Mrisho Gambo: Vyeti Feki walipwe, Serikali ilikurupuka!

HIV walitumia vigezo gani kuwaakuri na wakatumia vigezo gani kuwagundua?

Wewe unawatukana Hawa watu lakini ukipata akili utagundua aliyekuwa na kosa ni nani.

Basi serikali haikuwa makini wakati wa kuajiri. Inatakiwa ikubali na iwaombe radhi kwa kuwadhalilisha.

Kwanza serikali ilijidhalilisha sana kujivua nguo kwa wananchi wake na kuwaonyesha ajira zinavyofanyika.
 
CCM inaitaji kutuondolea wabunge wanafiki kama hawa kama inaitaji kubaki madarakani
.leo unasapoti ujinga kesho unaukataa
 
Agenda ya vyeti feki ilikua Sawa kabisa

Issue ya makonda, mkuu alikosea
Agenda ya vyeti feki ilikuwa sawa lakini iliyokosa malengo sahihi na kusudio lake halisi mpaka Leo halijulikani.
Kuna watu waliondolewa kazini kwa sababu tu ya kubadili majina aidha baada ya ubatizo au baada ya kuolewa. Cheti kimeandikwa Magadula Lufunga lkn kwenye ajira sasa anaitwa Joseph Magadula Lufunga, ni kweli kisheria ni watu wawili tofauti lakini kwa nini usifanyike uchunguzi kujua sababu ya huyu kubadilika ghafla? Gambo anaposema serikali ilikurupuka anajua anamaanisha mambo kama haya, usimpinge bila vielelezo.
Pia suala hili lilibagua baadhi ya taasisi kwa kisingizio cha unyeti au usalama. Kwa hiyo ni halali kuhudumiwa na Polisi mwenye cheti fake lakini ni haramu dereva mwenye cheti fake cha form IV lakini ana leseni na kasoma VETA? Kuna walimu waliodaiwa vyeti vya kidato cha nne vina kasoro lakini watu hao wana vyeti vya ualimu walivyopass vizuri kabisa na wamefundisha mashuleni wengine kwa zaidi ya 10-20 na hata baadhi ya viongozi wakubwa wa serikali wamefundishwa na haohao "Mburula". Gambo ana hoja.
 
... imeniuma sana. Ni zaidi ya shetani; rest in hell forever. Binadamu unafikiaje kiwango hiki cha ushetani? Mungu awafute machozi wahusika.
Ofisi yangu ilikuwa ya watu watano, wawili wakaondoka na vyeti majembe, wachapakazi hodari. Hata ndoa zao zilitetereka mabinti wale.
 
Waliobomolewa nyumba zao walipwe fidia.
Waliofukuzwa vyeti warejeshewe au walipwe chao maana walitoa nguvu zao kutumika.
Wa bureau de change warejeshewe pesa zao
Na mishahara ya watumishi iongezwe mara 5 baada ya kusimamishwa na mkurupukaji.
 
Akamatwe. Yaani ughushi cheti , serkali igundue ili ilikuwa inakulipa kwa taaluma usiyo nayo halafu ikikukamata IKULIPE?
Amejitoa akili aliyesema


Itafika sehemu kubaka akikuibia ukigundua unamlipa
Issue siyo kwamba hawana makosa.

Unapokagua vyeti feki halafu JESHINI na kwa WANASIASA unaacha, zoezi zima linakosa MAANA linabaki ni UONEVU tu.

Kwasababu wameshawafukuza, at least wawape MAFAO yao maana waliyafanyia kazi.
 
Issue siyo kwamba hawana makosa.

Unapokagua vyeti feki halafu JESHINI na kwa WANASIASA unaacha, zoezi zima linakosa MAANA linabaki ni UONEVU tu.

Kwasababu wameshawafukuza, at least wawape MAFAO yao maana waliyafanyia kazi.
Sio KWAMBA WANAHITAJIKA KUSHTAKIWA KWA KUGHUSHI NA KUJIPATIA KIPATO ISIVYO HALALI
 
Kagueni na JESHINI na WANASIASA.

Acheni uonevu na roho mbayaaaaaa
 
Siyo kweli

China values education a lot.... Ila kama huna elimu na ukapata chance watakupa.all elite Chinese wanasoma kwenye shule za maana na mitaala mahsusi

Kuna tpfsuti kubwa Kati ya kutumia cheti feki, na kusema ukweli Kwamba hujasoma
Swadaktaa!

China wanatumia billions kusomesha ndani na nje.

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Wewe ni mpuuzi.

Umefanya udanganyifu halafu unataka tumkamate aliyekuajiri? Kwa kosa lipi?

Haya majizi ya vyeti yalipaswa kupewa mashtaka ya jinai na kurudisha fedha zote walizozivuna kutoka kwenye wizi walioufanya!

Jesus! Lots of foolish people here!

Mwizi alipwe? Kweli?
 
Sio KWAMBA WANAHITAJIKA KUSHTAKIWA KWA KUGHUSHI NA KUJIPATIA KIPATO ISIVYO HALALI
Watu wote walioghushi vyeti wana makosa ikiwemo wanajeshi na wanasiasa.

Suala la kukagua wengine na wengine wanaachwa, linafanya zoezi zima linakosa UHALALI. Linakuwa ni UONEVU, UDHULMATI na UKATILI.

Mnakomaa na wasiojiweza tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…