Msaada: Nina presha 162/103 umri wangu miaka 33. Je, nianze dawa au nibadilishe lifestyle?

Msaada: Nina presha 162/103 umri wangu miaka 33. Je, nianze dawa au nibadilishe lifestyle?

Sasa mbona unamwambia aishushe mpk 140 hapo hapo asiiache ifike 130
BP ina presentiwa hivi SBP/DBP
Kwa mfano 140/90
DBP maana yake Diastolic Blood Pressure na kwa mfano huo ni 90
SBO maana yake Sytolic Blood Pressure na kwa mfano huo ni 140

DBP kupanda kwa DBP kuna mahusiano na kuwa na Bad outcome but not in all cases
 
Cheki sugar maana Presha na Sugar ni mtu na mpwa wake !!
 
Pole mkuu!
Nikupe hongera kwa kupata alert kuwa kuna tatizo na u need to work hard kuliepusha. Wengi wetu tunayo hayo matatizo lkn huja kugundulika late wakati hali ishakuwa mbaya sana... mfano ni pale mtu anapopigwa stroke.

Mimi kuna wakati nilikuwa na kg kama 89 hivi kwa height yangu nilikuwa overweight lkn sikujua kbs hilo suala... ilikuwa kawaida sana kuumwa kichwa na kuchoka sana hata kwa kutembea kidogo tu....

Siku moja kichwa kiliniuma sana kila nikipiga panadol wapi, maji litre na litres wapi....

Nikaenedha gari hadi Hosp ya GEMSA kwa watu wa Arusha wanaifahamu. Kufika hapo nikafuata taratibu na kufika pale kwa nurse kwa ajili ya vipimo vya awali yaani pressure na weight na height.

Baada ya kuoima pressure niliona nurse kama amwshtuka kidogo ingawa alijitahidi kujizuia... mara akaseme subira nakuja, akaingia chumba cha daktari, dakka kama 7 hv nikaona kile kiuzio cha kijani kinasogezwa pale kwangu na maktari wakaja kama 5 hivi.... nikashtuka...

Wakaanza kunipima baadae wakanipa dawa fulani nikaweka kwenye ulimi zikawa zinayeyuka kidogo baadae wakanioima tena pressure ikawa imeshuka 140/96 kama sikosei. Hapo wakanambia ndo imeshuka.

Baada ya hapo nikabaki na madaktari wawili tukahamia consultation room

Daktari akanihoji style yangu ya maisha akanieleza kuwa nipo katika risk kubwa na nisipochukia hatua hali haitakuwa shwari. Akanishauri kuounguza wanga, sukari na fried +junk food. Na kwamba nikizembea hilo nitaanza dawa tena ikiwa sitopata mqdhara makubwa zaidi.

Nilirudi nyumbani mnyonge sana
From that day nilianza jogging naenda 1.5Km, it was 2017 nipunguza kabisa wanga, sukari, soda mitungi ikawa No etc... maisha yangu yalikuwa ni mazoezi kama 6 months nikaanza kupungua sana, mwaka hv nikawa nimekata 15kg....kukimbia nKo nikagain nikawa naenda 10km-21.1kms nikaanza kushiriki marathons na nikawa addicted na ruuning. Gym ni kidogo sana kuhudhuria.

Niseme ukweli hali ile imenisaidia sana sasa kila mtu anatamani kuwa kama nilivyo nipo slim, No wese mwilini na katika kipindi hicho sijawahi tumia dawa yyt ya pressure zaidi ya mazoezi.

Kwa sasa nishakuwa nguli i run 200km kwa mwezi last year nilijiwekwa target y kukimbia 2000km na nilifanikiwa. Nipo kwenye ckub mbalimbali za runners, na member wa gym kadhaa hapa mjini.

Nikutie moyo ndugu yangu una nafasi ya kubadili life style yako kbl hujakutwa na makubwa.... i have a friend alipigwa stroke ofcn akaka bench 2 yrs ashukuriwe Mungu amekaa vzr sasa.

I have friend pia alipigwa stroke hadi sasa ahajaka sawa ni kama 4 year.

Nilichoamua from 2019 ni kuwahamasisha marafiki zangu na ndugu zangu juu ya kufanya mazoezi, namshukuru Mungu wengi wanaitikia vzr and they are doing good.

Download application inaitwa strava itakusaidia kukupa motivation na uta-grow vzr kwenye mazoezi hasa walking na running.

Kama unaweza kuruka kamba ni nzr sana pia it will help.

Gym sikushauri wengi wanaenda kwa show off tu hakuna kitu wanafanya cha kuwasaidia.

Apart from afya mwonekano wako unakuwa super sana. Unene haujawahi kumpendeza mtu nadhani ni kwa sababu ya madhara yake.

Karibu sana ukihitaji ushauri.

Ngoja nilale kesho chap 05:00Am niamke nipige 10kms kwa pace ya 5:00
Ukifata huu ushauri hatojuta
 
SBP ikiwa imakaa kwenye 142 na DBP 82 VIPI hapo unaweza kuwa na hofukuwa pressure iko juu?
 
Wakuu habari zenu,

Kama nimevoandika hapo juu nimepima presha Leo na presha yangu ni kama hiyo nlioandika Ila sikuwahi kuwa na presha. Sasa wakuu ushauri wenu nianze dawa au nianze lishe ya kuacha wanga na sukari?
Kwanza wewe unahisi Nini mwilini mwako mkuu
1.Kama ulipima Mara TU baada ya kufika Hapo ulipopimia kipimo majibu hayo SI sahihi
2.Kama ulipima ukiwa na njaa majibu hayo SI sahihi
3.UZITO WAKO NI KG NGAPI?
 
Juzi usiku nlipika chapati za Maji nliweka sukari Na chumvi nikala nlivomaliza nikashushia Na Pepsi nikaenda kulala usiku kwenye SAA 9 nliharisha Sana tangu Muda Huo mpaka Sasa najisikia Vibaya nkilala nahisi kama Moyo unaelemewa nakosa pumzi pia nahisi kama kitu kina nichoki shingoni
 
Juzi usiku nlipika chapati za Maji nliweka sukari Na chumvi nikala nlivomaliza nikashushia Na Pepsi nikaenda kulala usiku kwenye SAA 9 nliharisha Sana tangu Muda Huo mpaka Sasa najisikia Vibaya nkilala nahisi kama Moyo unaelemewa nakosa pumzi pia nahisi kama kitu kina nichoki shingoni
mrembo ulitakiwa ule matunda ulale unaona sasa yatakukuta mengi zaidi
 
Wakuu habari zenu,

Kama nimevoandika hapo juu nimepima presha Leo na presha yangu ni kama hiyo nlioandika Ila sikuwahi kuwa na presha. Sasa wakuu ushauri wenu nianze dawa au nianze lishe ya kuacha wanga na sukari?
Mimi kama muathirika wa shinikizo la damu kwa miaka arobaini sasa na kutibiwa JKCI na kufanyiwa vipimo vyote na shinikizo langu ni chini ya yako natumia dawa Kila siku miongo mitatu sasa.
BP ya juu hailetwi na lifestyle pekee huenda kama mimi nilivyo ni hitilafu kwenye moyo.
USHAURI: Nenda hospital kafanye vipimo vyote hasa vya ECHO na umeme wa moyo pia Chunga lifestyle yako haswa pombe.
 
Mimi kama muathirika wa shinikizo la damu kwa miaka arobaini sasa na kutibiwa JKCI na kufanyiwa vipimo vyote na shinikizo langu ni chini ya yako natumia dawa Kila siku miongo mitatu sasa.
BP ya juu hailetwi na lifestyle pekee huenda kama mimi nilivyo ni hitilafu kwenye moyo.
USHAURI: Nenda hospital kafanye vipimo vyote hasa vya ECHO na umeme wa moyo pia Chunga lifestyle yako haswa pombe.
Hivi presha nayo huwa ya kurithi
 
hiyo pressure kwa wewe siyo labda mtu mwenye miaka 60 kwenda juu
 
Acha wanga na sukari kabisa , anza kwenda gym lift weight, piga aerobics ndani ya miezi 3 utajihisi kama kijana wa miaka 23
Nina miezi 6 leo bila kutumia sukari. Nafanya steps aerobics nyumbani aisee hata enzi za ujana sikuwa hivi. Sitii sukari kwenye chai, sinywi tena soda, keki wala ice cream. Wala asali. Nimepunguza ubwabwa na ugali. Nakamata mdudu na nyama choma nasindikiza na wine glass moja. Makunyanzi ya uso kwisha. Ninashangaa hata siamini. My belly fats zimepungua dramatically. Weka bundle halafu bofya hapa

View: https://youtu.be/-si1MZD5MFE?si=7wX1kOfQABtfRSG4
 
Mimi kama muathirika wa shinikizo la damu kwa miaka arobaini sasa na kutibiwa JKCI na kufanyiwa vipimo vyote na shinikizo langu ni chini ya yako natumia dawa Kila siku miongo mitatu sasa.
BP ya juu hailetwi na lifestyle pekee huenda kama mimi nilivyo ni hitilafu kwenye moyo.
USHAURI: Nenda hospital kafanye vipimo vyote hasa vya ECHO na umeme wa moyo pia Chunga lifestyle yako haswa pombe.
Pole Sana Ni vyakula Gani unakula kumaintain afya yako
 
Nina miezi 6 leo bila kutumia sukari. Nafanya steps aerobics nyumbani aisee hata enzi za ujana sikuwa hivi. Sitii sukari kwenye chai, sinywi tena soda, keki wala ice cream. Wala asali. Nimepunguza ubwabwa na ugali. Nakamata mdudu na nyama choma nasindikiza na wine glass moja. Makunyanzi ya uso kwisha. Ninashangaa hata siamini. My belly fats zimepungua dramatically. Weka bundle halafu bofya hapa

View: https://youtu.be/-si1MZD5MFE?si=7wX1kOfQABtfRSG4

Kinywaji chako ni Nini hasa Mkuu.... breakfast yako lunch Na dinner zikoje
 
Acha sukari na Kila kinywaji cha sukari utakuja kunishukuru humu.


Niliacha kula sukari tangu mwaka 2017 nimeshuhudia mabadiriko makubwa sana kiafaya. Makubwa mno!


Punguza uoga fanya maamuzi magumu. Acha kula Bidhaa kula Vyakula. Bidhaa ni mavyakula yenye kemikali kama Coca-cola, chocolate n.k na vyakula ni Vitu fresh kama viazi , mohogo n.k
 
Juzi usiku nlipika chapati za Maji nliweka sukari Na chumvi nikala nlivomaliza nikashushia Na Pepsi nikaenda kulala usiku kwenye SAA 9 nliharisha Sana tangu Muda Huo mpaka Sasa najisikia Vibaya nkilala nahisi kama Moyo unaelemewa nakosa pumzi pia nahisi kama kitu kina nichoki shingoni
Elimu ya Lishe ni muhimu sana sana sana!


Hivi usiku unawezaje kula CHAPATI na Pepsi MLS 375 yenye masukari vijiko 10. Yani unakula mawanga na masukari Tena usiku. Hapo lazima upate likitambi. Ulale kama unakimbizwa au upate maluwe luwe.


Piga chini sukari kula kiafya.
 
Nina miezi 6 leo bila kutumia sukari. Nafanya steps aerobics nyumbani aisee hata enzi za ujana sikuwa hivi. Sitii sukari kwenye chai, sinywi tena soda, keki wala ice cream. Wala asali. Nimepunguza ubwabwa na ugali. Nakamata mdudu na nyama choma nasindikiza na wine glass moja. Makunyanzi ya uso kwisha. Ninashangaa hata siamini. My belly fats zimepungua dramatically. Weka bundle halafu bofya hapa

View: https://youtu.be/-si1MZD5MFE?si=7wX1kOfQABtfRSG4

Safi sana mkuu , Huwa nawashangaa watu wanamcheka Dr Janabi eti wanashindwa kuacha kula sukari.

Sukari ya kiwandani ni Jini inasababisha matatizo mengi sana sana Kwa Binadamu ni vile watu tumeshaingia kwenye chain kutoka ni ngumu.

Mtu akiacha kula sukari ndani ya mwezi mmoja ataona mabadiriko mengi sana sana. Kubwa zaidi ukiacha sukari ni Moja ya njia za Anti-aging. Utaonekana kama hukui kumbe umri unaenda.

Leo unakuta mtu anakunywa soda Kila siku na keki na mavyakula mengine ya sukari. Mtu anakuwa na miaka 25 ila anaonekana kama ana miaka 60. Hatari sana!

Mimi tangu mwaka 2017 sijawahi kuweka sukari mdomoni kwangu! Sina kitambi.


Tangu mwaka 2017 sijawahi kunywa hata hiyo chai ya asubuhi sijui. Na nimeshasahau kama watu Huwa wanakula asubuhi.
 
Back
Top Bottom