Mrejesho: Safari yangu ya kwenda kulima mkoa wa Katavi - Wilaya ya Tanganyika, kijiji cha Mwese 4

Mrejesho: Safari yangu ya kwenda kulima mkoa wa Katavi - Wilaya ya Tanganyika, kijiji cha Mwese 4

SSa
Mkuu kipindi nasoma hii reply yako kuna muda picha ilikuwa inanijia kichwani vile ulikuwa unaelezea. Sio siri kijijini ukiwa muaminifu na ukaishi poa na kila mtu hakika utaishi maisha poa sanaaaa.

Nimewahi shuhudia mzee mmoja alikuwa peace sana kwa kila mtu yule mzee watu walimpenda sana na alikuwa maarufu sana kwa kile alikuwa anafanya mpaka vitoto vidogo ni vinamfahamu kwa namna alivyo kuwa.

Ulicho kiandika ni ukweli mtupu, ujue kuishi maisha mazuri sio lazima ukae mjini. Ata kijijini unaweza ishi maisha uyatakayo muhimu ni kutumia akili uliyo pewa. Hongera sana una kitu na fikra nzuri sana, nikwambie tu yote yanawezekana muhimu ni kujitambua tu.

Hii Tanzania kwa kijana unae jitambua, nikisema kujitambua namanisha uko vizuri kichwani na mwenye ndoto na uchu wa kutaka mafanikio. Achana na hawa mabishoo, namanisha mwanaume kweli na una kiasi cha million 1.5 tafuta kijiji chenye rutuba nzuri kwa kilimo huko ndani ndani kisha piga kambi yako ndani ya miaka mitatu utakuja kuleta ushuhuda hapa.

Shida asilimia kubwa ya vijana wanapenda maisha ya kufumba na kufumbua matokeo yake ndio maana leo hii tuna wimbi kubwa la vijana wavivu na wa hovyo kabisa. Hii Tanzania ukiwa makini huko vijijini kutoboa ni kugusa tu na umaarufu, vijana badilikeni maisha hayapo kukusubili kila siku zinasogea. Leo una miaka kadhaa mwaka ujao ni miaka kadhaa pia na kila siku uko pale pale, badilika sasa na uchukue maamuzi sahihi bado hujachelewa. Anaekupenda zaidi ni wewe mwenyewe, tubadilike vijana.
Sahii kama huku nilipo..vijijiji ukienda unakuta hekari inauzwa elfu 70 mpaka laki,..ukijiwekeza mbona kutoboa nirahisi
 
Basi timu imekamilika,Missy Gf andaa begi la safari mama mtumishi katuhakikishia uhakika
😅😅😅Sana tuuuu
Maana kwenye Kila ardhi Kuna wenyeji na miungu Yao
Ss we unaenda na Mungu wako ,kule hawatakuelewa ,lzm umuondoe aliyepo ummilikishe wa kwako,maana ndie mdhamini wako!
Baba, Mwakasege kasema 2024 Yesu awe mdhamini wako kwenye Kila eneo
Bampa to bampa na Yesu...
Vigezo na mashart kuzingatiwa,lazima uingie nae agano!😅
 
Hongera sana kapambane mkuu, mi najipanga nije niweke kambi huko kwenye msimu wa mahindi panapo majaaliwa. Huenda tukawa wote tuombe afya njema na uhai mpaka wakati huo.
Amina mkuu wangu tuombe uzima Leo nimetoka kuongea na wadau huko wanasema ngoma Feb mwisho kuja march patakuwa patamu Sanaa Kwa ajil ya harakati
 
Mkuu unanikumbusha nilikuwa nikenda kwa wakala pale kutoa pesa yule wakala maalufu na mfanya biashara maalufu pale kijijini yani yule jamaa dukani kwake kila kitu unakitaka dukani kwake utakipata.Basi ukienda kutoa pesa utachukua namba ya wakala unaenda kutegeshea kwenye kichugu flani then ukishatoa ule muamala unaenda kumuonyesha ile msg anakukabidhi mpunga wako unasepa.
Lakini cha ajabu yule jamaa ni mjanja sana dahhh ila wachaga ni level zingine kwenye biashara[emoji1787][emoji1787][emoji1787]yani utafanya pale muamala alafu unafanya tena palepale manunuzi mwisho wa siku pesa ile inabaki tena pale unaondoka hata mia una mfukoni[emoji1787][emoji1787][emoji1787].Yani ni maalufu pia kwa nunua maharage,wakulima walio na njaa naela wanapeleka kuuza pale na bei anajipangia atakayo.Unakuta wamama wanopiga nyoka waume zao wanapeleka kuuza pale kisirisiri yani uwe robo,nusu,kilo nzima,debe,gunia,kikombe yanj haachi kitu.Ila kubaliana na bei yake utaki tembea.
Unaona jamaa anavyo make pesa pale.
Ahàaa pale wakala nakujua mkuu vyema wachaga sio watu wazur pemben ya duka wamepanda migomba kibao siku hizi Wana Costa .......siku tunatoka mwese namba kuja mpanda abiria unajua wa kutega mahali walikuta msiba jamaaaa wakapaki gari kusubir abiria wako msibani wale watu bus muda wa kula ikabidi wakale msibani wazike na waondoke na abiria wapya
 
😅😅😅Sana tuuuu
Maana kwenye Kila ardhi Kuna wenyeji na miungu Yao
Ss we unaenda na Mungu wako ,kule hawatakuelewa ,lzm umuondoe aliyepo ummilikishe wa kwako,maana ndie mdhamini wako!
Baba, Mwakasege kasema 2024 Yesu awe mdhamini wako kwenye Kila eneo
Bampa to bampa na Yesu...
Vigezo na mashart kuzingatiwa,lazima uingie nae agano!😅
Imagine mdhamini ni Yesu!hakuna utakapokataliwa...I like it 🥰
 
Muda mzuri wa kujiandaa Kwa walima mahindi na maharage mwezi wa tatu au wa pili mwisho uanze safari ya kwenda huko mwese na lubalisi ......... wandewa wanasema tayari maharage yameanzwa pandwa ya mbegu kwenye Feb yatakuwa tayari kwenye march unaweza panda rasmi Kwa mlimaji ardhi inakuwa na rutuba ya kutosha.
 
Mahindi huko si wanalima msimu mmoja tu? Ule wa mwezi wa 9 ama?
Muda mzuri wa kujiandaa Kwa walima mahindi na maharage mwezi wa tatu au wa pili mwisho uanze safari ya kwenda huko mwese na lubalisi ......... wandewa wanasema tayari maharage yameanzwa pandwa ya mbegu kwenye Feb yatakuwa tayari kwenye march unaweza panda rasmi Kwa mlimaji ardhi inakuwa na rutuba ya kutosha.
 
mifugo.Hapo jifunze matumizi ya dawa mabalimbali za mifugo,kuchoma sindano nk,kwakuwa utakuwa na Simu janja mengine unajiongeza Google search ndugu yangu hapo wafugaji watakuwa wanakimbilia kwako kupata huduma na ushauri.
Wasukuma wanatibu wenyewe mifugo yao. Ukiweza kuuza dawa hapo sawa ila mwanzoni utapata taabu sana maana wanaenda kwa kujuana! Kama anayewauzia vizuri yuko Kapanga au Manyonyi watamfuata huko huko!
 
Jioni palikuwa na wingu na upepo wa mvua kuanguka huko lubalis na viunga vyake nahisi na mwesee itakuwa ilibeep
 
Back
Top Bottom