Msaada: Nimefikia hatua ya kunywa Pepsi 4 kwa siku, nifanyeje kuacha?

Kuna kipnd nilikuwa addicted na peps,,,, asbh nikipiga supu au chai napata peps, mchana after lunch peps,,, now sijaacha ila nimepunguza,,, kwa wiki naweza kunywa tatu au 2 ! Jitahd upunguze mdogo mdogo
 
Mimi nilikua nakunywa 2 kwa siku, once nilikosa pepsi nikashindwa kulala, saa saba usiku nikaingia barabarani for 1 hour kwenda kutafuta 24hours sheli yenye duka ninunue pepsi, hapo ndiyo nilijishtukia nina tatizo.

Niliacha kwa sababu Orthodontist aliniambia after 10 years nitakua sina nusu ya meno nikiendelea kunywa hizo soda. Niliogopa na toka siku hiyo sijanywa pepsi, that was 9 years ago. Dr. Martin, Muhimbili 🙌 🙌🙌🙌
 
Aisee punguza hata miye zamani nilikuwa nakunywa sana yaani nikipita tuu Dukani ni Pepsi. Ila kwa sasa ni mchana tuu baaasiii.
 
Umelipia tangazo?
 
Hiyo ni hatari. Unatengeneza mazingira ya kuja kusumbuliwa na Kisukari.
 
Ikiwa ya baridi na hili jua si unaelewa lakini?😅
Mimi namshukuru Mungu ki ukweli nimeweza....naweza maliza hata wiki sijanywa soda..Maajabu sasa nikija kuinywa chupa simalizi...

Sasa hivi nimekuwa addicted na chai jamani...Nazeeka🤣

Nilikuwa addicted na pepsi, nikaamua kuacha mara moja pasipo kujishauri. Sasa hivi nikihisi kiu nakunywa maji.

Hapo kwenye chai, sijui ndo kuzeeka kwenyewe msemo wako.
Nisipokunywa tangawizi jioni sijisikii poa, hata kuwe na joto namna gani.
 
Nilikuwa addicted na pepsi, nikaamua kuacha mara moja pasipo kujishauri. Sasa hivi nikihisi kiu nakunywa maji.

Hapo kwenye chai, sijui ndo kuzeeka kwenyewe msemo wako.
Nisipokunywa tangawizi jioni sijisikii poa, hata kuwe na joto namna gani.
Na akiweza kuji'control kwenye soda na kg's pia zitapungua...

Mimi ni chai hata mchana....Kahawa tu majani siwezi...😄
 
Ni hatari mkuu, kuacha uwe unachanganya kidogo na konyagi iwe chungu, utaachwa kwa mbinu hiyo.
 
Kawaida tu ila jita hi idi upunguze
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…