Nilichojifunza na kukiona kwa hawa wasaidizi, wana walimu wengi sana hasa majirani zetu wenye wivu. Wanawajaza maneno hasi mengi kiasi kwamba anawaona kwa mtazamo mwingine kabisa mbaya.
Kingine wanatumiwa sana na Shetani, hasa wale ambao hawajasimama kwenye imani sawasawa. Utakuta wanakamatwa na mapepo, ndio yanayowafanya wafanye vituko na wengine wanakuwa maajenti wa Shetani.
Ukiwa na watoto ambao umewaweka huru kukueleza vitu, watakueleza mengi kuhusu mlezi wao huyo.
Muhimu ni kuwa makini na kumwomba Mungu awasaidie, maana wanaweza kufanya jambo baya la kukuletea maumivu na majuto.