Msaada: Naomba nijue stahiki za watoto wangu

Kwenye maugomvi ya mahusiano sidhani kama watoto hua wanahusika na lolote " naa achukiwe mtu anaetumia watoto kama kigezo cha ushetani wake " wakati watoto hawausiki!

Umri huo wa watoto wako bado wana muhitaji mama zaidi kuliko baba, hata baba awe na uwezo upi ila kwa umri huo bado mtoto ni wa mama!

Mwambie akatishe huduma mkutane watoto wakiwa wametimiza miaka 7, watoto watakula unachokula wewe basi!
 
alishaenda yeye kudai watoto ustawi naona wamepewa hongo maan wananishaur baba ana haki ya kuwachukua eti watoto ndo maan nikataka kuenda mahakamani
Mkuu kama una tabia kama za ex wangu Mungu anakuona. Ndiye chanzo cha ndoa kuvunjika na ni jeuri kweli kweli. Mkitengana na mwenza wako kusema kweli maisha hayawi tena 100% sawa hasa kama watoto ni wadogo. Na mbaya zaidi mkianza kukorofishana kwenye mambo ya matumizi, nani akae na watoto, uelewano hakuna.... maisha yanakuwa magumu kweli kweli.
 
Safi sana. Endelea hivyo hivyo na kuna siku utalipwa mazuri yako. Nilichojifunza kwenye maisha ni kuwa ndoa inapovunjika yule ambaye alikuwa chanzo cha ndoa kuvunjika ataendelea kutangatanga na yule victim atakuja kusimama na kuwa imara.
 
😳😳😳😳😳😳😳
Duuuuh!! Kazi mnazo!!
Ni kweli ni kazi dear ila sio kazi kubwa kama kazi ya kulea watoto wawili kwa kipato cha kuuza mandazi.

Kama kina Beyonce na Rihana na kina Hillary Clinton walikubali kuonekana wajinga na dunia nzima ndo sembuse yeye?
 
Daah pole sana Dada
 
Na ndio maana nikamwambia ajishushe kwa mama mkwe wake maana kasema mama ndio alikua mwiba.

Ukute kuna vitu alikua anafanyia mumewe vinamuuma huyo mama.
 
Another one
 
huyo mume wako ni msomi sn had kufikia hatua hio ina maana kuna jambo kubwa lipo nyuma yake

Mwanaume hawez acha shindwa lea watoto wake kama haluna jambo kubwa lililokuwa nyuma

Pengine anahis akiendekea toa hizo hela utakula na hawara yako(nawaza tu lkn) mana tunajiuliza kwann agome had kutunza familia wakat ana hela nzur tuuu

Na je mlifunga ndoa?ipoje kuachana kwenu?

Dada labda nikwambie ukweli tu kuwa wanaume wengi huwa tunavisiran sn hasa tukigundua pengine mke wako sio muaminif au pengine anatoa sir za ndan anapeleka nje,n k

Hata tukikupa ushaur humu bila kujua chanzo chenu cha kutengana bado tutakuwa tunatwanga maji kwenye kinu
 
huyo mume wako ni msomi sn had kufikia hatua hio ina maana kuna jambo kubwa lipo nyuma yake

Mwanaume hawez acha shindwa lea watoto wake kama haluna jambo kubwa lililokuwa nyuma

Pengine anahis akiendekea toa hizo hela utakula na hawara yako(nawaza tu lkn) mana tunajiuliza kwann agome had kutunza familia wakat ana hela nzur tuuu

Na je mlifunga ndoa?ipoje kuachana kwenu?

Dada labda nikwambie ukweli tu kuwa wanaume wengi huwa tunavisiran sn hasa tukigundua pengine mke wako sio muaminif au pengine anatoa sir za ndan anapeleka nje,n k

Hata tukikupa ushaur humu bila kujua chanzo chenu cha kutengana bado tutakuwa tunatwanga maji kwenye kinu
 
Watoto bado ni wadogo sana wabaki kwa mama; muhimu baba wa watoto atoe huduma muhimu kwa watoto.
 
Pole lakini kuachana haijawahi kuwa suluhu ya changamoto zinazokabili wanandoa, jitahidini kuweka changamoto zenu kando mlee familia mliyoianzisha kwa pamoja. Kuachana kwenu panaathiri pakubwa hata mustakabali wa watoto wenu wasiokuwa na hatia
Unaweza kuishi na nyoka?
 
Usiwatumie watoto kama kitega uchumi chako
 
Sasa unalazimisha kukaa nanwatoto then unataka yeye ndo awatunze, kama hauwezi kuwatunza waache waende kwa baba yao. And ni stahiki gani unazitaka kwake na yeye atapata stahiki gani kwako.
 
Usiwatumie watoto kama kitega uchumi chako
Hakuna kitu kinakera kama kulea mtoto peke yako wakati mwenzio uwezo anao, ugomvi wa wazazi halafu baba akakataa kutoa matumizi anayemuumiza ni mtoto wake.
Wanaume wengi wanafikiria akimpa matumizi mama mtoto wake amemfanya kitega uchumi na anafaidi sana ila trust me kama mngekuwa mnajua jinsi wamama wanavyojitoa kwa watoto wenu hata kama hana uwezo msingefikiria kuumia kutoa hata cent.
 

Jibu ndo hilo hataki wewe ufaidike chochote kwenye huduma atayotoa kwenda kwa watoto. Hatawewe unalijua ilo bado unahitaji msaada wake ndo maana unataka kwenda mahakamani.

Sikushauri utafute haki ya watoto kwa nguvu ivo itakughalimu sana ndo utazidi kupandikiza chuko juu yenu.

Chagua moja ishi na wanao bila msaada wowote wa baba yao chakalika mwenyewe wanao wale yani assum baba yao angekua kapuku hana lolote kwani ungesumbuana nae mahakamani? Au kubali vile baba watoto anavyotaka watoto uzuri mpaka sasa watoto kama washafikia umri wa miaka mi3 hawata kusahau watakutafuta tuu

Ila najua kwenye nafsi yako unahitaji kutumia hao watoto kufaidika na uyo ex wako wanawake ndo mlivyo ila angekua hana lolote hapo saivi ungesha moveon zamani na hata watoto ungewabambikizia baba mwingine ila kwakua unaona kunakitu ndo maana unachelewa kumoveon.
 

Iyo yote anajisumbua mkuu maana mentality ya mama mkwe anajua uyu anamtaka mwanae sababu ya mali, so hawezi kuona thaman yake kwenye kujipendekeza huko. Mi naona yeye mwanamke ndo amoveon kijeshi aache kutia huruma maana anataka kua kati wakati wao washamua vita ni either awape watoto au abaki na watoto.

Mama watoto yeye anataka awe kati kati yani asitoe watoto ila baba alee wanae kupitia yeye so vitu kama mawasiliano na support viendelee inshot mwanamke hajamoveon na itamtesa sana.

Ukichunguza utaona anapenda mume anapenda na watoto vyote anavitaka. Na am sure value ya mume ipo kwa uyu mwanamke sababu ya uwezo alonao uyo mwanaume ikitokea akafukuzwa kazi akarudi kua zero fukara sidhan kama uyu mwanamke atababaika nae.

So to conclude dada inabidi achague moja na ajiamini katika maamuzi yake asibabaike atapoamua kufanya maamuzi either ampe watoto ye awe anaomba kuwaona au aachane na uyo ex asimsumbue kwa chochote apambane kijeshi kuwasomesha na kuwalea wanae bila kujali utajiri wa baba yao na yote yanawezekana kama akiamua na akamtanguliza mungu.
 
Why msitoe matumizi na nyie, watoto wakikaa kwa baba zao huwa mnatoa matumizi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…