio chako
 
Aisee we jamaa mbona Kama umepiga vitu vikali mchana kweupe
 
Daah
 
Thubutuu

Kuna wanawake ukifariki anapata basha
Huyo basha anamdanganya danganya mwisho ana badili umiliki anakua anasomeka basha wake

Wanawake akili zao unazijua au unazisikia?

Au basha linamdanganya tuuze hapa tujenge pengne

Na huko wanakojenga basha anajiandika yeye
 
Unless nina miaka juu ya 45, ila kama ni below 45 siwezi kaa hapo nagombana na mwanamke kisa alinunua kiwanja nikajenga. Ntajenga tu nyingine, ya pili na ikiwezekana ya tatu. Na viwanja vilivyo vingi mpaka unanunua na kulipa kwa mafungu fungu nikae nabishana? Huo muda bora nitafute rejesho la kiwanja kipya. Halafu mwanamke ambaye hatuelewani kuhusu mali huyo hanifai. Tutalea tu watoto. Mambo ya kulogana na kuuana nani anataka.
 
Kama kweli una nia nzuri kwa mkeo na watoto basi fanya yafuatayo:-
1. Usilazimishe kuandika jina lako peke yako kwani hautakuwa tofauti na huyo mkeo anayetaka kuandika jina lake peke yake hata kwenye suala dogo tu la kuunganishiwa maji
2. Andikeni majina yenu wote wawili kwenye umiliki wa nyumba ili likitokea la kutokea msiisumbue mahakama bali mali igawanywe 50/50 fasta kila mtu afe na chake.
3. Ikishindikana ya kundika majina yenu wote wawili basi jilipuwe andika majina ya watoto wenu kama ambavyo umeshasema mwenyewe kuwa wewe huna shida sana na hiyo nyumba bali unapambania watoto wako wasije dhulumiwa jasho lako..
4. Usije kuachia hiyo nyumba kwa hasira kwani huyo mwanamke namna anavyokujibu ni kama tayari kashapata mwanaume mwenzio. Mbaya zaidi kama kashampenda hachelewi kumzawadia hiyo nyumba au hata akashauriwa kuiuza kama mchangiaji mmoja alivyoeleza hapo juu halafu waende wakajenge upya nyingine ili huyo mwanaume mwingine awe na umiliki au sehemu ya umiliki.
5. Tafuteni muda mkae wawili tu muulizane mlioana kwa ajili ya kujenga familia au mlioana ili mjenge nyumba halafu hiyo nyumba iiangukie ndoa yenu isambaratike. Jibu mtakalopata hapo kwa pamoja ndio litakalotoa mwelekeo wa ndoa yenu. Na hapo ndio kila mmoja wenu atachagua kusuka au kunyoa.

Mwisho kuanzia sasa kuwa na tahadhari sana na huyo mkeo kwa sababu huko anakokwenda kuchukua ushauri akikutana na washauri wajinga wajinga wasioelewa maana na thamanai ya ndoa ni nini hachelewi kulishwa matango pori akija shtuka ndoa yenu imeishaparaganyika kwa suala dogo tu la kugombea umiliki wa nyumba.
 
Hakuna ndoa pale, wanaelekea kwenye divorce wasipokuwa makini
Hatuombei hilo mkuu. Sema kuna wakati busara ingekuwa inauza ungenunua tu. Mimi sio kwamba ni mwema sana au mwenye busara sana hapana. Na wadau wanaweza kuona ni mbinafsi sana ila hapana ninachotetea pia inaweza kuonekana cha kibabe lakini sina lengo hilo ila ninahitaji kulinda kwamba mke wangu aendelee kuwa mke na Mimi niendelee kuwa mume na tuwe wazazi wa watoto wetu tukielewana. Sasa nafahamu mapungufu ya mwenzangu kwa muda tuliyoishi wa miaka sita sasa vyake huwa vinampa kiburi na hivyo kuhatarisha mahusiano yetu kama wana ndoa. Umiliki hata ikowa wangu wala sitakuwa na usumbufu wowote kwake yeye na watoto lakini popote nitakapokuwa niweze kutoa maelekezo yakafuatwa na familia ijengeke kwenye umoja na amani. Sio Jambo dogo ila najaribu kulitatua kwa umakini sana na naamini sitaharibu bali nitaiwekea msingi imara. Ikitokea huo muda aliyoomba kutafakari ndio ametumia kufuatilia huo utaratibu wa umiliki kwangu haitakuwa mshangao na sitapanic bado nitakuwa imara na maisha yatasonga. Watu wanasema naanika mambo ya familia yangu hahaha kwani mnanijua? Na sijamhusisha hata ndugu yangu Jambo hili bado lipo katika level yetu Kama familia ila humu wengine pia watajiifunza nami nitajifunza kutoka kwenu lakini mwisho wa siku Mimi ndio nitaamua kwa busara nilizojaliwa na ushauri mzuri kutoka kwenu wadau. Nashukuru matusi sio mengi mbarikiwe lakini mtuombee pia
 
Asante mkuu. Kweli kazi ni kwangu ila nashukuru kwa muda wako na ushauri.
 
Kuna watu wapuuzi kweli. Mpaka sasa kiwanja sio chako wala huna haki ya kiwanja. Hapo sanasana unaweza kubargain aandike muwa wamiliki wa pamoja (joint occupiers).

Ubabe unaoleta ungekuwa na maana kama kiwanja ungenunua wewe.
 
Kiufupi huyo mwanmke kwanza.amekuheshimu sana

Yaani kiwanja changu

Hata ujenge ghorofa jina la kiwanja linakua langu, hakuna mjadala.
Jina lako.labda liwe kwenye luku
 
Kaka mkeo hawezi kuwatelekeza watoto ila anaweza kukutelekeza wewe, shwetani akutoke kichwani haraka sana. Amka ulikolala kumekucha
Nani kakuambia mwanamke hawezi telekeza watoto wake? Wapo wangi tu wanatelekeza watoto akiwemo wifi yangu. Mali zinatakiwa ziandikwe majina ya wanandoa . Hata mkiachana hakuna sijui mali za watoto au la maana hawakuchangia kuzitafuta hizo mali.
 
Shukrani kwa ushauri mkuu. Ingawa kuandika majina hakumaanishi kumiliki. Hata nikiandika Kwa majina yangu haitimaanisha nina umiliki wa 100%, kwenye kutengana kuna kugawana 50/50.
Kwa taarifa yako ,anaweza kubadili umiliki kinyemela akaansika jina la mama yake mzazi. Siku mkiachana umiliki unaonekana wa mama yake, ndio itajua hujui
 
Hata sijataka kusoma uzi wote, nimeishia tu kudoma hizo sehemu za kufuatilia mambo muhimu unaishia kumtuma mkeo ndio afuatilie...

Hadi hapo nimepata picha aina ya mwanaume ulivyo, na ukiendelea na tabia hiyo ya uvivu utapigwa kama ngoma...
 
MBUZI MWENYE BUSARA mkuu naona hapa baadhi ya watu wanazidi kukushambulia ni wapumbavu hao na wataka sifa na kujifanya wao ni hawana tatizo lolote kwenye familia zao

Hiki unachokipigania wewe hata kwangu ni vilevile ila nimekaa nimetafakari mkuu MBUZI ebu achana na hicho kitu jitahidi kajenge kwenye uwanja ulionunua wewe kaweka husia kwamba hiki kiwanja na nyumba hii nikifa ni mali ya watoto wangu hakikisha mtoto mmoja anakuwepo mbele ya wakili na shahidi atakaesahini huo wosia then endelea na ujenzi kwenye kiwanja chako usiumie kwenye kiwanja cha huyo mwanamke na acha acha kabisa kufanya maendeleo yoyote fanya kama umetoa sadaka kwa hivyo vitofali vya chumba mbili sijui na sebule, mkeo mbinafsi mpotezee anza upya kwenye kiwanja chako.

Sent from my SM-J111F using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…