Msaada: Mke wangu anataka tuwe tunaishi na mtoto wa dada yake kila wikiendi na likizo

Msaada: Mke wangu anataka tuwe tunaishi na mtoto wa dada yake kila wikiendi na likizo

Mkuu hakuna mtu namchukia hadharani kama mtu mchoyo wa chakula😡😡😡

Ngoja nikupe hiki kisa kinanihusu mimi Chakorii.

mwaka 1999 nakumbuka kabisa mtoto wa babangu mdogo alikuwa amefikish 40 tangu kuzaliwa kwake...so kulikuwa kuna tafrija kidogo lakni shughuli ilikuwa ni kumbwa tu..watu wengi walikuwepo.
Nakumbuka watu walikuwa wameshaanza kula(kuna kitu mama alinituma nakumbuka)so wakati wameanza kula sikuwepo.

Niliporudi eneo la tukio njaa ilikuwa inauma nakumbuka..nilimkuta binamu yangu mtoto wa Dadake na baba(yeye alikuwa upande wa chakula).nikamfuata nikamwambia binamu njaa inauma sijakula bado...akaniangalia hakunijibu(kuku kuwa kuna watoto wengine wa mtaani na wenyewe walikuw hawajala..so ni kama walikuwa wananisikilizia)

Nikamuona binamu anachukua ungo(kuu kuu kidogo)akatupakulia makoko (chakula kingine kizuri kilikuwepo.nilikiona) tulikula lkni hakuna siku nilikuwa mnyonge kama siku ile😢😢😢niliumia mnooooo..hapo ndipo siku niliyogundua kuwa ninakuwa yangu ni mchoyo wa chakula.

Sikuwahi kusema Kwa yeyote zaidi ya leo hapa JF na hakuwahi kujua kamwe.
Miaka ikapita.mwaka jana tulikuwa tunaenda mkoa fulani kwenye msiba ni mbali kabisa mkoani huko..hakuna na nauli na anataka kwenda kuzika,akaniomba nimkopeshe kiasi fulani cha pesa ni kidogo tu ☹️☹️☹️Ghafla nikakumbuka mwa 1999
Nikajawa namajonzi sijui kwa nini.😩😩
Sikumkopesha ile hela bali nilimpa.nilimwambia nitakulipia nauli usijali mpka tutakakofika msibani.
Sikuwahi kuwa na furaha nae..

So kila nikimuona mtu mchoyo wa chakula ninakasirika na kumuona ni fukara wa nafsi.
Kwahiyo,mtu akileta uchoyo wa chakula na kama nammudu namchana au ninamziria chakula chake ale mwenyewe mpka ashibe au nitoe niwape mbwa wale😒😒😒.

Siwezi ficha hasira kwa mtu mchoyo...niko hivyo.
Pole Sana kwa yalio kupata, binadamu ndivyo tulivyo wengine wanakosa Imani kwa vitu vidogo tu Ila sababu kubwa tunaweza kusema ni hulka ya mtu, tabia inayo tokana na malezi tu ya kwao ama roho mbaya tu ambayo mtu huumbwa nayo.

Cha muhimu ni kuwasamehe tu watu wa namna hiyo wasikupe mzigo nafsini mwako.
 
Nilikuwa-ga najiuliza sana ni kwanini wazazi huwapa watoto majina kama vile Sinandugu, baada ya kudadisi sana moja ya majibu niliyopewa ni kama hii hoja
 
Usiwasikilize wanaokuambia habari za mala mchoyo mala gubu wewe ongea na nafsi yako utachoamua fanya ,imeandikwa kila punda abebe mzigo wake mwenyewe ( watz 4: 16)
 
Mbona umekazania tu hapohapo kwamba mtoto ameambukizwa tabia za jike?,kwani huyo mtoto ana umri gani?,ni utoto tu akikua ataacha Tania za kike
 
Usikute mkeo ni mama wa huyo mtoto
Hili watu hawalioni. Kwanza sidhani kama huyo shemeji yake angekubali hili. Mtoto wake ateseke kisa, au huyo mkewe angelishaachana na hilo wazo maana anajua mumewe hapendi. Jamaa anauziwa mbuzi kwenye gunia na yeye anakubali
 
Hio tabia ya kipuuzi alitakiwa awe nayo mkeo ila inashangaza sana kama kidume cha mbegu ndio kinakuwa na tabia ya hovyo namna hio!

Choyo ni tabia ya kike mkuu!
 
upo sahihi 100%.si ndo ile wageni wamekuja eti watoto wangu walale sebuleni wageni chumbani..Kwangu hiyo hakunaga..watoto wangu acha wajitanue room wageni sebuleni.Yaani watoto wangu wasubirie wengine walale ndo wao walale..Hell No!! kisa kuwafurahisha watu wakati uki ukifariki wanaanza kuwaangalia kama takataka hao hao uliowafadhili na kuwafurahisha.
Kwani hao wageni wanakaa kwako milele?
 
Roho mbaya ipi mkuu wakat mtoto nipo nae kila siku weekend nachozungumzia nikukataa wazazi mtoto kwenda kwa baba yake nahuyo hai na eneo Hilo hilo jiran kisa mama wakambo nababa kutomhudumia mtoto ipasavyo ukiachilia mbali hayo mengne yakuadapt tabia zakike
Sasa aslong as hulipishwi ada swala la mtoto kukatazwa kwenda kwa babaake si swala la maamuzi ya mama yake! Kama hataki kumpeleka mwache mtoto akikua na kujitambua atamtafuta baba yake. Kwanini unakuwa kama unataka kuwalazimisha watu wazima wenzio kitu ambacho wao binafsi hawakiafiki?

Power yako inaishia kwenye ushauri tu, kama wameopt kutokumpeleka kaa kimya fata mambo yako. Kama unaona mtoto wa shemeji yako ni kero mfukuze na uvunje ushemeji na dada wa mkeo usilalamike kama mtu ambaye hana maamuzi.
 
Kwahiyo tumsuse mtoto kwasababu baba yake yupo na hataki kuwajibika?
.
.
Wanaume mna matatizo...mtu kampa mimba mtoto wa kike kamsababishia usingle maza (hatufahamu sababu za kutoishi pamoja, cases zipo nyingi)...bidada kaamua kusaidiana na mwenzake mtoto apate malezi hlf anatokea mwanaume mwingine kuleta vikwazo, Wala hajaombwa amsomeshe ni chakula tu.
Huwa nashangaa sana mnavyosema wanawake hawapendani lkn wanaume ndo hawajawahi kupendana, kutwa kuharibu jamii badala ya kurekebisha. Nyie ndio source ya jamii mbovu.
Mamii huyu jamaa anataka kutufanya wote tuonekane vituko ila trust me wanaume wenye choyo ni 1% tu ya population na hawa huchangiwa na malezi mabovu.
 
Habari wakuu mke wangu ana dada yake ambaye kazalishwa mtoto mmoja na Dada yake hayuko katika ndoa, hajaolewa na aliyemzalisha alikuja akaoa mwanamke mwingine

Sasa basi mimi na mke wangu tuna mtoto mdogo wa umri sawa na mtoto wa Dada yake.. mke wangu amekuwa akimchukua mtoto wa Dada yake kila Ijumaa na kumrudisha Jumapili kwa Dada yake

Sasa akiwa anataka kumrudisha mtoto hataki kurudi kwa mama yake anataka kuendelea kuishi nasi wakati huo baba wa mtoto hana muda na mtoto wake kwa mahitaji ya mtoto yaani hamuhudumii.

Mama wa mtoto hataki hata siku moja kumpelekea mtoto kwa baba yake sababu ana mke mwingine atamtesa, Sasa amekuwa akimsukumia kwangu kwa kigezo cha kuja kucheza na mwenzake

Je, ni sawa baba wa mtoto yupo na mama wa mtoto kukataa mtoto kwenda kwa baba kutembea kwa kisingizio Cha mama wa kambo atamtesa hivyo kuona ni sahihi aende kwa mama yake mdogo hali ya kuwa baba yupo na anajichana na maisha?
Mkuu hapo sijaona kosa zaidi nahisi utakuwa una viashilia vya uchoyo,
Nakushauri mwambie mkeo ili amwambie dada yake achangie pesa kidogo ya uji na ubwabwa ili roho yako iridhike,
Maana sijaona hapo hoja ya msingi kwa upande wako zaidi ya uchoyo,,
2021 uchoyo haulipi!!
 
. Hapo wewe kinachokuuma Ni kuwa kwanini unamsaidia mwanaume mwenzio?
Haswaa, ila kama jamaa hataki kuwajibika afanyeje sasa 😁😁😁? Shemejie amemsogeza mtoto ili apate ile moral support ya baba ila lenyewe halielewi limetanguliza kijiba cha roho na choyo mbele.
 
Bwana shemeji Lea tuu huyo mToto kwa hyo part time tuu si vbaya

Akihamia apo ndio itakuw changamoto kuja kumsomesha Kama unakipato kdogo au Kama mwanao unatak asome private


Ila kwa mfumo huo vumilia tuu maan hao watoto wa nje unawez kuta jamaa Hana unakika nae huyo mToto labda kutokan na mwenendo wa huyo mama ake kpnd hichoo
Yeah huenda ndio chanzo akamtema huyo mwanamke. Maana hawa wanawake wengine sio kabisa.
 
Mambo kama haya hukaribisha umaskini sana ktk familia zetu za kimaskini, hii tabia imenikosti sana.
Kuna watu hapa watasema kwani sh ngapi lkn hawajui chochote kile ni gharama hata kama ni sh 100. Mjue tu bajeti ya familia haiwezi kua ileile

Mkuu nakuelewa sana
 
Mkuu Hana tabia za kishenzi Ila tatizo ni kuwa mtoto kashaadapti michezo ya kike maana hata umletee vitu vya mchezo wa kiume havitumii muda wote unakuta anacheza michezo ya kike na mwezie Sasa kwangu naona ni tatizo Hilo maana mama mtu Hana habari kwake nisawa
Mkuu acha ukimya mpige marufuku mbona simpo tu, sioni haja ya kuja kuomba ushauri huku maamuzi unayo wewe
 
Du mkuu una roho ngumu Sana ,mtoto mdogo tu unamuanzishia uzi humu?. Wengine tunakaa na wakubwa zaidi ya hao 3. Akili inatanuka ya utafutaji ,maisha yanaenda .Mwisho wa siku wananisaidia kwenye shughuli nyingi na zinaenda poa.Nawaona moja ya familia yangu ,maisha yanaendelea.Unapowafanyia mazuri ,wanaposhukuru Mungu nawe anakuongezea
 
Back
Top Bottom