Msaada aliyewahi kupata changamoto hii kwenye ajira

Msaada aliyewahi kupata changamoto hii kwenye ajira

Mimi nilivyoona inawezekana Cheti chake kina matatizo sio halali au kinatumika na MTU tayari.

Ukifanya mtihani hapa Tz wa necta data base zako unakuwa nazo kuanzia result sleep mpaka cheti.

Nadhani yeye hakupaswa kuwa accountable kwa namna yoyote ile.

Kama anaongea ukweli aende necta wampatie matokeo ya kidato cha nne 2002 then alinganishe na cheti chake .


Maana katika taasisi za serikali ambazo huwa zinajitahidi kufanya Kazi vizuri ni necta , yaani necta wanawazidi hadi TCU so afatilie na Kama cheti anakitumia MTU atajua akifika necta.

Then mfumo wa Ajira unatumia cheti cha form four so hawawezi kuingiza watu wawili katika system Kwa kutumia Cheti kimoja japo inawezekana kiujanja ujanja.
 
Habari ndugu zangu, wakubwa shikamooni na wadogo habari zenu. Nasimama na kuleta hoja hii kwa niaba ya Ndugu (Brother from another Mother).
Mwaka jana 2023 huyu ndugu alifanikiwa kuomba ajira (Ajira Potal) na kufanikiwa kuitwa kufanya usaili alifanikiwa kufanya written na baadaye oral na hivyo alifaulu na kupata barua ya kuitwa kazini na Utumishi. Baada ya muda mfupi, kabla ya kufika kituo cha kazi aliombwa cheti halisi cha Form IV alikipeleka Necta, Baada ya hapo, aliombwa kutoa maelezo ya cheti chake alifanya hivyo kwa asilimia mia moja
Alitumiwa barua yenye kuonyesha wasiwasi wa matokeo ya masomo yake, hivyo akaombwa aende shule ya sekondari aliyosoma alifanya hivyo na alipewa yale yale matokeo ya awali ni zamani kidogo 2002. aliweza kufanya comparison na aliona somo moja lililoandikwa Agriculture Science badala ya Agricultural Science, Huyu ndugu anateseka sana hivi sasa ukizingatia muda aliosota kwenye masomo ni mwingi, pia Umri umesonga anategemewa na familia . Tunatafuta msaada kwa wenye uwezo watusaidie kupata Suluhu ya hili Tatizo na kama kuna Sehemu sahihi ya kufika. Mpaka hivi sasa huyu bwana amepata Frustration na ufanisi wake wa kazi umeshuka kwani hajui pakuanzia na ni kweli alisoma na alifanikiwa kupata cheti na kuendelea na masomo ya Elimu ya Juu.
Kwa heshima na Taadhima naomba Msaada wa Mawazo, Ushahuri chanya juu ya nini chakufanya kufanikisha hili jambo. Naomba Kuwasilisha
Jaribu kuongea na nekta awaunganishe na watu wa ajira portal kudhihirisha taarifa ni za kwl
 
Back
Top Bottom