Msaada: Namna ya kukagua gari used Tanzania kabla sijanunua

Msaada: Namna ya kukagua gari used Tanzania kabla sijanunua

profesawaaganojipya

JF-Expert Member
Joined
Apr 21, 2015
Posts
1,595
Reaction score
3,416
Wadau nimejichanga kiasi fulani cha pesa, ingawa hakitoshi kuagiza gari used Japan lakini naweza nunua ya mkononi hapa Dar walau nitimize ndoto yangu ya kutembea nikiwa nimekaa.

Naomba msaada vitu vya kukagua kwenye gari kujua kama nzima au nabambikwa, pia kama imewahi pata ajali au la, nitajuaje?

Shukrani.
 
Kwa kifupi na kifupi sana tena ,ukitaka gari nzuri kwa hapa bongo land uwe na kuanzia milioni nane mpaka 13 nje ya hapo sijui uba milioni sita sijui tano yatakukuta kama yaliyonikuta mimi kwa kifupi kama bajeti yako ndogo sana bora uongezee ongezee ukishindwa nunua hilo gari na turubai lake kabisa nna uhakika utalifunika tu
 
Kwa kifupi na kifupi sana tena ,ukitaka gari nzuri kwa hapa bongo land uwe na kuanzia milioni nane mpaka 13 nje ya hapo sijui uba milioni sita sijui tano yatakukuta kama yaliyonikuta mimi kwa kifupi kama bajeti yako ndogo sana bora uongezee ongezee ukishindwa nunua hilo gari na turubai lake kabisa nna uhakika utalifunika tu
🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣
 
Wadau nimejichanga kiasi fulani cha pesa,ingawa hakitoshi kuagiza gari used japan,lakini naweza nunua ya mkononi hapa dar walau nitimize ndoto yangu ya kutembea nikiwa nimekaa.
Naomba msaada vitu vya kukagua kwenye gari kujua kama nzima au nabambikwa,pia kama imewahi pata ajali au la,ntajuaje?
shukrani.
Kama ni gari ya 10m au zaidi sina shaka utapata ilio nzima ila kama ni ya chini ya 8m kuwa makini sana.
Gari ni engine ila pia body nzuri
 
Wadau nimejichanga kiasi fulani cha pesa,ingawa hakitoshi kuagiza gari used japan,lakini naweza nunua ya mkononi hapa dar walau nitimize ndoto yangu ya kutembea nikiwa nimekaa.
Naomba msaada vitu vya kukagua kwenye gari kujua kama nzima au nabambikwa,pia kama imewahi pata ajali au la,ntajuaje?
shukrani.
Well,ukifika kwenye gari kwanza kabisa kagua kwa kuiwasha,sikiliza mlio wake wa engine,kisha ukiwa ndani ya gari funguo bonet moja kwa moja nenda upande wa engine ya gari lako,chomoa deep stick kisha iache ingurume kwa sekunde kadhaa,ukiona pale ulipo chomoa deep stick kuna fuka/toa moshi basi jua engine ipo njiani kusumbua,kisha rudisha deep stick yako kisha funguo mfuniko wa engine kagua kama oil inapanda kwa usahihi,hapo utaona vijitone vya oil vinaruka mithili ya mtu anaekaanga labda kitu kwenye jikoni kwa kutumia mafuta kuna vile vijitone huwa vinaruka vidogo sana,ukiona vitone hivyo havitoki basi jua engine haipandishi oil kwa usahihi hapo kuna mawili uchukue ukarekebishe tatizo hilo au uachane na hiyo gari,vuta accelerator ili ukague vizuri mlio wa engine yako,nock alert kama ipo kwenye engine pia kagua exhaust kama kuna moshi unatoka ambao tofauti,ukikuta kwenye exhaust kuna moshi mweupe basi jua engine ya gari ina SMOKE pia itakuwa engine inakula oil ili utatue tatizo hilo yapasa overhaul ihusike,na ukifanya overhaul engine hiyo kuna mawili ikae sawa kabisa ama iendelee kukusumbua hivyo nakushauri uachane nayo.Kagua Arternator kama inachaji vizuri tumia kitu chenye asili ya chuma gusisha pembeni mwa Arternator kama unahisi kuna mvutano flan kama wa sumanku basi jua hiyo ipo fresh kwenye kufua mfumo wa umeme na swala zima la mfumo wa Ac pamoja na kupoza joto la engine kwa kuwa engine inapozwa kwa vitu vitatu{maji,fan belt,na fan yenyewe}.

Kila kitu kikikaa sawa hapo kwenye mfumo mzima wa engine basi funika bonnet rudi ndani washa Air condition ukiona hewa safi baridi inatoka vizuri basi jua ipo vizuri,ukiona gari inatetemeka basi jua kuna vitu vichache vya kubadilisha ama kurekebisha.

Endesha gari ili ukague uzima wa miguu ya gari hapa nakushauri uingize gari kwenye barabara za mtaani haswaa zile zilizopo rough ukisikia kuna milio inayotoka tofauti na ile ambapo upo kwenye lami basi jua uandae hela ya kutosha ili ukarekebishe.

Ahsante karibu Pm kwa ushauri zaidi

Note
Swala la kukagua gari sijui imepata ajali sijui haijapata hili lisikusumbue,hata gari tunazo letewa kutoka huko nje baadhi zimepata wewe kagua vitu hivyo nilivyokuambia.
Kama ntakua kuna sehemu sijaiweka sawa ama nimekosea basi humu kuna wataalam zaidi na watarekebisha pia
 
Watu wengi hukimbilia ubora wa gari lakin mi niongezee kwa msisitizo mkubwa,
UNAPONUNUA GARI YA MKONONI ZINGATIA SANA UHALALI WA GARI YENYEWE.
Maana madhara ya ubovu wa gari yenyewe yanarekebishika(hakuna gari isiyotengenezeka).
Lakin madhara ya kisheria kumiliki gari yenyewe hayarekebishiki kirahisi.
Kwahiyo utahitaji ukaguzi wa aina 2 (duo diligence)
1 . Fundi wa mechanical/electrical.
2. Mkaguzi wa uhalali.
 
Kwa kifupi na kifupi sana tena ,ukitaka gari nzuri kwa hapa bongo land uwe na kuanzia milioni nane mpaka 13 nje ya hapo sijui uba milioni sita sijui tano yatakukuta kama yaliyonikuta mimi kwa kifupi kama bajeti yako ndogo sana bora uongezee ongezee ukishindwa nunua hilo gari na turubai lake kabisa nna uhakika utalifunika tu
Duh mkuu mbona unatutisha sana. Kwa uchumi huu kibubu kitaongezeka au kupungua
 
Kwa kifupi na kifupi sana tena ,ukitaka gari nzuri kwa hapa bongo land uwe na kuanzia milioni nane mpaka 13 nje ya hapo sijui uba milioni sita sijui tano yatakukuta kama yaliyonikuta mimi kwa kifupi kama bajeti yako ndogo sana bora uongezee ongezee ukishindwa nunua hilo gari na turubai lake kabisa nna uhakika utalifunika tu
sio kweli,unataka kunivunja moyo tu,ina maana nikitaka starlet nzuri niwe na m 13,hiyo c bei ya yard au?
 
Well,ukifika kwenye gari kwanza kabisa kagua kwa kuiwasha,sikiliza mlio wake wa engine,kisha ukiwa ndani ya gari funguo bonet moja kwa moja nenda upande wa engine ya gari lako,chomoa deep stick kisha iache ingurume kwa sekunde kadhaa,ukiona pale ulipo chomoa deep stick kuna fuka/toa moshi basi jua engine ipo njiani kusumbua,kisha rudisha deep stick yako kisha funguo mfuniko wa engine kagua kama oil inapanda kwa usahihi,hapo utaona vijitone vya oil vinaruka mithili ya mtu anaekaanga labda kitu kwenye jikoni kwa kutumia mafuta kuna vile vijitone huwa vinaruka vidogo sana,ukiona vitone hivyo havitoki basi jua engine haipandishi oil kwa usahihi hapo kuna mawili uchukue ukarekebishe tatizo hilo au uachane na hiyo gari,vuta accelerator ili ukague vizuri mlio wa engine yako,nock alert kama ipo kwenye engine pia kagua exhaust kama kuna moshi unatoka ambao tofauti,ukikuta kwenye exhaust kuna moshi mweupe basi jua engine ya gari ina SMOKE pia itakuwa engine inakula oil ili utatue tatizo hilo yapasa overhaul ihusike,na ukifanya overhaul engine hiyo kuna mawili ikae sawa kabisa ama iendelee kukusumbua hivyo nakushauri uachane nayo.Kagua Arternator kama inachaji vizuri tumia kitu chenye asili ya chuma gusisha pembeni mwa Arternator kama unahisi kuna mvutano flan kama wa sumanku basi jua hiyo ipo fresh kwenye kufua mfumo wa umeme na swala zima la mfumo wa Ac pamoja na kupoza joto la engine kwa kuwa engine inapozwa kwa vitu vitatu{maji,fan belt,na fan yenyewe}.

Kila kitu kikikaa sawa hapo kwenye mfumo mzima wa engine basi funika bonnet rudi ndani washa Air condition ukiona hewa safi baridi inatoka vizuri basi jua ipo vizuri,ukiona gari inatetemeka basi jua kuna vitu vichache vya kubadilisha ama kurekebisha.

Endesha gari ili ukague uzima wa miguu ya gari hapa nakushauri uingize gari kwenye barabara za mtaani haswaa zile zilizopo rough ukisikia kuna milio inayotoka tofauti na ile ambapo upo kwenye lami basi jua uandae hela ya kutosha ili ukarekebishe.

Ahsante karibu Pm kwa ushauri zaidi

Note
Swala la kukagua gari sijui imepata ajali sijui haijapata hili lisikusumbue,hata gari tunazo letewa kutoka huko nje baadhi zimepata wewe kagua vitu hivyo nilivyokuambia.
Kama ntakua kuna sehemu sijaiweka sawa ama nimekosea basi humu kuna wataalam zaidi na watarekebisha pia
asante mkuu,umenyooka sana.
 
Watu wengi hukimbilia ubora wa gari lakin mi niongezee kwa msisitizo mkubwa,
UNAPONUNUA GARI YA MKONONI ZINGATIA SANA UHALALI WA GARI YENYEWE.
Maana madhara ya ubovu wa gari yenyewe yanarekebishika(hakuna gari isiyotengenezeka).
Lakin madhara ya kisheria kumiliki gari yenyewe hayarekebishiki kirahisi.
Kwahiyo utahitaji ukaguzi wa aina 2 (duo diligence)
1 . Fundi wa mechanical/electrical.
2. Mkaguzi wa uhalali.
hapo namba 2,umeongea point sana,mungu asaidie,magari mengi ya bongo ni ya dili.
 
Well,ukifika kwenye gari kwanza kabisa kagua kwa kuiwasha,sikiliza mlio wake wa engine,kisha ukiwa ndani ya gari funguo bonet moja kwa moja nenda upande wa engine ya gari lako,chomoa deep stick kisha iache ingurume kwa sekunde kadhaa,ukiona pale ulipo chomoa deep stick kuna fuka/toa moshi basi jua engine ipo njiani kusumbua,kisha rudisha deep stick yako kisha funguo mfuniko wa engine kagua kama oil inapanda kwa usahihi,hapo utaona vijitone vya oil vinaruka mithili ya mtu anaekaanga labda kitu kwenye jikoni kwa kutumia mafuta kuna vile vijitone huwa vinaruka vidogo sana,ukiona vitone hivyo havitoki basi jua engine haipandishi oil kwa usahihi hapo kuna mawili uchukue ukarekebishe tatizo hilo au uachane na hiyo gari,vuta accelerator ili ukague vizuri mlio wa engine yako,nock alert kama ipo kwenye engine pia kagua exhaust kama kuna moshi unatoka ambao tofauti,ukikuta kwenye exhaust kuna moshi mweupe basi jua engine ya gari ina SMOKE pia itakuwa engine inakula oil ili utatue tatizo hilo yapasa overhaul ihusike,na ukifanya overhaul engine hiyo kuna mawili ikae sawa kabisa ama iendelee kukusumbua hivyo nakushauri uachane nayo.Kagua Arternator kama inachaji vizuri tumia kitu chenye asili ya chuma gusisha pembeni mwa Arternator kama unahisi kuna mvutano flan kama wa sumanku basi jua hiyo ipo fresh kwenye kufua mfumo wa umeme na swala zima la mfumo wa Ac pamoja na kupoza joto la engine kwa kuwa engine inapozwa kwa vitu vitatu{maji,fan belt,na fan yenyewe}.

Kila kitu kikikaa sawa hapo kwenye mfumo mzima wa engine basi funika bonnet rudi ndani washa Air condition ukiona hewa safi baridi inatoka vizuri basi jua ipo vizuri,ukiona gari inatetemeka basi jua kuna vitu vichache vya kubadilisha ama kurekebisha.

Endesha gari ili ukague uzima wa miguu ya gari hapa nakushauri uingize gari kwenye barabara za mtaani haswaa zile zilizopo rough ukisikia kuna milio inayotoka tofauti na ile ambapo upo kwenye lami basi jua uandae hela ya kutosha ili ukarekebishe.

Ahsante karibu Pm kwa ushauri zaidi

Note
Swala la kukagua gari sijui imepata ajali sijui haijapata hili lisikusumbue,hata gari tunazo letewa kutoka huko nje baadhi zimepata wewe kagua vitu hivyo nilivyokuambia.
Kama ntakua kuna sehemu sijaiweka sawa ama nimekosea basi humu kuna wataalam zaidi na watarekebisha pia

Hongera sana mkuu kwa maelezo yako mazuri sana sana. Kuna umuhimu JF ikawapa thamani ya pekee watu kama hawa . Siku za hivi karibuni JF imekosa michango ya maana kwenye madaa nyingi labda kizazi kipya hiki lakini.. kwa ufupi HONGERA SANA!
 
Duh mkuu mbona unatutisha sana. Kwa uchumi huu kibubu kitaongezeka au kupungua
Sio kweli mimi nmenunua gari used 3 mbili ndizo zilikuwa zinachezea 12, moja ilikiwa 7.5 na zote nilikaa nazo kila moja zaidi ya miaka 3 na kwa kipindi chote hazikuwah niletea shida yoyote zaidi ya service ya kuchange brake pads, oil, bush.
Ni umakini wako tu
 
Wadau nimejichanga kiasi fulani cha pesa,ingawa hakitoshi kuagiza gari used japan,lakini naweza nunua ya mkononi hapa dar walau nitimize ndoto yangu ya kutembea nikiwa nimekaa.
Naomba msaada vitu vya kukagua kwenye gari kujua kama nzima au nabambikwa,pia kama imewahi pata ajali au la,ntajuaje?
shukrani.
Kama gari ilipata ajali, ikanyooshwa vizuri, taa ya Airbag ikang'olewa au kuzibwa hutokaa ujue kama hiyo gari ilipata ajali.

 
Duh mkuu mbona unatutisha sana. Kwa uchumi huu kibubu kitaongezeka au

sio kweli,unataka kunivunja moyo tu,ina maana nikitaka starlet nzuri niwe na m 13,hiyo c bei ya yard au?
Narudia tena na sauti naongeza hayo magari ya milioni tatu sijui nne na nusu utakuja ufe na presha au uwe mtu wa hasira hasira mpaka nyumba nzima ikuogope nna ushuhuda sasa wewe jichanganye useme hukuambiwa, hakuna cha starlet wa stargo wewe ndugu yangu tusiyejuana ongezea hela usije kufanya makosa kama niliyofanya mimi haya
 
Wadau nimejichanga kiasi fulani cha pesa,ingawa hakitoshi kuagiza gari used japan,lakini naweza nunua ya mkononi hapa dar walau nitimize ndoto yangu ya kutembea nikiwa nimekaa.
Naomba msaada vitu vya kukagua kwenye gari kujua kama nzima au nabambikwa,pia kama imewahi pata ajali au la,ntajuaje?
shukrani.

Nilikuwa sijawahi kununua gari mkononi maisha yangu yote,ila mwaka jana nilinunua na maelezo ya screenshot hii yalinisaidia kuna uzi umezungumzia hilo suala nimesahau jina ila nilibahatika kuscreenshot
Screenshot_20220514-230959_Chrome.jpg
 
Narudia tena na sauti naongeza hayo magari ya milioni tatu sijui nne na nusu utakuja ufe na presha au uwe mtu wa hasira hasira mpaka nyumba nzima ikuogope nna ushuhuda sasa wewe jichanganye useme hukuambiwa, hakuna cha starlet wa stargo wewe ndugu yangu tusiyejuana ongezea hela usije kufanya makosa kama niliyofanya mimi haya
Kuna nyingine zinakuwa nzuri tu sio kila gari watu wanauza kisa bovu wengine wanauza kwa shida ya haraka wengine wanauza gharama za maintenance na services za gari husika zimekuwa ghali wanashindwa kuzihandle,hata hapa Jf kuna watu wanauza magari used ya bei hiyo yamenyooka kinoma na bei ni chee hakuna shida wala nini
 
Kuna nyingine zinakuwa nzuri tu sio kila gari watu wanauza kisa bovu wengine wanauza kwa shida ya haraka wengine wanauza gharama za maintenance na services za gari husika zimekuwa ghali wanashindwa kuzihandle,hata hapa Jf kuna watu wanauza magari used ya bei hiyo yamenyooka kinoma na bei ni chee hakuna shida wala nini
Nisije kuonekana mbishi hapa haya jameni kanunueni hayo magari ya aftatu alafu muone kama mtu hajaenda kutubu kwa mfalme zumaridi hapa
 
Back
Top Bottom