Msaada: Nimewapa ujauzito wanawake wawili, nawapenda ila dini yangu hairuhusu kuwa na wake wawili

Msaada: Nimewapa ujauzito wanawake wawili, nawapenda ila dini yangu hairuhusu kuwa na wake wawili

Kwahiyo dini yako inaruhusu kuzini na watu wawili?
Huu ni unafiki wa Kiafrika.
Zuchu anasema hawezi kutangaza pombe dini yake haimruhusu , sasa ukimuuliza hizo bikini ambazo unazivaa majukwaani dini yako imeruhusu hana majibu.
 
Dini yako hairuhusu kuwa na wake wawili lkn inakuruhusu kuzini na wanawake wawili?

Ifike mahala muache kuficha uchafu wenu na upumbavu wenu kwenye vivuli vya dini.

Huwa siku zote nasema, Kama huyo Mungu wenu wa dini yupo, basi percentage kubwa ya atakaowachoma moto ni ninyi wanadini, wanadini ambao mnaficha maovu yenu kwenye kichaka cha imani.

Nasemaje oa hao wanawake au ukachomwe moto, mnavyoparurana hamkujua suala la dini?
Dini imekua kichaka aisee ..fact mkuuu wambie
 
Mdogo wangu kwa jinsi ulivyo hadithia umekaa kama wewe ndio starring ila hapo kuna mawili.

Mwanzo uliwaumiza vichwa wao, means kila mmoja hawezi kwenda kukaa kizembe lazima apange mikakati ya kukuteka bwamdogo.

Hapo, What if huyo R kapewa kitu huko mkoani kaja kwako na mbinu ya mimba!?

S nae ulipotezana nae, hivi unadhani mwenye mkongojo ni wewe tuu, yaani na yeye alikuwa anakusubiria wewe baada ya madhira yote yale, sasa probably nae kaja na same mbinu.

Uliwaumiz vichwa wao, saaa wanakuumiza kichwa wewe.

Ndio maana ukileta mada kama hii hapa, watu wanaulizaga umri wako na wengine wanauliza jinisa yako [emoji23]mvulana au mwanaume.

Kafikirie hayo kabla ya dini.
 
Wala usijali mzeya wee nitakupa ukiwazalisha huku hujawaoa huo ni uninga wao wenyewe wala sitakilaumu kwa maana mwanamke ndio anaye amua either apate au asipate mimba
Nyege hazina breki
 
Lovely ..wicked mate!!!
Wee jamaa mie naona tukupe urais wa chama letu la wanaume. Ni mwendo wa kuwazalisha tuu hapana kuoa. Wee hao wala wasikuoe presha. Ulisha wapa mimba hawana ujanja tena. Saka ndalama uweze kuwahudumia watoto na mama zao basi..
Jamaa ni mwamba,tumpe Nishani 🤣
 
Wakuu salamu natuamini mnaendelea na mapambano ya kila siku na mapambano ya Tozo. Samahani kwa uandishi wangu mimi sio expert sana wa kujielezea kwa maandishi.
Mwaka 2019..
Nilikuwa na mahusiano na binti mmoja, ambaye kwa muda huo ndo alikuwa main huyu tumuite R. Basi nilikuwa na mahusiano nayo kama miaka miwili hivi.. kufikia 2019 alihamishiwa mkoa fulan kwenye halmashauri fulan. Basi nikabaki kidume mwenyewe DSM ikaenda kama miezi sita.. basi kama ujuavyo upweke mbaya, nikaja kuwa na mazoea na binti fulani huyu tumuite S .. basi nkawa na mazoea mwisho wa siku yakawa mahusiano na huku R hajui hili wala lile.. kama Dec R akaomba likizo kuja DSM.

Sasa kwenye likizo yake 2020 akaja kujua nina mahusiano na S. Na ugomvi ukawa mkubwa wakaitakana huko na kutaka kuja kwangu kunifanyia fujo. Uzuri rafiki yangu alinitonya(huyu jamaa anaongea na R). Baada ya ugomvi si unajua tena wanaume kila sehem nkaenda kuomba msamaha na kumfanye amuone adui mwenzake (wazungu wansema divide and conqur) basi baada kuona hiyo inashindanyika nikamuacha R akarudi zake kazini. Mimi nkipambna na S..

Sasa kwa upande wa S nikaendela nae lakini huku nikimuwaza R.. sasa kuna kipindi mambo yakaja kuwa mabaya na nikatengana na S maana nae alisafiri.. nikaendelea na shughuli zangu..

2021
Nikakutana na R si unajua tena (kiporo hakihitaji moto mwingi) nkashangaa nimerudiana na R na mapenzI shamu shamu .. msamaha nkaomba na maisha yakaendelea..

2022 Feb
Mungu akatujalia R akashika ujauzito na nikawa najipanga kwaa ajili ya taratibu za kwenda kujitambulisha.. wakati nipo kwenye harakati za kuweka mambo sawa.. mara jion nashangaa txt iniangia kwenye simu yang, na alienitxt, S na tukaongea machache nkamsadia ya shida kuna sehem alikuwa amekwama kipesa.

2022 June
Sasa mama watoto wang future wife wakati yupo mkoani.. Bas mazoea na yule binti S yakawa kama yamerudi na kimasiraha, nikawa nimeshaweka na kipindi hicho amesema hakuwa na mtu, kiasi fulan hakuwa mtu wa mambo mengi na mimi ndo nilimzinguaga kipind kile..

Sasa juzi hapa kaja kwangu na kuniambia kuwa ana ujauzito wangu.. yaan kama nina watoto wawili wapo njiani.. na kwao pia nimeambiwa natakiwa niende nikajitambulishe..

Kiukwel wote nawapenda ila dini yangu hairuhusu kuwa na wake wawili.. Na hata kama zinaruhusu ila wao hawapatani.​
Mkuu,Dini yako ni ipi hiyo!?
Wasomi wa elimu ya Dini tupo hapa tunaweza kuona nanna ya kukusaidia kwa muongozo wa Dini yako.
 
Back
Top Bottom